Sangomwile
JF-Expert Member
- Aug 17, 2012
- 3,227
- 1,104
Mkuu watupie watu utamu,kwenye gazeti imeshatoka tangu juzi.
Raha ya utamu uchelewe kuupata kma hivi yan kma unautoa vile alaf unaubania...yan burudan... safi sana mzizimkavu...
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-33
ILIPOISHIA:
Baada ya kusubiri kwa muda waliona watu wakitoka makaburini, walijawa na hamu ya kutaka kujua nini kimejiri huko.
Alibahatika kumpata mmoja wa watu waliokuwa wakitoka mazishini kwa kuvizia ili wengine wasijue anamuuliza nini.
Vipi unatoka makaburini?
Ndiyo.
Vipi za huko?
Mmh! Nzuri kiasi.
Kwa nini unasema hivyo? Andendekisye moyo wake ulianza kufurahi kwa kuamini walichokikusudia kimetimia.
Tumezika katika wakati mgumu sana.
Hakukuwa na tukio lolote?
Mmh! Mwaka huu mbona kijiji kimefanywa cha majanga ya uchawi.
SASA ENDELEA...
Ehe! Andendekisye alijiandaa kumsikiliza.
Alielezwa matukio yaliyotokea makaburini tukio la bundi kumfuata mke wa Amangise lakini kabla ya kumfikia mganga alifanya mambo yake na yule bundi kuganda kisha alipasuka vipandevipande kabla hajamfikia mkusudiwa.
Tukio lingine lilikuwa la nyoka aliyedondokea kaburini akiwa amekufa huku mwili wake wote kutapakaa damu kila kona kama alikuwa akiogelea kwenye dimbwi la damu.
Duh! Andendekisye alishtuka kusikia vile.
Yaani kila kukicha kinazaliwa kituko kipya.
Kwa hiyo Amangise na mkewe wanaendeleaje?
Kivipi, kwani walikuwa wakiumwa?
Hapana kutokana na tukio lile kipi kimewatokea?
Wapo salama, lakini inasemekana bila mganga basi Amangise na mkewe wangemfuata mtoto wao kuzimu.
Umesikia tetesi watu wanasema nani anahusika na matukio yake? Andendekisye alidodosa.
Mmh! Kwa kweli kila mmoja anasema lake japo kuna watu wanakuhusisha wewe kutokana na kauli zako.
Mi sihusiki bali siku ile nilisema kwa hasira, Andendekisye alijisafisha.
Basi kauli yako imeumba, watu wote wanajua wewe ndiye uliyemuua Ambakisye na kutaka kuwaua Amangise na mkewe.
Mbona hawasemi Amangise alivyomuua mwanangu?
Ni vigumu kujua kwa vile wewe ulijitapa mbele ya watu kuwa ulimuua Ambakisye sasa unafyeka ukoo mzima.
Hakuna siwezi kufanya hivyo zile zilikuwa hasira.
Watu wanasema mara ya kwanza ulipoondoka ghafla kabla ya kumzika mwanao ulienda kumtengeneza Ambakisye.
Si kweli.
Wewe unasema hivyo, lakini kila mmoja anajua wewe ndiye mhusika mkuu, pia tukio la leo linaambatana na wewe na mkeo kuondoka jana usiku baada ya mazishi ya mwanao. Inasemekana ulienda kuwamaliza Amangise na mkewe lakini mpango wako safari hii umefeli.
Watakuwa wamenielewa vibaya, hakuna kitu kama hicho.
Basi ndiyo hivyo kauli yako haijaondoka vichwani mwa watu.
Kwa hiyo hakuna yeyote aliyeathirika na tukio lile? Andendekisye alizidi kuchimbua.
Wapo wachache waliochubuka wakati wa kumkimbia bundi na mmoja ameumia mkono wakati wa kumkimbia chatu aliyeangukia kaburini.
Amangise hakuingia kaburini?
Ndiyo.
Kwa nini hakumzika mwanaye si mnaona mnaniita mchawi wakati mchawi mnamuacha.
Alikatazwa na mganga alisema akiingia angezikwa na mwanaye.
Mmh! Huyu mganga anatoka nchi gani? Andendekisye aliuliza macho yamemtoka pima.
Walaa, wa hapahapa nchini.
Haiwezekani lazima Amangise alisafiri mbali.
Mbona mganga mwenyewe unamjua wa kijiji cha pili.
Nani?
Si yule kijana aliyemrudisha mtoto wa Mwakasege.
Yule si mganga alipanga ili kuvutia biashara yake nilichunguza na kuujua ukweli.
Basi ndiye aliyefanya kazi ya kuokoa maisha ya Amangise na mkewe.
Kama yule hana lolote yule kijana tapeli, mganga awe kijiji cha jirani? Andendekisye aliendelea kubisha.
Andendekisye aliupinga uwezo wa mganga kwa yule kutokana na kuamini sana waganga wa kweli wapo Malawi na si Tanzania.
Halafu mganga amesema kila mmoja anayejihusisha na ushirikina aache mara moja, wote tumeambiwa tukitoka makaburini tukachome tunguri zetu kama tunazo.
Na wasipochoma?
Amesema kiama chao kinakuja cha watu kuumbuka hadharani.
Anawatisha tu watu, hana jeuri hiyo.
Wewee! Yule kijana anatisha, nina wasiwasi wachawi wa kijijini siku ya kuumbuka inakuja kwa atakayekaidi amri yake.
Kama kweli basi ataanza kuumbuka Amangise na mkewe, maana wale wanatisha kwa uchawi.
Basi wacha niwahi msibani watu wamepita muda.
Hakuna tatizo tutaonana baadaye.
Andendekisye aliagana na mtu aliyempa taarifa ya makaburini na kumfanya kichwa kizidi kuchanganyikiwa alirudi ndani kwa mganga aliyekuwa akisubiri majibu ya kazi yake makaburini. Sura ya Andendekisye ilimshtua mganga na kutaka kujua kulikoni.
Vipi?
Mambo mabaya.
Mabaya kivipi?
Tumefeli tena.
Muongo!
Kweli, hakuna cha bundi wala chatu.
Kwani imekuwaje?
Andendekisye alimweleza yaliyotokea makaburini ya kupasuka vipandevipande kwa bundi na kuokotwa kwa nyoka kaburini akiwa ametapakaa damu mwili mzima kama alikuwa akiogelea kwenye bahari ya damu.
Mmh! mganga aliguna baada ya kuona ngoma aliyokuwa akicheza si ya kitoto.
Sasa tunafanyaje?
Yaani nazidi kukutana na vikwazo, sielewi nimekosea wapi, hebu twende nyuma ya nyumba tukaangalie bomu lingine. Siamini kama mtu ninayepambana naye ana uwezo mkubwa kama huo lazima kuna kitu nimekosea.
Nasikia kuna kijana mmoja ndiye aliyezuia zoezi letu bila hivyo kazi ingekwenda vizuri.
Hakuna kiumbe kinachoweza kuzuia kazi yangu, hebu tukaangalie ili niangalie nimekosea wapi. Wachawi walioshindikana hupiga saluti mbele yangu itakuwa mganga huyu kwanza anatoka wapi?
Kijiji cha jirani.
Hapahapa Tanzania?
Ndiyo.
Tanzania hakuna waganga, subiri nikamtie adabu.
Walizunguka nyuma ya nyumba kuangalia mtego mwingine unaonesha kitu gani.
Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia simulizi hii ya kusisimua Kesho.........
Liati kungelikuwa kuna uchawi wa kupata Pesa ningelikuwa mimi pia Mchawi lakini hakuna uchawi wa Mtu kuwa Tajiri kuna faida gani kujifunza Uchawi wa kuwadhuru watu? Ndugu mbaluLeo nimeinjoi sana, MziziMkavu angalia naweusijekuwa mchawi maana hizi hadithi duh......!!!!!!