Nikajikuta navua viatu vyangu na
kuvishika mikononi huku nikiitupa
ile miwani kwani niliona haina
umuhimu tena kwangu,
Nilijitahidi sana nisiweze kupiga
makelele eneo lile, nikabaki nafuta mchozi tu huku
nikiwafatilia polisi kwa nyuma
nijue watampeleka
wapi,nikawaona wakiingia kituo
cha polisi pale pale
ubungo,nikashusha pumzi,kisha nikatazama ni jinsi gani naweza
kuongea na Gervas,nikiwa bado
najifikiria pale ghafla nikapigwa
kikumbo na Mama Ali.,
"Na huyu hapa tumchukuwe
aliniambia ni ndugu yake..!" "Nani..? Mimi...!,hapana...!, aah...!
aah..!"
Nilijikuta namkana Kama Petro
alivyomkana Yesu mara tatu,huku
nikijifanya kama simjui Gervas
kwakuwa nilikuwa tayari nilishalikoroga nilipomwambia
mwanzoni kuwa Gervas ni ndugu
na jirani yangu.,
"We binti.? Embu potea hapa
haraka...!"
Aliongea kwa sauti ya juu askari mmoja pale huku kanikazia
macho.
"Hapa leo siendi popote kama
kurudishwa gerezani wacha
nirudishwe mie na sio Gervas
ambaye hana hata hatia.." Nilijisemea kimoyo moyo huku
naongoza njia ya kutokea,
" Lakini haiwezekani narudi,
aah...! aah...!"
Nilijikuta narudi tena huku
nikiangalia saa yangu ikinionesha ni saa mbili kasoro usiku, hilo
sikulijali kikubwa ni jinsi gani
nitamtoa Gervas,Nikajikuta
halmashauri yangu ya kichwa
inafanya kazi fasta na kuchukuwa
simu yangu tayari kwa kumpigia 'Afande Deus'..,
"Haloo... Shikamoo Baba Deus..!
Nipo hapa polisi
"Wapi.? Na umefanya nini tena
Levina...?"
"Nipo hapa kituo cha polisi ubungo ndani ya stendi ya basi..."
Nikiwa bado naendelea
kumuelekeza Afande Deus
nilipo,nikashangaa ananikatia
simu..
Nilizidi kuumia moyoni kwani mi ndo nlikuwa mtu wa kumsaidia
Gervas ili aweze kutoka pale.,
Ilimchukuwa lisaa tu kwa afande
Deus kuweza kufika eneo
lile,nikamshuhudia akipitiliza na
kuingia ndani kituoni nadhani hakuniona vizuri nilipo hivyo
nikamfuatilia kwa nyuma,
"Jambo afande"
"Habari, kuna binti yangu yupo
humu ndani..?"
"Hakuna binti yeyote aliyeletwa leo humu....!"
Wakiwa bado wanajibizana
nikajitokeza kwa nyuma taaratibu
huku nikinyata.,
"Mimi hapa Baba...!"
"Twende nyumbani..!" Alinichukuwa kiaskari zaidi huku
nikitetemeka na kuelekea upande
aliokuwa amepaki gari
yake,nikaingia na kupanda gari
yake kabla hajaondoka
nikamwambia ukweli, "Baba...!"
"Unasemaje tena..?"
"Aliyekuwa amewekwa ndani siyo
mimi..?"
"Nani sasa..?"
"Ni Gervas..." "Naaaaaaaaaaaaaaaan.!"
* * * *
Nikiwa nimetulia kwenye gari
peke yangu huku nikimwacha
Afande Deus akirudi tena kituoni
kumalizana na mapolisi wenzake
kuhusu kutoka kwa Gervas,
haikuchukuwa mda nikamwona anarudi peke yake huku
akitingisha kichwa kuashiria kuwa
kashindwa kumtoa Gervas,
"Wamesemaje..?"
Nilijikuta naropoka nikitaka
kujua.. "Imeshindikana mpaka kesho
kwani ni kesi kubwa sana..!"
Miguu ilinilegea,mwili ukaingiwa
na ganzi,kichwa kikawa kizito mda
huohuo huku nisijue nini cha
kufanya, gari ikawashwa tayari kwa kwenda nyumbani.,
Baada ya nusu saa tukawa
tumeshaingia nyumbani kwani
njiani hakukuwa na foleni
kabisa,tuliweza kuingia nyumbani
kwakuwa afande Deus alikuwa na haraka akaniacha nje na kuniaga
kwa kuniambia kuwa kesho
asubuhi atadamkia kwa
Gervas,nikamuitikia na kuingia
ndani,
Nilipoingia ndani nikakuta hali si shwari kwani Mama alikuwa akilia
sana bila kujua nini tatizo,
"Au kwasababu nimechelewa
kurudi..?"
Nilijikuta najipa maswali yasiyo na
majibu, Nilijaribu kumnyamazisha lakini
ilinichukuwa mda mpaka
akanyamaza na kwikwi ikamuisha
kisha akanipa barua aliyokuwa
ameshikilia,nikaichukuwa na
kuanza kuisoma huku presha ikinipanda na kushuka,nikiwa
natetemeka..
Niliendelea kuisoma ile barua
huku nikihisi kichwa changu
kizito,huku ganzi ikinijaa
mwilini,kadri nilivyokuwa naendelea kusoma ndipo
kizunguzungu kikanizidia..,
"LEVINA CHRISTIAN"
Unahitajika Mahakama ya
mwanzo mkoani Mbeya haraka
upatapo barua hii.. Uchunguzi wa kina uliofanywa na
jopo la Madaktari kutoka Iringa
imebainika kuwa Marehemu
Pendo amefariki kwa kuchomwa
na kitu chenye ncha kali na mwili
wake kuokotwa porini huko Iringa,
Na siku alioachiwa huru gerezani
alikuwa na wewe Levina Christian
ambao wote mlikuwa wafungwa,
hivyo ukiwa kama mtu ambaye
uliongozana naye kutoka gerezani mara ya mwisho unahitajika na
mahakama haraka iwezekanavyo
kwa ushahidi juu ya kifo cha
Pendo Abel..."
Nilipomaliza tu kuisoma
nikamgeukia Mama nakuanza kwani alikuwa bado anaendelea
kulia tena kwa sauti ya chininini,
kichwa na akili yangu vikiwa
havifanyikazi, nilijihisi kujiharishia
huku nikiwahi kulibana tumbo
langu lililokuwa linaunguruma kwa kasi kisha nikamtazama
mama yangu.
"Nani ameileta hii barua..?"
"Vijana wawili waliovalia nguo za
kiraia wakiwa na gari..."
Sikuhitaji kujua la zaidi,nilichofanya ni kumuhadithia
Mama yote yaliyonikuta
kuhusiana na Gervas,
"Mama haiwezekani,inanibidi leo
leo tena sasa hivi nifanye juu chini
tena kabla hata afande Deus hajajua kitu chochote niwe
nimeshaondoka na kwenda
kulimaliza hili tatizo najua kesho
asubuh Gervas atatolewa kwahiyo
Mama nakuomba Gervas
usimwambie lolote juu yangu" "Mama nakuomba sana.,sana
tena sana..,
Hii barua na hata hizi taarifa
asizijue afande Deus,atashindwa
kunisaidia kumtoa Gervas..!"
"Mwanangu kwanini ni wewe tu jamani..?
.......Kwanini mikosi yote inakuja
kwako tu..?"
Aliongea kwa sauti ya kukwaruza
kuonesha kwamba amelia sana
na sauti inataka kumkauka.., "Mama Naumia na nitaendelea
kuumia.,Najua na wewe unaumia
lakini ninachokuomba uwe na
moyo wa subira nitarudi salama
tu wala usihofu?
"Sawa mwanangu..,ila chunga sana mwanangu.."
Haraka bila kupoteza mda
nikaingia chumbani kwangu na
kuvaa suruali yangu ya
jinsi,nikajivika tsheti yangu ya kijani
iliyokuwa na maandishi makubwa kwa mbele yaliyosomeka 'YOTE
MAISHA' chini nikadondoka na
raba za rangi ya kijivu,kisha
nikachukuwa kijibegi changu cha
mgongoni, nikatoka sebuleni na
kumuaga mama, "Chukuwa hii itakusaidia huko
ukipatwa na matatizo itakuepusha
nayo"
Alinivulia cheni yake ya dhahabu
kisha akanivalisha,
"na hii nauli itakusaidia uko uendako"
Akafungua upindo wa kanga yake
na kunipa kiasi cha shilingi elfu
sabini,
Haikuwa na jinsi ilinibidi
nichukuwe hivyo vitu kisha nikafanya ishara ya msalaba na
kuondoka zangu huku
nikimsisitizia Mama afanye juu
chini Afande Deus asijue chochote
na amdanganye vyovyote,
Sikuhtaji Mama anisindikize kwa usiku ule kwani nilijua kabisa
inaweza kutokea Afande Deus
akaja pale usiku kwa kushtukiza,
Nikiwa nje natoka naelekea stendi
ya mabasi japo nikaambulie gari
lolote,nikashangaa mwanga mkali wa gari ukinimulika
machoni,nikiwa najaribu kujizuia
na kulikwepa mara nikashuhudia
likisimama mbele yangu..
"Levina...! Levina...! Levina...!
Unaenda wapi usiku huu., Hapa huwezi kututoroka hata
mara moja,Na tupo hapa nje
tangu ulipoletwa na Afande
Deus..!"
Moyo ulilia paaah..! Kisha nikahisi
kama mlango unafunguliwa nyumbani nilipotoka,
"Kwani nyie wakina nani?"
"Huitaji kujua ila utajua ukifika
mahakamani kule mbeya"
Nikashuhudia afande mmoja
akishuka kwenye gari kisha akanifuata na kunifunga pingu
haraka akaniweka kwenye gari
aina ya 'Toyota land Cruiser'
nyeupe.,
Niliumia moyo,nguvu nilikuwa
tena sina nilipojaribu kuangalia nyumbani macho yalikutana na
Macho ya Mama yangu akiwa
amesimama mlangoni huku
macho yake yakionesha kuwa na
simanzi tele,mara gari ikitoka pale
kwa kasi ya ajabu.. "Mwanaangu....!"
Ndio neno la mwisho nililoweza
kuambulia kwa mama huku
akiniliza na kunisisimua mwili wote
kwani alinikumbusha aliniambia
hivyo kipindi kile nahukumiwa mahakamani.,
* * * *
Safari ilianza kuanzia Dar lakini
tulipofika Morogoro nilijikuta
Nalia sana kutokana na mauaji
niliyoyafanya ila nikajipa moyo na
tulipofika Iringa haswaa tulipofika
kijiji cha 'Liamkena' machozi mengi yalinitoka huku nikilia kwa
sauti ya chini chini na kwikwi kwa
mbali kila nikikumbuka mateso
niliyopata pale kwa wale
wanafunzi,pia nilipomua rafiki
yangu Pendo bila kukusudia, Nilipigwa na baridi lakini sikuweza
kulisikia nadhani hii ni kutokana
na kuchanganyikiwa kwanza ni
kuwaza itakuwaje kwa Gervas
asubuh pili huko niendako kutoa
ushahidi, Ilituchukuwa masaa kama kumi
na moja mpaka kufika Mbeya,
Tulifikia mahakamani moja kwa
moja kwani kesho yake ndo kesi
itasomwa ila nilishangaa
kupelekwa pale mahakamani asubuhi asubuhi, wale askari
wakanichukuwa hadi kwenye ofisi
nisiyoifahamu pale pale
mahakamani, nikiwa nashangaa
shangaa huku na kule ghafla
nikashangaa nasemesha kwa upande wa nyuma yangu..
"Hujambo binti..? Za masiku..?"
Alikuwa ni baba yake na Pendo
yule niliyomdanganya kipindi kile
kuwa nafanya kazi za ndani na
sasa alikuwa pale ofisini.. "Ba..a..a..a..a..b..a...Pe..ndo...Mi
sijamuua mtoto wako.. ******************** * * *
Mdomo wa kuropoka
umemponza tena Levina
itakuwaje..?
* * *
Je.,Gervas kashatolewa,na
Afande Deus atajua kuhusiana na
Levina? Itaendelea