Inaendelea
Maisha yalikua yanasonga tu hivyo hivyo kibishi...Nadhani jamaa aliona hela zake zinazid kupotea akaamua kutokutunza humo ndan mwake..ilo lilikuwa pigo kwetu na hela nilivyokua nazitumia vbya hata ningejua niwekeze tu kwenye biashara.
Ka hali kakanza kuwa kagumu demu nae akawa anataka hela basi ikawa ni mwendo wa kusema uongo ili nihurumie.kuna siku nilimwambia demu kuwa saiv mishe zangu haziko poa ko hela ni ngumu kidogo alinuna wiki nzima anitafuti na mimi simtafuti ( nilianza kumuona ni kero kwenye maisha yangu )...mpk siku moja ndo akanitext kunipa hi na blah blah nyingi tu kuwa eti me ndo mwanaume wake wa moyoni wengine ni wa kupita
Wivu ulinipata kusikia hvyo kuwa siko mwenyew ila me ndo napendwa..nilisema haiwezekani lazima nimkomoe huyo Manz ili tukiachana nisiwe na majuto..nilikuwa nawaza nitamkomoaje huyo demu..niliona njia bora ni kumrekod wakti namgonga ili akija kunizingua na expose video mtandaoni..kuna siku alikuja ni mgonge sikumrekod nilishindwa kabisa kufanya hivyo sijui kwa sababu nilikua Nampenda sana.
Kuna siku moja nilikua church ( siku hyo tulisali kimtaa ) basi bna me kwa vile ni muimba kwaya ilinibid nikae sehemu ya waimbaji kwa ajili ya kutoa huduma kwa washiriki ya nyimbo...siku hyo Lizzy alikua amependeza na kigauni chake ambacho nilimnunulia kidume mie...basi tulikua tuna chat akanitaka niende sehem alipo kuwa amekaa tukae wote ( alikua amekaa nyuma kabisa ) siku shindwa kukataa mbele yake..ko nilimdanganya teacher kuwa naenda chooni..teacher alinitaka niwai maana kwaya yetu ndo tulikua tunaimba huduma kuu..basi nilienda sehemu alipo manz angu tukakaa stor za hapa na pale...basi tuliita kuimba nikawai kuimba tulivyo maliza nikarud kukaa na manzi yangu.
Manzi ilikua iko fb ila sasa ilikua imesahau password yake..aliniomba nimsaidie..nilimshauri afungue account mpya tu aanze moja na kweli alikubali nikamfungulia mpya.
Usiku wake nikiwa home nimelala niliamua kuingia kwenye hyo account yake ya fb mpya..aisee Ila Wanawake wanapata wakati mgumu sana mitandaoni kutongozwa kama kote...niliingia nilikutana na text nyingi tu za wanaume just imagine mpk Mzee wangu alikua amemtumia text "
hi mrembo " nilimchuna maana nilijua ndo zake hizo...ukiachana na text nyingine za kuomba namba,hello mrembo,cjui unaishi wapi mrembo na nyingine nyingi kuna text iliingia ilinistua sana.
Ilikua ni ya jamaa mmoja hivi tunasali ila yeye alikua ni mwanachuo ( udom ) alikua likizo..text ilikua inasema hivi " we lizy wewe mbn siku unanikwepa au vivulana vyako hvyo vinakudanganya "...niliamua kuwa lizy cku hyo niliamua kuchat nae nikijifanya mimi ndo lizy sasa.
Jamaa alitiririka mengi sana nilikua namuuliza maswali ya kumtega nae anatiririka tu bila kujua anae chat nae..nikimuuliza kama alisha sex nae kiujanja sana..alisema hivi " niwie radh bby siku ile ulivyokuja tukasex c unajua ckua nimejiandaa vizur ndo maana nilishindwa kukuridhisha kipenzi" ( hizi chatting mok leo bado zipo kwenye account ya lizzy )...nilijisikia vbya hasira na wivu vikaambatana yaani manzi yangu inaliwa na hilo lijamaa nilisema sikubali aisee.tuliendelea kuchatt nikaamua nimuombe hela huyo msela wa manz yangu....nilimuomba 50k akasema hana hapo alipo labda kesho yake, nikamwambia potezea tu.Aliniomba no ya simu ya M-PESA nikampa yangu, cjakaa sawa ikaingia text ya imethibitishwa umepokea 55k kutia kwa huyo fala...asubui ilifika nikawai kwa wakala na kweli nikatoa 50k huku nikisema ngoja nijipooze na hicho ki hela.
Ila nilisema nitakulaje hela ya mwanaume mwenzangu...wakat na waza hayo text iliingia ya bro wangu ( yule mtoto wa bamkubwa tulie kuwa tunaiba nae ) akitaka nimpelekee kadeti town anipe hela.
Hizo Kadeti zilikua za huyo hyo mtoto wa mwenye nyumba..tulivyoona hela kahamisha tukaamua tuchukue nguo tuwe tunauza nyingine nazimodoa navaa tena ananiona nimevaa.Nitaelelezea baadae ngoja niendele na huyu manzi kwanza.
Kweli nichukua Kadeti ( zilikua suruali mbili ) nikachukua na zile 50k za yule fala nikaingia town.Nilifika kazin kwa huyo bro akaona mzingo kisha akanipa 20k na kunitaka nimtafutie mzigo mwingine.
Niliamua niende dukani nikamnunuliee nguo Manzi yangu kwa ile ile hela ya huyo fala wake...nilinunua kigauni cha 35k chenj iliyobaki nilimpelekea huyo manz angu pamoja na hilo gauni.demu alifurah akijua kuwa nimempa zawadi kumbe alkua hajui ni pesa ya boy wake ndio imefanya hayo mambo.
Kesho ilifika siku nilikua natoka tizi la kukimbia kwa ajili ya kutafuta pumzi ya kuimba.nilifija kuchukua simu nakuta text ya huyo boy wa manzi angu ilikua inasema hivi

"
yaani wewe Holly holm ndo wakunifanyia hivi aisee rudisha hyo hela au umpe muhusika yaani Church minister mzima unakua tapeli" nilimjibu tu kawaida kuwa hela simpi ng'o na cha kunifanya hana.
Jamaa kumbe ile no niliyompa kutuma ile hela ilikua whatsapp na picha yangu juu kumbe alisave na kuniona mimi badalaya ya demu wake.Alinitishia kuwa atanifanyia kitu kibaya me nilimwambua nakisubiri hicho kitu.Wakat huo hata manz ajui hyo inshu sikuona ni vyema kumwambia.
Nitarud nielezee jinsi nilivyo mfanya huyo boy wa manzi angu....
kikoozi