Zillion
JF-Expert Member
- May 15, 2017
- 1,389
- 1,889
Umenena vyema mkuu,Umekata tamaa sana, kuna wanaokupenda ila hawajapata access na wewe. Mwanadamu yoyote anapendwa na wastani wa watu wasiopungua 5 kati ya billion 7 waliopo.
Kule kwetu kuna usemi wa "mbwa hakosi wifi" ukilenga kumaanisha hakuna "aso mtu"..
Umekomaa vyema kifikra.
Mifano miwili aliyoitoa mleta uzi ni dhaifu na haikidhi kuhalalisha hoja yake.
Kwani mdogo wake alipofungwa jela ndugu wote walikuja kumwona?
Marafiki wa kweli wapo na marafiki wabaya wapo
Ndugu wema wapo na wafitini wapo
Wapenzi wa kweli wapo na wapita njia wapo
Wazazi wenye upendo wapo na wasiojielewa wapo
Ishu sio kwamba hawapo tatizo ni umekutana na nani, wapi,
bond yenu ikoje
Mmeunganishwa na nini
Unawezaje kukutana na mtu kazini au company ya kunywa bia na stories alafu utegemee mtu huyo awe msaada mkubwa kwenye matatizo ilhali hamna bond yoyote zaidi ya bia.
Hiyo sio sawa.