Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Hadithi ya kweli ya maisha yangu

Inaendelea

Mwaka 2017 kiukweli ulikua ni mwaka wangu wa kushika hela tena bila kutoa jasho yaan nilikua ni kuingia nakuchukua kama zangu vile...

Nilinunua Godoro na kitanda nikatunza kwa mshikaji wangu mmoja hivi maana home nilihisi watakuja kuni stukia huo mpango wangu.

Jamaa naona alianza kuhisi kuwa kuna kitu hakiko sawa kwenye hela zake..siku moja usiku aliniita chumbani na kuanza kunielezea kuwa kuna vitu vyake vinapotea...roho ilianza kunidunda hofu juu ila sikutaka agundue hilo.

Alisema tu kuna vitu vyake vinapotea na ajui ni nani anachukua ila alikua ana muhisi jamaa ni jiran yetu.kuna siku alifua boksa zake akaanika nje c huyo muhuni akapita nayo alafu alivyo fala akaenda nayo location kupiga picha...sasa jamaa alimuona fb huyo msela kapiga picha kifua wazi ko boksa ikawa inaonekana ( ndo maana alikua anamtuhumu huyo msela kuwa ndo mwizi wake)

Siku hyo nilimsikiliza na ushauri nikatoa wa kinafki dhen nikasepa kulala.Nilimwambia dogo langu asiingie kuiba asubiri kwanza jamaa hofu imuishe..

Huyo Mtoto wa mwenye nyumba licha ya kuwa mkubwa kwetu ( Ana miaka 40+ ) ila jamaa ni muoga hatare yan hata panya alikua hawez kuua..afu kingine licha ya kuwa na pisi kali kali lakin alikua ana matatizo ya nguvu za kiume maansa kuna siku aliniomba ushaur atumie madawa gani, nikamuuzia yale madawa niliyokua nauza kule kisiwa ( kuna mengine nilimuibia dokta home kwake ).

Ko jamaa alikua ananikubali sana ila alikua anadharau sana..alitudharau sana kwasababu mzee alikua halipi kodi kwa wakati basi ataenda kuwaambia sisi ni nothing pale kwao.hicho kitu kiliniuma sana.sasa ndo nikaamua nimuibie kisawa sawa ili kumkomoa...lakin nilikuta zile hela za kwenye kapu hazipo kaziamisha.

Nilitafuta sana ni wapi alipozitunza lkn siku fanikiwa kuzipata..Mdogo wangu cjui alikua na madawa gani aisee siku aliinita na kunionesha kimfuko hivi kilikua chini ya sofa lake huyo jamaa.

Huo mfuko ulikua na hela nyingi ckujua ni shngap...nilitaka kuzibeba zote sema dogo alinizuia nikachukua 400k nikasepa zangu.kesho nilirud nikakuta hazipo hela cjui alizificha nilitafuta kila kona ckupata...nikaona ili nichukue tu Baritika zero kwenye fridge yake nikaonge demu.

Huyo manzi angu ( Yule wa mwanzoni tumuite Lizy maana alikua ana nguo yake imeandikwa Lizzy ndo me nilikua hivyo ) Manzi ilifaidi sana hela za wizi japokuwa hakuwa mwaminifu kwangu.

Kuna kipindi nilikua chumban humo nakosa hela kabisa yaan nilikua naambulia 5k mpk buku....nilikasirikia balaa nikawa najiuliza jamaa anatunza wap hela zake ama anaweka benki..Siku moja ilikua jumamosi sikwenda kanisani nilikuepo home tu nachek movie.Siku hyo jamaa nae hakwenda kazini maana alikua ni zamu yake Jumuia kufanyikia hapo kwao.ko waumini wa kanisani kwao walikuja wakafanya ibada pmj pale kwao.

Me nilikua nawachora tu dirishani jinsi wanavyo abudu..niliona wanatoa SADAKA kwenye kisonzo alafu wakamkabidhi yule jamaa walivyoondoka nilimuona jamaa amezibeba akaingia nazo chumbani..nilikua namchora nikajisemea tu Mungu anisamehe kwa tabia hyo.

Nili subiria jamaa akaondoka cjui alienda hyk ikawa nafasi yangu niliingia chumban kwake kasi ya ajabu mpk kwenye hilo li briefcase lake..nilifungua nikazikuta zile sadaka mule..Nilizichukua zote nikaacha tu kile kisonzo na kaunta book.

Kipindi hicho sina roho ya huruma kabisa tena nilikua nikiingia kwake nabeba kisu kabisa ili nikishikwa tu nijitete na kisu.Jamaa siku alinihisi kabisa kuwa mimi ndo mwizi.

Jamaa wasiwasi wake wa kupotelewa na hela vilimfanya akaamin kuwa kuna chuma ulete kwake.Siku moja alirudi na kajamaa flani hivi kalikua kamebeba begi...akaingia nae chumbani kwake, Mara jamaa akatoka na kutuita me na wadogo zangu.

Kumbe kale kajamaa kalikua ni kaganga kalituita akatwambia yukae chini tumsikilize aliyo tuitia

*Nitarudi tena *
 
nilifurahi sana kusikia hivo mpk nikawa natetemeka kwa furaha )

Daah nimechekaaaa hatari, nimetengeneza kaclip kichwani, namuona, Yule mbilikimo wa aki Na ukwa,
 
Inaendelea...

Tulifika sehemu moja inaitwa Biyswa ( cjui kama nimeliandika vizuri ) kulikua na kivuko hapo cha kwenda Ukara ( wataalamu mtanisaidia kidogo jina lingine la Biyswa maana nimesahau )....Kwa vile ilikua ni Jumamosi tuliamua kupumzika kwenye guest moja hivi maarufu ( Green Parachichi ).Siku hyo tulikuta guest nyingi zimejaa na hata hapo green parachichi tulibahatisha tu chumba kimoja.Kulikua na mkutano wa kidini wa Waroma sasa ndo walichukua karbia guest zote.

Chumba tulipata kimoja tu ko ikatubidi tulale wote wa tatu hakukua na namna.Dokta alituaga kuwa kuna sehemu anaenda kumchek ndugu yake ko alitwambia akichelewa kurud tule ibada tumsubirie yeye tufanye kwa pamoja.

Rafiki angu alinitaka tukatembee kuona mazingira ya Ukerewe na kweli nilimsindikiza akaona sehemu wanauza simu akanunua kasimu ka batani ( maana yake ilitumbukia ziwani tukiwa kwenye bot ).

Wakati tunarudi madansa fulani hivi walikua wanatoa show njian.tulivutiwa na yale mauno ya wale plus kumwaga radhi mpk kuna kijana mmoja alituita akatuuliza " mnataka yupi hapo " tulikataa tukasema sio type zetu hao, tulielekea guest kupumzika kusubiria msosi wa jioni.baada ya msosi wa jion yule dokta alikua ameshakuja tukapiga ibada fresh tukalala tumebanana hivyo hivyo kibishi.

Siku iliyofuata asubui na mapema tukawai kupanda feli kuelekea Ukara tulipanda feli ile ya Mv Nyerere ( Iliyozama 2018 ).safar ilikua ni ya saa mbili mpk kufika ukara visiwa vya huko nimevisahau kiukweli maana vina majina magumu.

Kama kawaida tuliingia mzigoni kuuza madawa na kama kawaida yangu nilikua nawauzia watu madawa tofauti, rafiki angu nae alikua anawapa tofaut maana nilimwambia awe mjanja.

Wale wanaotaka dawa ya kuacha pombe me nilkua na wapa dawa yoyote isipokua ile ya uzazi.

Kuna sehemu moja nilipita nikakuta wavuvi wanacheza draft kuna mzee mmoja alinitoa pembeni akanieleza shida yake kuwa Mashine yake haisimami na mimi nilikua nimemaliza dawa ile ya Nguvu ya kiume ( Nguvu Men ndo ilikua inaitwa )..nilimtext rafiki angu kuwa aniletee hyo dawa kama anayo akasema anazo tatu na zina watu wake.

Niliona isiwe kesi nikampa dawa ya kutibu kichocho eti ndo ya Nguvu za kiume ( ila mimi jamani ) mzee nilimpa maelezo jinsi ya kuitumia asubui kabla hajala kitu chochote na jion wakat wa kulala, alinishukuru sana akanipa 10k nilisema tu " sorry kapone kichocho mzee wangu " ila moyoni nilikua najutia kidogo baadae nasahau.

Tulirudi Biyswa kesho yake na kulekea sehemu moja inaitwa chibasi ( sijui ipo ukara au byswa maana nimesahau kiukweli mtanikumbusha kwa wanao pajua )

Tulifika hapo na kuanza kuuza madawa kwa wavuvi kama kawaida.Hyo sehemu watu hata hawaoneani aibu yaani wanaume na wanawake waoga karibu karibu uchi wa mnyama na hakuna anaemjali mwenzie.nilikua nadindisha balaa nilipokua nikiwaona wamama nyuchi zao ila nilijikaza.

Kuna mdada mmoja aliniita niende sehemu aliyokua amekaa, kiukweli alikua ni mrembo sana mweupe umbo lenye neema, nilimtamani sana huyo mrembo ingawa alikua ni mkubwa kwangu ila nilisema na mmudu.Alivyonielezea tatizo lake hata kumtaman kukaisha.Alikua na tatizo la bawasili ( najua sio vizur kueleza privacy za mtu lakin mnisamehe ).Nilishindwa hata namsaidia vipi maana dawa ya hilo tatizo lake sikutaka nimtapeli maana huruma ilinishika sana kwa jinsi alivyokua anaelezea hilo tatizo lake.Nilimshaur tu vizur aende hospital.

Niliachana nae njiani nikakutana mzee mmoja yeye alivunga ni msomi sana maana alini challenge sana.

Alitaka ni mtajie aina tatu za Enia ( Ngiri ) kijasho kilinitoka joto likapanda maana niliona naaibika ( nilikua najitambulisha kuwa mimi ni dokta kutoka musoma ).ila me mjanja nilimbadilishia mada kijanja bahat nzur alijaa na uzur alikua na shida ya ngiri kweli niliona ili iwefundisho kwake na kwa wengine nilimpa dawa ya vidonda vya tumbo badala ya ngiri ( ujuaji wake ulimponza ) tena alinipa 45k nikala kona kubwa.

Visiwa tulivyoenda ni vingi sana mpk vingine nimevisahau.

Ila hii trip ya kwenda kisiwa cha Siza,ghana na izinga nakumbukumbu navyo sana.

Tulienda hivyo visiwa kupitia sehem moja hivi inaitwa Kakukuru ( cjui kama nimetamka vyema ) tulipanda bot hapo kakukuru.Bot zilikua ni kubwa tena za injini tatu mpk mbili.Bot tuliyopanda ilikua ni kubwa na ilikua na mizigo mingi na abiria wengi lakin bot ilkua tv ko movie na muziki kama kawaida.

Me binafsi sikua na mawazo ya kuangalia tv nilikua nawaza tu kama tutafika salama ( kulikua na mawimbi makali cku hyo ).

Mungu alitusaidia tukafika salama Siza tukaenda kutafuta guest kama kawaida.


Nitarejea tena kumalizia Safar yangu ndan ya kisiwa
Nimecheka sana, maana wenyewe wanataka dawa we huna, unapiga sounds unauza zilizopo hapo nakupa kongolee.
Kuna kipindi jamaa niko kitengoni wamepiga sana nyagi badala ya Gordon gin,Valeur badala ya Remy Martin na mnaenda sawa tu.🤣🤗🤣
Kuna maskini mkenya ndo alituumbua, akaja na mchupa wa Gordons kaagiza kwetu tukampa za uso nyagi akapiga makelele tukamtoa kwenye game akafie mbele
 
Nimecheka sana, maana wenyewe wanataka dawa we huna, unapiga sounds unauza zilizopo hapo nakupa kongolee.
Kuna kipindi jamaa niko kitengoni wamepiga sana nyagi badala ya Gordon gin,Valeur badala ya Remy Martin na mnaenda sawa tu.🤣🤗🤣
Kuna maskini mkenya ndo alituumbua, akaja na mchupa wa Gordons kaagiza kwetu tukampa za uso nyagi akapiga makelele tukamtoa kwenye game akafie mbele
Alielewa hapa anieleweshe
 
Duuh hayo maisha kwingine ilikua miaka ya 80 na 90 enzi hizo disco lazima zipigwe au mechi ikiisha fujo mji mzima mnajifungia. Hii tulifanyaga pia shuleni kantalamba miaka ya 90 watu tuliamka alfajiri sa 11 tukaenda kupiga mawe mabasi ya sumry yanayoenda mbeya kisa yalibeba team pinzani kuwaleta uwanjani ikatufunga
Kantalamba sumbawanga hahah

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Mimi ni mgeni huku musoma lakini story yako imegusa maeneo mengi sana ambayo nimeshafika pengine sijafika.
Mimi ni msabato nilivyofika hatua ya kwanza nikatafuta kanisa lilipo karibu yangu nikapapata hapa kariakoo (nyarusuliya)...

Kwa mda mfupi niliokaa huku musoma (i'm temporary teacher hapa musoma kuna shule hapa)
Nimegundua vitu vingi sana......

Madogo wengi wa huku wana dhana kwamba kuleta ukorofi au kua mkorofi ndio unaonekana kidume, yaani mtu huko na mishe zako huna hili wala lile anakuchokoza ujae then akawaite wenzake wakupige (ushamba mkubwaa )...

Huku hata kama mpira unachezwa saa 3 usiku, ukumbi mzima unakuta wana silaha za jadi, mapanga, mikuki, sime n.k wanasema ni za kujilinda duh..

Huku bado kuna miziki ya usiku haswa kwenye sherehe au harusi (hata Leo usiku kuna mziki hupo huko bweri, naona majirani zangu hawa wamezoea kuniita teacher wananoa visu na mafyekeo, wanasema wanajihami na watoto wa mbwa ).....

Nafundisha physics na mathematics (sipendagi dharau maana wanafunzi wa huku ni wakubwa kuliko mimi so sometimes wanadhani wanaweza fanya chochote tu, nachoshukuru waaosoma hayo masomo ni wachache na wanaojielewa )....

Musoma kuna joto sana kipindi hichi fursa huku ni adimu sana, watu wa huku wamejaliwa maneno ni wajuaji haswa pia usisahau kuna wachawi kinoma..

Ukiwa muhuni sana wa kuogopa basi ukitaka binti unavuta tu huku umemtishia panga..

Hii ndio musoma vijana wengi tabia za kindezi kwao ndio ujanja.
Huu ndo ukweli kuhusu Musoma niliishi huko kwa zaidi ya miaka 6 lakin sina ninacho kimiss hata kimoja ambacho kinanifanya nitamani kurudi kuishi huko, mwaka juzi nilikuja huko kusalimia baadh ya jamaa zangu ilikua nimepanga nikae siku mbili lakin nilikaa siku 1 tu nikasepa maana sipakubali tu **** ushamba ni mwng mno huko baadh ya marafik zangu wa miaka hiyo tukiwa bado wadogo, walikua na tabia ya kupora icecream za wanafunzi shulen na kukimbia nazo lakin sahiv ni waizi kamili na wamekaa gerezan sana tu kila mwaka anachezea miez 6 ndan miez 6 nje

Kwakweli huko ukiwa na familia yako inatakiwa uiweke chin ya uangalizi mkubwa laa sivyo wanaweza kuiga tabia za baadhi ya vijana wengi wa huko ambao wanaamini kuwa na makundi ya kihuni ndo ujanja
 
Inaendelea


Kama nilivyosema siku hyo huyo jamaa alikuja na huyo mtu ajiiatae Mganga..Tuliitwa mimi na wadogo zangu wawili pamoja na Jamaa mmoja muhuni muhuni nae walimuhisi ni mwizi.

Basi tuliingia chumbani kwa huyo jamaa tukakuta Mganga kashaanda mambo yake tayar kwa kazi iliyomleta.

Nahisi ilikua ni mind game ya huyo jamaa na huyo Mganga wake.niliuliza kuna nini kwani jama ndo akaanza kutiririka kwann tumeitwa pale me nilikataa sihusikii na wizi pamoja na wenzangu pia walikataa kata.nilikua na mwangalia dogo kama ana wasi wasi lakni alikua mweupe hata wasiwasi hana.

Baafmda ya kila mtu kukana kuwa hausiki na wizi Mganga alimuomba ruhusa huyo jamaa aanze uganguzi wake..🤣🤣🤣😂😂 ila kuna watu wana visa dunia hii acha mganga awashe kamshumaa kekundu na aliletewa sufuria la maji akawekapo vidawa fulan,na kidude fulan hivi kama sabuni pamoja na sindano rungu.niliwaza kuwa naumbuka siku ile ila nikakaza nilisema hata kama nashikwa ni fresh tu kwanza uzur sina urithi kwa Mzee sio mbaya nikikamatwa ( nilikumbuka ile kauli ya mzee wangu hapo nyuma ).

Mganga alisema tu " kama kuna mtu anajua kabisa hausiki na wizi achome hicho kipande na anawe mikono kwenye sufuria alafu aondoke "...niliogopa kiasi chake ila sikutaka nionekane kama na hofu...unajua kipindi cha nyuma bado nasoma kuna jamaa nilimuibia dictionary class alinihisi me ndo nimemuibia ko aliamua kunipiga mikwara mizito ya kijini jini ila ndo sikuogopa ( kisa chake nilisahau kukielezea )sasa hyo mganga nilimuona ni kama tu yule jamaa wa dictionary.

Alianza mdogo wangu ( sio mwizi ) kuchoma kile kidude kwa sindano Rungu aka fuata yule muhuni kisha dogo alafu me kidume ndo nikamalizia..wakati naondoka nilimwambia yule Jamaa kama nisipokuwa kitu utanilipa fidia ( nilikua nimemkazia sura utadhani me sio mwizi )

Usiku wake siku lala vizur kiukweli nilkua nasubiri tu matokeo ya ile dawa ya mganga ( tapeli tu ) nilikua najishika viungo vyangu nione kama kuna mabadiliko yoyote lakin sikuona, usingi cjui ulinipitia sangap

Asubui yake niliamka nikawai chumban kwa madogo nione kawaje na yeye lakin sikumkuta dogo niliogopa kuangalia chooni na bafuni hayupo nikawa najiuliza kaenda wapi tena?...kumbe dogo alikua anamlia target yule jamaa asepe ampige tukio ( mdogo wangu kunakipindi niliamini karogwa )....siku hyo ilipita fresh tu tuko vizur na siku iliyofuata pia nikasema kumbe jamaa wamempiga hela za bure na Mganga wake.

Dogo langu alikua anaiba mpk to much aisee...sio tu kwa huyo msela mpk kwa baadhi ya majirani alikua anawacheza...nilimkanya kama Kaka aache kupiga matukio kwa watu mwishoe azoee sikupenda kwa kweli dogo apite njia zangu..

Bahat nzur aliacha kuiba kwa majirani ila akawa anampiga tu huyo jamaa...


Me kipindi hicho mapenzi yangu na Lizzy yameshika kasi kinoma kumuhudimia kama kote..ila Mapenzi ni mapenzi tu Lizy alianza kuniletea mambo ya kifala sana alikua anani cheat me najua lakin namkaushia tu maana bado nilikua sina demu mwingine ( yule Ney alikua kashasepa Musoma ko lizy ndo aminio langu alafu ndo alikua Moyoni mwangu ko sikutaka kumuacha ghalfa nilikua namtafutia mbadala wake 😉😂😂 )

Kuna siku moja Huyo Lizy aliniomba 10k ya chips nikamwambia sina alinuna akidai simjali..alafu alikua ananituhumu kuwa natembea na demu mmoja hivi mwimba kwaya ko alianza kuleta visa vya kifala...siku hyo alinuna balaa hata akutaka tuonane siku hyo jioni ( ilikua ni kawaida yetu kuonana jioni )..basi kesho yake jioni baada ya kutoka kwenye mahubiri niliamua kumpelekea 10k yake alio niomba..nilienda mitaa yao majita road ilikua saa moja hivi..nikamtuma mdogo wake aniite na kweli akaja amenuna sio kidogo..nilongea nae nikawa naona hayuko interested na mimi nikamwambia anisindikize basi akakubali...tulipita kiuchochoro flani kili hakina watu sana basi nikamtolea noti ya 10k..acha demu anirukie na kuanza kuninyonya mate 😂😂😂 me nae nikayapokea na kunyonya yake pia 😘😘.

Alianza kujibebisha sasa na kutaka nimnunulie Sendo nilimwambia nitampa hela lakin alikataa akidai nimnunulie..kidume ilibid nikubali na kwa vile hela ilikuepo ya wizi sikuona uchungu kupotea...kesho nilienda town nikamchukulia sendo nzur tu za wadada kumpelekea jioni akizipima na kuzivua na kunitupia..akaanza kulalamika kuwa ina maana me cjui size ya miguu yake yani size za mademu wengine najua ila size yake sijui...nilikua kimya tu niaviokota na kurudi home nikampa dogo langu ( wa kike ) kesho yake nikarudi town tena kuchukua sendo nyingine siku hyo alifurahi akanipa mate nikala kona kwenda home...nacho mkubali huyu demu alikua anibanii nikimuomba show alikua yupo free sana.....

Nitarudi tena.
 
Back
Top Bottom