shushushu VIP
JF-Expert Member
- Jul 24, 2016
- 4,806
- 4,303
Nmeelewa sanaaa
Watu wanapuyanga tu mkuuWatu kama mtihani 90 percent mngefeli, swali liko wazi kwa nn iitwe mahakama ya hakimu mkaazi? Unataja kazi zake, mara level yake halafu unalalamika necta wanapendelea.
Asante kwa ufafanuzi mkuuHata haihitaji kusomea sheria. Sisi tulifundishwa Form Two habari za mihimili ya dola ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama.
Mfumo wa mahakama Tanzania wa Tanzania Bara unaanzia Mahakama ya Mwanzo. Hii ni mahakama ya ngazi ya chini. Inaweza kughukulika na mashauri ya kisheria kwenye kata au tarafa. Mashauri ambayo thamani yake haizidi elfu 50.(Japo busara pia inatumika). Hakimu wake anaitwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo au PCM kwa maana ya Primary Court Magistrate.
Mahakama inayofuata ni Mahakama ya Wilaya. Hii mahakama unspoken rufaa kutoka mahakama za mwanzo ndani ya Wilaya husika. Pia hupokea mashauri ambayo yanathamani zaidi ya shilingi elfu hamsini yasiyozidi laki mbili na nusu. Hakimu wake anaitwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya lazima awe walau na degree ya Sheria.
Mahakama ya Hakimu Mkazi inafuatia. Hii mahakama imepewa hadhi juu kidogo ya Mhakama ya Wilaya na inaweza kuthikiliza kesi ambazo thamani yake inazidi kidogo kiwango cha zile za wilaya. Hushughulikia mashauri ya ndani ya mkoa au Kanda. Hakimu wake anaitwa Hakimu Mkazi (idadi yao inategemea na mahitaji). Mara nyingi inaongezewa jina la mahali ilipo.
Mahakama inayofuata ni Mahakama Kuu. Hii inapokea rufaa kutoka Mahakama ya Wilaya na Mahakama ya Hakimu Mkazi. Pia hushughulikia mashauri ya jinai kubwa kama mauaji au kesi ambazo thamani yake ni kuanzia laki tano (busara). Mahakama kuu ni moja japo inafanya kazi kwa kanda. Hivyo haijalishi kosa lilopotendeka ila popote ndani ya Tanzania Bara shauri linaweza kufunguliwa. Kiongozi wa Mahakama hii anaitwa Jaji na anateuliwa na Rais.
Mahakama ya juu kabisa ni Mahakama ya Rufaa kwa Tanzania Bara. Kiongozi wa Mahakama hii ni Jaji Mkuu. Nayo inashughulikia rufaa kutoka Mahakama Kuu.
Huo ndiyo mfumo wa Mahakama ya Tanzania Bara. Kwa upande wa Zanzibar wao mfumo ni Tofauti kidogo japo. Hiyo ni knowledge ya Form Two.
AiseeYule hakimu wake anaishi ndani ya jengo hilo la mahakama,
ndo maana inaitwa mahakama ya makazi kisutu,
yaani mahakama ya hakimu mkaaji wa mule mule ndani ya mahakama ya kisutu
KweliHiyo ilikuwa Form Two Mkuu miaka hiyo.
UmeonaeWeka hapa kwa faida ya wote............
Hapo ni sawa na unauwa mbu kwa rungu kwenye kichwa cha mtoto mchangaNimekupata vyema mkuu naomba niswalishe nami kidogo juu ya
kazi za hawa ni zipi mahakamani?
1.KARANI
2.WAKILI
3.PP
Natamani sana kujua kazi zao na pia elimu zao.
Karibu mkuu..
Hahaaaaa umenikusha mbaliAsante kwa updates! Natumia General Studies na Civics za sekondari.
AiseeKwa hakimu mkazi kuhusu kesi kuendeshwa na majaji tuu ni uongo.Andy Lyamuya alikuwa jaji lini? Mahskimu hspa huitwa wakazi na mkuu wao ni principal resident magistrate yaani hakimu mkazi kiongozi.
Shukrani mkuuMahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Kwanza fahamu kuwa neno Kisutu yaweza kuwa ni eneo au mtaa au mahali ilipojengwa mahakama.
Pili elewa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi ni level ya mahakama katika mfumo au muundo wa mahakama katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo huanza na mabaraza ya usuluhishi yaitwayo ward tribunals, baada ya hapo hufuata mahakama ya mwanzo ambazo husimamiwa na mahakimu wa mahakama ya mwanzo.
Pili ni mahakama ya wilaya ambayo husimamiwa na mahakimu wa wilaya chini ya usimamizi wa Hakimu Mkazi.
Tatu ni mahakama ya Hakimu Mkazi yenye wajibu wa kupokea rufaa toka mahakama, za chini na kesi nyingine zinazoletwa kwake moja kwa moja. Hapa ndipo ufahamu ya kuwa Kisutu ni jina la mahakama kama ilivyo sehemu nyingine zenye mahakama ya Hakimu Mkazi.
Nne ni mahakama kuu ambazo ziko kikanda na zina division au vitengo mbalimbali kama biashara, ardhi, kazi n.k. Mahakama hizi husimamiwa na majaji na husikiliza kesi nzito kama treason, murder na hupokea rufaa toka mahakama za chini.
Tano na mwisho ni mahakama ya Rufani inayosimamiwa na jaji mkuu na majaji wateule.
Hivyo pamoja na michango ya wengine nadhani umeelewa.
Shukrani mkuu ila usidhani unachokijua wewe na wengine wanakijuaShida iko kichwani kwa mleta mada sio mfumo wa elimu yetu
Zamani zile kulikuwa na somo tulikuwa tunafundishwa lilikuwa linaitwa siasa, mwalimu wetu alikuwa anaitwa Rugimbi mashoto a.k.a iskariote, alikuwa anaandika mahakama za mkoa/mahakama za hakimu mkaziHakuna kitu kama mahakama ya mkoa kwenye mfumo wa sheria zetu. Mfumo wa mahakama unaanzia 1. Mahakama ya Mwanzo. 2. Mahakama ya Wilaya. 3.Mahakama ya Hakimu Mkazi. 4.Mahakama Kuu, na 4. Mahakama ya Rufaa.
Mpaka sasa mahakimu wakazi wako mahakama za mwanzo ila wameweka critelia lazima awe kafaulu lawschooltafuta magistrate act usome nenda government bookshop
kwa vile watanzania ni wa vivu wa kusoma hata kugooge imekushida acha
nikupe kiduchu. hakimu Mkazi kaainshwa ktk hiyo sheria ni nani
kwa Tanzania ni graduate wa LLB, ambae kafanya interview na kufaulu vema usahili wa kuwa hakimu mkazi
ataapishwa na jaji mkuu.
huyo anakuwa na uwezo wa kusikiliza mashauri ktk mahakama ya hakimu kazi
zamani ilikuwa ni mahakama za mikoa pekee ila kwa sasa hata mahakimu wakazi wanapelekwa ktk mahakama za wilaya ambako walikuwa district magistrate ambao zamani walikuwa na diploma
kwa hivo hakimu mkazi akipelekwa wilayani anaitwa district resident magistrate
jurisdiction zao ni kesi zote za jinai,madai nk ispokuwa mauaji,nk
mengineyo watakujuza wengine.
Maelezo Mengi lakini bado hujajibuHata haihitaji kusomea sheria. Sisi tulifundishwa Form Two habari za mihimili ya dola ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama.
Mfumo wa mahakama Tanzania wa Tanzania Bara unaanzia Mahakama ya Mwanzo. Hii ni mahakama ya ngazi ya chini. Inaweza kughukulika na mashauri ya kisheria kwenye kata au tarafa. Mashauri ambayo thamani yake haizidi elfu 50.(Japo busara pia inatumika). Hakimu wake anaitwa Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo au PCM kwa maana ya Primary Court Magistrate.
Mahakama inayofuata ni Mahakama ya Wilaya. Hii mahakama unspoken rufaa kutoka mahakama za mwanzo ndani ya Wilaya husika. Pia hupokea mashauri ambayo yanathamani zaidi ya shilingi elfu hamsini yasiyozidi laki mbili na nusu. Hakimu wake anaitwa Hakimu wa Mahakama ya Wilaya lazima awe walau na degree ya Sheria.
Mahakama ya Hakimu Mkazi inafuatia. Hii mahakama imepewa hadhi juu kidogo ya Mhakama ya Wilaya na inaweza kuthikiliza kesi ambazo thamani yake inazidi kidogo kiwango cha zile za wilaya. Hushughulikia mashauri ya ndani ya mkoa au Kanda. Hakimu wake anaitwa Hakimu Mkazi (idadi yao inategemea na mahitaji). Mara nyingi inaongezewa jina la mahali ilipo.
Mahakama inayofuata ni Mahakama Kuu. Hii inapokea rufaa kutoka Mahakama ya Wilaya na Mahakama ya Hakimu Mkazi. Pia hushughulikia mashauri ya jinai kubwa kama mauaji au kesi ambazo thamani yake ni kuanzia laki tano (busara). Mahakama kuu ni moja japo inafanya kazi kwa kanda. Hivyo haijalishi kosa lilopotendeka ila popote ndani ya Tanzania Bara shauri linaweza kufunguliwa. Kiongozi wa Mahakama hii anaitwa Jaji na anateuliwa na Rais.
Mahakama ya juu kabisa ni Mahakama ya Rufaa kwa Tanzania Bara. Kiongozi wa Mahakama hii ni Jaji Mkuu. Nayo inashughulikia rufaa kutoka Mahakama Kuu.
Huo ndiyo mfumo wa Mahakama ya Tanzania Bara. Kwa upande wa Zanzibar wao mfumo ni Tofauti kidogo japo. Hiyo ni knowledge ya Form Two.
Hili swali linapaswa kujibiwa na mtu yeyote aliyesoma Civics Form Two na kuendelea. Kabla yakukujibu naomba kujua wewe umefikia level ipi ya elimu? Kama umevuka form two basi kuna shida kwenye mfumo wa elimu yetu.
Yule hakimu wake anaishi ndani ya jengo hilo la mahakama,
ndo maana inaitwa mahakama ya makazi kisutu,
yaani mahakama ya hakimu mkaaji wa mule mule ndani ya mahakama ya kisutu