Ilipoishia...
Mara nikaona karatasi pale
Mezani imefunikwa kwa hofu
niliyokuwa nayo nikaiwahi haraka
haraka kwenda kuichukua lakini
kabla sijafika pale ndo nakaribia
tu mara..
'
Endelea.....
Nikasikia kama sauti ya mtu
anabisha hodi,haraka haraka
nikaikodolea saa yetu ya ukutani
ikanionesha ni saa Tisa na robo
usiku, nikawa najiuliza.,
"....Huyu ni nani anayebisha hodi sa hivi..!"
Sikuitikia ile hodi nilichokifanya
nikaichukuwa ile karatasi na
kuanza kuisoma.,
"...MWANANGU WA PEKEE
LEVINA, KWANINI UNATAKA KUNIUA BILA YA KOSA
LOLOTE?.., NIMEHANGAIKIA
MAISHA YAKO KWA MDA
MREFU MPAKA
SASA.,NIMESIKITIKA SANA
KUKUTA TIKETI YA NDEGE CHUMBANI KWAKO NA SAFARI
NI KESHO,BILA HATA
KUNIAMBIA CHOCHOTE
MWANANGU..?MPAKA
NIKAAMUA KUCHUKUWA
UAMUZI HUU WA KUJIUA NITANGULIE MBELE YA HAKI,
NAKUTAKIA MAISHA MEMA,
Mimi MAMA YAKO,
Mama Levina."
"..No..! No..! No..! Mama..!
Kwanini umewahi kufanya hiivyooo...!"
Nikajikuta nauvua moyo wa
kikatili na kuanza kumuonea
huruma tena Mama huku
nikielekea mlangoni kwa yule mtu
aliyekuwa anabisha hodi, "...Hapa mezani nimekuta kikopo
cha sumu ya panya na hii
karatasi, yeye Mama atakuwa
wapi sasa..?"
Kabla sijaufungua mlango
nikalipenyeza jicho langu kwenye tobo la kuwekea ufunguo.,
"...Mungu mkubwa.,huyu ni
Mama yangu kabisa, ona na
kanga nilizomnunulia kipindi
kileee ni hizi hizi...!"
Sikutaka hata kuuliza ni nani kwani sauti nilikuwa siiskii lakini
kwanilivyokuwa nimemchungulia
dhahiri atakuwa ni Mama yangu,
"..Itakuwa alienda chooni kipindi
kile nilivyoenda chumbani..? Lakini
ile sumu na barua kwanini aliamua kuandika vile..? Inamaana
anajua picha lote
litakavyokuwa....?"
Ni kati ya maswali niliokuwa
nikijiuliza bila kupata majibu
kwani ni kweli choo chetu kimejengwa nje ya nyumba na
yule niliyemchungulia ni Mama
yangu kabisa.,
Nikachukuwa vile vitu nilivyokuwa
nimeshika ambavyo ni kamba
kubwa nene pamoja na Panga kisha nikavitupia uvunguni mwa
kochi ili Mama asijue lolote kisha
nikarudi pale kwa ajili ya
kumfungulia.,kadri nilivyokuwa
nashika kitasa ndivyo nilikuwa
naona mlango unazidi kuwa mgumu nikausukuma kwanguvu
kuelekea ndani nilipo, mara
nikasikia kishindo cha mtu
amedondoka mbele yangu,
"...Mamaa...! Mamaa...! Ni wewe
Mama.....!" Niliugeuza ule mwili nakuanza
kuutingisha maskini ni kweli
alikuwa Mama japo Mwili ulikuwa
umeshabadilika na kuwa mweusi
kama mkaa,huku damu yake
ikibadilika na kuwa maji kama kamasi ikiteleza kutokea
masikioni,puani na Mdomoni,
Ngozi yake ilijikunja sana lakini
halmashauri yangu ya kichwa
ikafanya kazi fasta na kujua kuwa
huenda alikunywa ile sumu kidogo halafu akaenda chooni
wakati anarudi ikamzidia.,
Bila kupoteza mda nikauvuta ule
mwili nakufunga mlango kwa
ufunguo halafu nikamburuza
mpaka sebuleni kisha nikaingia chumbani na kutoa Biblia.,
"Eeeh Mungu Baba muweza wa
yote...! Natubu mbele za haki
najua kama mimi ni Mwana
mkosefu kwa kitendo nilichofanya
na nitakachoendelea kukifanya ila naomba kusamehewa...Amina.."
Nilipomaliza nikaingia chumbani
kwangu na kuchukua Gunia
kubwa na koleo kisha nikalipitia
lile panga pale uvunguni sebuleni
na kuuburuta ule mwili kuelekea nje ya nyumba yetu,nawaombeni
sana wasomaji mnisamehe kwa
nilichokifanya mbeleni,
Nikauburuta ule mwili mpaka
karibu na eneo lilipokuwa na
kaburi la Baba,nikaulaza na kuchukuwa panga langu kisha
nikaanza kutenganisha upande
mmoja mmoja nikianzia na
mikono,Shingo na miguu yote
miwili hakika sikuwa levina yule
mlokole bali nilikuwa Levina Mkatili tena mnyama kama simba
Dume tena yule anayoogopewa
na kila mtu duniani.,Nilichana
kitambaa cha nguo yangu na
kujifunika usoni kisha nikaanza
kumkatakata Mama eneo la usoni ili nipoteze ushahidi kama ikija
kujulikana,nahisi damu ilikuwa
imeganda kwani sikushuhudia
hata chembe ya damu ikimtoka.
Nilipomaliza nikachukuwa viwiliwili
nikaanza kudumbukiza kwenye ule mfuko kisha
Nikachukuwa koleo nakuanza
kuchimba kashimo kadogo kwa
ajili ya kumfukia ili niendelee
kupoteze ushahidi kabisa, nikiwa
ndo namalizia kuchimba mara simu yangu ikaita,
"...haloo..! Aaah Gervas"
"...enh Mmefikia wapi..?"
"...Mama tayari nimemwacha na
mtu na keshokutwa safari
itakuwepo usijali mpenzi wangu..!" "...Okey, msalimie sana Mama
yako mwambie bado
namkumbuka na kuna zawadi
yake tayari nimemwandalia..,"
"...Usijali Gerva,amekusikia..!"
Nikakata simu nakumalizia kuchimba pale fasta fasta
nilipomaliza nikashindilia na
kokoto zilizokuwa karibu.,kisha
nikaingia ndani kwa mbwembwe.
"...Zoezi la kwanza limeisha na
bado Mama yake Gervas, atanitambua huko tunapoenda..!"
Nilijisemea kimoyo moyo huku
nikijiamini kwa kile nilichokifanya
mda si mrefu,nilipofika sebuleni
nikapiga magoti na kuomba tena.,
"...Najua jamii yote itachukizwa nami, lakini mtetezi wangu ni
wewe Baba uliye juu mbinguni..,
Eeeh mwenyezi Mungu mlaze
Mama yangu Mahala pema
peponi,Amina.."
Nilipomaliza kusali tu ghafla nikaanza kujihisi mabadiliko
makubwa kwenye mwili wangu
sana sana eneo la tumbo, niliumia
sana,nilijikaza bado ikawa haisaidii
uchungu ulinizidia mpaka nikajihisi
mimba inataka kuchomoka,nilishindwa kuvumilia
nikaanza kugala gala pale chini
lakini nikawa kama ndo
nalichochea tumbo liendelee
kuuma,miguu ikavimba kwa
haraka nikawa najiburuza sasa kuelekea chumbani..,kwa
maumivu yaliokuwa yamenizidia
mpaka nikajikuta nimeingia
chumba cha Mama ambaye tayari
nimeshamuua,kwa kujikokota
taaratibu mpaka eneo la 'dressing tebo' huku nikitafuta dawa yeyote
ya kutuliza maumivu,nikajishikiza
kwa mkono mmoja huku mkono
mwingine ukiwa unafungua droo
za lile 'dressing tebo'..
"....Mamaaaaaaa..! Mamaaaaaa...! Mamaaaaa...! Mi sijakuua Mama
ulikunywa sumu mwenyewe
Mama...!"
Sura yangu ilikuwa imekutana na
kioo cha ile 'dressing tebo' ghafla
ikatokea sura ya Mama katika kile kioo, Nilichanganyikiwa na kujiona
zaidi ya kichaa kwani usiku ule ule
nilitokomea kusikojulikana huku
nikiwa mtupu nimevalia 'nait dres'
na nywele zikinivuruga,
Kulipokucha asubuhi kila mtu alikuwa akinishangaa kwani
nilikuwa tayari majalalani
nikiokoteza vyakula vichafu,
ukinisogelea utakuwa unatafuta
balaa na Mimi kwani nikaa si
Levina tena., "Ng'aaam...! Ng'aaam..! Piiiiiipi..!
Pipiiii...! Oya pisha njia gari inakasi
hiyo we fala nini..? Embu pisha
nitakuitia Mama yangu aje
akugonge..?"
Nilikuwa tayari chizi kwani Mikononi nilikuwa nimeshika
mifuniko ya ndoo huku
nikiendesha kama gari nazunguka
zunguka wapita njia
wakinishangaa..
"...Gervas panda twende wewe...konda wadai nauli haoo..!"
Uchizi wangu uliendelea na
ilipofika mda wa usiku sana,Vijana
kama sita hivi nafikiri walikuwa ni
majambazi kwani walikuwa na
makoti makubwa huku wamekunja sura zao walipita
eneo nililokuwa nimejibanza na
kujikunyata pale jalalani.
"....Oyaa masela eenh..!"
"...washkaji huyu chizi vipi..,embu
mchekini..!" "...Oyaa hapa si Marekani.?"
"...Fala nini..?"
"...Masela mi nina nyege sana
kama vipi njooni basi..!"
Niliwaita wakanifanya kitendo
kibaya wote wale huku nikifurahia kwa kile kitendo.
"...kama vipi na kesho mje basi..!
Au siyo masela..?"
Nikatoka eneo lile nikiwa na
mimba yangu huku nikijitembelea
kusiko julikana usiku ule, hata nilipowaona polisi sikuogopa
kabisa,
"...We binti chizi nini? Unafata nini
hapa Polisi..?
Nilijikuta nimeingia kituo cha polisi
huku nikiwa sina hata chembe ya woga..!
"...Kwani masela nyie vipi? Mi
muuaji Mmesikia..? Mimi ndo
niliomuua Baba Ali, Pendo na
hata Mama yangu nimemuua
mimi..!" "....Afande John, unarisikia hiri
ritoto rinavyoropoka..? Binti
unaitwaga rinani?"
"...Mi naitwa Levina.,oyaa kwanza
nipe bangi nitoe stimu..!"
"...Haroo hiri siro ri revina tunaroritafutaga..?"
"...Hamuwezi kunitafuta nyie
mabwege labda mumtafute
Afande Deus..!"
"Nani...? embu riingize rokapu
ritatusaidia kumpata huyo revina..,nakujua juu ya rimkuu
rifande Deus..!"
* * *
Levina tayari chizi na kaingia
Polisi bila kujijua,itakuwaje?
* * *
Vipi Gervas akija kujua
atamsaidia?
* * *
Itakuwaje mwili wa mama
yake Levina ukijulikana?
Inaendelea