Inaendelea...
Tulifika sehemu moja inaitwa Biyswa ( cjui kama nimeliandika vizuri ) kulikua na kivuko hapo cha kwenda Ukara ( wataalamu mtanisaidia kidogo jina lingine la Biyswa maana nimesahau )....Kwa vile ilikua ni Jumamosi tuliamua kupumzika kwenye guest moja hivi maarufu ( Green Parachichi ).Siku hyo tulikuta guest nyingi zimejaa na hata hapo green parachichi tulibahatisha tu chumba kimoja.Kulikua na mkutano wa kidini wa Waroma sasa ndo walichukua karbia guest zote.
Chumba tulipata kimoja tu ko ikatubidi tulale wote wa tatu hakukua na namna.Dokta alituaga kuwa kuna sehemu anaenda kumchek ndugu yake ko alitwambia akichelewa kurud tule ibada tumsubirie yeye tufanye kwa pamoja.
Rafiki angu alinitaka tukatembee kuona mazingira ya Ukerewe na kweli nilimsindikiza akaona sehemu wanauza simu akanunua kasimu ka batani ( maana yake ilitumbukia ziwani tukiwa kwenye bot ).
Wakati tunarudi madansa fulani hivi walikua wanatoa show njian.tulivutiwa na yale mauno ya wale plus kumwaga radhi mpk kuna kijana mmoja alituita akatuuliza " mnataka yupi hapo " tulikataa tukasema sio type zetu hao, tulielekea guest kupumzika kusubiria msosi wa jioni.baada ya msosi wa jion yule dokta alikua ameshakuja tukapiga ibada fresh tukalala tumebanana hivyo hivyo kibishi.
Siku iliyofuata asubui na mapema tukawai kupanda feli kuelekea
Ukara tulipanda feli ile ya Mv Nyerere ( Iliyozama 2018 ).safar ilikua ni ya saa mbili mpk kufika
ukara visiwa vya huko nimevisahau kiukweli maana vina majina magumu.
Kama kawaida tuliingia mzigoni kuuza madawa na kama kawaida yangu nilikua nawauzia watu madawa tofauti, rafiki angu nae alikua anawapa tofaut maana nilimwambia awe mjanja.
Wale wanaotaka dawa ya kuacha pombe me nilkua na wapa dawa yoyote isipokua ile ya uzazi.
Kuna sehemu moja nilipita nikakuta wavuvi wanacheza draft kuna mzee mmoja alinitoa pembeni akanieleza shida yake kuwa Mashine yake haisimami na mimi nilikua nimemaliza dawa ile ya Nguvu ya kiume ( Nguvu Men ndo ilikua inaitwa )..nilimtext rafiki angu kuwa aniletee hyo dawa kama anayo akasema anazo tatu na zina watu wake.
Niliona isiwe kesi nikampa dawa ya kutibu kichocho eti ndo ya Nguvu za kiume ( ila mimi jamani



) mzee nilimpa maelezo jinsi ya kuitumia asubui kabla hajala kitu chochote na jion wakat wa kulala, alinishukuru sana akanipa 10k nilisema tu " sorry kapone kichocho mzee wangu " ila moyoni nilikua najutia kidogo baadae nasahau.
Tulirudi Biyswa kesho yake na kulekea sehemu moja inaitwa chibasi ( sijui ipo ukara au byswa maana nimesahau kiukweli mtanikumbusha kwa wanao pajua )
Tulifika hapo na kuanza kuuza madawa kwa wavuvi kama kawaida.Hyo sehemu watu hata hawaoneani aibu yaani wanaume na wanawake waoga karibu karibu uchi wa mnyama na hakuna anaemjali mwenzie.nilikua nadindisha balaa nilipokua nikiwaona wamama nyuchi zao ila nilijikaza.
Kuna mdada mmoja aliniita niende sehemu aliyokua amekaa, kiukweli alikua ni mrembo sana mweupe umbo lenye neema, nilimtamani sana huyo mrembo ingawa alikua ni mkubwa kwangu ila nilisema na mmudu.Alivyonielezea tatizo lake hata kumtaman kukaisha.Alikua na tatizo la bawasili ( najua sio vizur kueleza privacy za mtu lakin mnisamehe ).Nilishindwa hata namsaidia vipi maana dawa ya hilo tatizo lake sikutaka nimtapeli maana huruma ilinishika sana kwa jinsi alivyokua anaelezea hilo tatizo lake.Nilimshaur tu vizur aende hospital.
Niliachana nae njiani nikakutana mzee mmoja yeye alivunga ni msomi sana maana alini challenge sana.
Alitaka ni mtajie aina tatu za Enia ( Ngiri ) kijasho kilinitoka joto likapanda maana niliona naaibika ( nilikua najitambulisha kuwa mimi ni dokta kutoka musoma ).ila me mjanja nilimbadilishia mada kijanja bahat nzur alijaa na uzur alikua na shida ya ngiri kweli niliona ili iwefundisho kwake na kwa wengine nilimpa dawa ya vidonda vya tumbo badala ya ngiri ( ujuaji wake ulimponza ) tena alinipa 45k nikala kona kubwa.
Visiwa tulivyoenda ni vingi sana mpk vingine nimevisahau.
Ila hii trip ya kwenda kisiwa cha Siza,ghana na izinga nakumbukumbu navyo sana.
Tulienda hivyo visiwa kupitia sehem moja hivi inaitwa Kakukuru ( cjui kama nimetamka vyema ) tulipanda bot hapo kakukuru.Bot zilikua ni kubwa tena za injini tatu mpk mbili.Bot tuliyopanda ilikua ni kubwa na ilikua na mizigo mingi na abiria wengi lakin bot ilkua tv ko movie na muziki kama kawaida.
Me binafsi sikua na mawazo ya kuangalia tv nilikua nawaza tu kama tutafika salama ( kulikua na mawimbi makali cku hyo ).
Mungu alitusaidia tukafika salama
Siza tukaenda kutafuta guest kama kawaida.
Nitarejea tena kumalizia Safar yangu ndan ya kisiwa