Hakuna namna, ualimu ndio njia ya kutokea

Hakuna namna, ualimu ndio njia ya kutokea

Hahahahahahahah..Umetiiiisha sana Mkuuu......
Tupe mbinu na sisi bhasi, ulivyoacha;unajishughulisha na nini nowadays...?
Mpwa wangu suijali, MUNGU ni wa ajabu sana, ametupa akili na maarifa mengi. Kwa sasa najishughulisha na Ukulima na Ufugaji lakini pia huwa nikipata kazi za muda mfupi kwenye NGOs nafanya, ila najitahidi nisipoteze lengo langu. Fanya kazi upate mtaji ufanye mambo mengine ambayo kweli unahisi unayweza na unayapenda, usifanye jambo ili kuufurahisha ulimwengu, Kuwa asubuhi unaamka umevaa Tai na suti unaingia kwenye gari unaenda ofisini, wakati unajua kabisa kuwa unaitesa roho yako hakuna cha maana unachokipata.

Nilisoma mahali Fulani kuwa WEKA MALENGO AMBAYO YATAKUFANYA KILA UKISHTUKA KITANDANI UNATAMANI UKIMBILIE HUKO TUUUU, PIA NIKASOMA MAHALI PENGINE KUWA UKITAKA KUFANIKLIWA FANYA KILE KITU AMABCHO UNAKIPENDA SANA SANA, kwa sababu utakua unakifanya huku unafurahi na ukikifanya huku unafurahi maana yake ni kwamba utafanikiwa. Ni hayo tu kwa leo! Uko tayari?

Kumbuka, njia ninayoipitia mimi si lazima na wewe uipitie, kipindi Fulani nilipoacha kazi kuna mtu wa karibu sana akasema "Elli hana kazi sasa ataacha kuringa" hahahaha usisikilize watu, usikilize moyo wako tu. Amen, Blessed
 
Nyie tokeeni, pitieni, vukieni, katizeni mie ualimu ni alfa na omega upo kwenye damu, yani hadi damu yangu ina vumbi la chaki....hata nikiwa na PhD hata nikiwa bi/milionea kufundisha siachi
I love this! I am not a teacher lakini nina uhakika kwa 100% wala nisingejuta endapo ningekuwa mwalimu! Tatizo wengine wanadhani kwenye hizo sekta zingine ndo peponi! Wakiwaona wale wa kwenye sekta binafsi na t-shirt zao mzuri siku za Ijumaa wanadhani wamepatia kumbe, kimsingi, walimu wamepatia kuliko majority ya wale wanaodhaniwa wamepatiwa! Thanks God kwamba nimepata kufanyia kwenye sekta zile ambazo wengi wanadhani ndo wamepatia ile mbaya kwahiyo mtu hawezi kunidanganya... YES, wapo waliopatia lakini majority hawana tofauti yoyote na walimu huku mwalimu akiwa na comparative advantages nyingi zaidi.
 
Kazi yeyote ukiifanya kwa Malango na umakini uliotukuka hakika utafanikiwa...hakika ukiwa mzembe utakufa kizembe kazi ni kazi...pambana utafanikiwa Kijana....kwani kuna wangapi wanakazi nzuri ila maisha yao bado ni yakupanga Na kuhamahama? Wangapi kila siku ukiomba msaada anakwambia pessa hakuna...vijana tujipange tuache kuchagua kazi Na tuchangamkie fulsa za mazingira
 
.
WANAUME ndio wabeba mizigo

Mwisho tujue tunatofautiana matamanio, malengo, aina ya maisha tunapenda kuishi na vision.
.
Wenzangu na mie kila siku unaota kuendesha atleast VX, umeshindwa sana hata mark X, lazima ualimu usiwe kazi ya maana kwako


Ualimu kwa wanaume kwa mtazamo wangu sisi wenye njozi kubwa.

Kwa wanawake ninyi fieni humo tu kwasababu mnafanyakazi kutafta pesa ya saloon na mashindano ya mavazi stuff.

Your post was so sexist. Umeongea utafkiri tuko karne ya 16, mwanamke kakaa kwao anaota kuolewa na tajiri.

Ingawa kweli bado wanawake wengi wanawaza kuwa mwanaume ndo main bread winner, Hata wanawake tuna ndoto.

Wengine tuna lifestyle tunatoyaka kuishi kwahiyo kuna kazi tukifanya tutakonda kwa msongo wa mawazo.

Wengine tunataka kuwa ever financially secure, and that doesn't mean being married to a wealthy man.

Wengine tunapenda kujitegemea na uhuru.

Ingawa maneno yako Yana ukweli kwenye jamii yetu, soon itabidi ubadilishe kauli. Useme tu some jobs are not for the ambitious.
 
Kwa mshaara huu mkia wa mbuzi kwa nini tusiseme hivyo? Tumekuja huku kutoka tu mi nasubiri nipatiwe barua ya kudhibitishwa niingie benk nipate mkopo then nifanye bussiness. Hii sio kazi ya kusema mbele za watu aisee.

Hahahaha kazi gani unayoweza kuisema mbele za watu!?

Jifunze kupenda kitu chako, JIKUBALI
 
kweli wewe ni mwanamke.. nyumba za kupangisha ndio biashara kubwa..

biashara za uhakika ni manufacturing.. ndio maana magu anawaambia nssf na ppf wawekeze kwenye viwanda.. waache biashara za kizembe za kujenga majengo na kupangisha...

tatizo la wanawake mnajifanyaga mna akili kutupumbaza mabwana zenu.. kesho mkikutana na jambe linalofanya biashara za kiume mnatukimbia kwa spidi kali

Kuna walimu nafanya nao kazi wanaume, ni watu wenye pesa tu wana biashara zao kubwa wana nyumba zao wamwpangisha, haya mambo kila mtu na akili zake kwenye huu huu ualimu ukiamua kua Tajiri utakua ukiamua kuwa masikini unakua, watu wawili wanaweza kupewa m1 kila mtu, mmoja akafanya mambo ya maana mwingine akala bata kazi kwako kuchanga karata hakuna kazi isio na changamoto ila walimu tumezidi kulia lia
 
Ni kweli nilikuwa nikisubiri kwa hamu kupata hiyo ajira lakini sasa hivi cha moto nakiona ila kinachonisikitisha ni kuona ubaguzi
unaofanywa na serikali yetu kwa kuamua kulipa wafanyakazi wa kada nyingine mishaara mirefu alafu wengine mishaara kiduchu na bila kupewa posho yoyote. Mimi hapa kwenye halmashauri niliyopo kuna kambi ya jeshi na watu wa game reserve ndo watu waliojenga nyumba na kutupangisha sisi walimu alafu wanakula bata kama kawaida na kusaidia kwao.
Tatizo walimu mnalow esteem na kuishi kwa kuskia,mnawaza mambo ya kufikirika tu.ni kada gani serkalini inayofananana na yako,preservice training period wanapata mshahara mkubwa?ebu nitajie badala ya kulalama....!!Blame game for teachers is customary activity
 
Km mtu umeona smwhere kuna green pastures why cant you go kama una meet criteria badala ya kubweka tu...!!!
 
Kuna shule nyingine wanafika hadi 100 ndo maana siku hizi tumeamua kugawana hadi subtopics, hatuna kazi za kufanya.
Na bado kuna shule vijijini zina walimu wa5 tuuu wanafundisha vipindi 20 kwa wiki.........

Kweli life halipo FAIR.....
[emoji57] [emoji57] [emoji57] [emoji57] [emoji34] [emoji34] [emoji34] [emoji34]
 
Ndugu yangu maisha ndivyo yalivyo, never be Fair. Usitegemee kuwa ipo siku Mwalimu atakuwa na mshahara mkubwa na Marupurupu. Why? Idadi ya walimu ni kubwa sana, Low quelification during enrollment, hawaingizi mapato yoyote moja kwa moja serikalini, sio Kipaumbele cha kwanza kwa serikali nk.

Good thing kwa ualimu ni kwamba wanaajirika serikalini siku zote. Yaanii wewe ukisomea ualimu tu, ujue ajira serikalini ipo tu. Ni kada mbili tu kwa sasa hapa Tanzania zina uhakika wa Ajira serikalini. Elimu na Afya.
Something is better than nothing.
Huo uhakika wa ajira serikalin umesema wewe!......

Tuulize sie tunaousubiria mwaka na½ sasaa na hakuna hata dalili........

Ni lazima walimu warudishiwe HESHIMA yao kama zamani kwa kutengenezewa mazingira mazuri ya kazi na marupurupu.....

Kazi gani isokuwa na posho bana!....


Now Askari anamzidi mwalimu karibia 40% na mnataka tukae kimyaaaa!......

KUJITAMBUA kwa mtu individual ndo kutamfanya ATUSUE lakin isiwe ni kigezo cha kuwakandamiza baadhi ya watu..hata MUNGU anaona na atalipa fadhila kwa wavujajasho wasiothaminiwa.
 
Mie nadhani it suits women hii profession kuliko wanaume, ndio maana kuna kamsemo kanasema strong men merry teachers, wanawake ni walezi by nature.

Niliposoma comparative education nilikuja kugundua/ na imeandikwa nchi zilizoendelea walimu wanaume ni wachache sana, mathalan wingereza karibu 78% ya walimu wote ni WANAWAKE.

Kwanini wanawake na sio wanaume, WANAUME ndio wabeba mizigo, familia nk, tunahtaji kupata kipato kikubwa ili kuendeleza maisha, kusomesha nk. Sasa akina Evelyn Salt hawa ni wanawake, wanaume wenzangu kazi ipo, tusidanganyane eti ualimu kuna muda wa kutosha kufanya kazi za ziada, labda kama kwenu huko mlipo mna loopholes na hamsimamiwi hakuna wakuu wa shule makini.

Muda wa masaa ya serikali ni masaa 9 kwa wafanyakazi wote, una saini asubuhi 1:30 na kutoka uwe na kipindi huna ni saa 9.30 cjui ninyi hz muda wa kutosha mnapata wapi? Tena kada nyingine wenzetu akikaa mpk saa 11 sio kua kabanwa no anatumikia allowance na atapewa ama atajiandikia/andikiwa.

Kuna biashara huwezi simamia saa 10 mpk saa 12 ni uongo lazima uitaji muda wa kutosha, ikibd full time.

Ualimu ni kazi ambayo unaenda likizo, unafanya vikao, unafanya overtime bureeee na utapokea pesa tarhe 30 mpk 30 mwezi unaofuata ya mshahara wako tu tena uliokatwa na CWT

Ualimu ni kazi unayoweza dhurumiwa na huna pakusema wala kudai, maana hata bosi wa kazi yako kumjua ni issue, kazi ina wasimamizi kibao, juu ya mwalimu wa kawaida, kuna walimu wenzangu wa msingi wakimuona hata mratibu elimu kata wanatamani kujinyea. Ualimu suits women the most.

Mwisho tujue tunatofautiana matamanio, malengo, aina ya maisha tunapenda kuishi na vision.

Kuna mtu, kwa mf rafiki yangu mmoja aliajiriwa kufundisha primary, salary yake ni kama 270k alipoanza, aisee huyu alilidhika akawa bonge, kanenepeana kama tetea la bata hata ukimwambia kasome ufikie kidiploma anakwambia nisome ili iweje, kwake maisha ni kuwa na uhakika wa kula na nyumba ya vyumba viwili na sebure bila finishing basi, watoto wanasoma elimu kata bure maisha yamekoma.

Wenzangu na mie kila siku unaota kuendesha atleast VX, umeshindwa sana hata mark X, lazima ualimu usiwe kazi ya maana kwako, maana kupanda madaraja tu ni kesi mpk usugue magoti kumeomba mungu.

Ualimu hata usome ufike masterz hutatambulika kwa elimu hiyo uta push tu madaraja basi, sasa mpk nifikie daraja I lenye milioni 1 na point ni leo?

Life begins at 40 alafu wewe unasubiri kufika daraja I, lini?

Ualimu kwa wanaume kwa mtazamo wangu sisi wenye njozi kubwa ni sehemu ya kukusanya mtaji, or mark time area ukijiandaa kwa safari au mchakamchaka.

Kwa wanawake ninyi fieni humo tu kwasababu mnafanyakazi kutafta pesa ya saloon na mashindano ya mavazi stuff. Kila siku mnachukiana kwa mashindano ya kuuza bagia na karanga stuff
Daaah umenigusa sana aisee mi mwenyewe ni ticha since day one nilijiapia nitaachana hiyo kazi.baada ya muda.

Saivi naandaa tu mazingira ya Mimi kutoka huku nikitoka ni mperampera tu
 
Natamani niwaone hao walimu cjawai kutana nao thou nimepita shule kadhaa, walimu wenzangu wengi wenye atleast visible life success ni wenye privilege kiasi mf wakuu wa shule.

Maana kwanza hawana muda wakukaa shule akiwa na makamu mzuri basi yeye kazini anakuja hata once a week au anakuja ana saini anasepa.

Hawa walikuwa/wanauwezo wa kutumia pesa ya shule na ya ziada na mishahara yao ikakaa.

Hizi case study zenu/zetu ziwe real ni walimu wangapi wanafikia hayo? Maana atleast kila staff ina watu(walimu) kumi na kuna uhakika ukatembelea shule 10 ukakuta wawili tu, nao sio maisha kusema maisha.

Eneo ninalokaa mie kuna chuo cha ualimu, sekondari 2 na shule za msingi 3 around kijiji kimoja na taasisi nyingine za serikali kama mbili hivi na chuo cha kilimo lkn ukitembelea madukani hapa center utakuta madaftari ya walimu ya madeni mpaka ya sembe 2kg, bado wanapigwa pesa kukopa mitaani kwa riba ya 50% yan laki kwa laki na nusu. Hawana jinsi wanakopa.

Sasa huwa najiuliza ina maana walimu tu ndio hawana akili ya kujiongeza ili kuongeza kipato? Ina maana ukienda fani nyingine kama kilimo, udaktari/nurse nk ambao tupo nao huku vijijini unakuwa na akili ya maisha?

Jibu linabaki ni hapana, ila ualimu sio kazi inayotoa malipo stahiki. Na marupurupu ya kujikimu.

Ngoja nikuoneshe yanayotokea huku vijijini, na walimu mnajifanya hamyaoni mnataka tusifiwe hapa wakati kazi hii haina malipo halisi.

Mwl anaeanza saizi daraja la IIIA, take home ni kama 270 kama sio chini ya hapa ila ipo maeneo hayo hayo. Huyu anaanza kazi pesa ya kujikimu anapewa laki na nusu, nyumba ya kupanga miezi sita inahtaji 240000/= hapa nimepigia anaanza na chumba cha elfu 40 kwa mwezi, wanaoanzia mijini kabisa ndio shida zaidi.

Anahtaji godoro la kuanzia, utakuta mahtaji yote kuanza kazi ni kama laki 5 minimum, alafu kapewa 150000/= tu bila shaka hii ataitumia kwa chakula tu nakununua sufuria na jiko la mkaa/mafuta na sahani wakati akisubiri mshahara wa kwanza, na pengine huwa hautoki kwa mwezi husika.

Mwishowe anaamua kukopa kwa mtu/ndg na jamaa au walimu aliowakuta ili maisha yaanze, (madeni yanaanza RASMI) sasa kila akifika mwisho wa mwezi anajikuta analipa deni anakosa pesa ya kula, hii trend inaendelea, mwisho anakuwa mwenyeji eneo husika anaanza kukopa madukani, hapo hajawai nunua chochote cha ziada ndani,hata kuchonga kitanda.

Miezi kadhaa badae anaona kujitoa katika tabu nikakope bank, anaenda kukopa bank, kwa mshahara wake anapata mil 4 ikikatwa anabaki na 3.8mil anarud nyumbani analipa madeni mpk inabaki karibu nusu.

Anaamua basi na yeye ni binadamu ananunua kitanda, labda na ka tv ka kichina ka 250000/= Familia za kiafrika nazo zipo nyuma, mama/baba anaomba pesa au mdogo mtu kafukuzwa ada, home hawana chakula anatuma kidogo, akiangalia balance kesha baki na laki 2

Mwisho wa mwezi salary inaanza kukatwa sasa hapokei 270000/= tena anapokea 190000/= hapa mdipo shida za walimu zinaanza.

Kesho anaingia vicoba (shida tu hiz) kesho yake finca, kesho kutwa blacc uko nako anakopa si zaidi ya laki 2 maana salary yake haina dhamana kubwa.

Kabla mkopo haujaisha bank inabdi atop up maana shida zinazidi na kazi kubwa ya ziada anauza bagia kwa wanaume anakomaa na tution ambazo siku hz pia hakuna, au anafungua kiduka cha elfu 50 ambacho kwa mzunguko wa alipo ni mdogo hapo anapambana na wazawa.

Walimu wengi waliopo vijijini wanajua shida ya wazawa huko hawataki kuona una biashara, wana kitu tunaita undewa, wivu wa kimasikini "atapataje mshahara alafu aje ashindane na sisi pia".

Walimu haya yote mnajua ila hamtaki kusema, wanawake ninyi mlioolewa mnakuwa supplied wala hamuoni, wengine walimu huku wa kike ni malaya (samahani kwa neno kali) ila wanafanya, wanatembea leo na diwani, kesho mtendaji, jioni afisa nanii wa hapa kijijini anaeonekana anaweza mpa walau tsh 10000 ya ziada.

So maisha ya umasikini inakuwa ni trend, walimu wamebaki kuwa walevi wengi wetu, stress anaingia darasani na yeboyebo, ananyonga baiskeli shati linanuka jasho anavaa siku 3

Walimu wenzangu haya yapo, mie nayaona kila siku, tupo wachache tuna mantain personality na heshima ya kutokuwa na madaftari ya madeni ya unga madukani lkn sio wote. Wengi wana dhiki

GOD SAVE TEACHERS
Dumelang umeongea ukweli mtupu aisee daaah.

Yaaani haya uliyosema hapo ndo yanayotokea huku ninako kaaa hahhaahhaha

Hatari aisee daaah


Ualimu ni shiiiiidah[emoji3]

Ila kujipanga muhimu.
 
Kwa mshaara huu mkia wa mbuzi kwa nini tusiseme hivyo? Tumekuja huku kutoka tu mi nasubiri nipatiwe barua ya kudhibitishwa niingie benk nipate mkopo then nifanye bussiness. Hii sio kazi ya kusema mbele za watu aisee.
 
Nyie tokeeni, pitieni, vukieni, katizeni mie ualimu ni alfa na omega upo kwenye damu, yani hadi damu yangu ina vumbi la chaki....hata nikiwa na PhD hata nikiwa bi/milionea kufundisha siachi
Nimempenda sana huyu mama
 
Back
Top Bottom