Godee jr
JF-Expert Member
- Apr 17, 2012
- 1,906
- 2,699
ILIPOISHIA:
Aliwaeleza hatua walizochukua tokea mwanzo kwa
wagonjwa wote na kufanikiwa kwa mmoja na
sehemu walipokwama na kuhitaji msaada wa
matibabu zaidi kwa mmoja nje ya nchi.
SASA ENDELEA...
Waliulizia kama kuna uwezekano wa mgonjwa
kupona, walijibu upo wa hamsini kwa hamsini.
Waliuliza gharama ya matibabu yote walielezwa
milioni ishirini na tano kwa awali kama itazidi
watajulishwa kwa vile mgonjwa hakuwa wa kutoka
mapema.
Walikubali kugharamia matibabu ya Cecy mpaka
hatua ya mwisho. Baada ya makubaliano, zilifanywa
taratibu zote za kumsafirisha mgonjwa na mtu wake
wa karibu.
Siku ya tatu, Cecy alisafirishwa pamoja na mama
yake kwenda India kwa matibabu ambayo wengi
waliamini madaktari wa Tanzania waliona aibu
kusema ukweli kuwa Cecy ameisha kufa
anachosubiri kupoa tu. Baada ya safari ya angani
Cecy alitua katika jiji la Mumbay na kupelekwa
katika Hospitali ya Apolo.
Alipokelewa mara moja alianza kupatiwa matibabu
kwa kuchukuliwa vipimo vyote ili kuangalia tatizo
lipo wapi. Baada kurudi majibu ya vipimo ilionesha
Cecy atapona lakini itachukua muda kurudi katika
hali ya kawaida kutokana na kupoteza kumbukumbu
kutokana na ubongo wake kucheza kidogo, lakini
alikuwa na bahati nzuri ubongo haukuvia damu.
Hali ya Colin iliendelea vizuri kwa kuimarika kwa
kasi kubwa tofauti na walivyotegemea. Baada ya
wiki aliweza kuzungumza vizuri na kuanza
kumkumbuka mpenzi wake Cecy. Wakiwa wamekaa
kitandani Colin alimuuliza mama yake.
Mama mbona simuoni Cecy wala mama yake leo
siku ya tatu?
Cecy alisafiri walifiwa na bibi yao kabla hujapata
ajali.
Mama ina maana nilipata ajali peke yangu?
Swali lile lilimchanganya sana mama yake
aliyeamini mwanaye baada ya ajali alipoteza
kumbukumbu na hakutaka kumshtua kutokana na
hali na mchumba wake ambaye aliamini aliondoka
mfu kwa asilimia tisini na tano.
Kwani unakumbuka nini?
Unajua mama nakumbuka wakati napata ajali
nilikuwa na Cecy tukitoka mazoezini na sababu ya
ajali ni Mage.
Mage? mama yake alishtuka.
Ndiyo mama.
Mage kasababisha kivipi?
Colin alimweleza tukio zima la ajali ilivyotokea
mpaka kupata ajali, baada ya kumsikiliza aliguna na
kusema:
Kwani Mage aliandika ujumbe gani?
Kwa kweli sikuuona bali usomaji wa Cecy
ulionesha ujumbe siyo mzuri.
Sasa wewe nini kilikupelekea kupata ajali.
Mama baada ya kumwangalia Cecy usoni moyo
ulishtuka na kujua hakuna tena usalama kwa vile
aliisha mshutumu Mage mapema baada ya hukumu
ya mchumba wake kabla ya simu na kutishia
kusitisha mkataba. Mage alinipigia simu na
kuzungumza maneno ambayo ni uchokonozi kwa
vile anajua kabisa nipo na nani.
Inaonekana alikuacha bado anakupenda ulikuwa
una hiyari kukubali au kukataa au hata kumfanya
spea taili.Mama Cecy ni kila kitu kwangu ndiye
mwanamke wa pekee moyoni mwangu sina nafasi
nyingine.
Lakini ulitakiwa kujua ameandika ujumbe gani
kabla ya kupagawa na kusababisha ajali mbaya.
Kwani gari limeharibika sana?
Limeungua lote na moto.
Mungu wangu na..na Cecy?
Naye alipata majeraha kama yako.
Yupo hapa hospitali?
Hapana yeye inaonekana alipata matatizo
makubwa na kukimbizwa India.
Maskini mpenzi wangu, Colin alishika kichwa kwa
mshtuko.
Lakini taarifa zinasema anaendelea vizuri, mama
yake alimpa moyo.
Hospitali natoka lini?
Wiki hii lakini utatakiwa kuja kila siku asubuhi
kufanya mazoezi ya viungo ili kuurudisha mwili
katika hali ya kawaida.
Nikijisikia vizuri kidogo nakwenda India kumwona
mpenzi wangu.
Hakuna tatizo tutakwenda wote, mama Colin
alimkubalia mwanaye kumpa moyo lakini aliamini
kabisa Cecy hakuna kitu siku zake zilikuwa
zikihesabika walichosubiri taarifa za msiba wake.
***
Mama Mage na mwanaye walikuwa wakizungumza
kuhusiana na hali ya Colin na mchumba wake.
Mama unafikiri mchumba wa Colin anaweza
kupona?
Mmh! Kwa kweli ni Mungu tu mwenye uwezo wa
kumponya, taarifa nilizopata kutoka kwenye
hospitali aliyokuwa anatibiwa kupona ni asilimia
ndogo na hata akipona bado hatakuwa sawa.
Kwa hiyo mama nina imani hii ni nafasi yangu ya
kurudi kwa Colin?
Ni nafasi yako kama ukiifanyia kazi bila hivyo
itakupita huku unaiona.
Sasa mama niifanyie kazi vipi au niende kwa
Karumanzila?
Si kwenda kwa Karumanzila bali kujipendekeza
muda huu wa matatizo kuonesha unamjali sana
Colin kwa kwenda asubuhi unarudi usiku
ikiwezekana ulale hukohuko.
Mama tena naondoka muda huu.
Mwanangu kijua ndicho hiki lazima uuanike sasa,
huenda Mungu alikuwa na kusudio lake la
kuirudisha ndoa yenu iliyoyeyuka kwa kifungo cha
Hans na kufa kwa Cecy.
Umeona eeh, mama utakuwa nabii kwa kuliona
hilo, japo siwezi kufurahi kwa matatizo ya Cecy
lakini kila kitu hupangwa na Mungu.
Halafu nimeambiwa Colin atatakiwa kila siku
asubuhi apelekwe hospitali kwa mazoezi, nataka
kazi hiyo uifanye wewe tena utachukua gari la
kifahari la kumpelekea hospitali.
Mama hilo si la kusema mbona kikohozi kimepata
mkohoaji nitahakikisha mahaba ninayompa
anamsahau marehemu wake(Cecy).
Baada ya mazungumzo Mage alimuaga mama yake
kwenda kumwona Colin nyumbani kwao ili
aurudishe ukaribu wao kutokana na matatizo ya
mchumba wake Cecy. Mage maombi yake alitaka
Cecy afie India, Tanzania urudi mwili tu usio na
uhai, aliendesha gari hadi nyumbani.
Itaendelea wiki ijayo!
Aliwaeleza hatua walizochukua tokea mwanzo kwa
wagonjwa wote na kufanikiwa kwa mmoja na
sehemu walipokwama na kuhitaji msaada wa
matibabu zaidi kwa mmoja nje ya nchi.
SASA ENDELEA...
Waliulizia kama kuna uwezekano wa mgonjwa
kupona, walijibu upo wa hamsini kwa hamsini.
Waliuliza gharama ya matibabu yote walielezwa
milioni ishirini na tano kwa awali kama itazidi
watajulishwa kwa vile mgonjwa hakuwa wa kutoka
mapema.
Walikubali kugharamia matibabu ya Cecy mpaka
hatua ya mwisho. Baada ya makubaliano, zilifanywa
taratibu zote za kumsafirisha mgonjwa na mtu wake
wa karibu.
Siku ya tatu, Cecy alisafirishwa pamoja na mama
yake kwenda India kwa matibabu ambayo wengi
waliamini madaktari wa Tanzania waliona aibu
kusema ukweli kuwa Cecy ameisha kufa
anachosubiri kupoa tu. Baada ya safari ya angani
Cecy alitua katika jiji la Mumbay na kupelekwa
katika Hospitali ya Apolo.
Alipokelewa mara moja alianza kupatiwa matibabu
kwa kuchukuliwa vipimo vyote ili kuangalia tatizo
lipo wapi. Baada kurudi majibu ya vipimo ilionesha
Cecy atapona lakini itachukua muda kurudi katika
hali ya kawaida kutokana na kupoteza kumbukumbu
kutokana na ubongo wake kucheza kidogo, lakini
alikuwa na bahati nzuri ubongo haukuvia damu.
Hali ya Colin iliendelea vizuri kwa kuimarika kwa
kasi kubwa tofauti na walivyotegemea. Baada ya
wiki aliweza kuzungumza vizuri na kuanza
kumkumbuka mpenzi wake Cecy. Wakiwa wamekaa
kitandani Colin alimuuliza mama yake.
Mama mbona simuoni Cecy wala mama yake leo
siku ya tatu?
Cecy alisafiri walifiwa na bibi yao kabla hujapata
ajali.
Mama ina maana nilipata ajali peke yangu?
Swali lile lilimchanganya sana mama yake
aliyeamini mwanaye baada ya ajali alipoteza
kumbukumbu na hakutaka kumshtua kutokana na
hali na mchumba wake ambaye aliamini aliondoka
mfu kwa asilimia tisini na tano.
Kwani unakumbuka nini?
Unajua mama nakumbuka wakati napata ajali
nilikuwa na Cecy tukitoka mazoezini na sababu ya
ajali ni Mage.
Mage? mama yake alishtuka.
Ndiyo mama.
Mage kasababisha kivipi?
Colin alimweleza tukio zima la ajali ilivyotokea
mpaka kupata ajali, baada ya kumsikiliza aliguna na
kusema:
Kwani Mage aliandika ujumbe gani?
Kwa kweli sikuuona bali usomaji wa Cecy
ulionesha ujumbe siyo mzuri.
Sasa wewe nini kilikupelekea kupata ajali.
Mama baada ya kumwangalia Cecy usoni moyo
ulishtuka na kujua hakuna tena usalama kwa vile
aliisha mshutumu Mage mapema baada ya hukumu
ya mchumba wake kabla ya simu na kutishia
kusitisha mkataba. Mage alinipigia simu na
kuzungumza maneno ambayo ni uchokonozi kwa
vile anajua kabisa nipo na nani.
Inaonekana alikuacha bado anakupenda ulikuwa
una hiyari kukubali au kukataa au hata kumfanya
spea taili.Mama Cecy ni kila kitu kwangu ndiye
mwanamke wa pekee moyoni mwangu sina nafasi
nyingine.
Lakini ulitakiwa kujua ameandika ujumbe gani
kabla ya kupagawa na kusababisha ajali mbaya.
Kwani gari limeharibika sana?
Limeungua lote na moto.
Mungu wangu na..na Cecy?
Naye alipata majeraha kama yako.
Yupo hapa hospitali?
Hapana yeye inaonekana alipata matatizo
makubwa na kukimbizwa India.
Maskini mpenzi wangu, Colin alishika kichwa kwa
mshtuko.
Lakini taarifa zinasema anaendelea vizuri, mama
yake alimpa moyo.
Hospitali natoka lini?
Wiki hii lakini utatakiwa kuja kila siku asubuhi
kufanya mazoezi ya viungo ili kuurudisha mwili
katika hali ya kawaida.
Nikijisikia vizuri kidogo nakwenda India kumwona
mpenzi wangu.
Hakuna tatizo tutakwenda wote, mama Colin
alimkubalia mwanaye kumpa moyo lakini aliamini
kabisa Cecy hakuna kitu siku zake zilikuwa
zikihesabika walichosubiri taarifa za msiba wake.
***
Mama Mage na mwanaye walikuwa wakizungumza
kuhusiana na hali ya Colin na mchumba wake.
Mama unafikiri mchumba wa Colin anaweza
kupona?
Mmh! Kwa kweli ni Mungu tu mwenye uwezo wa
kumponya, taarifa nilizopata kutoka kwenye
hospitali aliyokuwa anatibiwa kupona ni asilimia
ndogo na hata akipona bado hatakuwa sawa.
Kwa hiyo mama nina imani hii ni nafasi yangu ya
kurudi kwa Colin?
Ni nafasi yako kama ukiifanyia kazi bila hivyo
itakupita huku unaiona.
Sasa mama niifanyie kazi vipi au niende kwa
Karumanzila?
Si kwenda kwa Karumanzila bali kujipendekeza
muda huu wa matatizo kuonesha unamjali sana
Colin kwa kwenda asubuhi unarudi usiku
ikiwezekana ulale hukohuko.
Mama tena naondoka muda huu.
Mwanangu kijua ndicho hiki lazima uuanike sasa,
huenda Mungu alikuwa na kusudio lake la
kuirudisha ndoa yenu iliyoyeyuka kwa kifungo cha
Hans na kufa kwa Cecy.
Umeona eeh, mama utakuwa nabii kwa kuliona
hilo, japo siwezi kufurahi kwa matatizo ya Cecy
lakini kila kitu hupangwa na Mungu.
Halafu nimeambiwa Colin atatakiwa kila siku
asubuhi apelekwe hospitali kwa mazoezi, nataka
kazi hiyo uifanye wewe tena utachukua gari la
kifahari la kumpelekea hospitali.
Mama hilo si la kusema mbona kikohozi kimepata
mkohoaji nitahakikisha mahaba ninayompa
anamsahau marehemu wake(Cecy).
Baada ya mazungumzo Mage alimuaga mama yake
kwenda kumwona Colin nyumbani kwao ili
aurudishe ukaribu wao kutokana na matatizo ya
mchumba wake Cecy. Mage maombi yake alitaka
Cecy afie India, Tanzania urudi mwili tu usio na
uhai, aliendesha gari hadi nyumbani.
Itaendelea wiki ijayo!