Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

Hadithi ya kusisimua: Vita ya wachawi

miss ngatara
Inaelekea darasani ulikuwa mzembe,au mpiga chabo.
Hapo jiongeze utajuwa tuu,usitafuniwe kila kitu.
Je unakumbuka
666 Nyayo ya kuzimu iliishia wapi?
Basi ndo ivo,unaji tune unajua whre is it ended.

Lait tungesoma darasa mmoja ndio ungejua kama nilikuwa mzembe au vip ,na kama kuhisihisi ndio akili nadhan watabir wangekuwa maprofesa nilichokiona kwako we inahisihis tu ndio maana nilipokwambia elezea ukawa huna uhakika ukabakia kuropokaropoka
 
Last edited by a moderator:
Lait tungesoma darasa mmoja ndio ungejua kama nilikuwa mzembe au vip ,na kama kuhisihisi ndio akili nadhan watabir wangekuwa maprofesa nilichokiona kwako we inahisihis tu ndio maana nilipokwambia elezea ukawa huna uhakika ukabakia kuropokaropoka

Aiseeee.....
 
Ndiko ilipoishia kule anapokopy coz jamaa sijui ana uhusiano na Global Publishers, hii hadithi ilishaandikwa kwnye gazeti la Risasi (Ukigoogle waweza kuipata yote kwny web ya global). Ile ya NCHI YA WACHAWI ni Kitabu kimeandikwa na Irene Ndauka (nnacho hapa) na ile ya 666 nyayo za kuzimu ilikuwa inaandikwa kwny page moja ya fb inaitwa simulizi na mashairi (Sasa sijui Mzizimkavu ndo mhusika mwenyewe or na yeye mwizi tu wa Intellectual Property za watu, nna mashaka).
 
HADITHI YA KUSISIMUWA VITA YA WACHAWI-29

ILIPOISHIA:
Andendekisye alifunua kitambaa na kushtuka baada ya kuona watu wakiwa ndani ya beseni kama sinema.
“Umeona nini?”
“Watu wawili.”
“Unawafahamu?”
“Ndiyo.”
“Nani na nani?”
“Amangise na mkewe.”
“Ni wenyewe?”
“Ndiyo.”
“Hebu shemeji angalia.”
Mke wa Andendekisye alichungulia na kusema:
“Ni wenyewe.”
“Sasa tunafanya kazi moja.”
“Ipi?”
“Iliyowaleta. hapa ni pigo moja ila hakikisha unachoma kwenye moyo.”
“Sawa.”
“Uchawi huu haukopeshi ukichomoa kisu na mtu kule ameondoka.”
SASA ENDELEA...

“
Dah! Hii ni kiboko.”
“Tena nitakupa dawa hii kila anayekuchezea unaweka maji kwenye beseni na dawa nitakayokupa, lazima kwanza uchinje kuku mwekundu ambaye damu yake utaweka kidogo kwenye maji na kumuona mbaya wako hapo lazima afanye kama hapa haipiti muda utasikia mtu yupo chali.”
“Mbona mwaka huu nitawafyeka wabaya wangu wote,” Andendekisye alijigamba.
“Unaanza na nani?” mganga alimuuliza.
“Na huyu mbaya wangu namba moja,” alimuonesha Andendekisye.
“Haya chukua dawa hii jipake mkononi .”
Andendekisye alichukua dawa na kujipaka mikononi kisha akashikishwa kisu na kuambiwa:
“Nyanyua juu kisha teremsha kwa nguvu choma kwenye moyo kwa mikono miwili.”
Andendekisye alishika kisu na kukinyanyua juu na kukiteremsha kwa nguvu kwenye maji kuchoma kwenye kifua cha Amangise mpaka maji yakaruka juu.
Baada ya kuchoma kisu mganga alimsifia.
“Vizuri kazi ya kwanza umeifanya vizuri.”
Wakati anachoma ndani ya maji mkewe alishtuka na kupiga kelele huku akijishika kifua. Wakati huo maji ndani ya beseni yaligeuka rangi na kuwa damu tupu yenye kutoa harufu ya damu mbichi.
“Nini mke wangu?” Andendekisye aliuliza baada ya kumuona mkewe ameshika kifua.
“Nimesikia kitu kama kisu kikinichoma kwenye moyo wangu.”
“Eti nini?” mganga alishtuka.
Ghafla mikono iliyopo kifuani ilianza kutapakaa damu na kufanya mke wa Andendekisye alalamike.
“Jamani nakufa, nasikia maumivu makali kifuani.”
“Mungu wangu,” Andendekisye alishtuka kuona mikono ya mkewe imejaa damu.
“Mganga hii nini?”“Mmh! Hebu subiri,” mganga alisema huku akiangalia kwenye beseni na kushtuka kuona kitu tofauti.
“Kabla ya kuchoma uliona picha gani?”
“Ya Amangise na mkewe.”
“Si kweli hukuangalia vizuri.”
“Vizuri kivipi hata mke wangu aliona picha hiyo.”
“Nasema hukuangalia vizuri wakati unachoma ilibadilika na kuwa picha ya mkeo, kumbuka nilikukataza usifumbe macho,” mganga alimlaumu.
“Mganga unataka kunilaumu bure, nimefuata yote sikufumba macho na niliyemchoma alikuwa Amangise si mke wangu.”“Mbona hapa kuna picha ya mkeo akielea kwenye damu.”
“Eti nini?”
“Hapa panaonesha aliyechomwa ni mkeo.”
“Mungu wangu sasa tutafanya nini?”
“Nitajitahidi lakini sijui.”
“Mganga chondechonde okoa maisha ya mke wangu,” Andendekisye alipagawa.
Wakati huo mkewe alikuwa ameegemea ukutani macho yakiwa yamechoka kama mtu aliyefanya kazi ngumu iliyomchosha.
“Mmh! Hebu subiri.”
Mganga alisema huku akitoka nje na kumuacha Amangise na mkewe. Alimsogelea mkewe aliyekuwa akimtazama kwa jicho kama ana usingizi mzito.
“Mke wangu.”
“A..aa..bee.”
“Unajikiaje?”
“Mmh! Nasikia baridi kali moyoni.”
“Subiri mganga atakupa dawa.”
“Siwezi kupona lazima nitakufa inaonesha kabisa mganga hawezi kurudisha alichokitoa.”
“Una maana gani mke wangu?”
“Dawa imeshafanya kazi hawezi kuirudisha ni wazi amekata tamaa.”
“Huwezi kufa, kama ameroga mwenyewe ashindwi kuzuia.”
‘Mume wangu baridi linazidi nahisi viungo kufa ganzi, nakufa mume wangu.”
“Huwezi...huwezi.”
Andendekisye alishtuka kuona mganga akichelewa kurudi wakati hali ya mkewe ilizidi kuwa mbaya. Alitoka nje kumtafuta mganga alishangaa kumkuta akiwa amekaa na msaidizi wake akivuta tumbaku. Hali ile ilimshangaza sana baada ya kumkuta mganga akipiga stori na msaidizi wake wakati ndani amemuacha mkewe kwenye hali mbaya.
” Mkuu vipi?” Andendekisye aliuliza.
“Bado natafuta njia ya kuyaokoa maisha ya mkeo.”
“Unatafuta vipi wakati nimekukuta unazungumza na msaidizi wako huku unavuta tumbaku?”
“Umeshawahi kuniona navuta hata sigara?” mganga alimuuliza Amangise akiwa amemkazia macho.
“Sijawahi kukuona ndiyo leo.”
“Basi ukiona hivi ujue akili imegota mwisho kuvuta huku ni kutaka msaada wa mizimu.”
“Mmh! Mpaka mizimu ikusaidie mke wangu bado atakuwa hai?”
“Mkeo ana nafasi ya kuishi kwa asilimia moja tu na siwezi kukuahidi kumponya. Dawa ile huwa haina kinga ikimpata mtu.”
“Sasa ilikuwaje ikampata mke wangu?”
“Andendekisye niache kwanza nitafute tiba ya mkeo unavyonisemesha unaongeza ukubwa wa tatizo.”
Ilibidi Andendekisye awe mpole na kusubiri maagizo ya mganga, kuendelea kuwa nje kulimshinda na kumfanya arudi ndani kumtazama mkewe.
Alipoingia alimkuta mkewe ameegemea kwenye ukuta shingo ikiwa imeanguka. Alimshika na kukuta mwili umepoa. Hakukubali alimtikisa mkewe huku akimwita jina lake.
“Sara mke wangu mbona hivi?”
Mkewe hakuwa na jibu kwa vile roho ilikuwa imeachana na mwili, alitoka nje huku akilia mpaka kwa mganga.“Mganga njoo umuone mke wangu.”
“Hata nikija sitabadili kitu.”
“Hapana mganga njoo umuone mke wangu.”
“Najua kilichotokea hata mizimu imeona, asilimia moja haikuwa na nguvu kuzuia kifo cha mkeo.”
Kusikia vile Andendekisye aliangua kilio kama mtoto mdogo huku akiapa kumfanyia kitu kibaya Amangise. Zoezi la kumteketeza Amangise na mkewe lilisitishwa na kuushughulikia mwili wa mke wa Andendekisye.
Kwa vile nyumbani Tanzania ilikuwa mbali na safari yake haikufuata taratibu za uhamiaji walikubaliana mwili wa mkewe uzikwe kulekule Matipa nchini Malawi.
Mganga hakutaka maiti ilale kwani ingemletea picha mbaya kwa wateja wengine, ilibidi kaburi lichimbwe usiku uleule na watu watatu kwa kupokezana Mganga msaidizi wake na Amangise mwenyewe kwa vile wagonjwa waliokuwepo walikuwa wanawake watupu.

Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia Jumatatu ijayo.......
 
VITA YA WACHAWI-30

by-GLOBAL

10 hours ago

ILIPOISHIA:
Mganga hakutaka maiti ilale kwani ingemletea picha mbaya kwa wateja wengine, ilibidi kaburi lichimbwe usiku uleule na watu watatu kwa kupokezana mganga msaidizi wake na Amangise mwenyewe kwa vile wagonjwa waliokuwepo walikuwa wanawake watupu.
SASA ENDELEA...

Japokuwa Andendekisye alikuwa na uchungu wa kifo cha mkewe lakini alilazimishwa na mganga kusaidia kazi ya kuchimba kaburi kisha waliuchukua mwili wa mke wa Andendekisye na kwenda kuuzika watu watatu usiku uleule. Baada ya kuzika walirudi nyumbani kwa mganga ambaye kichwa kilimuuma kwa kilichotokea, toka aanze uganga hakuwahi kutokewa na kitu kama kile.

Alipofika kilingeni kwake aliangalia rada zake, ajabu kila alipoangali ilikuja sura yake kuonesha ndiyo iliyofanya vile. Kila njia alitumia ili aone nani aliyefanya vile hakukuwa na jibu lingine zaidi ya kujiona yeye kuwa ndiye mhusika wa kifo cha mke wa Andendekisye.

Baada ya kuchemka alimwambia Andendekisye:
“Inaonekana jirani yako makombora ya mbali hayamuwezi nitaondoka na wewe mpaka kwako nikatege bomu langu karibu. Hawezi kunichezea akili sijawahi kuchezewa akili, naapa nikimshindwa naacha uganga.”

“Yaani siamini kama ukishindwa nitakwenda popote ili nimtie adabu hawezi kunitia hasara mara mbili,” Andendekisye alisema kwa uchungu.
“Tunaondoka muda huu ili mchana itukute Tanzania natega vyangu baada ya majibu naondoka usiku kurudi kwangu.”

“Yaani nipo radhi kutumia kiasi chochote cha fedha hata kuuza shamba langu lote ili nimtie adabu.”
“Wala hutaingia hasara yoyote majibu utayapata leo hii hii kama yeye anajua hivi sisi tunajua vile. Sijawahi kushindwa na kitu chochote, wachawi wote wanajua mimi ni nani. Kama kombora la mbali limemkosa sasa vita naihamishia Tanzania, kitu nitakachomfanya hakitasahaulika katika midomo kijijini Ibungu na vitongoji vyake- na Tanzania nzima.”

“Nataka pigo limalize mpaka kizazi chake chote hata kama kuna ndugu zake hakikisha unafagia mpaka sisimizi anayemuhusu.”“Hiyo kazi ndogo, hata jengo analoishi litageuka kichunguu, amenichokoza huwa sichezewi, mimi ndiye mchawi niliyeogopwa mpaka na shetani,” mganga alijitapa kwa hasira.

Baada ya mganga kuchukua makombora ya maangamizi, waliondoka alifajiri ile na kuacha wagonjwa chini ya wasaidizi wao huku akiwaeleza atarudi usiku wa siku ile ili kuendeleza tiba zao na kama kuna mmoja atakuwa bado hajapata nafuu japokuwa aliamini dawa aliyowapa ilikuwa ni nzuri, wamuongezee dozi.

Walipanda magari mpaka mpakani na kuvuka mpaka hadi Tanzania na kupitia baikeli yake mpaka Ibungu ambako walifika saa saba mchana wakati huo watu walikuwa katika maandalizi ya mazishi ya Ambakisye. Alipofika alikwenda moja kwa moja hadi nyumbani kwake na kuingia ndani.
“Mkuu taarifa wanazika saa kumi jioni,” Andendekisye alimweleza mganga baada ya kudodosa habari za kijijini.

“Basi kazi itaishia makaburini wote watarudi na pumzi lakini si Amangise na mkewe, hilo kombora ni moja ya silaha, huzitumia kwa nadra hasa kwa watu wenye kutaka kupimana nguvu na mimi.”
“Yaani nikisikia wamekufa mbona nitafanya sherehe, nitachinja ng’ombe wawili.”
“Hiyo kazi ndogo namaliza kazi yangu kachague hao ng’ombe kabisa.”

“Hilo halina tabu, yaani mpaka sasa nashindwa kulia kwa kifo cha mke wangu kipenzi, naona kama bado nipo ndotoni na asubuhi nikiamka naona kama zamelala pembeni yangu.”
“Najua, lakini moyo wako wa kuvumilia unanipa nguvu ya kuifanya kazi vizuri.”
“Nataka kilio changu kigeuke kicheko.”
“Jioni haipo mbali.”

“Sasa hivi sitasema kitu nasubiri majibu toka makaburi juu ya vifo cha Amangise na mkewe.”
“Mmh! Sasa kazi ndiyo inaanza kabla hawajaenda makaburini. Nipatie unga, ungo na chungu.”
Andendekisye alifanya vile haraka kwa kumletea mganga alivyoomba kisha alikaa pembeni. Mganga alifungua makombora yake na kutoa- dawa aliyochanganya na unga na kipande cha ngozi ya chatu na kufunika kwa ungo.

Kisha alichukua dawa nyingine na kuchanganya na unga- na kucha ya bundi na kuvifunika na chungu, walitoka nje na kuomba chungu kingine kipya.
“Nipatie kuku mwekundu.”

Andendekisye aliingia bandani na kuchukua jogoo jekundu na kumpa- mganga ambaye alimchukua na kumlisha hirizi ndogo kisha alimzika akiwa hai. Chungu alikichukua na kukiweka nyuma ya nyumba na kuomba kisu.

“Nichome tena kisu?” Andendekisye alishtuka.
“Hapana , kazi yote nafanya mimi kama bomu wacha linilipukie.”
“Mmh! Hapo sawa, maana sasa hivi kisu nakiogopa sidhani kama nitachinja hata kuku katika maisha yangu kwani sasa hivi nikishika kisu nitakuwa kama namuua mke wangu.”

“Ondoa wasi kazi yote nimeamua kuifanya mwenyewe wewe subiri majibu utajua huwa sibahatishi kwenye kazi yangu.”Baada ya mganga kuchukua kisu na chungu kipya alikiweka nyuma ya nyumba na kukiweka kisu ndani ya chungu bila kitu chochote.

Kisha walirudi ndani na kumwambia- Andendekisye. “Fungua kwenye chungu,” alimwambia afunue chungu- kilichowekwa dawa na kucha ya bundi.--- -
Andendekisye alisogea kwenye chungu na kufungua, alishtuka na kusababisha kukidondosha chungu baada ya kumkuta bundi mkubwa ndani yake aliyetengenezwa na dawa alizochanganya mganga ambazo ziligeuka kuwa ndege huyo
“He!”

“Unashangaa nini?”
“Siamini.”
“Kazi umeanza, hii ndiyo silaha itakayommaliza mke wa adui yako,” mganga alisema huku akimtoa bundi na kumuweka pembeni kisha alimgeukia Andendekisye aliyekuwa bado amepigwa na butwaa baada ya kuona maajabu yale kwa mchanganyo wa dawa kutoa bundi.

“Hii nitafunua mwenyewe kwa vile unaweza kufa kwa mshtuko, utakachokiona usishtuke ni silaha za maangamizi.”
“Kwani kuna nini?”
“Utaona tu.”

Je, ni nini hicho, fuatilia wiki ijayo.
 
Wiki ijayo unamaanisha jumapili? maana wiki inaisha siku ya Al-Sabut (siku ya Sabato) juma mosi.
 
Acha mambo yako. Anamaanisha jumatatu baada ya kuadhimisha siku ya ufufuko wa mkombozi wetu.

Acha kushikiwa hakili na viongozi wa madhehebu, imesalia raha ya SABATO kwa watu wa Mungu Waebrania 4:9
 
Acha kushikiwa hakili na viongozi wa madhehebu, imesalia raha ya SABATO kwa watu wa Mungu Waebrania 4:9

Ahsante kwa maana wasabato si dhehebu. Ila fuatilia injili na matendo ya mitume, uone Yesu alikuwa akiwatokea mitume wake siku zipi na walikuwa wakikusanyika siku hiyo kufanya nini. BWANA akuangazie nuru ya uso wake, akukinge na mafundisho ya ELLEN WHITE, akujalie kutambua maana ya Sabato ya kweli. Amen.
 
mkuu mzizi mkavu week mpya imeanza leo;tutapata hadithi yetu?
 
Ahsante kwa maana wasabato si dhehebu. Ila fuatilia injili na matendo ya mitume, uone Yesu alikuwa akiwatokea mitume wake siku zipi na walikuwa wakikusanyika siku hiyo kufanya nini. BWANA akuangazie nuru ya uso wake, akukinge na mafundisho ya ELLEN WHITE, akujalie kutambua maana ya Sabato ya kweli. Amen.

Acha tusije tukageuza jukwaa la dini. wengine ubishi si fani yetu.elewa unavyo elewa kwani sasa kuna uhuru wa kuabudu hata ukitaka kusbudu sanamu sawa
 
Back
Top Bottom