Tumesha sema na tunarudia kusema marafiki unaokutana nao ukiwa umeshafanikiwa au mmekutana nao kazini hao kuwa nao Makin wengi wao siyo marafiki maana siku ukianguka au ukapoteza kazi Basi na urafiki wenu utakua umeishia hapo na mazoea hatataka kabisa.
Jaribu kufikiria kipindi ukiwa haujafanikiwa au ulipokua hauna kazi kuna marafiki hata kama siyo wengi basi Kuna rafiki ambae alikua mtu wako wa karibu na alishakusaidia mambo flanflan hata kama siyo ya kipesa lakin hata ushauri wake au alikupa moyo ukiwa kwenye majaribu fulani , hao ndo wanakuaga marafiki wa kweli lakin kwa bahat mbaya huwa tukifanikiwa kidogo huwa tunawatupa hata Salam tunakata na badae tunaanzisha urafiki na watu fake.
Marafiki weng wa kazn urafiki wao huwa unakuzwa sana nyakati za starehe na pombe, ukiweza kujitenga na pombe au mambo ya starehe hapo kazin kwenu hautakua na rafiki wa karibu hata mmoja isipokua utabak urafiki wa kukutana ofisin tu.