Hechinodemata
JF-Expert Member
- Sep 16, 2016
- 1,487
- 3,356
Aisee hii imenigusa sana, nilijua ndugu tu ndo wanatabia hii kumbe hata mama wazazi, tuliache kuwaombea wazazi wetu kama ulivyosema hata kama wana tuchukia wakati mwingine
Mama yangu mzazi alinipenda sana na akawa anaongea na mimi muda mwingi na kuniombea sana. Leo pesa zimeisha hata nikipiga simu wanapewa watoto wa marehemu dada yangu waongee (shikamo mama.... jibu; ongea na wajomba zako mimi sina cha kuongea na wewe). nikienda kijijini hata chakula wakiivisha sipo wanakula sibakishiwi. Namshukuru Mungu wakati nina unafuu wa maisha nilijitahi kuboresha ustawi wa wazazi wangu hata nyumba nzuri nikawajengea. Nimeamua niende mbali na kijiji changu zaidi ya kilometa 800 nije nihangaike tena na sasa natafuta kwa tabu ili nipate tena nirudishe mahusiano mazuri na Mama yangu ambaye kumbe nikiwa na pesa ndo upendo unakuwepo. Tusiache kusaidia na kujitoa kwa ajili ya wazazi wetu.




