Hadithi: Mikataba ya kishetani

Hadithi: Mikataba ya kishetani

Nameless
 

Attachments

  • 1457533639482.jpg
    1457533639482.jpg
    59.2 KB · Views: 80
***

Kwa mara ya kwanza risasi ya ‘Mkono wa Jibril’ilikosa shabaha na kumpata mtu ambaye hakukusudiwa? Ni swali jingine ambalo lilimsumbua Joram. Mauaji yake mengine yote yalionekana kuwa na sababu fulani. Rais aliyeuawa alikuwa katika vuta nikuvute ya madaraka na wasaidizi wake wa karibu, hatua iliyopelekea mapinduzi. Bilionea aliyeuawa anaaminika kuuzwa na mkewe kwasababu za urithi, ingawa mahakama hazikupata kuwa na ushahidi. Kiongozi wa kidini aliyefumuliwa madhabahuni anashukiwa kuwa kifo chake kiliandaliwa na uongozi wa kanisa kwaajili ya kumwondoa katika orodha ya makadinali waliokuwa wakitarajiwa kuchukua nafasi ya papa. Cleopatra anaingia vipi katika orodha hiyo? Joram alikisumbua kichwa chake.

Jogoo aliyewika toka mahala fulani alimzindua Joram. Alipoitazama saa yake alishangaa kuwa ilikuwa saa kumi na robo za alfajiri. Kazi iliyokuwa mbele yake haikuwa lele mama. Alihitaji usingizi. Alihitaji akili zake zote na utulivu wake kuanzia kesho. Akaifunga kompyuta yake na kuzima taa.

Kwa mara ya kwanza, kwa kipindi cha miaka mingi, Joram alijikuta akipiga magoti na kusali kabla ya kupanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi.

10

Abdul Kopa hakuzaliwa muuaji. Dunia ndiyo iliyomtengeneza kuwa hivyo. Ni pale usiku mmoja alipojikuta mikononi mwa polisi akituhumiwa kwa ujambazi. Hakuelewa,kwani dakika tano zilizopita alikuwa mtu huru, mwadilifu, akitoka zake dansini. Dakika tano baadaye alikuwa mtuhumiwa, pingu mikononi, akipelekwa mahabusu, kisa? Kwamba alikuwa jambazi.

Kesho yake alipelekwa mahakamani na kusimamishwa kizimbani. Pamoja naye walikuwepowatu wengine watatu waliodaiwa kushirikiana naye. Walisomewa mashitaka matatu ya ujambazi wa kutumia silaha na moja la kuua. Washtakiwa hawakutakiwa kujibu lolote, hivyo walirudishwa rumande kwa maelezo kuwa ushahidi haujakamilika. Kila mtuhumiwa alikuwa mgeni machoni mwa Kopa, hali iliyofanya aone kama ndoto ile pindi wakivishwa tena pingu na kupelekwa gereza la keko chini ya ulinzi mkali.

Kuna mwanasheria mmoja wa kike aliyeuawa na jirani yake, Mtanzania mwenye asili ya Kiasia, ambaye alikuwa akipiga risasi ovyo kutishia majambazi alioambiwa kuwa walikuwa wakija dukani kwake. Mwanasheria huyo, aliyekuwa mlangoni kwake akishuhudia sakata hilo, alipatwa na risasi ya ubavuni na kuanguka. Jitihada za kumwokoa zilishindikana pale alipokata roho, katika hospitali ya Muhimbili, siku tatu baada ya kufikishwa hapo. Mtuhumiwa halisi wa mauaji hayo alikaa rumande nusu saa tu, akatoka. Miezi mitatu baadaye ndipo walipopatikana akina Abdul Koba ambaye mmoja wao alidaiwa kukiri kosa hilo.

Kama kawaida ya enzi hizo, kesi ilinguruma kwa miaka. Koba na wenzake wakisota rumande kwani kesi yao haikuwa na dhamana. Waliteseka kwa chakula kibaya, malazi duni na mateso tele ya Kisaikolojia. Robo tatu ya mahabusu wenzao wakiwa wahalifu wa kweli, Koba alijikuta katika darasa la aina mpya, darasa la mbinu za kukwepa hukumu, mbinu za uhalifu na mbinu za kuishi gerezani humo. Baadhi ya ‘walimu’ wakiwa wahalifu sugu, Koba alijikuta akipokea kile ambacho Waingereza huita ‘From the Horses mouth’ aidha kwa kukaa nao pamoja kwa muda mrefu, wakishirikiana kwa hili na lile, palepale alianza kujiona mmoja wao.

Hukumu ilipotoka Abdul alifungwa miaka kumi jela. Kwa kalenda ya jela na muda aliokaa rumande, alitumikia kifungo hicho kwa miaka minne tu. Miaka ya mateso, miaka ambayo kila siku aliyoishi gerezani humo ilimfanya azidi kupandwa na hasira, hasira ambazo alizielekeza kwa jamii nzima; wanasiasa wanaolea mfumo wa kishetani kama huo, majaji na mahakimu ambao wanatekeleza, wananchi ambao wanaufumbia macho na wengineo.

Hasira ambazo zilimfanya mara alipotoka gerezani humo aamue kuwa ‘mnyama.’ Alianza kwa kushiriki ujambazi wa kuvunja majumba na kupata magari. Alishiriki pia katika wizi wa kalamu pamoja na silaha katika mabenki. Mtu yeyote aliyejifanya kizingitikati yake na kazi yake hakumwacha hai.

Mahabusu paligeuka nyumba yake ndogo. Akiwa tayari anao mlolongo mrefu wa marafiki katika jeshi la polisi na vyombo vya sheria, kuingia na kutoka mahabusu ilisababisha muda mfupi baadaye aanze kupewa ‘kazi’ na baadhi ya polisi haohao. Mambo yalimnyookea zaidi pale alipojenga urafiki na kigogo mmoja wa usalama ambaye alimpa majukumu nyeti na kumlipa ujira wa kusisimua sana.

Miaka sita baadaye, Abdul Kopa, aliyetoka gerezani hakuwa yule aliyeingia. Huyu alikuwa mtu mwingine kabisa. Alikuwa na majumba sita ya wageni, ghorofa tano. Alikuwa na duka la kuuza magari na vifaa vyake. Kadhalika, alinunua shamba la ekari mia tano, ambalo alikusudia kulima maua. Badala ya Abdul sasa aliitwa ‘Bwana Abdul’ au ‘Mzee Abdul’ kila alikopita. Hata alianza kusali, akitoa zaka kubwa na kusaidia watoto yatima. Ndoto za ‘kununua’ ubunge ili asisumbuliwe hovyohovyo zilianza kumtembelea.

Hakuna aliyejua kazi yake ya usiku. Hakuna aliyejua chanzo cha utajiri wake. Hakuna aliyejishighulisha, kwani hizo zilikuwa ndio enzi za wakati huo nchini. Kila mtu alishika lake na kufanya atakalo.

Kwa Abdul Kopakuua ilikuwa moja ya kazi zake rahisi. Kigogo mmoja alimtumia atakavyo. Taarifa muhimu za kufa na nusu malipo kabla ya kazi, nusu baada ya Koba kumaliza kazi, ama kwa mkono wake mwenyewe, ama kwa kuwatumia vijana wake. Kazi moja wapo ilikuwa nyeti zaidi na dau lake pia pana zaidi. Ilihitaji kuwaondoa duniani maafisa wazito serikalini. Watatu waliondoka baada jitihada kubwa za muda mrefu lakini mmoja aliteleza kama kambare na kubadilika kama kinyonga. Kila lilipopangwa hili dhidi yake lilitokea lile na hivyo kuhairisha kifo chake. Mbaya zaidi, mhanga huyo alitoweka nyumbani kwake na kuishi hapa na pale kana kwamba alifahamu kuwa kifo kilikuwa kikimfuatilia. Hata hivyo, kabla hajazitumia fedha alizopewa kwaajili ya kifo cha mhanga yule, Koba alishuhudia kifo hicho katika matangazo ya televisheni. Aliuawa bila shaka kwa risasi ya mdunguaji, hadharani, mbele ya Rais wa nchi, majuzi tu kama watu wengine, Abdul Koba hakupata kumfahamu muuaji wala kufahamu kama kifo kile kilihusiana na hukumu ya kigogo au la. Zaidi hakufahamu iwapo risasi ilimkusudia yeye au Rais. Lilikuwa moja kati ya mambo ambayo asingethubutu kumtaka Kigogo ufafanuzi. Hivyo, alibakia na mshangao wake.

Mkutano wake wa pili hapa na kigogo huyo ulikuwa ule wa jana pale alipoitwa ghafla na kupatiwa picha ya afisa mwingine wa polisi ambaye alitakiwa kufa mara moja. Alipewa picha ya afisa huyo na maelekezo ya wapi aliko muda huo, lipi afanye. Ilikuwa kazi rahisi sana, kumkuta mtu kaketi peke yake ufukweni. Hivyo, pale Abdul alipopokea simu ya ‘kigogo’ mwenyewe akimtaka wakutane katika msitu wa eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kazi maalumu hakusita kuondoka mara moja. Hata hivyo, kinyume cha maelekezo ya kigogo huyo, kuwa awe peke yake alimwagiza mmoja wa wasaidizi wake mahiri kumtaka atangulie na kujificha katika eneo hilo, hatua ambayo ilitekelezwa kikamilifu.

Abdul Kopa alifika hapo dakika tano kabla ya muda. Alishangaa kumwona ‘kigogo’ akiwa tayari ndani ya msitu, chini ya mtu ambao umewahifadhi kwa zaidi ya vikao vitatu vya aina hiyo.

Urafiki wa kigogo huyo na Abdul haukupata kuwa wa kawaida. Kwa ujumla, ulikuwa urafiki wa mashaka. Walikutana kwa nadra sana, kwa siri sana na walizungumza kwa ufupi sana. Mara kwa mara kigogo alikuwa na haraka, huku akifanya kila jitihada kuhakikisha Abdul hamwoni vizuri kwa kiwango cha kumfahamu mara moja. Kigogo huyo hakumtambua vizuri Abdul Koba. Hakujua kuwa Abdul Koba wa leo sio yule wa jana, kwamba hakuwana Imani na mtu yeyote yule duniani, hata mama yake mzazi. Hivyo, bila ya kigogo kujifahamu msaidizi wake mmoja alikuwa amechukua picha yao, wakati wanapeana fedha, katika moja ya vikao vyao.

Kikao hicho kilikuwa kirefu zaidi, kwa viwango vyao. Dakika zipatazo kumi na mbili zilitumika wakati kigogo akitoa orodha ya watu wanne aliotaka kukaa naye kwa dakika moja, kabla ya kutoa bastola yenye kiwambo cha kupoteza sauti, kummiminia risasi tatu na kuondoka zake, mluzi mdomoni.

Haya, leo yuko hapa tena, mbele ya kigogo, akisubiri kupatiwa jukumu jingine! Pamoja na ukweli kuwa alipenda sana pesa, pamoja na ukweli alishapoteza kitu kinachoitwa huruma katika roho na msamiati wake, bado alianza kupatwa na hisia za mashaka kwa kazi hii ya muuaji. Yanahusiana na nini? Yataisha lini? Ni miongoni mwa maswali yaliyosumbua kichwa chake.

Kana kwamba alikuwa akiyasoma mawazo ya kigogo, alimsalimu na kisha kumwambia, “Usijali, jukumu ninalokupa leo ni la mwisho. Mimi na wewe hatutawasiliana tena baada ya leo. Ni mtu mmoja tu na hayuko mbali kutoka hapa.”

Kigogo alifungua begi lake kama anayetoa nyaraka fulani au fedha. Aliuchomoa mkono wake ghafla ukiwa umeshikilia bastola ambayo aliielekeza kifuani mwa Koba.

“Leo ni zamu yako.” Alimwambia.

Abdul Koba alikwishakuwa mtu mnene, mwenye kiri-batumbo. Lakini bado alikuwa mwepesi, hivyo hakuisubiri risasi kama ilivyo kwa watu wengine. Alichupa kukwepa ya kwanza na kumfanya imchubue kidogo ubavuni. Ya pili, ambayo ilimkuta akiwa tayari na bastola yake mkononi, ilimwingia tumboni. Alifyatua yake, ambayo pia ilikuwa na kiwambo cha sauti. Hakuwa amepata fursa ya kulenga shabaha, hivyo risasi zote mbili zilimkosa kigogo kwa mbali sana. Wakati huo, risasi tano zaidi ziliingia tumboni na kifuani mwake na kumfanya adondoke chini kama gunia la mtama. fahamu zilimtoka mara moja.

Kigogo aliitazama kazi yake na kuridhika nayo, akafanya haraka kuliacha eneo hilo kwa kulirejea gari lake aliloliacha mbele ya kituo cha jirani cha mafuta ya gari.

***

Pamoja na kutoka na tabasamu usoni, pamoja na kumtilia alama ya dole yule msichana wa mapokezi ili kumtoa mashaka, bado rohoni mwangu nilijawa na wasiwasi. Mwenendo wa mambo yangu ulikuwa ukifuata mkondo ambao sikuutarajia, mkondo ambao sikuumba mimi. Kifo cha yule kijana wa hoteli ni moja kati ya mambo yaliyofanya nihisi chombo kikienda mrama. Sikutarajia kuua mtu. Zaidi sikutarajia kuua katika chumba changu, hali ambayo kwa vyovyote ingeamsha udadisi na kisha uchunguzi wa kina dhidi yangu. Kwa bahati mbaya sikuwa na njia. Kijana yule alikisaka kifo kwa jitihada zake zote. Kumuua ilikuwa halali, kumwacha hai ilikuwa hatari zaidi.

Hivyo, nilitembea mtaani harakaharaka hadi mahala nilipokodi teksi na kuielekeza nje kidogo ya mji. Huko, baada ya kuingia katika duka moja na kununua shati na suruali ya jeans, nilikodi gari jingine na kuelekea upande wa pili wa mji. Nilipata choo cha kulipia nikaingia na kubadili mavazi yangu, lile shati la yule kijana nililichana chana na kulitupa chooni. Nilipotoka kwa kiasi fulani nilikuwa mtu mpya.

Nilijua kuwa wajibu wangu ulikuwa kuiacha Dar es salaam na Tanzania mara moja. Nilitakiwa kudandia ndege ya kwanza, treni ya kwanza na hata basi la kwanza mradi nitoke nchini humu mara moja. Hata hivyo, haikuwa rahisi kama inavyozungumzika. Upepo ulikuwa haueleweki. Baharia mzoefu hawezi kujitoma baharini bila uhakika wa safari yake. Hivyo, nilifikia uamuzi wa kujibanza tena nchini kwa siku mbili tatu ili niweze kuusoma mwenendo wa mambo kabla ya kuanza mikakati ya kutoka.

Dar es Salaam sio Hong Kong ambayo maelfu ya wagenu humiminika kila siku na kufanya vyumba vya wageni viwe adimu. Wala sio Bangdadambako mgeni huchunguzwa kwa makini sana kabla ya kupatiwa chumba kwa hofu ya kumkaribisha gaidi ambaye ataishia kujilipuakatika kadamnasi. Hivyo, haikuwa kazi ngumu kupata chumba kizuri katika hoteli moja iliyoitwa Bondeni Inn Resort, kilometa tatu toka katikati ya jiji. Sasa nikiwa mvulana mtanashati, mara tu nilipopatiwa kadi ya chumba nilijifungia chumbani humo na kufanya haraka kurekebisha kasoro ndogondogo ambazo zingeweza kunifanya niunganishwe na yule msichana aliyeuawa muda mfupi uliopita. Kazi ambayo sikuwa nimeridhika nayo baada ya kuifanya kwa pupa mara baada ya kuipeleka akhera roho ya yule mjinga.

Baada ya hapo nilijilaza chali juu ya kitanda, ubongo wa mambo na namna ya kujinasua. Jitihada kubwa ambayo niliuagiza ubongo wangu kufutilia mbali ilikuwa ile shahuku yangu ya kutaka kumfahamu mwajiri wangu aliyenipa kazi hiyo rahisi sana kwa dau nono sana, ni nani? Alinufaika vipi? Alinifahamu vipi? Na anafanya lipi kwa sasa? Nilijitahidi kulifukuza hilo kwa kujua kuwa shahuku hiyo ndiyo ilinifikisha katika mazingira haya kama ningekuwa nimeifanya kazi yangu na kutoweka mara moja, nyuma ya kisogo change. Pamoja na hayo, haikuwa kazi rahisi. Kila nilipopanga mikakati ya kutoka, shahuku ya kujua kila kinachoendelea ilinijia pale katikati ya fuvu la kichwa change, na hivyo kunipa mateso makubwa kisaikolojia.

Mkakati wangu wa kwanza ulikuwa wa kumwokoa mwanangu, kipenzi changu. Licha ya ukweli kuwa naye sambamba ilikuwa hatari, bado pia sikutaka apatwe na ajali yoyote mbaya, ingesababisha tutengane naye. Kwangu yeye alikuwa mwandani, mkono wangu wa pili, mguu wangu wa pili. Hivyo, kazi ya kwanza ilikuwa kumfumua; kichwa pale, mkono pale, mguu kule na kisha kumsafirisha atangulie nyumbani.

Kazi hiyo niliianza mara moja, nilifungua begi langu na kumtoa. Alikuwa tayari katika sehemu mbili. Nikambusu na kuanza kumtatua tena. Dakika chache baadaye alikuwa katika vifurushi vitano, vilivyoandikwa ‘sample’ ndani ya mifuko maalumu ya nailoni ambayo baadaye ilifungwa pamoja ndani ya kijiboksi kilichoelekezwa kwa kampuni fulani kwa anuani fulani ambayo ni mimi pekee niliyeifahamu. Muda mfupi baadaye mwanagu alikuwa tayari kwa safari. Hapa kama ingetokea muujiza, akamatwe njiani ni watu wachache sana duniani ambao wangeweza kutambua kuwa ‘mwanangu’ huyu aliitwa AK 47.

Nisingeweza kusahau mapenzi kwa mwanangu yaliyoanza. Ilikuwa baada ya yale mazoezi marefu ya shabaha na jaribio la kusafirisha yule mwarabu. Ilifuatia kazi nyingine ambayo niliambiwa kuwa ilikuwa nyeti sana.

Nilipewa ramani ya makazi ya mhanga huyo, ratiba yake ya kutoka na kuingia kwake. Hali kadhalika nilipewa picha zake mbalimbali. Alikuwa mtu maarufu sana duniani. Pia alikuwa machachari aliyehusishwa na mambo mengi ikiwemo undumila kuwili kati ya kikundi cha kigaidi cha Wayahudi MOSSAD na magaidi wa AL KAIDA. Iliaminika kuwa yeye alikuwa mtu pekee aliyekuwa na hakika ya kukutana na Osama Bin Laden na kuzungumza naye. Kwamba pia ndiye aliyekuwa akishikilia koba lake la pesa.

Kazi ya kumwinda mtu huyu haikuwa ngumu. Yeye mwenyewe alipenda sana kuwinda wanyama. Hivyo, jioni moja alipookotwa katika mbuga ya wanyama nchini Malawi, risasi ya mwanangu AK 47 ikiwa imejikita katika paji la uso wake kila mmoja aliamini kuwa alikuwa amevuna kile alichokipanda.

Nilisoma habari zote kwa siku kadhaa katika magazeti na kuzitazama katika televisheni. Kama ilivyo ada habari hizo zilididimia na kutoweka ghafla pale zilipokua nyingine, nyeti zaidi za Marekani kuivamia Iraq na baadaye kumkata kichwa mtawala wake, Saddam Hussein.

Kazi ya kuwinda binadamu kwa minajili ya kumtoa roho ni ngumu kuliko unavyoweza kufikiria. Kwanza, wewe mwenyewe unajificha usifahamike, kisha, yeye, kama tarehe yake haijajiri atakuhangaisha hata kwa miezi mkicheza mchezo wa paka na panya. Hivyo, wakati nikifikiria dau langu nono nililolipwa nilijua kuwa ninakula fedha ambazo nilizitumikia, kwani mara mbili tatu nilinusurika kutafunwa na simba, mara moja niliponea chupu chupu kugongwa utosini na nyoka aina ya kobra aliyekuwa tayari amejaza koo lake kwa sumu.

Miezi mitatu baadaye nilipewa jukumu jingine. Hili pia lilimhitaji mwanangu, kumfuta duniani ‘mbwa mweusi’ mwanasiasa mwenye asili ya Kiafrika ambaye alikuwa akija juu katika siasa za Marekani. Nilitakiwa kumfanyia vitu vyangu hadharani ili iwe fundisho kwa watu wengine waliodhani wana haki nchini humo sawa na weupe ingawa wao pia ni wahamiaji toka ulaya.

Haikuwa kazi ngumu. Akiwa mtu wa mikutano na mihadhara kila mara nilimvizia katika moja ya mikutano yake na uielekeza risasi yangu mdomoni wakati ameufungua akisisitiza jambo. Alifia hospitalini ambako inadaiwa kauli yake ya mwisho ilikuwa ‘Aluta Continue.’

Mwaka mmoja baadaye nilihisi natumiwa kwa ujira usiolingana na zigo zito la dhambi nilizokuwa nikichuma. Ndipo nikabuni na kuandaa kifo changu mwenyewe. Lilikuwa pigo kwa waajiri wangu lakini kwangu binafsi ilikuwa faraja.
 
***

Kwa mara ya kwanza risasi ya ‘Mkono wa Jibril’ilikosa shabaha na kumpata mtu ambaye hakukusudiwa? Ni swali jingine ambalo lilimsumbua Joram. Mauaji yake mengine yote yalionekana kuwa na sababu fulani. Rais aliyeuawa alikuwa katika vuta nikuvute ya madaraka na wasaidizi wake wa karibu, hatua iliyopelekea mapinduzi. Bilionea aliyeuawa anaaminika kuuzwa na mkewe kwasababu za urithi, ingawa mahakama hazikupata kuwa na ushahidi. Kiongozi wa kidini aliyefumuliwa madhabahuni anashukiwa kuwa kifo chake kiliandaliwa na uongozi wa kanisa kwaajili ya kumwondoa katika orodha ya makadinali waliokuwa wakitarajiwa kuchukua nafasi ya papa. Cleopatra anaingia vipi katika orodha hiyo? Joram alikisumbua kichwa chake.

Jogoo aliyewika toka mahala fulani alimzindua Joram. Alipoitazama saa yake alishangaa kuwa ilikuwa saa kumi na robo za alfajiri. Kazi iliyokuwa mbele yake haikuwa lele mama. Alihitaji usingizi. Alihitaji akili zake zote na utulivu wake kuanzia kesho. Akaifunga kompyuta yake na kuzima taa.

Kwa mara ya kwanza, kwa kipindi cha miaka mingi, Joram alijikuta akipiga magoti na kusali kabla ya kupanda kitandani na kuanza kuutafuta usingizi.

10

Abdul Kopa hakuzaliwa muuaji. Dunia ndiyo iliyomtengeneza kuwa hivyo. Ni pale usiku mmoja alipojikuta mikononi mwa polisi akituhumiwa kwa ujambazi. Hakuelewa,kwani dakika tano zilizopita alikuwa mtu huru, mwadilifu, akitoka zake dansini. Dakika tano baadaye alikuwa mtuhumiwa, pingu mikononi, akipelekwa mahabusu, kisa? Kwamba alikuwa jambazi.

Kesho yake alipelekwa mahakamani na kusimamishwa kizimbani. Pamoja naye walikuwepowatu wengine watatu waliodaiwa kushirikiana naye. Walisomewa mashitaka matatu ya ujambazi wa kutumia silaha na moja la kuua. Washtakiwa hawakutakiwa kujibu lolote, hivyo walirudishwa rumande kwa maelezo kuwa ushahidi haujakamilika. Kila mtuhumiwa alikuwa mgeni machoni mwa Kopa, hali iliyofanya aone kama ndoto ile pindi wakivishwa tena pingu na kupelekwa gereza la keko chini ya ulinzi mkali.

Kuna mwanasheria mmoja wa kike aliyeuawa na jirani yake, Mtanzania mwenye asili ya Kiasia, ambaye alikuwa akipiga risasi ovyo kutishia majambazi alioambiwa kuwa walikuwa wakija dukani kwake. Mwanasheria huyo, aliyekuwa mlangoni kwake akishuhudia sakata hilo, alipatwa na risasi ya ubavuni na kuanguka. Jitihada za kumwokoa zilishindikana pale alipokata roho, katika hospitali ya Muhimbili, siku tatu baada ya kufikishwa hapo. Mtuhumiwa halisi wa mauaji hayo alikaa rumande nusu saa tu, akatoka. Miezi mitatu baadaye ndipo walipopatikana akina Abdul Koba ambaye mmoja wao alidaiwa kukiri kosa hilo.

Kama kawaida ya enzi hizo, kesi ilinguruma kwa miaka. Koba na wenzake wakisota rumande kwani kesi yao haikuwa na dhamana. Waliteseka kwa chakula kibaya, malazi duni na mateso tele ya Kisaikolojia. Robo tatu ya mahabusu wenzao wakiwa wahalifu wa kweli, Koba alijikuta katika darasa la aina mpya, darasa la mbinu za kukwepa hukumu, mbinu za uhalifu na mbinu za kuishi gerezani humo. Baadhi ya ‘walimu’ wakiwa wahalifu sugu, Koba alijikuta akipokea kile ambacho Waingereza huita ‘From the Horses mouth’ aidha kwa kukaa nao pamoja kwa muda mrefu, wakishirikiana kwa hili na lile, palepale alianza kujiona mmoja wao.

Hukumu ilipotoka Abdul alifungwa miaka kumi jela. Kwa kalenda ya jela na muda aliokaa rumande, alitumikia kifungo hicho kwa miaka minne tu. Miaka ya mateso, miaka ambayo kila siku aliyoishi gerezani humo ilimfanya azidi kupandwa na hasira, hasira ambazo alizielekeza kwa jamii nzima; wanasiasa wanaolea mfumo wa kishetani kama huo, majaji na mahakimu ambao wanatekeleza, wananchi ambao wanaufumbia macho na wengineo.

Hasira ambazo zilimfanya mara alipotoka gerezani humo aamue kuwa ‘mnyama.’ Alianza kwa kushiriki ujambazi wa kuvunja majumba na kupata magari. Alishiriki pia katika wizi wa kalamu pamoja na silaha katika mabenki. Mtu yeyote aliyejifanya kizingitikati yake na kazi yake hakumwacha hai.

Mahabusu paligeuka nyumba yake ndogo. Akiwa tayari anao mlolongo mrefu wa marafiki katika jeshi la polisi na vyombo vya sheria, kuingia na kutoka mahabusu ilisababisha muda mfupi baadaye aanze kupewa ‘kazi’ na baadhi ya polisi haohao. Mambo yalimnyookea zaidi pale alipojenga urafiki na kigogo mmoja wa usalama ambaye alimpa majukumu nyeti na kumlipa ujira wa kusisimua sana.

Miaka sita baadaye, Abdul Kopa, aliyetoka gerezani hakuwa yule aliyeingia. Huyu alikuwa mtu mwingine kabisa. Alikuwa na majumba sita ya wageni, ghorofa tano. Alikuwa na duka la kuuza magari na vifaa vyake. Kadhalika, alinunua shamba la ekari mia tano, ambalo alikusudia kulima maua. Badala ya Abdul sasa aliitwa ‘Bwana Abdul’ au ‘Mzee Abdul’ kila alikopita. Hata alianza kusali, akitoa zaka kubwa na kusaidia watoto yatima. Ndoto za ‘kununua’ ubunge ili asisumbuliwe hovyohovyo zilianza kumtembelea.

Hakuna aliyejua kazi yake ya usiku. Hakuna aliyejua chanzo cha utajiri wake. Hakuna aliyejishighulisha, kwani hizo zilikuwa ndio enzi za wakati huo nchini. Kila mtu alishika lake na kufanya atakalo.

Kwa Abdul Kopakuua ilikuwa moja ya kazi zake rahisi. Kigogo mmoja alimtumia atakavyo. Taarifa muhimu za kufa na nusu malipo kabla ya kazi, nusu baada ya Koba kumaliza kazi, ama kwa mkono wake mwenyewe, ama kwa kuwatumia vijana wake. Kazi moja wapo ilikuwa nyeti zaidi na dau lake pia pana zaidi. Ilihitaji kuwaondoa duniani maafisa wazito serikalini. Watatu waliondoka baada jitihada kubwa za muda mrefu lakini mmoja aliteleza kama kambare na kubadilika kama kinyonga. Kila lilipopangwa hili dhidi yake lilitokea lile na hivyo kuhairisha kifo chake. Mbaya zaidi, mhanga huyo alitoweka nyumbani kwake na kuishi hapa na pale kana kwamba alifahamu kuwa kifo kilikuwa kikimfuatilia. Hata hivyo, kabla hajazitumia fedha alizopewa kwaajili ya kifo cha mhanga yule, Koba alishuhudia kifo hicho katika matangazo ya televisheni. Aliuawa bila shaka kwa risasi ya mdunguaji, hadharani, mbele ya Rais wa nchi, majuzi tu kama watu wengine, Abdul Koba hakupata kumfahamu muuaji wala kufahamu kama kifo kile kilihusiana na hukumu ya kigogo au la. Zaidi hakufahamu iwapo risasi ilimkusudia yeye au Rais. Lilikuwa moja kati ya mambo ambayo asingethubutu kumtaka Kigogo ufafanuzi. Hivyo, alibakia na mshangao wake.

Mkutano wake wa pili hapa na kigogo huyo ulikuwa ule wa jana pale alipoitwa ghafla na kupatiwa picha ya afisa mwingine wa polisi ambaye alitakiwa kufa mara moja. Alipewa picha ya afisa huyo na maelekezo ya wapi aliko muda huo, lipi afanye. Ilikuwa kazi rahisi sana, kumkuta mtu kaketi peke yake ufukweni. Hivyo, pale Abdul alipopokea simu ya ‘kigogo’ mwenyewe akimtaka wakutane katika msitu wa eneo la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kazi maalumu hakusita kuondoka mara moja. Hata hivyo, kinyume cha maelekezo ya kigogo huyo, kuwa awe peke yake alimwagiza mmoja wa wasaidizi wake mahiri kumtaka atangulie na kujificha katika eneo hilo, hatua ambayo ilitekelezwa kikamilifu.

Abdul Kopa alifika hapo dakika tano kabla ya muda. Alishangaa kumwona ‘kigogo’ akiwa tayari ndani ya msitu, chini ya mtu ambao umewahifadhi kwa zaidi ya vikao vitatu vya aina hiyo.

Urafiki wa kigogo huyo na Abdul haukupata kuwa wa kawaida. Kwa ujumla, ulikuwa urafiki wa mashaka. Walikutana kwa nadra sana, kwa siri sana na walizungumza kwa ufupi sana. Mara kwa mara kigogo alikuwa na haraka, huku akifanya kila jitihada kuhakikisha Abdul hamwoni vizuri kwa kiwango cha kumfahamu mara moja. Kigogo huyo hakumtambua vizuri Abdul Koba. Hakujua kuwa Abdul Koba wa leo sio yule wa jana, kwamba hakuwana Imani na mtu yeyote yule duniani, hata mama yake mzazi. Hivyo, bila ya kigogo kujifahamu msaidizi wake mmoja alikuwa amechukua picha yao, wakati wanapeana fedha, katika moja ya vikao vyao.

Kikao hicho kilikuwa kirefu zaidi, kwa viwango vyao. Dakika zipatazo kumi na mbili zilitumika wakati kigogo akitoa orodha ya watu wanne aliotaka kukaa naye kwa dakika moja, kabla ya kutoa bastola yenye kiwambo cha kupoteza sauti, kummiminia risasi tatu na kuondoka zake, mluzi mdomoni.

Haya, leo yuko hapa tena, mbele ya kigogo, akisubiri kupatiwa jukumu jingine! Pamoja na ukweli kuwa alipenda sana pesa, pamoja na ukweli alishapoteza kitu kinachoitwa huruma katika roho na msamiati wake, bado alianza kupatwa na hisia za mashaka kwa kazi hii ya muuaji. Yanahusiana na nini? Yataisha lini? Ni miongoni mwa maswali yaliyosumbua kichwa chake.

Kana kwamba alikuwa akiyasoma mawazo ya kigogo, alimsalimu na kisha kumwambia, “Usijali, jukumu ninalokupa leo ni la mwisho. Mimi na wewe hatutawasiliana tena baada ya leo. Ni mtu mmoja tu na hayuko mbali kutoka hapa.”

Kigogo alifungua begi lake kama anayetoa nyaraka fulani au fedha. Aliuchomoa mkono wake ghafla ukiwa umeshikilia bastola ambayo aliielekeza kifuani mwa Koba.

“Leo ni zamu yako.” Alimwambia.

Abdul Koba alikwishakuwa mtu mnene, mwenye kiri-batumbo. Lakini bado alikuwa mwepesi, hivyo hakuisubiri risasi kama ilivyo kwa watu wengine. Alichupa kukwepa ya kwanza na kumfanya imchubue kidogo ubavuni. Ya pili, ambayo ilimkuta akiwa tayari na bastola yake mkononi, ilimwingia tumboni. Alifyatua yake, ambayo pia ilikuwa na kiwambo cha sauti. Hakuwa amepata fursa ya kulenga shabaha, hivyo risasi zote mbili zilimkosa kigogo kwa mbali sana. Wakati huo, risasi tano zaidi ziliingia tumboni na kifuani mwake na kumfanya adondoke chini kama gunia la mtama. fahamu zilimtoka mara moja.

Kigogo aliitazama kazi yake na kuridhika nayo, akafanya haraka kuliacha eneo hilo kwa kulirejea gari lake aliloliacha mbele ya kituo cha jirani cha mafuta ya gari.

***

Pamoja na kutoka na tabasamu usoni, pamoja na kumtilia alama ya dole yule msichana wa mapokezi ili kumtoa mashaka, bado rohoni mwangu nilijawa na wasiwasi. Mwenendo wa mambo yangu ulikuwa ukifuata mkondo ambao sikuutarajia, mkondo ambao sikuumba mimi. Kifo cha yule kijana wa hoteli ni moja kati ya mambo yaliyofanya nihisi chombo kikienda mrama. Sikutarajia kuua mtu. Zaidi sikutarajia kuua katika chumba changu, hali ambayo kwa vyovyote ingeamsha udadisi na kisha uchunguzi wa kina dhidi yangu. Kwa bahati mbaya sikuwa na njia. Kijana yule alikisaka kifo kwa jitihada zake zote. Kumuua ilikuwa halali, kumwacha hai ilikuwa hatari zaidi.

Hivyo, nilitembea mtaani harakaharaka hadi mahala nilipokodi teksi na kuielekeza nje kidogo ya mji. Huko, baada ya kuingia katika duka moja na kununua shati na suruali ya jeans, nilikodi gari jingine na kuelekea upande wa pili wa mji. Nilipata choo cha kulipia nikaingia na kubadili mavazi yangu, lile shati la yule kijana nililichana chana na kulitupa chooni. Nilipotoka kwa kiasi fulani nilikuwa mtu mpya.

Nilijua kuwa wajibu wangu ulikuwa kuiacha Dar es salaam na Tanzania mara moja. Nilitakiwa kudandia ndege ya kwanza, treni ya kwanza na hata basi la kwanza mradi nitoke nchini humu mara moja. Hata hivyo, haikuwa rahisi kama inavyozungumzika. Upepo ulikuwa haueleweki. Baharia mzoefu hawezi kujitoma baharini bila uhakika wa safari yake. Hivyo, nilifikia uamuzi wa kujibanza tena nchini kwa siku mbili tatu ili niweze kuusoma mwenendo wa mambo kabla ya kuanza mikakati ya kutoka.

Dar es Salaam sio Hong Kong ambayo maelfu ya wagenu humiminika kila siku na kufanya vyumba vya wageni viwe adimu. Wala sio Bangdadambako mgeni huchunguzwa kwa makini sana kabla ya kupatiwa chumba kwa hofu ya kumkaribisha gaidi ambaye ataishia kujilipuakatika kadamnasi. Hivyo, haikuwa kazi ngumu kupata chumba kizuri katika hoteli moja iliyoitwa Bondeni Inn Resort, kilometa tatu toka katikati ya jiji. Sasa nikiwa mvulana mtanashati, mara tu nilipopatiwa kadi ya chumba nilijifungia chumbani humo na kufanya haraka kurekebisha kasoro ndogondogo ambazo zingeweza kunifanya niunganishwe na yule msichana aliyeuawa muda mfupi uliopita. Kazi ambayo sikuwa nimeridhika nayo baada ya kuifanya kwa pupa mara baada ya kuipeleka akhera roho ya yule mjinga.

Baada ya hapo nilijilaza chali juu ya kitanda, ubongo wa mambo na namna ya kujinasua. Jitihada kubwa ambayo niliuagiza ubongo wangu kufutilia mbali ilikuwa ile shahuku yangu ya kutaka kumfahamu mwajiri wangu aliyenipa kazi hiyo rahisi sana kwa dau nono sana, ni nani? Alinufaika vipi? Alinifahamu vipi? Na anafanya lipi kwa sasa? Nilijitahidi kulifukuza hilo kwa kujua kuwa shahuku hiyo ndiyo ilinifikisha katika mazingira haya kama ningekuwa nimeifanya kazi yangu na kutoweka mara moja, nyuma ya kisogo change. Pamoja na hayo, haikuwa kazi rahisi. Kila nilipopanga mikakati ya kutoka, shahuku ya kujua kila kinachoendelea ilinijia pale katikati ya fuvu la kichwa change, na hivyo kunipa mateso makubwa kisaikolojia.

Mkakati wangu wa kwanza ulikuwa wa kumwokoa mwanangu, kipenzi changu. Licha ya ukweli kuwa naye sambamba ilikuwa hatari, bado pia sikutaka apatwe na ajali yoyote mbaya, ingesababisha tutengane naye. Kwangu yeye alikuwa mwandani, mkono wangu wa pili, mguu wangu wa pili. Hivyo, kazi ya kwanza ilikuwa kumfumua; kichwa pale, mkono pale, mguu kule na kisha kumsafirisha atangulie nyumbani.

Kazi hiyo niliianza mara moja, nilifungua begi langu na kumtoa. Alikuwa tayari katika sehemu mbili. Nikambusu na kuanza kumtatua tena. Dakika chache baadaye alikuwa katika vifurushi vitano, vilivyoandikwa ‘sample’ ndani ya mifuko maalumu ya nailoni ambayo baadaye ilifungwa pamoja ndani ya kijiboksi kilichoelekezwa kwa kampuni fulani kwa anuani fulani ambayo ni mimi pekee niliyeifahamu. Muda mfupi baadaye mwanagu alikuwa tayari kwa safari. Hapa kama ingetokea muujiza, akamatwe njiani ni watu wachache sana duniani ambao wangeweza kutambua kuwa ‘mwanangu’ huyu aliitwa AK 47.

Nisingeweza kusahau mapenzi kwa mwanangu yaliyoanza. Ilikuwa baada ya yale mazoezi marefu ya shabaha na jaribio la kusafirisha yule mwarabu. Ilifuatia kazi nyingine ambayo niliambiwa kuwa ilikuwa nyeti sana.

Nilipewa ramani ya makazi ya mhanga huyo, ratiba yake ya kutoka na kuingia kwake. Hali kadhalika nilipewa picha zake mbalimbali. Alikuwa mtu maarufu sana duniani. Pia alikuwa machachari aliyehusishwa na mambo mengi ikiwemo undumila kuwili kati ya kikundi cha kigaidi cha Wayahudi MOSSAD na magaidi wa AL KAIDA. Iliaminika kuwa yeye alikuwa mtu pekee aliyekuwa na hakika ya kukutana na Osama Bin Laden na kuzungumza naye. Kwamba pia ndiye aliyekuwa akishikilia koba lake la pesa.

Kazi ya kumwinda mtu huyu haikuwa ngumu. Yeye mwenyewe alipenda sana kuwinda wanyama. Hivyo, jioni moja alipookotwa katika mbuga ya wanyama nchini Malawi, risasi ya mwanangu AK 47 ikiwa imejikita katika paji la uso wake kila mmoja aliamini kuwa alikuwa amevuna kile alichokipanda.

Nilisoma habari zote kwa siku kadhaa katika magazeti na kuzitazama katika televisheni. Kama ilivyo ada habari hizo zilididimia na kutoweka ghafla pale zilipokua nyingine, nyeti zaidi za Marekani kuivamia Iraq na baadaye kumkata kichwa mtawala wake, Saddam Hussein.

Kazi ya kuwinda binadamu kwa minajili ya kumtoa roho ni ngumu kuliko unavyoweza kufikiria. Kwanza, wewe mwenyewe unajificha usifahamike, kisha, yeye, kama tarehe yake haijajiri atakuhangaisha hata kwa miezi mkicheza mchezo wa paka na panya. Hivyo, wakati nikifikiria dau langu nono nililolipwa nilijua kuwa ninakula fedha ambazo nilizitumikia, kwani mara mbili tatu nilinusurika kutafunwa na simba, mara moja niliponea chupu chupu kugongwa utosini na nyoka aina ya kobra aliyekuwa tayari amejaza koo lake kwa sumu.

Miezi mitatu baadaye nilipewa jukumu jingine. Hili pia lilimhitaji mwanangu, kumfuta duniani ‘mbwa mweusi’ mwanasiasa mwenye asili ya Kiafrika ambaye alikuwa akija juu katika siasa za Marekani. Nilitakiwa kumfanyia vitu vyangu hadharani ili iwe fundisho kwa watu wengine waliodhani wana haki nchini humo sawa na weupe ingawa wao pia ni wahamiaji toka ulaya.

Haikuwa kazi ngumu. Akiwa mtu wa mikutano na mihadhara kila mara nilimvizia katika moja ya mikutano yake na uielekeza risasi yangu mdomoni wakati ameufungua akisisitiza jambo. Alifia hospitalini ambako inadaiwa kauli yake ya mwisho ilikuwa ‘Aluta Continue.’

Mwaka mmoja baadaye nilihisi natumiwa kwa ujira usiolingana na zigo zito la dhambi nilizokuwa nikichuma. Ndipo nikabuni na kuandaa kifo changu mwenyewe. Lilikuwa pigo kwa waajiri wangu lakini kwangu binafsi ilikuwa faraja.
nakipataje hiki kitabu, na ni tsh ngapi
 
dah kama nakuona vile ukijiandaa kutupa continuation flan matata, endeleaaa....!
 
***

Msichana aliyekuwa mapokezi Hollyday Inn alishangaa kidogo alipomwona kijana mrefu wa kiume akivuta begi lake kutoka nje ya hoteli. Hakukumbuka aliingia lini wala hakujua alitokea chumba kipi. Alimtazama toka aliposhuka kutoka katika lifti na kisha kutembea taratibu kuelekea lango kuu.

Mgeni huyo alipomfikia alimsalimu na kumuaga kwa alama ya dole huku akitabasamu. Alipita hadi nje ambako alionekana akiita gari mojawapo la teksi za hotelini hapo, akaingia. Gari ikatiwa moto na kutokomea.

Mara msichana huyo akamkumbuka Mfaume. Alitazama eneo la kadi wanayoita ‘malaya’ ambayo aliichukua. Ilikuwa haijarudishwa. Hilo lilimtia wasiwasi. Kwa kawaida, kadi hiyo hutumika kwa amri ya Meneja wa hoteli tu, pale mgeni anaposahau na kuifungia yake chumbani au kuondoka nayo. Alikuwa amemwamini Mfaume kwa kujua kuwa ingemchukua dakika chache tu kuirejesha.

Kisha, msichana huyo akabaini kitu gani kilimfanya amkumbuke Tenga Mfaume. Ni shati alilovaa yule mgeni aliyetoka punde. Lilifanana sana na shati alilovaa Tenga Mfaume siku hiyo, shati ambalo siku zote amekuwa akijitapa hotelini hapo kwamba ni yeye pekee aliyekuwa nalo nchini. Lilikuwa moja ya zawadi zake nyingi ambazo alizipokea toka kwa rafiki zake mbalimbali wa ughaibuni waliopata kulala hotelini humo.

“Shati la milionea.” Mara kwa mara Tenga Mfaume alitamka.
















9

Moto ulilipuka upya kufuatia kifo cha Afande Chaku. Vigogo wa kamati maalumu iliyokuwa ikitafuta ufumbuzi wa kifo cha kutatanisha cha Bi. Cleopatra walikuwa bado hawajajinasua katika jinamizi la mwandishi wa habari ambaye walimtegemea kuwa ufunguo la sakata zima kwa kiwango fulani. Wakiwa bado wanalitafakari hilo mara yameibuka mengine. Mpelelezi mahiri, aliyetwishwa mzigo wa kuongoza timu mahususi ya kutafuta ufumbuzi naye ameuawa kinyama muda mfupi uliopita!

Taarifa za kifo chake ziliwasilishwa na Inspekta Matata katika kikao cha dharura kilichoitishwa usiku huo. Kwa mujibu wa maelezo yake kikaoni hapo maiti ya Chaku iligunduliwa katika hoteli ya Sunlight ya ufukwe wa bahari maeneo ya Msasani. Mmoja wa wahudumu wa hotelini hapo, ambaye alimuhudumia marehemu aliuarifu uongozi wa hoteli mara alipobaini kuwa alikuwa akizungumza na maiti wakati akijaribu kumwamsha ili amlipe pesa za vinywaji alivyotumia. Alihisi mteja wake huyo alikuwa marehemu pale alipomgusa kifuani na kushangazwa na jinsi alivyopoa. Baadae aliona damu iliyoganda kwenye kifua chake, ambayo marehemu aliilalia. Kijana huyo alikuwa jasiri wa kutozungumza hadharani tukio hilo hadi alipompeleka chemba meneja wake ambaye baada ya kuthibitisha aliitarifu polisi.

“Maiti amechukuliwa bila ya wateja wala wafanyakazi wengine kujua.kwao walidhani ni mlevi mmoja aliyezidiwa anabebwa kupelekwa nyumbani kwake.” Matata alikitaarifu kikao.

Wenzake, waliopigwa butwaa walimtazama kwa macho yaliyojaa maelfu ya maswali. Mkuu wa majeshi alikuwa wa kwanza kuyaweka maswali yake hadharani. “Kwasasa kinachoendelea ni kipi?” Alimuuliza.

“Kwanza tulichokifanya ni kumuhifadhi meneja wa hoteli na msaidizi wake. Tunaamini watatusaidia sana.” Alijibu.

“Kuwahifadhi kwa maana ya kuwatia ndani, sio?” Mkuu huyo wa majeshi aliuliza.

Inspekta Matata alikubali kwa kichwa kabla hajaongeza, “Wako ndani, lakini katika mazingira tofauti. Wako chumba cha peke yao, wanakula na kunywa wanachotaka.”

“Kwanini umewaweka ndani?” Kigogo mwingine aliingilia kati.

“Kwa usalama wao na wetu pia.” Matata alimjibu kwa sauti ambayo ilimwonyesha kila mtu katika meza hiyo ya mviringo ahisi anavyojisikia; mtaalamu anayezungumza na makinda katika taaluma hiyo.

“Fafanua…” Kigogo yule alisisitiza.

“Nini?”

“Hayo madai ya usalama wao na wetu. Sijakuelewa.

Matata alitabasamu kidogo kabla hajaeleza, “Hakuna anayejua Afande ameuawa na nani. Ni wao peke yao pamoja na muuaji wanaojua kuwa afisa muhimu kama yule ameuawa. Hivyo, tuliona ni hatari kuwaacha mitaani kabla upepo haujatulia.” Alikohoa kidogo. Akaendelea, “Hali kadhalika, wanao mwelekeo wa kutusaidia sana. Yule mhudumu anadhani kuwa alimuona muuaji na kuzungumza naye na kuwa anaweza kumtambua wakati wowote. Kwamba ni mtu mrefu na mtulivu aliyekwenda hotelini humo na kumuomba huduma ya kinywaji ambayo aliitaka ipelekwe ufukweni ambako marehemu aliketi peke yake. Kisha, alienda akaketi meza moja na merehemu. Wakati anampelekea oda yake mhudumu anadai alipishana na mteja huyo akiwa na haraka. Awali, alidhani kuwa anaelekea maliwatoni lakini alipoona kimya ndipo alipoiendea meza ile na kutoa vinywaji ambavyo havikutumika na kumdai Afande Chaku.”

Wenzake walimkazia macho. Alikuwa akisema ukweli lakini ukweli huo haukuweza kuwaridhisha. Mjumbe mmoja alishindwa kustahimili, “Nikuambie kitu Inspekta?” hata kabla ya kusubiri jibu la Matata aliendelea. “Maelezo yako ni matamu sana lakini vitendo hatuvioni. Sidhani kama kuna yeyote kati yetu aliyekutarajia kuwa mtoa habari za matukio badala ya ufumbuzi. Mtu kauawa mbele ya Rais, tunataka kujua kama muuaji alimkusudia Rais au la. Aidha, tunamtaka muuaji huyo akamatwe. Tulichoambulia kwako ni taarifa ya kifo kingine, ambacho kinahusiana sana na cha Cleopatra. Haya, hata kabla hilo pia kupatiwa ufumbuzi leo unatuletea taarifa nyingine ya kutisha zaidi; kuuawa kwa mpelelezi wako mkuu katika sakata hili. Mimi binafsi nasikitika kuwa naanza kupoteza imani na uwezo wako.”

Matata alijaribu kutabasamu kuficha hasira kali iliyompanda ghafla na kumpanda kooni. Tabasamu lilikataa. Akaishia kumkazia macho mjumbe huyo. Alikasirika zaidi alipowatazama wajumbe wengine na kuona wakitikisa vichwa kumuunga mwenzao mkono.

“Nadhani huu ni wakati wa kufikiria kung’atuka,” alinong’ona kwa sauti dhaifu.

***

Masudi Kipanya, Patrick Mgata, David Chikoko na wengineo walikuwa miongoni mwa wachoraji mashuhuri sita walioshangazwa na kitendo cha polisi kuwataka msaada. Kwa utamaduni wa Tanzania kuwasaidia polisi kuna maana moja tu, kukamatwa, kuwekwa rumande na kuanza kumiminiwa maswali na vitisho. Hivyo ilimshangaza kila mmoja wao, alfajiri hiyo walipotembelewa na polisi waliovaa kiraia.

“Kipanya?”

“Masoud Kipanya anaishi kwenye kurasa za magazeti.” Aliwajibu.

Polisi walicheka. Mmoja wao alitoa kitambulisho chake.

“Tunahitaji msaada wako. Unaweza kuvaa mara moja tutoke?” alieleza.

Moyo wake ulipoteza mapigo. Hata hivyo, sauti yake haikupotezan usanii pale alipowauliza, “Mbona hamna pingu?”

“Za nini”

Alioga upesiupesi, akabadili nguo toka katika mavazi ya kulalia na kisha kuongozwa kwenye gari lililokuwa na namba za kiraia. Ni humo alimowakuta wakina Chikoko na Mgatta. Tofauti na alivyotegemea, badala ya kupelekwa Kituo cha Kati, gari ilielekezwa nje ya mji likifuata njia ya Bagamoyo. Lilichepuka na kuelekea kulia hadi katika Hoteli ya Kunduchi ambako lilisimama. Walielekezwa katika moja wapo ya vyumba vya mikutano ambako waliombwa kujisikia huru.

“Tunahitaji msaada wenu katika suala nyeti la kitaifa.” Mmoja wa maafisa waliowaleta alieleza. “Jana kama saa kumi hivi zilizopita mtu mmoja muhimu sana ameuawa.Hapa tunaye mtu mmoja ambaye anaamini alimwona muuaji. Tumempa mamia ya picha za watuhumiwa sugu wa mauaji, ndani na nje ya nchi, hakuweza kumtambua. Hivyo, nyie kama wachoraji, tunadhani mkikaa naye na kumsikiliza huku mkifanya uchawi wenu kwenye makaratasi au kompyuta bila shaka tutaipata sura yake halisi.”

Kwa mara ya kwanza wachoraji hao walitabasamu kwa dhati. Kwa gharama za jeshi la polisi walipatiwa kifungua kinywa cha haja. “Ambaye hachori bila kutia vitu vikali tumboni anaruhusiwa kunywa chochote anachotaka.” Mwenyeji wao alizidi kuwakarimu.

Saa moja baadaye, mhudumu ambaye alikuwa akiwasaidia polisi kumpata mtuhumiwa alitambulishwa kwao. Kwa kila hali alikuwa taabani, kukesha, maswali elfu moja na moja aliyoulizwa na tukio la kuona maiti ya mtu bila kutegemea vilikuwa vimemmaliza. Hata hivyo, baada ya nusu saa ya mizaha ya wachoraji hao, chai ya nguvu na kushushia bia mbili baridi, alichangamka.

Aina nyingine ya maswali ikaanza.

“Pua pana kama hii?”

“Hapana, imechongoka kidogo.”

“Miwani?”

“Hakuwa nayo.”

“Nywele?”

“Fupi tu za kawaida.”

Na kadhalika na kadhalika. Ilitayarishwa michoro aina aina. Mhudumu huyo, ambaye baadaye alifahamika kuwa aliitwa Mwanakatwe, alitoa ushirikiano kwa kila mchoraji. Alitazama kila mchoro wa awali na kukanusha hapa na kuelekeza pale.

Siku ilipita bila mafanikio.

Siku ya pili matumaini yalianza kuonekana. Mwanakatwe alianza kutoa maelezo madogomadogo. “Urefu huu una tofauti kidogo… viatu vilikuwa vyeusi… na kadhalika. Wachoraji wawili walimtia matumaini zaidi. Alitazama picha zao kwa makini, nuru ya utambuzi ikizidi kuchanua katika macho yake.

Michoro hiyo ilipowekwa katika kompyuta na utaalamu wa Coral drawing na graphic designing kutumika baada ya marekebisho mawili matatu, Mwanakatwe aliangua kicheko.

“Ni huyu hapa,” alisema

Kipanya na Mgatta walitazamana kwa mshangao.

Maafisa wa upelelezi walipoitwa kutazama michoro hiyo miwili ambayo Mwanakatwe aliafikiana nao, wao pia walitazamana kwa mshangao. Walichukuana chemba ambapo mmoja alimuuliza mwenzake, “Nadhani unamfahamu mtuhumiwa wetu.”

“Bila shaka. Si mwingine zaidi ya Joram Kiango.”

“Inawezekana?”

“Nani anajua?” alimjibu.

***

“Joram Kiango!” ilinguruma sauti ya kigogo mwingine. “Ni Joram Kiango! Na bado mmekubali kumwacha hai katika swala nyeti kama hili! Mnajua mmefanya kosa ambalo tutalijutia maisha yetu yote?”

Inspekta Matata alimjua fika Joram Kiango. Kwa kiasi fulani, alimchukia kama ilivyokuwa kwa vigogo wenzake wengi wenye mengi ya kuficha. Ushoga wa siri ulioanza baina ya Inspekta mstaafu, Kombora ni moja ya mambo yaliyofanya mzee yule ajikute akistaafishwa mapema wakati alikuwa bado na nguvu na akili zake timamu. Moja ya ajenda alizopewa Matata ni kufuta kabisa Ujoram Kiango katika Jhamuhuri ya Tanzania. Hivyo yeye pia angeshusha pumzi kama bastola iliyomwondoa Chaku ingefanya hivyo kwa Joram Kiango pia. Kwa bahati mbaya, haikufahamika mapema kuwa mgeni ambaye alikuwa akitarajiwa na Afande Chaku angekuwa Joram Kiango. Kamwe asingeondoka akiwa hai.

Kwa sauti, Matata alisema, “Haikufahamika mapema. Lakini maadamu hili limetokea, tayari amejiweka katika mstari wa shabaha. Toka kesho soma magazeti, tazama televisheni uone. Hata kama atajifanya panya ajichimbie ardhini kama Saddam Hussein tutamchoropoa na kumfunga mdomo kabla hajaufungua.

Msikilizaji wake alimtazama kwa macho yenye mashaka. Akasema, “Inspekta, nadhani unamfahamu Joram Kiango. Kamwe si mtu wa kubeza na wala hatabiriki.”

“Namjua sana,” Matata alisema akitabasamu. “Ni play boy tu mwenye bahati. Naona bahati yake imefika ukingoni. Tulia uone.”

Kimya kifupi kilitawala kati yao. Mmoja akaitazama saa yake, wa pili akiwa amejiinamia. Aliyeinama aliinuka na kutazama huko na huko. Yeye pia aliitazama saa yake kabla hajasema, “Nadhani sina budi kuondoka.” Kisha, kama aliyekumbuka jambo aliketi tena na kumkazia macho Inspekta Matata. “Sidhani kama nina haki ya kukufundisha wajibu wako. Lakini kuna swala hili la huyu mtu ambaye tayari tumemtumia mara mbili, kumwondoa yule mwandishi na sasa afisa wa upelelezi. Unadhani tuko salama kuwa na mtu anayefahamu yote hayo miongoni mwetu?”

Matata aliangua kicheko, “Yule niachie mimi. Tutampa ujira wake wa mwisho kati ya leo na kesho. Ataupokea lakini hatautumia. Tayari amejichimbia kaburi lake mwenyewe.

“Nani ataifanya kazi hiyo?”

“Niachie mimi.”

Mgeni aliinuka tena, kisha akakumbuka jambo jingine na kumkazia macho Matata, “Hili ni kati ya mimi na wewe. Niambie tafadhali. Nani aliyemuua Cleopatra?

Inspekta Matata alicheka kidogo kabla ya kumjibu, “Sijui.”

“Una uhakika?” Kigogo alisisitiza.

“Kwanini nikudanganye?” alimjibu kwa swali jingine.

Kigogo alimtazama kwa macho ya kumsoma rohoni. Chochote alichokitafuta katika uso huo hakukipata. Akageuka na kuanza kuondoka. Matata akabonyeza tufe chini ya meza yake, sehemu ya ukuta ikafunguka na kuruhusu mlango wa lifti kufunguka, mgeni akaingia na kupaa toka katika chumba hicho cha siri hadi ghorofa ya pili ambako ilifunguka naye kutoka. Akatumia ngazi kushuka hadi chini ambako mlango wa kioo ulifunguka wenyewe mara alipoukaribia. Alipita ndani ya bustani kubwa yenye miti na maua mbalimbali hadi alipoliacha gari lake. Akalitia moto. Geti la lango kuu lilifunguka lenyewe vilevile kwa harufu au uzito wa gari lake, ingawa mlinzi mwenye sare za kampuni moja ya ulinzi aliketi pale akisoma gazeti.

Kigogo aliingia mitaani na kutokomea.

Matata alimtazama mgeni wake katika screen maalumu hadi alipotokomea mitaani. Screen hiyo ni moja ya vitu ambavyo vilikuwa siri hata kwa mkewe katika jumba hilo. Siri nyingine ilikuwa chumba hicho cha chini ya ardhi. Ni watu wachache sana waliofahamu uwepo wake. Na wachache zaidi walioweza kukifungua. Mhandisi aliyeongoza ujenzi huo alikufa kitambo kwa ajali ya gari. Msaidizi wake aliuawa na majambazi nyumbani kwake.

Machoni mwa wapiti njia, nyumba hii ilikuwa ya kawaida tu, yenye ghorofa mbili, ambayo kama nyumba nyingine nyingi jijini Dar es Salaam iliota na kupaa kama uyoga. Hakuna aliyefahamu fika jinsi ilivyokuwa ndani.

Kama ilivyokuwa kwa mwenye nyumba, machoni mwa watu wengi alikuwa Afisa wa juu wa ama jeshi la polisi ama usalama aliyekuwa akiongoza kitengo nyeti ambacho haakikutofautiana sana na kile cha polisi wa kimataifa INTERPOL. Kwa sura alikuwa mtu makini, mzalendo halisi, aliyekuwa tayari kupoteza maisha yake kulinda maslahi ya nchi yake. Lakini, kwa sura yake ya pili, ambayo daima ilifichwa katika kinyago cha umakini na uzito wa majukumu, alikuwa mtu wa kuogopwa. Toka miaka ya themanini, fisadi alipogeuka shujaa, uongozi ulipoanza kununuliwa kwa pesa, huku aibu ya kufanya madhambi ikizidi kuyoyoma; Matata alijikuta katikati ya dimba hilo. Alifanya chochote kilichomwongezea chochote, mradi mfuko wake wa mafichoni ulizidi kutuna. Wakorofi wengi waliokwenda kinyume cha matakwa ya watu wake ama walifutika duniani ama waliozea gerezani; wawili watatu walipata kuponyoka na kukimbilia nje ya nchi ambako hawakupata hali ya kutia tena miguu yao katika ardhi ya nchi yao. Mmoja kati yao tayari amefia huko ugenini kwa ajali yenye utata.

Zamani kidogo tatizo la Matata lilikuwa fedha, namna ya kuzipata. Sasa tatizo lake halikuwa fedha isipokuwa namna ya kuzitumia. Ingawa siku hizi haikuwa tena aibu kutangaza utajiri wake japo mchafu kiasi gani, bado kwa nafasi yake fursa hiyo hakuwa nayo. Kwa majina ya ndugu zake na watoto wake tayari alijenga hoteli nne za kitalii. Alikuwa na hisa nzito katika kampuni mbili za uwindaji, ikiwa ni pamoja na kumiliki hekta elfu kumi za ardhi ya kitalii. Nchini Kenya na Afrika Kusini alikuwa na majengo ya ghorofa kumi na tano yaliyotumika kibiashara. Pamoja na miradi yote hiyo kutumia fedha bado lilikuwa tatizo. Swala la mfuko wa madeni ya nje, EPA, swala la Richmond, mikataba tata ya madini na uwindaji kharamu ni miongoni mwa maswala ambayo yalikuwa yamemmwagia neema zaidi na zaidi. Dola za marekani bilioni mbili alizopokea katika harakati za kuziba na kuzibua mambo zilikuwa na miezi tele chumbani humu zikisumbua kichwa chake.

Katikakati ya fanaka zote hizo yule mwanamke wa Ikulu akafumuliwa kichwa. Halafu, toka kusikojulikana anaibuka huyu mtu anayejiita Joram Kiango.

“Atanitambua,” Inspekta Matata aliapa kimyakimya.

***

Mara nyingi Joram Kiango aliwapuuza polisi,lakini kamwe hakupata kuwadharau, hasa pale inapotokea mmoja wao kuuawa kinyama huku akiwa katikati ya suala nyeti, polisi, kama nzige au nyuki waliolala, huamka na kuanza mashambulizi makali kushoto na kulia.

Joram Kiango alilitegemea sana hilokwa kifo cha Afande Chaku. Ni kwa kuamini hivyo ndipo mara tu alipoiacha maiti ya Chaku alifanya haraka kurudi nyumbani kwake ambako alitumia dakika zisizozidi ishirini tu kuchukua vifaa alivyovihitaji; kompyuta yake ya mapajani, bastola, mabomu mawili ya machozi, suitcase yenye mavazi yake ya kazi ainaaina na nyaraka zake nyeti. Kisha alitegesha alarm yake ambayo humwarifu mara chumba chake kinapotembelewa na mtu ambaye hakumtegemea. Muda mfupi baadaye alifungia gari yake katika gereji na kwa kupitia mlango wa uani aliingia mitaani.

Dar es Salaam ina hoteli bubu nyingi sana. Baadhi zikiwa katika maeneo duni ambayo hayafikiki kwa gari isipokuwa vichochoro vya njia ya miguu. Moja ya hoteli hizo iliitwa Darajani Inn. Iko katika mtaa wa Manda, Magomeni, katikati ya uchochoro maarufu unaoiunganisha Magomeni na Kigogo, Mburahati hadi Luanga. Akiwa amefunika kichwa chake kwa kofia pana ya wachunga ng’ombe na sehemu kubwa ya uso wake kwa miwani mieusi, hakuna aliyeweza kumtambua mara moja. Alipatiwa chumba cha uani ambamo alishangaa kubaini kuwa kulikuwa na bafu na choo cha kujitegemea huku maji yakitoka katika mabomba kama kawaida. Aidha, kulikuwa na televisheni ndogo ambayo mwenyeji wake aliiwasha kumtia matumaini zaidi.

“Tukuletee nini, mzee?” tuna bia kila aina na kuku wa kukaanga.” Mhudumu huyo, mvulana wa miaka ishirini na mitano, aliuliza.

Joram Kiango alikuwa na njaa. Alikuwa na kiu vilevile. Lakini njaa na kiu yake kubwa zaidi ilikua kuijua hatma yake katika mkasa huu. Hivyo, alimruhusu kijana huyo kwa kumwambia kuwa pindi atakapohitaji chochote atamwarifu.

Mara kijana huyo alipotoka, Joram Kiango aliufunga mlango wake kwa komeo na kisha kuketi kwenye kiti pekee chumbani humo, daftari dogo la Afande Chaku likiwa mikononi mwake. Akijua kuwa atake asitake tayari amelazimishwa kuingia katika sakata la Cleopatra alijikuta akilazimika kulisoma daftari hilo kwa makini na utulivu mkubwa, kwani lilikuwa kiungo pekee baina yake na marehemu.

Afande Chaku alikuwa mwandishi wa aina yake. Kuna maeneo ambayo aliyaandika mambo mengi kwa ufupi sana, mara nyingine neno moja tu kama, ‘vurumai.’ Maeneo mengine, hasa pale alipohojiana na wahusika ana kwa ana alinukuu kila kauli kwa uzito wake. Jina la bosi wake Afande Chaku, Inspekta Matata, lilitajwa mara mbili tatu huku mara kwa mara likifuatiwa na alama ya kuuliza (?) au ya mshangao (!) ambazo Afande Chaku aliziandika kila baada ya nukuu mbili tatu. Haikumchukua muda Joram Kiango kushuku kuwa Afande Chaku alikuwa katika shinikizo zito ambalo halikutoka popote isipokuwa kwa Matata.

Tathmini ya Afande Chaku juu ya mauaji ya Cleopatra pia yalimfumbua macho Joram Kiangon kwa kiwango fulani. Maelezo hayo mafupi yalimthibitishia kile alichokuwa akikifikiria muda mrefu kwamba ili kumuua ama Rais ama mtu karibu na Rais, mbele ya halaiki kama ile na muuaji atoke salama salimini, kwa vyovyote alikuwa mbali na alitumia silaha kubwa. Afande Chaku alimtajia aina ya silaha, jumba na chumba ambacho aliamini muuaji alikitumia. Joram aliafikiana naye mara moja.

Mazingira ya kifo cha yule mwandishi koko pia yalimsisimua Joram. Mateso ya kishetani aliyoyapata na purukushani za chumbanihumo,vitu vyote hadi magodoro yakiwa yametupwa ovyo ilifanya Joram akubaliane na hisia za Afande Chaku kuwa chochote ambacho wauaji walikuwa wakitafuta ama walikipata kwa shida ama hawakukipata kabisa.

Mtu anayeitwa ‘King Suleiman’ katika kimemo alichokuwa nacho Afande Chaku ndani ya daftari lake nalokilimvutia Joram, hasa baada ya maelezo mafupi kuwa kilikuwa katika mfuko wa nguo alizovaa wakati mauti yanamkuta. Hata hivyo, yeye pia kama Afande Chaku, alivunjika nguvu baada ya kukuta nukuu za Afande Chaku katika mahojianao yake na mume wa marehemu zikifafanua kuwa ‘King Suleiman’ alikuwa yeye.

Nukuu ndogo ya Afande Chaku juu ya mtumishi wa hoteli, ‘anayehitajika kuzungumza naye,’ ikiwa pamoja na namba yake ya simu ilimvuta Joram. Baaada ya kuona alama ya nyota ambayo Afande Chaku aliichora juu kwa namna ya msisitizo. Joram Kiango alinukuu katika simu yake na kuamua kumuona yeye kwa niaba ya merehemu.

Baada ya kusoma nukuu zake kwa makini, ikiwa pamoja na zile ambazo hazikuhusiana na suala hilo, Joram Kiango alijikuta katika hali ile ile aliyomshuku Afande Chaku kuwa nayo; maswali mengi pasipo majibu. Swali la msingi likiwa lile lile ambalo lilimsumbua kila mtu; nani alimuua Cleopatra na kwasababu gani? Maswali mengine kama uhusiano uliopo baina ya kifo cha Cleopatra na yule mwandishi au kifo cha Afande Chaku na Cleopatra yalimsumbua pia. Hata hivyo, aliamini jibu la swali moja likimwelekeza kwa jingine. Alilihitaji jibu hilo, kwa udi na uvumba,akizingatia ukweli kuwa upatikanaji wake kwa namna moja hadi nyingine ulikuwa wake. Hakujisikia kama alikuwa na mtu mwenye uwezo wa kuishi hai mapangoni kama Osama walau kwa wiki mbili tu.

Tatizo lilikuwa aanzie wapi naswali lipi.

Alifikiri kwa muda wa dakika mbili tatu kabla hajakumbuka jambo. Akalichukua tena daftari la hayati Chaku na kulifunua taratibu hadi alipofikia ukurasa uliotaja aina ya silaha inayoshukiwa kumuua Cleopatra. AK 47 bunduki maarufu duniani hasa kwa wapigania uhuru wa misituni na wadunguaji katika nchi mbalimbali duniani. Bunduki hiyo,iliyogunduliwa na Mrusi, Avtmat Kalashnikova mwaka 1947 na baadaye kuboreshwa tena na tena na wataalamu mbalimbali, ilikuwa kipenzi cha wadunguaji wengi duniani. Ikiwa nyepesi, inayokubali mabadiliko katika maumbile yake ilikuwa imetumiwa mara nyingi katika shughuli hizo. Hivyo Joram hakusita kuafikiana na Afande Chaku katika hisia zake, kwamba ilitumika kumuua Cleopatra.

Baada ya kulitafakari hilo, Joram aliifungua suitcase yake na kuichomoa kompyuta yake. Akachomeka nyaya kwenye umeme kisha kuiwasha. Alifungua mtandao pepe na kutafuta mtandao wa Google ambako alipata kurasa zilizomweleza mengi zaidi kuhusu AK 47, majeshi ya nchi, ya waasi, vikundi na matukio mbalimbali yaliyoihusisha silaha hiyo. Alipotosheka na mtandao huo alihamia katika mitandao mingine, kama Yahoo, Gmail, Hotmail na mengineyo, na kupokea majibu ambayo aliyachambua kwa makini. Kwa mfano, alitaka kujua mauaji ya kigaidi ambayo AK 47 ilitumika toka miaka kumi iliyopita. Majibu yalikuwa lukuki, ya kusisimua.

Akiwa mdau katika ufuatiliaji wa maswala ya aina hii alitumia namba yake ya siri kuingia katika mitandao nyeti zaidi iliyoelezea matukio ya silaha hiyo kwa undani zaidi. Matukio yapatayo arobaini na nne yaliripotiwa kwa uwazi, majina au aina ya watuhumiwa yakitajwa au kupendekezwa na wahanga waliopata kupoteza maisha yao kwa silaha hiyo.

Carlos Ramirez, yule mtuhumiwa mashuhuri anayetumikia kifungo, alitajwa mara mbili tatu kuhusika na matukio yapatayo matatu ya udunguaji kwa AK 47. Katika tukio moja, mwanasiasa mmoja wa Amerika Kusini aliuawa. Tukio la pili, Marekani, Washington DC Gavana wa jimbo alijeruhiwa vibaya na kuponea chupuchupu. Tukio la tatu lililomhusu Carlos na kufanya ashukiwe lilitokea katika nchi za Kiarabu dhidi ya Rais mmoja ambaye alionekana kibaraka kwa utawala wa Israel. Huyu, alifia hospitalini, lakiniilikuwa baada ya kueleza jinsi mtu anayejiita mkono wa Zibril alivyomtumia ujumbe wa vitisho mara tatu kabla ya jaribio hilo.

Joram hakuona kama huyu alikuwa mtu wake, kwani tayari alikuwa gerezani, pia mara nyingi alitoa onyo kabla ya kutekeleza kusudio lake. Aidha Carlos alikuwa mwanasiasa zaidi.

Joram aliendelea kuchimbua. Watuhumiwa wengine kadhaa hawakumvutia kabisa. Matukio yao hayakuonyesha kuwa na uwiano wala malengo maalumu isipokuwa ama wazimu wa mtu aliyekuwa nyuma ya silaha hiyo ama uroho wa pesa.

Wakati akikaribia kuvunjika moyo Joram alikutana na tukio moja lililomfanya asite kuzima kompyuta na kutafuta usingizi. Ilikuwa baada ya kukutana tena na taarifa ya mauaji ambayo yamekuwa yakiwasisismua sana wanahabari na wachunguzi wa masuala ya ugaidi wa kimataifa, mauaji ambayo mtafiti mmoja alipata kuyaita ‘Mkono wa Jibril,’ jina ambalo liliwavutia wana habari hata wakaanza kulitumia kulitumia katika taarifa zao kila yalipotokea mauaji ya aina ile. Mauaji ambayo muuaji hakupata kuonekana wala kutuhumiwa kwa vigezo vya dhati na mpelelezi yeyote yule duniani. Ilikuwa kama mkono wa Jibril ulipita mahala kama upepo, akaua kwa namna ile ile na silaha ile ile, kabla ya kuibuka upya, miaka kadhaa baadaye katika nchi tofauti, kwa kazi tofauti.

Joram Kiango, kama tu yeyote yule aliyevutwa na habari yoyote iliyohusishwa na ‘Mkono wa Jibril’ alizisoma habari hizo kwa makini na tafakuri. Katika miaka mitano iliyopita zaidi ya matukio tisa yalihusishwa na mkono wa Jibril. Aina ya silaha iliyotumiwa, uhakika wa shabaha na kutoweka kwa muuaji bila kuacha chembe chembe yoyote ya kasoro ambayo ingeweza kumfanya apatikane. Hata hivyo mauaji matano kati ya hayo yalitibuliwa toka mikononi mwa ‘Mkono wa Jibril’ baada ya watuhumiwa kadhaa kupatikana na ushahidi kudhihirisha kuwa waliyafanya au kushiriki.

Mauaji matatu kati ya hayo yaliendelea kuwa kitendawili, moja likiwa kifo cha yule mrithi wa tajiri wa kiarabu, Abdul Karim. Kifo cha pili kilikuwa cha yule kadinali aliyetarajiwa kuwa papa kufuatia muda wa papa aliyekuwa madarakani kukaribia ukingoni. Cha tatu kilikuwa kifo cha Rais mmoja aliyefunguliwa. Vifo hivi vilikuwa vikimshawishi Joram Kiango kuwa vilitokea kwa mkono wa mtu mmoja, mkono wa Jibril.Joram aliamini kuwa matukio hayohayo yalifanyika kwa mkono mmoja hasa ikizingatiwa kuwa risasi ilikuwa ileile, ilifumua paji la uso vilevile na muuaji kutoweka kama tone la maji katika bahari.

Hivyo, aliposoma tena habari zilizokusanywa na watayarishaji wa mtandao huo juu ya ‘Mkono wa Jibril’ akili yake ilizinduka ghafla alipoyalinganisha na tukio la kifo cha Cleopatra. Kwa kusoma daftari la Chaku na aina ya risasi iliyotumika,ukamilifu wa shabaha na kutoweka kwa muuaji, hakuwa na shaka kuwa mkono uliotumika ulikuwa ‘Mkono wa Jibril,’

Kwa namna fulani, Joram alijisikia faraja kwa kulibaini hilo. Aliamini kuwa ilikua hatua moja mbele. Hata aliichukulia kuwa ilikuwa hatua fupi sana, kwani bado ilizua maswali mengi zaidi ya majibu. Mkono wa Jibril ni moja ya makusudi ya watu? Kwa uzoefu wake Joram alishuku kwa kuwepo kundi la magaidi kuliko mmoja mmoja kwani ndani ya kundi, kuna mmoja, siku moja atatapika ukweli, ama katika ulevi ama kwa matumizi ya fujo ama hata usaliti tu. Gaidi mmoja mmoja ni yeye na roho yake. Hatatoa siri zake kwa gharama zozote hata kwa kumwuza mama yake mzazi.
best leo umejitahidi,hauna lawama kabisa
 
Back
Top Bottom