Hakwambii ukweli sababu anakupenda

Hakwambii ukweli sababu anakupenda

Binafsi niliwah pitia mahusiano ambayo una mtext demu sms ila anakujibu baada ya 5 hrs au zaid so mm niliamua tu kuendelea na ratib zangu za vituo vinavyo fuata so alipokuja kugeuka nyuma alinikuta tayari nishabeba abiria mwingine yaan kimya kimya tu
Ulikuwa ni the other option... ila bora wewe, ushawahi ambiwa "Goodnight!" Saa nane ("8") mchana?! 😔
 
Kumfariji tu mtu inaua zaidi Mkuu mchane mapema afanye mambo yake tu ... hio utakuja kumuimiza vibaya sana !!
Kwanza mwingine hata asipokwambua utaona vitu vitu fulani vimebadilika hapo mapemaaa jiongeze
Ngoja nikupe mfano practical...., Mfano mpo sehemu mnakunywa kwa tamaa zenu wewe na rafiki yako wa siku nyingi mkafanya jambo ambalo mwenza wako litamuumiza; ingawa baadae utajutia maisha yako yote ila utamwambia mwenza wako ili iweje:-
  • Amchukie huyo rafiki yako na kuleta ugomvi
  • Akupunguzie guilty conscious yaani (ushare nae hayo maumivu yako uyahamishie kwake)
  • Akuone kwamba ni mkweli yaani huwezi kumdangaya kwa maneno wakati ulimdangaya kwa vitendo ?
In short ni kwa scenario ipi ya wewe kukwambia itajenga ? Wanasema whatever Happens in Vegas stays in Vegas.....
 
Ile feeling ya upendo wa kweli ni kitu muhimu sana

mapenzi ni matamu,
ni mazuri,
ni masafi mfano wa sufi,
NOTE.........hadi mpendani!!!!.
 
Kwahio ni selfish anajali nafsi yake na maumivu yake kuliko yako ? Sijasema akiwambia hakupendi bali nimesema anayekudanganya huenda anakupenda - anakuepusha na consequences / maumivu
Ni kweli..sema Bora apoge kimya tu
 
Kuna ukweli haujengi sanasana unabomoa tu (kama una uhakika hautajulikana na ulifanyika kwa bahati mbaya / tamaa) ile trust kwamba fulani hawezi kuku-let down au kufanya kitu fulani ikishavunjika it will never come back (nothing will ever be same)....., Wanasema Ignorance a Bliss

Kwaio mkifanya kwa bahati mbaya au tamaa na watu mnaowapenda wakijua huwa mnajisikiaje?
 
Kwaio mkifanya kwa bahati mbaya au tamaa na watu mnaowapenda wakijua huwa mnajisikiaje?
Ikitokea kila siku unaomba asijue na sababu hakuna siri ya watu wawili siku ya siku linaweza likajulikana kwahio wengine kupunguza mzigo wa roho kuwa juu kwamba huenda kesho itajulikana wanatanguliza kusema ili waweke story kama wanavyotaka wao.....

Ingawa wengine wanabisha mpaka hatua ya mwisho - Kama ule wimbo wa Shaggy it wasn't me..., yaani unashikwa kabisa lakini unasema sikuwa mimi.....;

Ubaya ni pale anakudanganya wewe lakini kila mtu kitaa anajua vinginevyo (hapo anakuchezea) - Kwahio sikubaliani na Shetta kwenye wenye wimbo wake.......


View: https://youtu.be/l2okzSIpbCc?si=idSrPyAcIDePXt-E



Nachosema ni pale ambapo hakwambii kilichotokea sababu anaku-protect na anahakikisha hafanyi tena, mpaka pale ikitokea tena bahati mbaya....
 
Back
Top Bottom