Hakuna binadamu anayekupenda kwa dhati

Hakuna binadamu anayekupenda kwa dhati

Siku ukitoka kwenu Dar..

Ukaenda kutafuta maisha Kigoma au Ruvuma huko.


Ndo utajua Maisha ni Watu na watu sio ndugu zako na wazazi wako. ( utakavyomuishi mtu, ndivo atakuishi ikiwa umechangamana na watu ambao kiakili mko ktk mstari mmoja)


Watu wengi tunapenda kupendwa na kutendewa mambo makubwa mazuri, ili hali sisi wenyewe hatupendi kuwatendea wengine ivo .


Alafu baadae tunakuja unasikia....Watu wabaya sanaa, wana roho mbayaaa mnoo.




Sikatai kwamba kuna watu hata uwatendee mema gan, wao watatafuta kukutenda ubaya, Hao dawa yao ni kuwafanyia ubaya pia .
Moyo wa mtu kichaka.Kule Musoma kuna jamaa alikuwa Mwalimu akamkopesha jamaa yake ambaye alikuwa ni mwananchi wa eneo lile, pesa hiyo wakadaiana muda mrefu,siku moja mdeni wake akamwambia yule Mwalimu kuwa aende nyumbani kwake ili amlipe deni lake, Mwalimu alienda kufika kule Kumbe Mwamba ameandaa vijana wenye silaha, Aisee walimchakaza yule Mwalimu hadi Umauti.Kisa Tshs.400,000/=, Ambazo ni zake mwenyewe, kwa hiyo akikosa pesa na uhai pia.Nyie Acheni tu, binadamu Wabaya sana.
 
Kama wale waliomchinja kama kuku dada yake na Msuya ikasemekana mchongo mzima ulianzia kwa mke wa msuya, akashirikishwa binti wa kazi yaan house girl na pia wachinjaji, kwahiyo wote mke wa msuya ambye ni wifi wa marehemu na binti wa kazi wote ni mashetani
Tobaaa!!!!,Ee Mungu utushike mkono,tunaangamia.Binadamu tunaowategemea ndio wanaotumaliza.
 
Eeeeee!!!,Mke tena?!!!!,Hao viumbe wanabadilika badilika Sana,usiwaamini hata kidogo.
Ni kweli mkuu,Ila huyu ni watatu mkuu,shida unakuta ubavu wako unaishi na MTU mwingine afu na we we unaishi na ubavu Wa mwingine,patamu hapo!!utaona madini yote mpaka yale yanayosadikiwa kuwa yako mbinguni tu yanaitwa LULU,ila we utayonea hapa duniani.
 
Huko chuga hasa waarusha Wana miroho mibaya na hawapendani Hadi ndugu wa damu hata kusalimiana mwiko kabisa ukichangia na ardhi za kurithi na kufungiana njia woooi, hapo ndio nilijua ndugu hawapendani
Kha!kha!,Noma sana.
 
Nimeshakaa sehemu tofauti tofauti na nyingine far away from ndugu na nilijifunza mengi sana hasa kwa kuishi na watu tofauti hasa kwa kuepuka kuvuka mipaka ila pendo lao bado mkuu kufikia bandugu ingawa lilikuwa la kiasi always napendaga win win situation na sio win loose situation nashikamana na watu wenye interest za kufanana
Hiyo nzuri
 
Moyo wa mtu kichaka.Kule Musoma kuna jamaa alikuwa Mwalimu akamkopesha jamaa yake ambaye alikuwa ni mwananchi wa eneo lile, pesa hiyo wakadaiana muda mrefu,siku moja mdeni wake akamwambia yule Mwalimu kuwa aende nyumbani kwake ili amlipe deni lake, Mwalimu alienda kufika kule Kumbe Mwamba ameandaa vijana wenye silaha, Aisee walimchakaza yule Mwalimu hadi Umauti.Kisa Tshs.400,000/=, Ambazo ni zake mwenyewe, kwa hiyo akikosa pesa na uhai pia.Nyie Acheni tu, binadamu Wabaya sana.
Hii nikweli, hasa suala la pesa , pesa imekua na changamoto sana

Imekua chanzo mpka cha undugu kufa
 
Ndugu, haya mambo uliyoandika hapa jukwaani mbona yanajulikana sana hapa duniani?
Kwani ulikuwa huyajui? Kama ulikuwa huyajui na umeanza kuyajua sasa, basi umeanza kukomaa.
Hakuna jipya chini ya mbingu.
Ndio hivyo, nimeanza kujifunza.
 
Umuhimu wa ndgu unapatikana pale kwenye msiba kuoa au kuuguza, ila ndg wengi hawapendi maendeleo ya ndg wegine, watakupenda sanaa ukiwa masikini wa kipato mwenye kujishusha mbele yao, ila usijifanye mujuaji watt wako kuenda English medium, nk hapo watakupenda kiunafiku tu.
Wanapenda uwe mtu wa shida na mahangaiko Siku zote.
 
Ni kweli mkuu,Ila huyu ni watatu mkuu,shida unakuta ubavu wako unaishi na MTU mwingine afu na we we unaishi na ubavu Wa mwingine,patamu hapo!!utaona madini yote mpaka yale yanayosadikiwa kuwa yako mbinguni tu yanaitwa LULU,ila we utayonea hapa duniani.
Dah!!!,we acha tu.
 
Huku kukopeshana sometimes huwa kunaua urafiki
Kuna jamaa yangu alikuja nimuazime hela , hiyo hela Ni nyingi Mimi sikuwa nayo
Jamaa akaenda kuomba mkopo sacos akaniomba niwe mdhamini mi kiroho saafi kabisaa nikamdhamini mshikaji wangu
Cha ajabu kaleta marejesho sita tu halafu kapotea na eti familia yake haijui aliko mke anasema hajui km mumewe alikopa sehemu

Kwahiyo mzigo umekuwa wa kwangu jamaa hata simu zakee hazipatikani

Hapa ndio niko najiuliza huo urafiki upo au ndio ushakufa Tena!
 
Huku kukopeshana sometimes huwa kunaua urafiki
Kuna jamaa yangu alikuja nimuazime hela , hiyo hela Ni nyingi Mimi sikuwa nayo
Jamaa akaenda kuomba mkopo sacos akaniomba niwe mdhamini mi kiroho saafi kabisaa nikamdhamini mshikaji wangu
Cha ajabu kaleta marejesho sita tu halafu kapotea na eti familia yake haijui aliko mke anasema hajui km mumewe alikopa sehemu

Kwahiyo mzigo umekuwa wa kwangu jamaa hata simu zakee hazipatikani

Hapa ndio niko najiuliza huo urafiki upo au ndio ushakufa Tena!
Duh!, pole sana Mkuu.
 
Umenena vyema mkuu,
Umekomaa vyema kifikra.

Mifano miwili aliyoitoa mleta uzi ni dhaifu na haikidhi kuhalalisha hoja yake.
Kwani mdogo wake alipofungwa jela ndugu wote walikuja kumwona?
Marafiki wa kweli wapo na marafiki wabaya wapo
Ndugu wema wapo na wafitini wapo
Wapenzi wa kweli wapo na wapita njia wapo
Wazazi wenye upendo wapo na wasiojielewa wapo

Ishu sio kwamba hawapo tatizo ni umekutana na nani, wapi,
bond yenu ikoje
Mmeunganishwa na nini
Unawezaje kukutana na mtu kazini au company ya kunywa bia na stories alafu utegemee mtu huyo awe msaada mkubwa kwenye matatizo ilhali hamna bond yoyote zaidi ya bia.
Hiyo sio sawa.
Ila upande fulani upo sahihi. Sijui ni ushamba wa kujifanya kujua jua watu, au kuzoeana zoeana na watu hivyo au nini??? Yaani tumekutana kwenye kazi, vilabuni n.k, halafu unalalamika hujasaidiwa? Tatizo watu wana ushamba mwingi wa mikoa na shobo nyingi.

Watu wanafanya wrong selection ya company ya kusaidiana nayo kwenye shida na raha, kabla hawajalaumu ni vema wajifunze kuchagua watu husika wa kuahirikiana nao. Wakiweza hivyo, hakutakuwa na malalamiko yao, ushamba ushamba tu!
 
Back
Top Bottom