Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

ILIPOISHIA:
“Hapana si kufa bali huduma za muhimu tumejitahidi
kadri ya uwezo wetu, hatuwezi kuendelea kumweka
hospitali na kuongeza gharama wakati huduma
nyingine anaweza kuzipata akiwa hukohuko
Tanzania. Sisi kazi yetu kubwa tumemaliza
kilichobakia ni kazi ya Mungu.”
“Mmh! Sawa.”
Mama Cecy alikubali kwa sauti ya kukata tamaa
kwani siku zote watu waliokwenda India hurudi
wamepona na ikishindikana basi mtu huyo huwa wa
kumzika. Aliamini ile ilikuwa kauli ya kumpa moyo
lakini siku za kuishi mwanaye zilikuwa
zinahesabika.
SASA ENDELEA...
Iliandaliwa mipango yote ikiwa pamoja na tiketi ya
kurudi Tanzania na kupangiwa siku ya kurudi.
Habari zile zilikuwa pigo mujarabu moyoni mwa
mama Cecy mwanaye mmoja kama mboni ya jicho
lake alimuona akitoweka katika sura ya dunia.
Lakini yote alimuachia Mungu kwa vile ndiye
muweza wa kila kitu.
Taarifa za kurudishwa Tanzania Cecy baada ya
ugonjwa wake kuonekana utachukua muda mrefu
kupata nafuu zilimfikia mama Colin na kuamini ile
ndiyo nafasi ya pekee kwa Mage kuichukua nafasi
ile baada ya kupata uhakika hali ile inaweza
kuchukua muda mrefu kupata nafuu au maisha
yake yote yawe ya kitandani alijua ilikuwa kuwapa
moyo lakini Cecy alikuwa maiti mtarajiwa.
Kwa taarifa ile aliamini mwanaye pamoja na
msimamo lazima atabadilika na kukubali kumuoa
Mage huku akijitolea kumsaidia Cecy kwa
kumwekea mtu wa kumhudumia na kumlipa kwa
maisha yake yote ili tu kumfurahisha mwanaye.
Alitamani siku moja aitwe bibi na hakuwa na mtoto
mwingine zaidi ya Colin ambaye ndiye
aliyemtegemea kumleta mjukuu. Ugonjwa wa Cecy
ulionesha hakukuwa na dalili zozote kuweza kubeba
ujauzito na yeye kupata mjukuu. Moyoni alijikuta
akipata mawazo mabaya ya kumuua Cecy kama
mwanaye atasimamia msimamo wake wa kutotaka
kuoa mwanamke mwingine.
Lakini kuna kitu kilimtisha baada ya kukumbuka
kauli ya mwanaye kufunga ndoa hata na maiti ya
Cecy. Hiyo ilimpa wakati mgumu. Lakini alipanga
kumtumia Mage kuyabadili mawazo yake na
kukubali kumuoa. Siku ya pili Mage alifika kama
alivyoelekezwa na mama Colin lakini hakutakiwa
kuonana na Colin mpaka mpango wake autekeleze.
Baada ya Mage kufika alifikia chumba cha msichana
wa kazi na mama Colin alikwenda chumbani kwa
Colin kumwamsha ili ajiandae kwenda hospitali.
“Jiandae basi ukafanye mazoezi.”
“Sawa mama.”
Colin aliingia bafuni kuoga baada ya kuoga alibadili
nguo na kutoka chumbani kwake na kwenda kukaa
sebuleni kumsubiri mama yake ili waende kwenye
mazoezi ya viungo (Physiotherapy). Mama Colin
alitoka chumbani kwake akiwa tayari kwa safari
begi lake begani. Colin alipomuona mama yake
alinyanyuka ili waondoke.
Lakini ghafla alishtuka kumwona mama yake
akiweka mkono kichwani katika paji la uso huku
amekunja uso.“Nini mama?” Colin alishtuka.
“Kichwa,” mama alisema kwa sauti ya
kujilazimisha.
“Mungu wangu! Kimefanya nini tena mama yangu?”
Colin alishtuka na kujitahidi kumfuata mama yake ili
amshike.“Hapana baba , niache nitakaa
mwenyewe,” mama Colin alisema huku akisogea
kwenye kochi na kukaa.“Nipe maji,” alisema akiwa
ameinama mkono kichwani.
Colin alipotaka kwenda kumchukulia maji
alimkataza na kutaka amwambie msichana wa kazi.
Baada ya kuitwa alileta maji kwenye glasi na kumpa
mama Colin aliyeyanywa yote na kupumua pumzi
nyingi kisha alisema.“Duh! Afadhali kidogo.”
“Sasa itakuwaje maana kwa hali hiyo huwezi
kuendesha gari?”
“Na kweli siwezi kuendesha gari, nimekumbuka
Mage alisema atakuja kukuona asubuhi.”
“Mage gani?”“Si aliyekuwa mchumba wako.”
“Mama niseme mara ngapi kuwa sitaki kumuona
yule shetani wa kike,” Colin alisema kwa hasira
kidogo.
“Mwanangu wewe ndiye uliyekuwa ukinieleza siku
zote nisikae na jambo baya moyoni muda mrefu
naweza kupata matatizo.
Kwa nini unamchukia hivyo Mage? Hata kama
alifanya kosa lililosababisha ajali bado alitakiwa
kusamehewa. Humtaki kuwa mpenzi wako lakini
bado ni mwanadamu anayetakiwa kusamehewa na
kumwona rafiki, hujui adui wa leo ni rafiki wa
kesho.”
“Ni kweli mama, najitahidi kumsamehe lakini moyo
wangu umekuwa mzito.”
“Huyo ni pepo mchafu tunatakiwa kumkemea.”
“Sawa mama nitajitahidi.”
“Kwa vile siwezi kuendesha gari leo basi naomba
Mage atatupeleka hospitali.”
“Sawa mama,” Colin hakutaka kukataa kwani
angemuudhi mama yake.
“Ngoja nimpigie simu.”Mama Colin alijifanya kipiga
simu na kujizungumzisha peke yake:
“Eeh! Umekaribia... tena umefanya vizuri... wahi basi
utupeleke hospitali...haya tunakusubiri...
Umekaribia... sawa... hakuna tatizo tupo tayari,”
mama Colin alijifanya kukata simu.
“Kwani kafika wapi?” Colin aliuliza.
“Yupo nje ya geti.”
“Sawa.”Mama Colin alijifanya kuelekea upande wa
vyumbani na kwenda chumba cha msichana wa
kazi na kwenda kuzungumza na Mage.
Itaendelea wiki ijayo Jumamosi.
 
ILIPOISHIA :
Mama Colin alijifanya kuelekea upande wa
vyumbani na kwenda chumba cha msichana
wa kazi na kwenda kuzungumza na Mage .
SASA ENDELEA .. .
“Mambo yamekwenda vizuri japokuwa
imenibidi nilazimishe kwa cheo cha umama ,
sasa pitia mlango wa nyuma kisha ingilia
mlango wa mbele kujifanya ndiyo unaingia .”
“Sawa mama .”
Mage alitokea mlango wa nyuma na kwenda
kulichukua gari alilokuwa amelipaki nje na
kuingia nalo. Aliteremka kwenye gari na kuingia
ndani.
“Karibu mama. ”
“Asante , za hapa ?”
“Nzuri .”
Mage alisogea kwa Colin na kumsalimia:
“Umeamkaje?”
“Namshukuru Mungu .”
“Nina imani hali yako itatengemaa muda si
mrefu ili urudi katika majukumu yako , sala
zangu zote hukutanguliza mbele nina imani
Mungu ataipokea .”
“Amina. ”
“Mage tunaweza kwenda.”
Mage alimshika mkono Colin na kunyanyua,
alitoka naye hadi nje na kuingia kwenye gari la
Mage ambalo aliomba walitumie kwa siku ile.
Colin muda wote alikuwa kimya hakutaka kutia
neno kwa kuhofia kumuudhi mama yake
ambaye muda huo aliamini kabisa hali yake
siyo nzuri hakutaka kuharibu kote kwani bado
hali ya mpenzi wake Cecy ilibakia kitendawili.
Walikwenda mpaka kwenye kitengo cha
mazoezi ya viungo (Physiotherapy ), walipofika
mama Colin alikaa pembeni na Mage alimsaidia
Colin kufanya mazoezi kwa kumshikilia
sehemu nyingine ambazo alihitaji msaada.
Kila dakika Mage alikuwa akitokwa na machozi
kitu kilichomshtua Colin .
“Mage unalia nini ?”
“Sijui moyoni mwako una hasira kiasi gani juu
yangu.”
“Sina hasira yoyote .”
“Hapana Colin una kitu kizito juu yangu
kutokana na yaliyotokea, ile ni mipango ya
Mungu tu, naomba Colin unisamehe najutia
kilichotokea ni mapenzi ndiyo yaliyonisukuma
kufanya vile . Hata kama hutaki kuwa na mimi
naomba unione rafiki na si adui.”
“Mage ningekuwa sijakusamehe tusingekuwa
karibu hivi na kuweza kukusikiliza.”
“Nashukuru Colin kwa kunisamehe, naamini
wewe ni mume mwema hakika Cecy kapata
lulu kwenye chaza. ”
“Nashukuru .”
“Vipi hali ya Cecy ?”
“Kwa kweli mpaka sasa sijajua, mama
amekuwa akinificha japo walinieleza inaendelea
vizuri .”
“Mungu atamsaidia siku moja atasimama na
kufanikisha mlichokipanga, ” Mage alimpa moyo
kinafiki.
“Amina. ”
“Colin .”
“Naam.”
“Baada ya Cecy moyoni mwako yupo nani?”
“Bado sijamuona labda mwanetu
atakayezaliwa.”
“Basi naomba baada ya mwanenu nafasi
inayofuata nipe mimi, naomba usiniweke mbali
na mawazo yako .”
“Hakuna tatizo . ”
“Naomba niwasiliane na wewe wakati Cecy
yupo mbali . ”
“Mage , suala la mawasiliano naomba tuliweke
pembeni kwanza. ”
“Kwa nini Colin, kukujulia hali tu. ”
“Ukitaka kuwasiliana na mimi tumia simu ya
mama lakini kwa sasa sitatumia simu kwa vile
ndiyo iliyoleta yote haya. ”
“Colin basi hujanisamehe .”
“Kukusamehe si kunilazimisha kufanya vitu
nisivyovitaka , nimekueleza sitaki kutumia simu
unanilazimisha kwa kisingizio cha
kutokusamehe. Kumbuka ubishi huo ndiyo
uliosababisha yote haya. ”
“Nimekuelewa Colin , nisamehe sana , nitajitahidi
kukuelewa ili tusije kosana tena. ”
“Itakuwa vizuri .”
“Colin nashukuru kunisamehe moyo wangu
sasa mwepesi nilikuwa kama nimebeba
mawe.”
“Kawaida katika maisha kuna kukosana na
kupatana. ”
“Nashukuru sana .”
Mama Colin aliyekuwa mbali kidogo
mazungumzo yale yalimtia moyo na kuamini
mpango wake umeweza kufanikiwa kwa
kuamini Mage ndiye chaguo lake la awali kabla
Cecy kuingilia penzi lile . Taarifa ya kurudishwa
Cecy kutoka India hakutaka kumweleza haraka
mwanaye mpaka atakapotua nchini kwani kwa
taarifa siku inayofuata ndiyo aliyokuwa
akiwasili.
Alipanga kuonesha ushirikiano mkubwa lakini
alibakia na siri yake juu ya Cecy na ugonjwa
wake ambao kama ulishindikana India basi
Tanzania ilikuwa ni kusubiri kifo . Kumweka
Mage karibu na Colin kungemsaidia kumweka
karibu kimapenzi hata akifa Cecy basi Mage
achukue nafasi ile.
Baada ya mazoezi walirudi nyumbani huku kila
mmoja akiwa na furaha moyoni mwake
japokuwa furaha ya Colin ilikuwa usoni na
mdomoni lakini moyoni bado alikosa raha
kushindwa kupata mawasiliano ya kujua hali ya
mpenzi wake Cecy . Lakini aliamini baada ya
muda hali yake itatengemaa na yeye
mwenyewe kwenda India kumuona Cecy .
Siku ile Mage alishinda pale na kufanya kila
kitu kwa ajili ya Colin , kuanzia usafi wa
chumba, chakula cha mchana vyote alifanya
yeye na muda mwingi alikuwa karibu yake ili
kuhakikisha anairudisha nafasi iliyoipoteza
kupitia matatizo ya Cecy . Kitu kile
kilimfurahisha sana mama Colin na kuuona
mpango wake taratibu utafanikiwa.
Siku ile taarifa ilifika kuwa Cecy anawasili toka
India, mama Colin hakutaka kumwambia
mwanaye ila saa sita usiku alikwenda
kuwapokea peke yake.
Baada ya ndege kutua , abiria waliteremka na
kutoka nje .
Alisimama macho yakiwa ndani huku akijiuliza
Cecy atarudi katika hali gani, akiwa mapokezi
alikiona kitanda kikisukumwa nyuma yake
alikuwepo daktari aliyeondoka naye na nyuma
ya daktari alikuwepo mama Cecy ambaye
alionekana amepungua mwili kutokana na
matatizo ya mwanaye.
Mama Colin alijitokeza kuwapokea kwa
kumkumbatia mama Cecy.
“Jamani dada karibuni, poleni na safari.”
“Mungu ni mwema. ”
“Karibuni, ” alikwenda kitandani kumwangalia
Cecy ambaye muda huo alikuwa amepitiwa na
usingizi.
“Vipi anaendeleaje ?”
“Tutazungumza nyumbani, vipi Colin naye
anaendeleaje ?”
“Kweli Mungu ni mwema anaendelea vizuri . ”
Itaendelea wiki ijayo.
 
Rich Pol, hii mimi naionaga sehemu so ikiletwa hapa nakuwa nimeshaiona
 
Last edited by a moderator:
ILIPOISHIA:
"Mungu ni mwema."
"Karibuni," alikwenda kitandani kumwangalia Cecy ambaye muda huo alikuwa amepitiwa usingizi.
"Vipi anaendeleaje?"
"Tutazungumza nyumbani, vipi Colin naye anaendeleaje?"
"Kweli Mungu ni mwema anaendelea vizuri."
SASA ENDELEA...

Kwa vile alikuwa amekuja na gari aina ya Toyota Noah aliyoelezwa ndiyo inayotakiwa kumpokelea mgonjwa, walimweka kwenye gari na kuelekea nyumbani kwa mama Cecy ambako siku ile kulifanyika usafi na kuiweka nyumba katika hali nzuri.
Hivyo walikuta nyumba ipo vizuri pamoja na msichana wa kazi aliyeachwa kwa ajili ya kuangalia nyumba kwa muda wote ambao hakuwepo.Baada ya kufikishwa nyumbani aliingizwa chumbani na kulazwa kitandani, muda wote mama Colin alimfuatilia Cecy na kuonesha hakuwa na dalili zozote za kupona.
Pamoja na huruma kumjia lakini bado aliamini kama Cecy atakufa basi Mage ndiye mbadala wake.
Baada ya kumlaza kitandani daktari aliyekwenda na Cecy India alikaa na wazazi wawili na kuwaeleza:

"Jamani nina imani maelezo tuliyopewa India unayakumbuka, lakini kwa kuongezea ninataka kuwaeleza, mgonjwa hali yake bado japo kuna mabadiliko makubwa sana tofauti na alivyokwenda. Ugonjwa wa Cecy umekuwa tofauti na ugonjwa mwingine ambao madaktari bingwa wamekutana nayo huu kidogo umewala akili.
"Inaonekana mwili wa Cecy unajenga mawasiliano taratibu sana inaweza kuchukua muda mrefu sana kunyanyuka kitandani. Hivyo anatakiwa uangalizi wa karibu sana, kama kuna uwezekano aajiriwe mtu kwa kazi hii ili kumpumzisha mama yangu hapa kwani namhurumia amefanya kazi kubwa usiku na mchana kwa ajili ya kumwangalia mwanaye japo nilimsaidia bado muda wote alikuwa halali.
"Mgonjwa ataendelea kupata huduma ya kuchukuwa kila siku mwili mzima ili kusisimua misuli ya mwili. Nina imani kwa uwezo wa Mungu anaweza kupata nafuu upesi kwa vile mwisho wa akili ya mwanadamu ndipo uwezo wa Mungu huchukua nafasi yake," dokta Mariamu Shaka aliwapa moyo kwa maneno ya hekima.
"Nina imani mpaka leo yupo hivi lazima turudishe shukrani zetu kwa Mungu wetu," mama Colin alisema.
"Kingine mama, huoni maajabu pamoja na mwili kukosa mawasiliano lakini vitu vyote vya ndani vinafanya kazi hata kuweza kula japo chakula laini kitu ambacho kimewashangaza hata madaktari bingwa."

"Ni kweli tuna kila sababu ya kumshukuru alichotupa si haba, kama leo katupa kidogo na kurudisha shukurani kwake basi hatasita kutupa kikubwa, nina imani mwanangu siku moja atasimama," alisema mama Cecy kwa hisia kali.
"Amina, Mungu wetu ni msikivu," alijibu dokta Mariamu.
Kwa vile muda ulikuwa umekwenda mama Colin aliaga kurudi nyumbani na kumwacha mama Cecy mgonjwa na daktari ambaye alilala pale ili kesho yake baada ya kumpatia mgonjwa huduma arudi nyumbani kwake.

Kutokana na hali aliyomuona nayo Cecy, hakutaka kumweleza mwanaye kwa kujua atamshtua hata kukosa raha na kumuongezea matatizo kwa vile alimpenda sana mchumba wake. Lakini alijiuliza mwanaye akijua lazima atamwelewa vibaya, alipanga kumwambia baadaye kuwa Cecy amerudi.
Aliamua kukaa kimya huku wiki ikikatika bila kumweleza kitu chochote mwanaye juu ya Cecy kurudi toka India. Siku zote alitoka peke yake kwenda kumwona Cecy na kuonesha kuguswa na hali ile huku akimlipa daktari aliyekwenda naye India pesa nyingi ili kumpatia huduma ya kumchua na kumwangalia kila siku baada ya kazi.
Wema wake ulikuwa wa mamba wa kutoka machozi lakini alikuwa na siri moyoni mwake kujionesha anamjali mgonjwa. Lakini aliamini kupona kwa Cecy ni ndoto, kila alipoulizwa na mama Cecy kuhusu hali ya Colin alisema hajambo kiasi.
"Hawezi kutembea?"
"Mmh! Kwa sasa amekatazwa kutembea."
"Kwa nini basi usimlete aje amwone mchumba wake?"
"Atakuja hali yake ikitulia.""Kwa hiyo hali yake inaonekana bado."
"Ni kweli."

"Mmh! Mpe pole isingekuwa hali ya Cecy ningekuja kumwona mkwe wangu."
"Mungu atawapa afya na kuweza kunyanyuka.""Mungu atasikia dua zetu, kila jambo la heri Mungu ulishika mkono nina imani Cecy na Colin watasimama na siku moja kusherehekea harusi yao."

"Amen," mama Colin aliitikia huku moyoni akijisemea "Labda harusi aliyosema mwanaye ya kufunga ndoa na maiti ya Cecy, lakini harusi ya sherehe ukumbini itakuwa muujiza."
Mama Cecy aliamini hali ya Colin ni mbaya ila mama yake anampa moyo, alipanga siku akipata nafasi afike kumwona kwani haikuwa vizuri mzazi mwenzie kuja kumuona mwanaye na yeye kutokwenda kumuona Colin. Kwa vile hali ya mwanaye alijua alipanga siku moja baada ya kumpatia chakula akilala atoke mara moja kwenda kumwona Colin na kuwahi kurudi.
Siku ya tatu ambayo mama Colin alipiga simu kuwa hatakwenda kwa vile kuna sehemu ambapo angerudi usiku. Siku hiyo mama Cecy aliitumia kumwandaa Cecy ambaye alishangaa kuona mabadiliko madogo baadhi ya sehemu kupata joto kama miguuni ambako kulikuwa na ubaridi kwa muda mrefu.
Baada ya kumpatia chakula chepesi na dawa alimwacha apumzike na yeye kukodi gari mpaka kwa mama Colin kumjulia hali mgonjwa. Wakati huo Mage alikuwa akiendelea kuwa karibu na Colin ili kujivuta karibu kwa kuamini baada ya kifo cha Cecy basi nafasi ile ni yake.
"Colin nina imani sasa hivi afya yako ni nzuri unaweza hata kuendesha gari."
"Namshukuru Mungu, pia nashukuru kwa msaada wako kwangu kwa muda wote wa kuniangalia."
"Usijali nipo kwa ajili yako, nitapigania afya yako hata kwa gharama yoyote."

"Usiwe na wasi nina imani sasa hivi sijambo na wiki ijayo nitakwenda India kumwangalia Cecy."
"Lakini hali yako si bado kwa nini usisubiri upone kabisa.""Mage, mimi sijambo sasa hivi naweza kufanya lolote, lakini afya ya mpenzi wangu siijui. Mpaka leo bado yupo hospitali huenda yupo kwenye hali mbaya lazima niende nikajue hali yake."
 
ILIPOISHIA: “Mungu ni mwema.” “Karibuni,” alikwenda kitandani kumwangalia Cecy ambaye muda huo alikuwa amepitiwa usingizi. “Vipi anaendeleaje?” “Tutazungumza nyumbani, vipi Colin naye anaendeleaje?” “Kweli Mungu ni mwema anaendelea vizuri.” SASA ENDELEA...

Kwa vile alikuwa amekuja na gari aina ya Toyota Noah aliyoelezwa ndiyo inayotakiwa kumpokelea mgonjwa, walimweka kwenye gari na kuelekea nyumbani kwa mama Cecy ambako siku ile kulifanyika usafi na kuiweka nyumba katika hali nzuri.

Hivyo walikuta nyumba ipo vizuri pamoja na msichana wa kazi aliyeachwa kwa ajili ya kuangalia nyumba kwa muda wote ambao hakuwepo.Baada ya kufikishwa nyumbani aliingizwa chumbani na kulazwa kitandani, muda wote mama Colin alimfuatilia Cecy na kuonesha hakuwa na dalili zozote za kupona.

Pamoja na huruma kumjia lakini bado aliamini kama Cecy atakufa basi Mage ndiye mbadala wake. Baada ya kumlaza kitandani daktari aliyekwenda na Cecy India alikaa na wazazi wawili na kuwaeleza:

“Jamani nina imani maelezo tuliyopewa India unayakumbuka, lakini kwa kuongezea ninataka kuwaeleza, mgonjwa hali yake bado japo kuna mabadiliko makubwa sana tofauti na alivyokwenda. Ugonjwa wa Cecy umekuwa tofauti na ugonjwa mwingine ambao madaktari bingwa wamekutana nayo huu kidogo umewala akili.

“Inaonekana mwili wa Cecy unajenga mawasiliano taratibu sana inaweza kuchukua muda mrefu sana kunyanyuka kitandani. Hivyo anatakiwa uangalizi wa karibu sana, kama kuna uwezekano aajiriwe mtu kwa kazi hii ili kumpumzisha mama yangu hapa kwani namhurumia amefanya kazi kubwa usiku na mchana kwa ajili ya kumwangalia mwanaye japo nilimsaidia bado muda wote alikuwa halali.

“Mgonjwa ataendelea kupata huduma ya kuchukuwa kila siku mwili mzima ili kusisimua misuli ya mwili. Nina imani kwa uwezo wa Mungu anaweza kupata nafuu upesi kwa vile mwisho wa akili ya mwanadamu ndipo uwezo wa Mungu huchukua nafasi yake,” dokta Mariamu Shaka aliwapa moyo kwa maneno ya hekima.

“Nina imani mpaka leo yupo hivi lazima turudishe shukrani zetu kwa Mungu wetu,” mama Colin alisema. “Kingine mama, huoni maajabu pamoja na mwili kukosa mawasiliano lakini vitu vyote vya ndani vinafanya kazi hata kuweza kula japo chakula laini kitu ambacho kimewashangaza hata madaktari bingwa.”

“Ni kweli tuna kila sababu ya kumshukuru alichotupa si haba, kama leo katupa kidogo na kurudisha shukurani kwake basi hatasita kutupa kikubwa, nina imani mwanangu siku moja atasimama,” alisema mama Cecy kwa hisia kali.

“Amina, Mungu wetu ni msikivu,” alijibu dokta Mariamu. Kwa vile muda ulikuwa umekwenda mama Colin aliaga kurudi nyumbani na kumwacha mama Cecy mgonjwa na daktari ambaye alilala pale ili kesho yake baada ya kumpatia mgonjwa huduma arudi nyumbani kwake.

Kutokana na hali aliyomuona nayo Cecy, hakutaka kumweleza mwanaye kwa kujua atamshtua hata kukosa raha na kumuongezea matatizo kwa vile alimpenda sana mchumba wake. Lakini alijiuliza mwanaye akijua lazima atamwelewa vibaya, alipanga kumwambia baadaye kuwa Cecy amerudi.

Aliamua kukaa kimya huku wiki ikikatika bila kumweleza kitu chochote mwanaye juu ya Cecy kurudi toka India. Siku zote alitoka peke yake kwenda kumwona Cecy na kuonesha kuguswa na hali ile huku akimlipa daktari aliyekwenda naye India pesa nyingi ili kumpatia huduma ya kumchua na kumwangalia kila siku baada ya kazi.

Wema wake ulikuwa wa mamba wa kutoka machozi lakini alikuwa na siri moyoni mwake kujionesha anamjali mgonjwa. Lakini aliamini kupona kwa Cecy ni ndoto, kila alipoulizwa na mama Cecy kuhusu hali ya Colin alisema hajambo kiasi.

“Hawezi kutembea?” “Mmh! Kwa sasa amekatazwa kutembea.” “Kwa nini basi usimlete aje amwone mchumba wake?” “Atakuja hali yake ikitulia.”“Kwa hiyo hali yake inaonekana bado.” “Ni kweli.”

“Mmh! Mpe pole isingekuwa hali ya Cecy ningekuja kumwona mkwe wangu.” “Mungu atawapa afya na kuweza kunyanyuka.”“Mungu atasikia dua zetu, kila jambo la heri Mungu ulishika mkono nina imani Cecy na Colin watasimama na siku moja kusherehekea harusi yao.”

“Amen,” mama Colin aliitikia huku moyoni akijisemea “Labda harusi aliyosema mwanaye ya kufunga ndoa na maiti ya Cecy, lakini harusi ya sherehe ukumbini itakuwa muujiza.”

Mama Cecy aliamini hali ya Colin ni mbaya ila mama yake anampa moyo, alipanga siku akipata nafasi afike kumwona kwani haikuwa vizuri mzazi mwenzie kuja kumuona mwanaye na yeye kutokwenda kumuona Colin. Kwa vile hali ya mwanaye alijua alipanga siku moja baada ya kumpatia chakula akilala atoke mara moja kwenda kumwona Colin na kuwahi kurudi.

Siku ya tatu ambayo mama Colin alipiga simu kuwa hatakwenda kwa vile kuna sehemu ambapo angerudi usiku. Siku hiyo mama Cecy aliitumia kumwandaa Cecy ambaye alishangaa kuona mabadiliko madogo baadhi ya sehemu kupata joto kama miguuni ambako kulikuwa na ubaridi kwa muda mrefu.

Baada ya kumpatia chakula chepesi na dawa alimwacha apumzike na yeye kukodi gari mpaka kwa mama Colin kumjulia hali mgonjwa. Wakati huo Mage alikuwa akiendelea kuwa karibu na Colin ili kujivuta karibu kwa kuamini baada ya kifo cha Cecy basi nafasi ile ni yake.

“Colin nina imani sasa hivi afya yako ni nzuri unaweza hata kuendesha gari.” “Namshukuru Mungu, pia nashukuru kwa msaada wako kwangu kwa muda wote wa kuniangalia.” ”Usijali nipo kwa ajili yako, nitapigania afya yako hata kwa gharama yoyote.”

“Usiwe na wasi nina imani sasa hivi sijambo na wiki ijayo nitakwenda India kumwangalia Cecy.” “Lakini hali yako si bado kwa nini usisubiri upone kabisa.”“Mage, mimi sijambo sasa hivi naweza kufanya lolote, lakini afya ya mpenzi wangu siijui. Mpaka leo bado yupo hospitali huenda yupo kwenye hali mbaya lazima niende nikajue hali yake.”

Itaendelea Jumamosi ijayo.
 
Back
Top Bottom