Mniwie radhi ndugu zangu kwa kuchelewa kuweka najua nawakata stimu lakin wikendi ndo nipo free sana.
Tuendelee......
Mwaka 2013 ckufanya matukio ya kuteka na kupora nilipumzika, niliwaza sana kuhusu maisha ninayoishi nikajisemea " niwe serious na kitabu " kumbe ndo nilijikosea kuwaza maana niliingia kwenye mahaba mazito na Jirani yangu ( Sugar mumy ) hii nilishaiongelea kwenye thread iliyopita ko tuiache kwanza.
Kimasomo nilkua chini sana plus skendo zangu kumfikia Mama kisha Mama kumwambia mzee.Mzee aliongea mambo magumu sana kwangu alinambia Live kuwa hajaniweka kwenye urithi wake mbele ya Mama angu na kudai me sio Mwanae ko nimalize tu form 4 then niondoke kwake.Binafsi siku yajali maneno yake.Kwenye akili yangu alikuwepo huyo sugar mumy wangu.
Maisha yaliendelea nikamaliza shule vizr nikabaki kusubir matokeo kama yatafanya nifukuzwe home ama nibaki.Kuna siku lilitokea tukio moja kubwa sana home yaani mpk sikuiz nikilikumbuka huwa cjiksikii poa kabisa.
Ni mgogoro wa kifamilia kati ya Mzee na Mama.Mzee wangu ni mzee wa totozi alikua anazila sana lakin sasa wivu kwa mke wake ndo usiseme.Nakumbuka tu siku ambayo ilkua ni jumapili usiku nisingekuwa pengine mimi Mama angu alikua anauwawa tena kikatili sana.
Siku tulikua mezani tunakula Mimi, wadogo wa tatu na Mama ghafla Akaja Mzee yupo tungi ila sio sana alijumuika na sisi kula vizur tu huku asemi chochote.Ghafla kwenye simu ya Mama text ikaingia simu ilikua kwenye meza ya tv ko Mama kama aliipuuza hyo text Mzee akainuka kwenda kuisoma naona akanawa akaenda chumbani mwake kisha akarudi na Nguo, alinambia " ukimaliza kula uninyooshe nguo " nikasema sawa baada ya kumaliza kula Mama nae alielekea Chumbani me nikabaki sebuleni na madogo wakati huo nanyoosha nguo za mzee.
Mara chumbani kukaanza kusikika makelele ya watu kugombezana.Mara Mother akaja sebuleni huku analia alitwambia tu anaondoka amechoka na vituko vya mzee kisha akarudi chumbani kukusanya nguo asepe zake ( wakati huo ni saa 4 inaelekea saa 5 usiku ).Mzee naye alitoka chumbani akaenda nje kisha akarudi ndani jikon kulikua na Panga nyuma ya mlango wa jikoni ( hilo panga me ndo nililitunza hapo siku za nyuma kidogo ) akaenda nalo chumbani aka lock mlango.
Hazikupita hata dakika tano tukaanza kusikia kelele za Mama akilia kuomba msaada kua anakufa.Bro wangu ( mtoto wa bamkubwa) na Yule jamaa ( mtoto wa mwenye nyumba ) waliamka kujua nini kinaendelea lakin hawakua na msaada wowote maana mlango ulilokiwa na mzee.Wakati huo mdogo wangu wa mwisho wa kike analia kweli.Wazo likaja kichwani mwangu kuwa kunafunguo za akiba hua zinakaa kwenye kabati sebuleni.Basi nikawai kuzichukua nikamletea huyo jamaa ( mtoto mwenye nyumba ) akakataa kufungua akidai hayo ni matatizo ya ndoa haweez kuingilia.
Niliamua kufungua me mwenyewe nilimkuta mama yupo chini mzee yupo juu yake.Mama akijaribu kujiokoa maana mzee alikua amemkabia chini mkono wake mmoja umenyanyua panga juu sema mama nae amelishika hilo panga kwenye makali akijaribu kulizuia.Nilichukua kiatu cha mzee kilikua pembeni nikampiga nacho mzee kichwani lakin hakumwachia Mama, nikaona iliamuachie ni mpige roba.Na kweli nilimpiga Roba moja matata yaani niliona anamuachia Mama na panga akaliangusha, akawa sasa anajiiokoa yeye ( najua kumpiga mzazi ni laana lakini sikuwa na jinsi siku hyo ) akili kichwani kwangu iliruka kidogo nilimpiga roba hadi nikawa naona mtu kama analegea, nikaona nitaua bure nikamuacha amelala sakafun nikakimbia nje wakati huo Mama alikua ameshachukuliwa na Bro wangu pmj na yule jamaa wakaenda kumficha nje.Nilkuta Mama kazimia nikajua amekufa wasiwasi ulikua mkubwa ikabidi nirud ndan kwa mzee nilikutana nae njian nikamwambia umeua huku, niliona amepata hofu akanambia yupo wap nikamuelekeza akamchukua mpk hospital ya Mkoa wa Mara.
Hospital walitaka pf 3 ko ikabid twende police ila cha ajabu mzee alisema Mama alivamiwa na vibaka wakat huo nikimuona mama alivyomjeruhi natamani tu tuzipige ngumi ila Wakat huo huo bado na mpenda Mzee pia.
Najua sio vizuri kusimulia mambo ya familia lakin hili nimeona niliandike humu kwenu ili muone ni jinsi gani nilikua naipenda familia yangu.Maana hata police sikusema kuwa Mzee ndo mwenye kosa nilimlinda hadi alishangaa.Mgogoro wao ulitulizwa na Bibi angu kizaa Baba maisha yakaendelea.
Tutaendelea tena kesho