Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Miaka ya 1980-90 kuna msichana mrembo aliishi Oyster Bay na baba yake. Baba yake alikua mfanya kazi wa ndani wa Mzungu na walipewa servants quater. Yule binti alikua na akili sana shule na alifaulu darasa la saba na kupata nafasi katika moja ya shule za wasichana za vipaji maalum Dar.
Wavulana wengi walimsumbua, hasa wale watoto wa vigogo walioishi karibu na yeye. Wengine walimdhihaki baada ya kuwalataa kingono kuwa anaishi nyumba ya kijakazi na maringo yamemjaa.
Sasa hivi yule msichana ni Mkurugenzi wa Shirika na Baba yake amemjengea nyumba nzuri anaishi kwa amani