Haki na Demokrasia havitakuja Tanzania kwa Rais kuwapa vyeo Serikalini Viongozi wa Upinzani

Jana nimemsikia Rais Samia Suluhu Hassan akidai kuwa ataanza kuteua nafasi za uongozi bila ya kuangalia vyama.Hilo halina ukakasi kwa mujibu wa sheria zetu ila kwangu mimi naamini kuwa hizo ni mbinu za kijanja janja za kurudisha utulivu wa kisiasa nchini baada ya ule uchafuzi wa wazi aliofanya mtangulizi wake Magufuli katika Demokrasia yetu.

Rais anatakiwa kuelewa kuwa political certainity haiji kwa kuteuwa wapinzani hasa wenye njaa kuwa serikalini.

Hali ya utulivu kisiasa Tanzania itakuja kwa:

1.Kuwa na chaguzi huru na haki.
2.Kuacha mihimili ya nchi kufanya kazi zake independently bila kuingiliwa wala kutishiwa na mhimili wa serikali.
3.Kuondoa uonevu wa vyombo vya usalama hasa polisi pale watu wanapotaka kufanya siasa ambayo ni haki yao kikatiba.
4.Kuwa na uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza.
5.Dola kuacha kutumika na wanasiasa katika kuwasaidia kuingia madarakani.
6.Kuondoa sheria kandamizi na za hovyo zinazolenga kukandamiza watu.
7.Kuacha civil society
ifanye kazi zake kwa uhuru na bila kuingiliwa na serikali na kupewa vitisho.
8.Kukubali kuwa nchi hii ni ya vyama vingi na siyo lazima tuwe na mawazo sawa na CCM na hata kama tuna mawazo tofauti basi siyo maadui wa CCM au nchi.
9.CCM iache ku-label watu wanaowapinga kuwa siyo wazalendo mara wanatumika na mabeberu etc.
10.CCM ifike mahali ikubali kuwa kuna siasa za ushindani na wanaposhindwa waache kutumia dola na uhuni kubaki madarakani kama walivyofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2020.

Rais kuteua na kuwapa vyeo wapinzani serikalini ni MBINU YA MUDA MFUPI YA KUDHOOFISHA UPINZANI NA NI UOGA KWA RAIS.Ni matumaini yangu kuwa Rais atasoma andiko hili ili ajue kuwa wenye akili tayari tumeshajua kuwa anachotaka kufanya ni danganya toto na wala siyo kusuluhisha matatizo yetu ya kidemokrasia.

Rais anataka kutumia njia za muda mfupi kutatua matatizo ya muda mrefu kitu ambacho ni kujidanganya tu na hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kujidanganya wenyewe kuwa hayapo.



Ushauri wako ni mzuri sana..lakini pia tusiyapinge sana mawazo ya mama...sababu yeye yupo uwanjani sisi ni watazamaji ...yamkini tungekua uwanjani tungemwelewa zaidi.... Kikubwa ni kuwaombea washauri wake waweze kumshauri vizuri...na yeye kukubali kushaurika....pia tusibanwe sana na historia katika utatuzi wa matatizo....yamkini njia zilizotumika Jana kutatua tatizo zilikuwa sahihi kwa Jana na siyo kwa tatizo la Leo... Tumpe ushauri ili tutapate kuyasemea matokeo .
 
Kwanza kuna upinzani au wapiga keleke tu waliyokosa fursa, wapinzani wanaounga mkono juhudi ndio hao uwape vyeo unategemea nini tena hapo?

Kwa masilahi ya wanasiasa hii ni habari njema kabisa na kwa vile wananchi wanapigania masilahi ya wanasiasa kuliko masilahi yao hivyo hili ni jambo jepesi kabisa, hivi nani atapinga atakapoona Mbowe na Lissu wamekula shavu?
 
Mpinzani atatekeleza sera za CCM au za upinzani?
Hii ndiyo hoja ya msingi mpinzani kuteuliwa kwenye serikali ya ccm maana yake haamini katika itikadi na sera za chama chake.

Kifupi ni wapinzani wasaka vyeo tu ndiyo wanaweza kuungana na ccm kwenye serikali yao.
 
Kwanza kuna upinzani au wapiga keleke tu waliyokosa fursa, wapinzani wanaounga mkono juhudi ndio hao uwape vyeo unategemea nini tena hapo?

Kwa masilahi ya wanasiasa hili ni habari njema kabisa na kwa vile wananchi wanapigania masilahi ya wanasiasa kuliko masilahi yao hivyo hili ni jambo jepesi kabisa, hivi nani atapinga atakapoona Mbowe na Lissu wamekula shavu?
Acha dharau watu aina yako ndio msiolitakia mema taifa.
 
Hii ndiyo hoja ya msingi mpinzani kuteuliwa kwenye serikali ya ccm maana yake haamini katika itikadi na sera za chama chake.

Kifupi ni wapinzani wasaka vyeo tu ndiyo wanaweza kuungana na ccm kwenye serikali yao.
Akitekeleza sera za CCM amekisaliti chama chake.

Akitekeleza sera za upinzani ameisaliti mamlaka yake ya uchaguzi.

Wazo zima limejaa contradiction.

Hiki kitu kinawezekana kwenye public service huko ambako siasa zinachukua backseat to public service. Na huko wala hakuna mjadala kuhusu hili anyway, rais alitakiwa kuchagua watu wa vyama vyote bila kujali vyama. Bila hata kuzungumzia vyama, kwa sababu kuzungumzia vyama kwenye public service ni kuchanganya siasa na public service.

Kwa hivyo rais kwa tamko hili pia anaweza kuwa anachanganya siasa na public service.

Uanachama wa CCM si qualification ya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege.

Kwenye vyeo vya siasa ni kizungumkuti.
 
Akitekeleza sera za CCM amekisaliti chama chake.

Akitekeleza sera za uoinzani ameisaliti mamlaka yake ya uchaguzi.

Wazo zima limejaa contradiction.

Hiki kitu kinawezekanankwenye public service huko ambako siasa zinachukua backseat to public service.

Kwenye vyeo vya siasa ni kizungumkuti.
Na nia ya rais ni kutaka kuzima vuguvugu la upinzani la kutaka mabadiliko makubwa ya mfumo wa utawala na kisera nchini.
 
Jana nimemsikia Rais Samia Suluhu Hassan akidai kuwa ataanza kuteua nafasi za uongozi bila ya kuangalia vyama.Hilo halina ukakasi kwa mujibu wa sheria zetu ila kwangu mimi naamini kuwa hizo ni mbinu za kijanja janja za kurudisha utulivu wa kisiasa nchini baada ya ule uchafuzi wa wazi aliofanya mtangulizi wake Magufuli katika Demokrasia yetu.

Rais anatakiwa kuelewa kuwa political certainity haiji kwa kuteuwa wapinzani hasa wenye njaa kuwa serikalini.

Hali ya utulivu kisiasa Tanzania itakuja kwa:

1.Kuwa na chaguzi huru na haki.
2.Kuacha mihimili ya nchi kufanya kazi zake independently bila kuingiliwa wala kutishiwa na mhimili wa serikali.
3.Kuondoa uonevu wa vyombo vya usalama hasa polisi pale watu wanapotaka kufanya siasa ambayo ni haki yao kikatiba.
4.Kuwa na uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza.
5.Dola kuacha kutumika na wanasiasa katika kuwasaidia kuingia madarakani.
6.Kuondoa sheria kandamizi na za hovyo zinazolenga kukandamiza watu.
7.Kuacha civil society
ifanye kazi zake kwa uhuru na bila kuingiliwa na serikali na kupewa vitisho.
8.Kukubali kuwa nchi hii ni ya vyama vingi na siyo lazima tuwe na mawazo sawa na CCM na hata kama tuna mawazo tofauti basi siyo maadui wa CCM au nchi.
9.CCM iache ku-label watu wanaowapinga kuwa siyo wazalendo mara wanatumika na mabeberu etc.
10.CCM ifike mahali ikubali kuwa kuna siasa za ushindani na wanaposhindwa waache kutumia dola na uhuni kubaki madarakani kama walivyofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2020.

Rais kuteua na kuwapa vyeo wapinzani serikalini ni MBINU YA MUDA MFUPI YA KUDHOOFISHA UPINZANI NA NI UOGA KWA RAIS.Ni matumaini yangu kuwa Rais atasoma andiko hili ili ajue kuwa wenye akili tayari tumeshajua kuwa anachotaka kufanya ni danganya toto na wala siyo kusuluhisha matatizo yetu ya kidemokrasia.

Rais anataka kutumia njia za muda mfupi kutatua matatizo ya muda mrefu kitu ambacho ni kujidanganya tu na hatuwezi kutatua matatizo yetu kwa kujidanganya wenyewe kuwa hayapo.



Naona kama umeshindwa kutofautisha kati ya mahitaji wanasiasa na mahitaji ya wananchi.

Tegemea kuwa dissappointed.
 
Acha dharau watu aina yako ndio msiolitakia mema taifa.
Kama kusema kuwa tuna wapinzani wenye kuunga mkono juhudi ni dharau basi ni wao wenyewe ndio wanajidharirisha hivyo nina haki ya kuwadharau, kuna wapinzani wangapi wameunga juhudi na huwasikii tena kukosoa sasa na hawa wengine ukiwapa vyeo unategemea nini tena hapo?

Tukubali tu hatuna upinzani.
 
Bandiko zuri kabisa si lazima wapinzani wapate nyadhifa ndo tusonge mbele,maana mpinzani akiwa sehemu ya serikali ladha ya upinzani inakosekana.Chaguzi zifanyike kwa haki ili tuwe na upinzani Malini kwa maendeleo ya nchi.
 
Back
Top Bottom