"Niliendelea kuisoma ile barua
huku nikihisi kichwa changu
kizito,ganzi ikinijaa mwilini,kadri
nilivyokuwa naendelea kusoma
ndipo kizunguzungu kikanizidia..,
Ndio maneno ya mwisho ninayoweza kuyakumbuka kwani
nilivyoshikwa na kizunguzungu
wakati naisoma ile barua
iliyokuwa inaelezea kuvunjwa kwa
nyumba za mtaani kwetu huku na
nyumba yetu ikiwemo, ukijumuishwa na upande wa
nyuma kulipokuwa na kaburi la
marehemu Baba ukisisitiziwa
utabomolewa upande wote wiki
hii,ndicho kilichomuumiza na
kumliza sana Mama,na ilinifanya mwili wangu ujae joto
haraka,kuanza kutetemeka na
hapo hapo niliitupa ile barua
huku nikidondoka na kupoteza
fahamu..,
* * * *
"Yuko wapi Gervas..?"
Ndio neno nililoweza kulitoa
baada ya kuzinduka pale hospitali
Juhuku nikishangaa nimetundikiwa
dripu na kujua kuwa kumbe zile
zote zilikuwa ni ndoto na hisia za ajabu eti mpaka napelekwa
mahamakani,Nikakutana na 'Baba
Pendo' na kuanza kumlilia kuwa
sijaua,
"Ooooohhh...! Uuuuuuuuhhh..!
Mungu waaaaangu..! God forbid.....!"
Nilijikuta nalitoa hilo neno la
kiingereza japo sikuwa najua
maana yake kwani nilimsikia mara
nyingi Afande Deus analitumia
anapokabiliwa na matatizo,huku kichomi kikinizidi kuniuma na
kupumua haraka zaidi..
Kucheki pembeni yangu
nikamshuhudia Mama akiwa
amenishikilia dripu tena akiwa
bado machozi yakimlengalenga kuonesha kuwa bado analia huku
akinitazama..
"mwanangu...! nisamehe mimi...!
mwanangu...! Najua mimi ndo
chanzo cha yote hayo...!
"Najuta kukuonesha ile barua....!" "Hapana Mama kwani mbona
mimi mzima tu....!"
Nilimjibu Mama bila ya kuwa na
wasiwasi wowote huku nikijiamini
mimi ni mzima tu,
"Usilie mama...." "Hapana mwanangu....
Daktari amesema kuwa u..."
* * * * *
Juhudi za afande Deus kumtoa
Gervas katika kituo cha Polisi pale
ubungo zilifanikiwa kwani alikuwa
akiheshimika na kufahamika hivyo
alijitahdi kumtetea Gervas kwa kila
njia mpaka akafanikiwa lakini ilikuwa kwa masharti kuwa Gervas
hatakiwi kabisa kuönekana Dar es
salam na Tanzania kwa ujumla
kwani kuonekana kwake
kutamletea matatizo makubwa
Levina ikiwa ni pamoja na kuwekwa Gerezani tena kwa mara
ya pili,hivyo
Afande Deus alichokifanya ni
kumchukuwa Gervas moja kwa
moja mpaka kwa wazazi wake
kisha kuwapa masharti aliyopewa baada ya kuafikiana wazazi wa
Gervas wakahaidi kumtorosha
Gervas na kwenda kuendelea
masomo yake nje ya nchi,
Mwanzoni Gervas hakuliafiki
kabisa na yote hiyo ni kotakana na kumpenda sana Levina kutoka
moyoni,lakini baada ya wazazi
wake kumsema sana ikabidi
wakubaliane tena kishingo
upande kuwa ataondoka tu haina
jinsi, Walienda nyumbani kwa kina
Levina asubuhi asubuhi lakini
waliwakosa hivyo Afande Deus
akampigia simu Mama Levina na
kuambiwa kuwa Levina kalazwa
na wapo hospitali ya 'Ocean Road'..
* * * *
......Kabla Mama hajamalizia
kuongea Mara akaingia Afande
Deus akiwa na Gervas pamoja na
Wazazi wa Gervas..
Nilijihisi nimepona pale kitandani
lakini kila nikitaka kunyanyua mkono niinuke nilishindwa,
"Nesi...! Nesi..! Nesi....!"
Msaada hapa....!, Msaada Nesi...!"
Ilikuwa ni sauti ya Mama
iliyokuwa ikiomba msaada kwa
Nesi aje kwangu kunisaidia.., Nikashuhudia Nesi akija haraka
kunihudumia huku akiniinua
mgongo..,
Kisha akamwambia kitu afande
Deus na Mama..
"Huyu mnyanyueni taratibu,kwani upande huu wote wa kushoto
haufanyi kazi kabisa..,
Hapo hapo Halmashauri yangu ya
kichwa ikagundua moja kwa moja
neno la mwisho alilokuwa
anataka kuniambia Mama kabla afande Deus hajaingia ilikuwa ndo
hilo kuwa nimepooza upande
mmoja.,
Nilijikuta kama mtu asiye na
bahati hapa duniani ikabidi
nikabiliano nayo, "Pole Levina utapona usijali..."
Sauti ya chinichini tulivu
iliyopenyeza kwenye maskio
yangu ikitokea kwa Gervas huku
akionesha kuwa anahuzuni sana
machoni, "Nakupenda Gervas....!"
"Nakupenda pia Levina..!"
Bila kuonesha woga wowote
kutoka kwa wazazi wa Gervas na
kwa kujiamini niliweza kuiona
mikono ya Gervas ikinipapasa katika mkono wangu mmoja kwa
kuteleza nikibaki namtolea jicho
la aibu kisha akashika ile dripu
huku akiugusa kwa kuupapasa
ule mrija wa kupitishia damu na
kuanza kutoa mchozi huku akiniangalia kwa huruma,Haraka
pale nikashtuka kwa msisimko
uliokuwa unaendelea kisha
Nikabadilisha mada kwani afande
Deus alikuwa akinitolea macho
sana... "Vipi mmeshayamaliza huko
Polisi..,
Kabla hajanijibu Gervas
nikamwona Nesi ameshawasili
kwenye wodi niliyolazwa na
kuwafukuza watu lakini sura ya huyu Nesi haikuwa ngeni machoni
mwangu ila sikuweza kuwa na
kumbukumbu vizuri kutokana na
fahamu kutonirudia vizuri na kwa
haraka...
"Jamani wapendwa mda wa kuona wagonjwa umeisha...,
Tunawaomba muondoke sasa ni
zamu ya daktari kuja kumtibia
mgonjwa wenu.."
Iliongea kwa ukali tena mara mbili
mbili ile sauti ya Nesi wa zamu aliokuwa amevalia mavazi rangi ya
machungwa.,
"Levina..,Ugua pole, Jioni tutakuja
tena kukutembelea na kukuletea
chakula..."
"Haya...,Ahsanteni" Nikawajibu wazazi wa Gervas na
afande Deus kwa sauti ya upole
kwani hata na sauti yangu
ilishindwa kabisa kutoka..
kisha hao wakaondoka huku
Mama akiwatoa nje na kuniahidi kuwa kesho asubuhi watakuja
tena kunitembelea..
* * * *
Mpaka kufika saa Kumi na Mbili
jioni hakuna mtu yoyote aliyekuja
kututembelea hivyo Mama
alinilazimisha kula chakula (mtori)
kile cha mchana nilichokuwa
nimewekewa katika hotpoti nikala na kupumzika,
Sikuweza kupata usingizi
kabisa,sauti tulivu za ndege kwa
mbaaali na mlio wa maji ya bahari
niliyokuwa naiskia kutoka nje ya
hii hospitali ya 'Ocean Road' ndo kati ya vitu vilivyochochea hisia
zangu za mimi kuanza kupata
usingizi taaaaratibu,
Hata hivyo ilipotimia saa saba za
usiku usingizi ulikuwa tayari
umeshaanza kunipitia huku Mama yangu akiwa amejiegesha
upande wa pembeni yangu
akiniangalia kwa msaada,
Kitanda cha pembeni yangu
kulikuwa na mgonjwa aliyekuwa
analia sana huku akihitaji msaada wa Nesi,Punde yule Nesi aliwasili
na ni yule niliyemwona mchana
na ndiye aliyewaondoa kwa mara
mwisho wakina Gervas hapa
hospitalini,
"Nimeshamkumbuka huyu mshenzi...! Nilishaweka ahadi na
kuapa lazima nimteketeze huyu
mtu...!"
Hasira zilinijaa sana kwani
sikuamini kuwa huyu Mama
atakuwa Nesi? "Ina maana siku zote ni Nesi..?
Mungu wangu nani aliyempa
kazi...?"
Ni kati ya maswali yaliyonishtua
baada ya fahamu kunirudia vizur
na kugundua kuwa huyu alikuwa ni yule Mama aliyenifanya mpaka
nimekuwa hivi,yule ambaye
nilikuwa namuota ovyo kwenye
matukio mojawapo lile la
kumnyonga na mtandio,na hata
juzi nilivyoenda kumpokea Gervas tulipanda naye dalalada japo
sikumgundua vizuri mpaka
alipovua baibui yake tena kwa
mbali ndo nikawa nimemgundua..
Kila nikimwangalia pembeni
yangu ndivyo hasira ilinizidi kuninyemelea akilini mwangu
kwakuwa nilikuwa sina nguvu
tena upande mmoja kwa kupooza
nilijikuta naropoka kwa sauti ya
chinichini bila yeye kusikia..
"Unabahati sana nimepooza...kwani ilikuwa ni
safari yako sa hivi..."
Kisha nikajiegemeza taratibu
kutafuta tena usingizi,
Baada kama ya nusu saa usingizi
ukawa umenipitia na kilichokuja kunishtua ni Mkojo uliokuwa
umenibana ukiambatana na haja
kubwa pia nilikuwa najisikia
kizungu zungu sana huku
kichefuchefu kikinishika niliweza
kumwamsha Mama na kumuelezea ikabidi amuite Nesi....,
Alitoka na kwenda mbio na
kumuita Nesi, Punde akarudi
naye,
"Hata kama naumwa....,lazima
nikumalize..., Mmbeya mkubwa wee...!"
Niliongea taratibu na kuachia
fyonyo kali huku nikimwacha yule
Nesi pamoja na Mama wakishtuka
na kushangaa wasielewe
imekuwaje pale, kilichofuatwa yule Nesi
alichukuwa kibaiskeli cha
kupakizia wagonjwa na
kunichukuwa tukatoka wote kwa
pamoja na Mama lakini tulipofika
mlango wa chooni nilimsikia yule Nesi akimwambia kitu Mama...
"Mama...! Mama....! wewe
usisumbuke huyu wacha niingie
naye nimhudumie mimi tu..!"
"Hapana Mama twende wote...!"
"Levina acha ubishi..! Hata huyo atakusaidia tu kama mimi..!"
Nilimbishia Mama kwani niliamini
kabisa yule Nesi tayari alikuwa ni
adui yangu na anaweza
kunidhuru...
Basi tukaingia chooni kisha yule Nesi akafunga mlango kwa ndani
kwa kutumia ufunguo huku
tukimuacha Mama nje
akitusubiria..
"We muuaji upo..? !...Umetoka
gerezani lini..?" Alianza kuongea kwa dharau
huku akinibenulia mdomo wake
lakini mimi
Nilikaa kimya huku nikimwangalia
yule Nesi akichomoa dripu ili
aweze kuniinamisha choöni niweze kujisaidia..
".....Kama uko gerezani
walikuacha leo mi sikuachi......!"
"....kwani nimefanyaje...?"
"..Ssshhhh...! We si Levina yule
muuaji aliyewekwa gerezani miaka kama sita au saba iliyopita...?"
"Aaaahhh....! Aaaaaahh....!
Si...o..o..o.. mi..m..i.."
Nilimjibu kwa kujiuma uma kisha
nikashangaa kitendo
kilichofanyika pale kwani alichukuwa kichwa changu
akaniinamisha kwenye tundu la
choo tena kile choo cha kuflashi
kwa mda mrefu..,
Nilishindwa kuongea chochote
kwani sura yote ilikuwa imeinama kwenye tundu la choo, sikuwa na
nguvu kwani upande wangu
mmoja ulikuwa umeshapooza,kwa
lile tukio nilijikuta natoa haja
kubwa na ndogo papo hapo...
"Nyoooooo...! Ushajinyea enhh..? Maana harufu ya kinyesi chako
kishaanza kunuka tena
sanaaaaaa.."
Aliongea kwa sauti ya chini chini
ambayo mtu yeyote hawezi
kuisikia kisha akanivua nguo yangu ya ndani ambayo ilikuwa
tayari na kinyesi na kuitupia
kwenye tundu la chooni likawa
limetapakaa kile kinyesi changu
kisha kabla hajaflashi akinikamata
shingo tena kwa nguvu na kuniinamisha tena kwa mara ya
pili chooni, maskini Levina mimi
nilijikuta nakutana na kinyesi
changu,huku nikikosa pumzi
nilijikuta naachia mdomo wazi
hivyo mdomo wangu ukakutana na kinyesi changu
mwenyewe,nilikuwa sina jinsi zaidi
ya kujikuta nikikimeza,
Alinifanya atakavyo kisha akaflashi
kile choo huku kichwa changu
kikiwa bado mule ndani ya choo,nilitapika sana,maskio
yaliziba kwa mda na macho
yakawa kama kipofu kwani
sikuweza tena kuona mbele kwa
mda ule zaidi ya kuhisi bado
nimekabwa shingoni.., ".....Bado hujafa tu....!"
"Utakufa wewe......! sio mimi....!"
Nilimjibu kwa hasira ya hali ya juu
huku nikizidi kumchochea na
kumjaza hasira tena yule Nesi
akiendelea kunitolea mimacho.. "..Unajifanya mbishi
enh...? ...Hapa nakutoa maiti tu
nampa Mama yako akakuzike
muuaji mkubwa wee..."
Ghafla nikamshuhudia yule Nesi
akiingiza mkono kwenye mfuko wa gauni lake na kuchomoa vile
Visu vidogo vikali vya kufanyia
operesheni na kuanza kukata
kata mirija ya ile dripu ikaanza
kuvuja kisha akaniangalia usoni....
"Embu niambie wewe Muuaji nikuanze wapi...? Halafu uanze
kusali sala zako za mwisho
hapahapa...!"
"Tuuuhhh.....! Tuuuuhh...!
Nikamtemea mate usoni mwake
kwani nilikuwa sina nguvu za kumpiga, akakasiria na kunitoa
kwenye kile kigari..
"Haya simama tupigane sasa...!
Simama wewee..!"
Alinitoa kwenye kigari akinitaka
nisimame,sikuweza kusimama kwakuwa nilipooza upande
mmoja hivyo nikadondoka moja
kwa moja mpaka chini huku
nikiwa uchi wa mnyama..
Alichoanza kukifanya ni
kuchukuwa miguu yangu miwili na kuitanua,kisha akiwa kashikilia
viwembe vyake tayari alikuwa
amenishika matiti yangu na
kutaka kuyakatakata..,
Akiwa anataka kunikatakata na
vile viwembe mara Mama akaanza kugongo hodi kwa nje..
"Nesi...! Nesi...! Nesi...!Bado
hamjamaliza tu..! Levina....!
Levina...! Levina....! Mwanangu...!"
Nilitamani niitike lakini tayari vile
viwembe vilikuwa mdomoni mwangu.,
"Ole wako uitike...! Nakuchana
chana sasa hivi..!"
"..Namvalisha Mama tunatoka
sasa hivi...!"
Aliongea kinafki yule Nesi huku akinivalisha haraka haraka kisha
vile viwembe akavitupa kwenye
tundu la choo naku flashi..
Alinitoa pale nikiwa sijielewi ila
ninachoweza ni kutoa macho na
kusikia sauti kwa mbaaali sana, huku yule Nesi akinikokota na
Mama mpaka wodi yangu
wakanilaza,
Baada ya mda kidogo nikaanza
kusikia sauti kwa mbali ya
minong'ono nilihisi tu atakuwa ni Mama na Nesi wakizungumza..
"Yani Mama..Mtoto wako
alinisumbua sana kule chooni..!,
haswa pale alipohtaji kujisaidia
kwani ilikuwa ndo mara yake ya
kwanza ndo mana tukawa tumechelewa kutoka..!"
"Usijali mwanangu...asante kwa
msaada wako Mungu
atakubariki...kaendelee na kazi
tu...!"
Nilitamani niropoke pale pale lakini sikuweza kumuonesha wazi
Mama kama namchukia sana
huyu Nesi pia kwa vitendo
alivyonifanyia..
Sikuweza kupata usingizi kabisa
zaidi ya kutoa macho mpaka alfajiri kulipopambazuka na
kumshuhudia Gervas akiwa mtu
wa kwanza akiingia pale wodini..
"Shikamoo Mama..!"
"Marahaba mwanangu Mama na
Baba umewaacha wazima..?" "Wazima tu Mama"
Taratibu Gervas akaweka ule
mfuko aliokuja nao ukiwa na
chupa ya chai na ki hotpoti
kidogo japo sikujua ndani yake
kunanini..,kisha Gervas akanisogelea kitandani na
kuongea na mimi huku akitokwa
na machozi..
"vipi unajiskiaje Levina toka
tulipokuacha...!"
Sikuweza kumjibu kwani sauti ilikauka nikabaki machozi
yakinichururuzika mithili ya maji
ya sabuni yakiteleza mwilini,
"Levina...! Levina....! Naomba japo
nisikie sauti yako jamani...!"
Nilipenda sana nimuitikie Gervas nakuongea naye lakini
ilishindikana kwani kitendo
alichokuwa amenifanyia yule nesi
kilinifanya nishindwe kufanya
lolote., * * * *
~ NYUMBANI KWA KINA GERVAS
~
Wazazi wa Gervas hawakulala
walifanya juu chini kuhakikisha
Gervas anaondoka, mchana wa
jana yake uleule waliotoka
hospitalini walianza kufanya
mipango na watu wa uhamiaji kwa ajili ya kumhangaikia pasipoti
yeye Gervas na Baba
yake,kwahiyo leo watachukuwa
pasipoti zao na ndani ya siku mbili
watakuwa wameshapata Viza ya
kuingia Marekani.. Gervas alijitahidi sana kufanya kila
liwezekanalo awe amemuweka
Levina wazi lakini haikuwezekana
kutokana na hali aliyomkuta nayo
Levina..
~ HOSPITALI ~
Kweli hujafa hujaumbika mpaka
leo siku ya pili na sasa hivi jua
linaelekea kuzama hakuna hata
ndugu yeyote aliyekuja
kunitembelea zaidi ya Gervas na
Mke wa Afande Deus kuja kuniletea chakula,Nilijiona tangu
matatizo yangu ya jela ukiongezea
na haya yamenifanya nitengwe na
ndugu mpaka baadhi ya Majirani..
"Kwanini ni mimi na mama yangu
tu....! Kwanini wanatunyanyapaa kama wagonjwa wa ukimwi....?"
Hayo maswali niliojiuliza
yalinifanya hata nishindwe kupata
chakula kwani hasira iliniongezeka
maradufu na kubaki namuangalia
Mama huku mchozi ukinidondoka taratibu..
"Kula basi mwanangu upate
nguvu....!"
Niliitikia kwa kutikisa kichwa
nikimaanisha siwezi kula kwa mda
ule lakini alinielewa... "Kunywa basi angalau uji wa ulezi
umechanganywa na maziwa ni
mtamu sana mwanangu....!"
Nilikubali aninyweshe ule
uji,nilikunywa japo taratibu
sana..,mara nikatapika uji wote..,niliumia sana kwani
Nilimuona yule Nesi mbaya
wangu na ndio aliyenifanya
nitapike,haraka haraka akaja...
"Ooohh...! Pole mgonjwa enhh...!
Mama embu lete huo uji nimmnyweshe mwenyewe...!"
"Chukuwa mwanangu labda
wewe kwakuwa Nesi atakubali
kunywa bila hata kutapika....!"
Kila nilipotingisha kichwa
nikionesha kukataa Mama hakunielewa,akamkabidhi yule
Nesi kibakuli cha uji kikiwa na
kijiko aninyweshe...
"Nesi...! Nesi...! Ngoja niende
uwani nikajisaidie,nakuomba
uendelee kumlisha huyu... "....Usijali Mama....! Haya Levina
kunywa uji basi...!"
Nilijikuta nakunywa ghafla
nikamtapikia yule Nesi kwa
makusudi huku akibaki kakunja
sura yake.... "Unajifanya mjanja siyo....?"
Akaingia kwenye mfuko wa gauni
lake na kuchomoa sindano kisha
nikamuona akiichanganya kwenye
kichupa kidogo...
Nilikuwa niko tayari kwa lolote,sikuweza kufanya chochote
huku nikibaki nguvu zikizidi
kuniishia...
"Haya chagua sasa nikuchome
wapi wewe muuaji...!"
Nilibaki kimya,mara nikasikia sauti...
"Nichome mimi tafadhali..!"
Alidakia yule mgonjwa aliyekuwa
amelazwa pembeni yangu na yeye
hakuwa na msaidizi nadhani
alikuwa katoka au hayupo kabisa, lakini sikujua kwanini amesema
vile...
"Huyo hana hatia...njoo kwangu
unichome nife...! Njoo...! Njoo...!"
Kabla hajamalizia kusema
nilishuhudia yule Nesi akimrukia yule mgonjwa na kumchoma
sindano ya shingoni halafu
akamfunika mpaka usoni...
* * * * *
Haikuchukuwa mda mrefu Mama
akawa amerejea pale huku
akimkuta yule Nesi anajiandaa
kwa ajili ya kuondoka,
"Mgonjwa wako mwenyewe
kagoma kunywa uji...!" Akiwa anageuza na kuondoka
zake yule Nesi mara...
"Nesi...! Nesi..! Nesi...!
...Samahani msaada pale kwenye
kile kitanda yule mgonjwa pale
anaonekana anatapatapa pliz kamsaidie Nesi....!"
Haraka haraka yule Nesi
akamfata na kumshika kifuani
kisha akafunika mwili wote..
"Hatunaye tena...! Mungu ailaze
roho yake mahali pema peponi Amina...!"
Aliongea yule Nesi huku akikimbia
eneo lakutokea na baada ya mda
nikamwona akirejea na wenzake
huku wakibeba kitanda cha
kubebea maiti wakaichukuwa ile maiti na kuondoka nayo...
"Maskini mimi Levina...ilikuwa
mimi ndo nife..!"
Nilijisemea kimoyomoyo huku
nikimwangalia mama yangu
akimwaga mchozi kwa kumlilia yule mtu aliyekufa...
Niliogopa sana ilipofika usiku tena
kila nikijifikiria kuhusiana na yule
Nesi kwa jinsi alivyomkatili,
Hatimaye usiku ukawa,kwa kuhisi
ingeweza kuwa imeshafika kwenye saa Nne kwani mama
alianza kujikunyata kuashiria
ananisubiria nilale naye apate
japo kausingizi...
Nikiwa na mawazo tele huku
nikimuangalia Mama akiwa kachoka sana nami nilijikuta
napitiwa na usingizi.,kitu
kilichokuja tena kunishtua usiku
ule ni kama mtu niliyemhisi kama
ananyata,niliogopa sana na kila
nilipojitahidi kuvuta mkono wangu wa kulia japo Mama ashtuke
haikuwa hivyo kwani Mama
alikuwa amelala fofofo,yule mtu
alipofika karibu yangu
akaninong'oneza karibu na sikio
langu la kulia... "Nimekuja kukuua wewe...!"
"Hivi nimekufanya nini we
Mwanamke...?"
Kwa mara nyingine nilijikuta sauti
yangu imeweza kutoka..
Mara yule Nesi akavuta mto niliokuwa nimejiegemeza nao na
kuuchukuwa kisha akanifunika
usoni kwa nguvu akaniziba usoni
huku akinibana kwa nguvu zake
zote...
Nilijihisi vichomi mwili mzima vilivyoambatana na mafua ya
ghafla kutokana na kukosa
pumzi...Nilitapatapa japo upande
mmoja ndo ulikuwa
mzima,nilitumia upande wa kulia
ambao ulikuwa haujapooza,mpaka nikafanikiwa
kudondosha dripu ndipo Mama
akashtuka..,
"Vipi tena Nesi...!"
"Hapana Mama namsaidia
kumwekea dripu sawa kwani iliachia hivyo ikawa haitembei...!"
"...Ooohh Mungu wangu...!
Ahsante sana Nesi kwani nilipitiwa
na kausingizi kabisa,nisamehe kwa
hilo...!"
"...Usijali Mama na wala usiwe na wasiwasi nipo kwa ajili ya kazi
hiyo...!"
Maneno waliokuwa wanaongea
kati ya Mama na yule Nesi
hayakuniingia akilini hata kidogo
kwani baada ya Nesi tu kuondoka...
"Mama pliz...! Iwe isiwe..! Utake
usitake...! Nakuomba asubuhi
nirudi nyumbani hapa hakunifai
Mama...! Nitakufa Mama si kuzuri
hapa kabisaa Mama...!"
~ SAFARI YA NYUMBANI ~
Alfajiri na Mapema Mama
hakutaka kupoteza mda akafanya
njia zote nikakubaliwa kutoka
pale hospitali lakini ilinibidi nitoke
na kigari cha wagonjwa na
kwenda kumalizia kutibiwa nyumbani kwa kuwa nilikuwa
nimepooza tu pia kuwa na
gharama kubwa ambazo Mama
asingeziweza nazo zilichangia
mimi kutoka pale hospitali
haraka... Mama alikodi taxi yakutupeleka
nyumbani na kabla hatujaingia
maeneo ya nyumbani hofu ilianza
kunitanda na kila nikimwangalia
Mama naye alikuwa anatetemeka
huku akifungua pochi na kumlipa dereva teksi shilingi elfu kumi..,
"Mungu wangu nini tena hiki..."
"Kwani ni nini Mama..?"
"Levina....! Tumekwisha Levina....!
Tumekwisha mwanangu...! Na
hatuna mtetezi kwa hili tena...! .....Levina
Mwananguuuuuuuuuu....!" ************************ * * *
Je.,Levina na Mama yake
wamekutana na nini? * * * Levina anajua juu ya Mauaji
yaliyofanywa na Nesi, nini hatma
yake yule Nesi...?
Itaendelea Usiku