Hadithi: Kizuizi

Hadithi: Kizuizi

Jose B, bora usihangaike kumtafuta lameck, unaenda kukutana na kifo chako sasa, umbea umekuzidi mtoto lol!
 
Jose B, bora usihangaike kumtafuta lameck, unaenda kukutana na kifo chako sasa, umbea umekuzidi mtoto lol!

Kama namuona sumu itakavyomuua taratibu.Ila amezidi kwa kweli na jose B bila shaka atakuwa ni mjita
 
  • Thanks
Reactions: ram
Yaani atakufa aache kibanda cha tigo pesa, Jose B ni mjita huyu, kama sio mjita atakuwa mkerewe

Au mkara maana ndo tabia zao zilivyo za kupenda umbea.Ila namuonea huruma kwa maisha aliojichagulia kuishi.Na hii story itakuwa na kuuana tu
 
  • Thanks
Reactions: ram
HADITHI: KIZUIZI.


SEHEMU YA KUMI NA TANO



****

Hakuna chozi linaloweza kubadili msiba kuwa sherehe, na hakuna kilio kinachoweza kumbadili aliyekufa aweze kurejea.

Kilio huwa ishara ya uchungu, kisha maisha yanaendelea katika hali ya utofauti kwa muda mrefu kisha huzoeleka.

Emmy hakupata mtu sahihi wa kumtuliza, kila aliyejaribu kumtuliza ni sawasawa alikuwa anampigia Kondoo zeze ili akate mauno, jambo lisilowezekanika.

Mama yake alikuwa amekufa kwa kushambuliwa na sumu kali iuayo mara moja baada ya kupenya katika ngozi.
Mtu aliyejaribu kwa kiasi fulani kumtuliza Emmy japokuwa sio sana alikuwa ni mwanaume shujaa aliyeyakabidhi maisha yake kutetea wengine na kuwalinda.

Mwanajeshi kamili Lameck John Sulube.

Emmy alitulia kwa sababu hakuwa na taarifa ya marejeo ya mwanajeshi huyo, na pia ile hatia ya kuzini nje ya ndoa ikaibuka upya. Akausahau msiba kwa sekunde kadhaa. Maneno ya Lameck yalikuwa yaleyale ‘Ni mipango ya Mungu!! Usilie sana utakufuru!!, Bwana ametoa na bwana ametwaa!!’. Maneno ambayo huwa hayana maana kwa mfiwa.

Ukaribu wa Emmy na Lameck Sulube haukumshtua mtu yeyote ambaye aliijua kwa uchache familia ile. Waliwatambua hawa kuwa ni mtu na baba yake mdogo.

Hata James mumewe hakutilia mashaka yoyote. Alikuwa anamjua vyema Lameck, anamfahamu fika kwani wakati anamrandiarandia Emmy aliwahi kukunjana mashati na huyu bwana. Lakini hakuchoka hadi alipofanikiwa kumuoa na sasa ni mjamzito.

Ila jicho moja lilikuwa na mashaka na ukaribu ule.

Akiwa amejivika suti nyeusi iliyomkaa vyema kijana huyu anayekimbilia miaka ishirini na mbili, kichwa chake kikiwa na nywele fupi zilizopakwa mafuta ya kung’ara, kiatu cha bei ghali kikiuvaa mguu wake. Kijana huyu alikuwa mtulivu sana, leso yake mkononi akipambana na jasho ambalo linataka kumharibia mwonekano wake. Mkono mmoja alikuwa na funguo zilizofanana na za gari.nani anajua huenda nayeye alikuwa ameegesha gari lake nje ya nyumba.

Kwa kumtazama usingeweza kudhania yupo katika dunia nyingine, akijadili mambo yake tofauti kabisa na msiba unaoendelea.

Zilipigwa nyimbo za kusihi watu waandae nyoyo zao kwa sababu hatujui saa wala dakika ya mwisho wetu, yeye hakuzisikia bali alihisi anapigiwa makelele na wachina wanaoimba nyimbo zao kwa lugha yao ngumu.
Hatimaye ukafika wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.

Kutokana na uwingi wa watu katika msiba huu, ilibidi mwongozaji atoe utaratibu maalumu kabisa wa kuuaga mwili wa marehemu Devotha.

Alianza kwa kuiita familia ya marehemu, hapa akawaita watoto na baba. Wakaaga.
Dada, mawifi, shangazi, mama wadogo. Wakaaga.
Baba wadogo, baba wakubwa, mashemeji, wajomba, kaka. Nao wakajongea waweze kuaga.

Yule kijana aliyekuwa amejikita katika kujipangusa jasho akasitisha zoezi lile, akaiacha jasho itiririke, akajisahau kuwa alikuwa amevaa suti, akaanza kuhaha huku na huko.

Akazidi kujiuliza ile sura kwa nini inamvutia.

Mwanzoni alidhani kuwa ni mteja mmojawapo aliyewahi kufika katika banda lake kwa ajili ya huduma za kuweka na kutoa pesa.

Lakini sasa akili ikamruka hakutaka kuamini kuwa yule ni kama anavyomdhani.

“Samahani kaka mambo vipi. U mwenyeji wa maeneo haya.” Aliuliza kwa sauti tulivu, akiwa amelitoa koti la suti na kulitupia begani.

Jose B waukweli anaingia kazini.

“Kiasi fulani kwani vipi?.”

“Hivi yule jamaa aliyevaa kadeti ndiye Thomas, mdogo wake na marehemu?” alihoji kiujanja Jose B.
Mng’aro wake na mavazi yake yakamfanya aheshimike.

Yule bwana hakuwa anajua sana juu ya ile familia. Lakini alimuita mwenye ukaribu na familia ile.
Jose B akauliza swali lilelile. Akapatiwa jibu kuwa yule anaitwa Lameck, ni shemeji wa marehemu.
“Na yule mwanamke waliyekuwanaye ni kama mtoto wake.” Alijibu hata ambayo hajaulizwa.
Na hivyo ndivyo Jose B alikuwa anapenda. Ili ajue mengi.

Kuna jambo hapa!! Si bure. Aliwazua Jose, huku akijituliza na kujiuliza inakuwaje amhisi vibaya yule bwana.

Baada ya ndugu wa karibu kumaliza kuaga. Wasindikizaji wengine nao waliaga.

Jose B hakwenda kuaga, akabaki kumfuatilia Lameck na nyendo zake.

Mara Lameck akakutana na kipande cha mtu, kilikuwa kinampa pole.

Jose B akashtuka, kile kipande alikuwa anakifahamu vyema. Aliwahi kukiona maeneo fulani jijini Dar es salaam.

Ubungo. Zamzam guest house.

Kipande kile cha mtu kilikuja kumpokea Emmy, kikamuingiza ndani kisha kikatoka nje.
Sasa ikajengeka picha ya mwisho ya kumaliza utata kwa Jose B waukweli mshakunaku wa kimataifa. Yule aliyebaki ndani pamoja na Emmy ndiye huyu anayeitwa baba mdogo.

Jose B akacheka kisha akamshukuru Mungu kwa kumbariki na kipaji hicho cha kipekee.

Kwa hiyo baba na mwana wanamahusiano ya kimapenzi....eeh!! Mungu ameumba dunia na maajabu yake, ndo maana nikashangaa kivipi napewa malipo makubwa hivyo.

Kumbe ni baba na mwana. Jose B akamaliza kwa kicheko kifupi.

Safari ya kuelekea kuzika ikafuata.

Jose B alikuwa amekuja na gari ndogo, ilikuwa ngumu kujua iwapo ni yake ama amekodi, aliingia katika gari na kumuamuru dereva aondoe.

Alifungulia mziki wa taratibu kwa sauti ya chini.

Wakati mziki ukiendelea, Jose B akaanza kumfikiria upya Emmy, akajisahaul,isha kuwa mwanamama huyu kwa sasa yupo katika machungu makubwa ya kumpoteza mama yake mpenzi.

Jose B akamuwaza kama mwanamke ambaye amejaribu kumtapeli ama wamefanya biashara isiyokuwa sahihi.

“Mimi nilielewana naye kuwa anipe milioni saba ama nyumba nikidhani kuwa alikuwa na mtu wa kawaida tu wakimsaliti James, lakini kumbe alikuwa na baba mdogo? Hii biashara kamwe nisingeweza kuifanya kwa milioni saba au kinyumba kile, hii ni hasara tena hasara kubwa tu. Yaani mtu na baba yake niiuze kwa milioni saba? Si bora hata nisingeiuza kabisa. Mtu na baba yake unadhani mchezo!! Yaani hapa sikubali kudhulumiwa kiwepesi wepesi. Lazima haki itendeke hapa.” Aliwaza Jose B kwa hisia kali sana kama mtu aliyewekeza mahali kisha akadhulumiwa pesa yake halali.

Jose B hakuwekeza chochote!! Cha ajabu analalamika.

Au huyo baba mdogo amsaidie huu mzigo, kweli ngoja nimtwike na yeye mzigo wa kulipia hasara niliyoingia. Alibadili mawazo yake Jose B, akaugeuzia upepo kwa Lameck Sulube.

****

Laiti usingekuwa ukakamavu wa jeshi, huenda Lameck angeweza kuanguka wakati wa kutupia mchanga wa mwisho katika kaburi la Devotha, mama yake Emmy.

Ama hakika damu ni nzito kushinda maji.

Lameck kwa mkono wake alikuwa ameteketeza maadui wengi waliothubutu kukatiza mbele yake katika vita huko Sudani.

Wengine aliwalipua vichwani na wengine aliwapasua matumbo kwa bunduki. Hayo yote yalikuwa ya kawaida kwake, iweje kifo cha mtu huyu kimguse kwa kiasi hicho.

Alikuwa nyumbani kwake wakati akiwaza haya.

Lakini ni ubishi wake..

Lameck aliyakumbuka mazungumzo yake ya mwisho na mama yake Emmy katika hoteli iliyopo pembebi kidogo ya jiji. Mazungumzo nyororo yaliyoishia pabaya baada ya mada mpya kuletwa mezani.
Mtu na shemeji yake wakaanza kulumbana baada ya Lameck kumgusia mama Emmy kuwa anampenda mwanaye sana.
Kumpenda halikuwa tatizo, Lameck akaleta hoja ya nyongeza kuwa wamewahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi tangu wakiwa watoto.

“Mnaendelea hadi sasa?” Devotha alimuuliza.

Lameck akapinga. Devotha akashusha pumzi kali.

Lameck akaendelea kuikaribia maana aliyoitaka.

Akamgusia Devotha kuwa Emmy ameolewa akiwa si bikra.

“Acha upumbavu wewe...mbona mumewe alileta shukrani ng’ombe mbili nyumbani kwa kumkuta Emmy akiwa mzima na usichana wake huko Uganda?” Alijibu kwa kebehi kiasi fulani huku taharuki ikianza kuchukua mkondo.

Lameck akashtuka, hakutegemea kusikia hayo kutoka kwa yule mama. Kumbe James alienda kujisifu. Kujisifu kwa Bikra feki iliyotengenezwa na daktari mashuhuri Lameck John Sulube, kwa kutumia Shabu, Ndimu na kisha kuiweka makini zaidi ikawekewa dondoo za sabuni aina ya KAISIKI. James akadanganyika na kutoa ng’ombe mbili.

“Au nimpigie James simu hapa akuumbue??” aliongezea yule mama Lameck akiwa bado kimya.

“Haina maana shemeji kufanya hivyo” Lameck aliweka nidhamu mbele.

“Kumbe ulichoniitia.”

“Kuna jambo la ziada....”

“Lipi?” aliuliza kisharishari.

“Ni kuhusu Emmy na mimi, nimeamua nianze kujadili na wewe kiutu uzima kisha tutamuita Emmy.......”
kabla hajaendelea yule mama mweupe ambaye uso wake ulikuwa umeanza kuwa mwekundu kutokana na hasira alimkatisha, “Shem Lameck naomba tusivunjiane heshima, yaani mimi wewe na mwanangu tukae kuzungumzia bikra mara sijui mlikuwa na mahusiano utotoni, unamshutumu mwanangu hana bikra, hiyo bikra uliitoa wewe mpuuzi mkubwa, na kwa taarifa yako ni kwamba Emmy ni mama mtarajiwa, ana kitoto kinaimba kwa furaha tumboni, sitaki kabisa umkere mwanangu, nenda ukapambane na wanajeshi wenzako huko si mwanangu....jitu zima hata aibu huna na nitaenda kumwambia mume wake....mshenzi wewe....yaani umekosa wanawake mtaani huko unakuja kujishebedua kwa mtoto wako loooh aibu kweli na nitakushtaki ukiendelea nasema nitakushtaki Lameck...ukome, umkome mwanangu” mama alipaza sauti, ikawa kazi ya Lameck kumsihi mama huyu asiongee sauti ya juu.

Mara akasimama aweze kuondoka. Lameck akamdaka mkono, akaanza kumlaghai kuwa alikuwa anatania, lakini yule mama alikubali kinafiki tu kuwa hawezi kuyafikisha mahali popote maneno yale.
Lameck kwa kumsoma macho yake akaugundua unafiki wake. Lameck alikuwa amechukizwa sana na maneno makali kutoka kwa yule mama, hasahasa maneno ya mwisho ya kumtishia kumshtaki. Lameck akaongozwa na hasira, na kwa kujilinda siri ile isitoke mapema.

Akatumia msemo wa heri mmoja afe wengi wapone.

Kitendo cha sekunde kadhaa kutoka kwa mwanajeshi huyu.

Sumu ikaugusa mwili wa mama Emmy.

Yeye akanawa upesi upesi.

Akarejea nyumbani, taarifa aliyoitegemea ndiyo ambayo aliipata kuwa mama Emmy alikufa akiwa katika gari iliyokuwa inamrudisha nyumbani akitokea hotelini. Bila kujulikana na nini alikuwa anafanya.
Sasa amezikwa tayari na ni usiku mwingine Lameck anawaza yaliyotokea.
Lameck ameua.

*************

***LAMECK amemuua DEVOTHA ili kujilinda asichafuliwe...amemuua kabla hajamwambia ni kipi alichomwitia wajadili.

***JOSE B anapata kitu kipya kabisa msibani, kumbe LAMECK na EMMY ni ndugu wa karibu. Dili jingine!!

ITAENDELEA
 
HADITHI: KIZUIZI

SEHEMU YA KUMI NA SITA


Sumu ikaugusa mwili wa mama Emmy.
Yeye akanawa upesi upesi.
Akarejea nyumbani, taarifa aliyoitegemea ndiyo ambayo aliipata kuwa mama Emmy alikufa akiwa katika gari iliyokuwa inamrudisha nyumbani akitokea hotelini. Bila kujulikana na nini alikuwa anafanya.
Sasa amezikwa tayari na ni usiku mwingine Lameck anawaza yaliyotokea.
Lameck ameua.

****

ENDELEA.....

Kwanza alijihisi yupo katika hatia kubwa sana ya mauaji, lakini aliamini fika kuwa si mategemeo yake kufanya mauaji yale. Akafikiria kwa nukta kadhaa ni nani wa kumbebesha mzigo ule wa mauaji ama la waweze kugawana naye.

Akafumba tena macho yake akayakumbuka maneno ya daktari wa kijeshi nchini Sudani aliyemhakikishia kuwa kamwe hatoweza kuzalisha kwa hali aliyonayo.

Anakumbuka kwa mara ya kwanza katika maisha yake alilia kama mtoto mdogo akabembelezwa na wenzake pasi na mafanikio.

Walimbembeleza sana huku wakimpamba na maneno tele ya kishujaa. Walimwita jasiri ambaye amedhurika kishujaa akilipigania bara lake la Afrika, maneno hayo hayakumuingia akilini hasahasa akifikiria hao waliokuwa wakimwambia walikuwa na familia zao tayari, na hata ambao hawakuwa na familia bado muda wowote ule wangeweza kuzianzisha maana walikuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Lameck alijikaza kiume akawakubalia kwa shingo upande. Nafsi yake ilikuwa inamlaumu naye akailaumu kwa kitendo cha kumwonea huruma yule msichana asiyemfahamu katika nchi ya Sudani kusini, ni msichana huyo aliyepelekea risasi ya bwana wa kiarabu kumlipua na kusambaratisha sehemu zake za siri kwa kiasi kikubwa.

Giza likatanda.

Mwanga ukatokea baada ya siku tano, alijikuta akiwa na bandeji kubwa katikati ya mapaja yake. Hakuwa anakumbuka ni nini kimetokea mpaka pale aliposimuliwa jinsi alivyookolewa na wanajeshi wa jeshi la umoja wa mataifa kutoka Senegal na Ghana.

Walimuelezea kama mfu aliyekishinda kifo katika dakika za majeruhi.

Hakuna hata mtu mmoja aliyetegemea kuwa angeweza kupona, lakini imewezekana na alikuwa hai tena.
Baada ya upasuaji ndipo yakatolewa yale majibu kuwa kizazi kimevurugwa huku akisaliwa na kipisi cha maungo yake.

Jambo lililomtia simanzi kubwa.

Jambo kuu aliloweza kufanyiwa ni kuwekewa maungo ya bandia ambayo hayakuwa na kazi kubwa zaidi ya kumpamba. Siri alibaki nayo yeye.

Anarejeshwa katika nchi yake kabla ya mapambano kumalizika. Siri ile inazikwa katika mioyo ya wanajeshi shupavu wa umoja wa mataifa.

Siri nzito isiyotakiwa kuvuja juu ya hali ya Lameck.

Kimyakimya anarejeshwa nchini baada ya kidonda kupona.

Kisingizio kikatangazwa kuwa ni hali ya hewa nzito ya nchi ya Sudani imepingana na afya yake. Habari hiyo ikapambwa zaidi kuwa licha ya kuzidiwa na mgandamizo wa hewa Lameck alipigana kiume na alikuwa mfano wa kuigwa na kila mwanajeshi, na jeshi la umoja wa taifa limemwandalia zaweadi ya ushindi na ushujaa.

Sababu za uongo lakini kwa ajili ya kuutunza utu wa Lameck. Na zawadi aliyoahidiwa ilikuwa pole kwa kizazi kilichopotea vitani.

Risasi ya mwarabu.

Baba, mama na ndugu wote hawakujua lolote. Walimpa pole kwa maswaibu huku wakijipongeza wao kwa wao kwa ushindi mkubwa wa mwanao na sifa aliyowaletea.

Kati yao hakuna aliyekijua kilio cha mwanajeshi huyu.

Baada ya mapokezi haya. Lameck akaendelea na maisha ya uanajeshi huku akiwa na likizo ya muda mrefu ili aweze kutulia kiakili.

Ni katika likizo hii anawaza juu ya maneno ambayo baba yake alimwambia siku ya kumpongeza; ukizaa mtoto atajisifu sana kwa kuwa na baba kama wewe, tena ikibidi na yeye ajiunge kabisa na jeshi.

Maneno haya ya mzee yakamkumbusha matatizo aliyokumbana nayo nchi za kigeni.

Lameck akawaza na kuwazua akamkumbuka Emmy. Aliyakumbuka mapenzi motomoto aliyompa siku ya kuagana naye. Kisha akakumbuka lililo kubwa zaidi. Mimba ya Emmy. Lameck na akili zake za kiutu uzima alikuwa na uhakika kabisa kuwa ile mimba haikuwa ya James kama inavyodhaniwa, aliamini kuwa ilikuwa inamuhusu yeye na mtoto atakayezaliwa alikuwa halali yake. Kile kichefuchefu ambacho Emmy alimtangazia kuwa kinamsumbua kwa kutumia zile dawa za kurejesha bikra kilizidi kumshawishi kuwa Emmy alikuwa mjamzito na amefunga ndoa akiwa na mimba ya takribani mwezi mmoja mimba ambayo sasa inadhaniwa kuwa ni ya James.
Lameck akaamua kuipigania damu yake ambayo ipo katika tumbo la Emmy ambaye kiukoo ni ndugu wa karibu sana.

Lameck anaamua kuzungumza na mama yake Emmy kiutu uzima ili wapate pa kuanzia. Tofauti na matarajio yake mama Emmy anataka kuvuruga mambo mapema zaidi, Lameck anajikuta anafanya mauaji kwa kutumia sumu kali inayopenya katika ngozi upesi.

Devotha yu kaburini, Lameck katika kitanda akiwa na siri nzito.

Hatua iliyofuata Lameck akaamua kumfuata mtu mwingine ambaye anaweza kumshirikisha katika jambo lile zito.


****

Wakati Lameck akiumaliza usiku wake katika namna ya kuwaza na kuwazua. Kamanda mwingine wa jeshi la mtaani alikuwa katika kitanda chake akirusharusha miguu huku akifanya tafakari. Alikuwa akimtafakari huyu bwana aliyemaliza siku yake akiwa na mawazo lukuki.

Aliwaza jinsi ya kuchuma pesa kutoka kwake. Alipofikiria kuhusu pesa akaanza kumthaminisha Lameck, kwanza alimchukulia kama maskini wa kutupwa ambaye anaweza kumwajiri katika banda lake la kuweka na kutoa pesa. Alimshusha thamani kutokana na mahali ambapo alimuona kwa mara ya kwanza; Zamzam guest house. Alimchukulia kama mtanzania mwenye kipatgo cha chini sana na kamwe asingeweza kuzikimu gharama za hoteli kubwa kubwa.

Pia siku ya msiba bwana Lameck alikuwa hajachana nywele zake na nguo alizokuwa amevaa zilizidi kuishusha thamani yake mbele ya Jose B waukweli.

Jose B hakujua kama Lameck ana mambo mengi magumu yanapita kichwani mwake, mambo ambayo yangevuja na kumfikia yeye basi ni biashara kubwa.

"Hivi yule hata laki moja anaweza kutoa kweli? Hoteli nzuri imemshinda kulipia amempeleka yule malkia uswahilini" Jose alijiuliza huku akiijenga picha ya Lameck. Akajichagulia jibu kuwa ni hapana. Bwana yule hana pesa.

Kwa jibu hilo Jose B akahisi ni kujipotezea muda kumfuatilia maskini kama yule.
Jose B akalala huku akiuvunja mpango wa kumfuatilia Lameck. Ule mzigo aliotegemea kumtwisha Lameck akaamua kuurejesha kwa muhusika ambaye anaweza kutoa pesa. Emmy.

Jose B aliamini kabisa kuwa ataonekana mnyanyasaji sana, mshipa wa aibu ukakumbuka kufanya kazi yake, akajifikiria mara mbilimbili aanze vipi kumweleza Emmy juu ya siri hiyo. Hakutaka kumweleza ana kwa ana.

Akiwa katika banda lake la biashara siku iliyofuata alikuwa analo jibu tayari. Akafanya mawazo yalivyomtuma.

Akachukua simu yake na kumpigia Emmy.

Alipopokea akamuuliza kama yuko peke yake, akakubali kuwa alikuwa peke yake ofisini.
Jose B akamwomba afike nyumbani kwake jioni ya siku hiyo akitoka kazini kuna jambo la kuzungumza.
Emmy akakereka kutokana na huu usumbufu lakini hakutaka kumwonyesha Jose B waziwazi kwa sababu angeharibu mahusiano yao ambayo yameanza kuwa katika urafiki.

Emmy akakubali wito.

Majira ya saa kumi jioni Jose B alikuwa katika hekalu lake dogo akimngoja Emmy. Hapo kinywani alikuwa amepanga maneno ya kumweleza yule binti.

Majira ya saa kumi na moja jioni. Emmy akiwa amemuaga James kuwa atachelewa kiasi kurudi nyumbani kwani atapitia saluni, alielekea nyumbani kwa Jose B. Kichwani akijiuliza huyu kijana alikuwa na lipi jingine la kumshirikisha.

Kutokana na foleni za hapa na pale Emmy akafika kwa Jose B majira ya saa kumi na mbili jioni. Alimkuta Jose akiwa anamngoja.

Jose B alipoteza dakika kadhaa kumpa Emmy pole ya msiba na stori nyinginezo za kumfariji kutokana natukio lile.

Katika kupewa pole ya msiba, Emmy akamkumbuka mama yake, mara akaanza kulia.

Jose B alikuwa pekee katika nyumba ile, akamsogelea Emmy na kuanza kumbembeleza, Emmy aliendelea kulia Jose B naye akazidi kumfariji huku akimfuta machozi, kigiza kiliendelea kutanda pale ndani kumaanisha kuwa usiku unaingia.

Jose B ambaye hakuwa mtu wa wasichana hovyohovyo akajikuta yu majaribuni, Emmy alikuwa amemlalia huku akiendelea kulia kwa kwikwi. Zile bastola zilizomteka James nchini Uganda, zikakichoma kifua cha Jose B.

Akili ikamuhama kijana huyu mara akampapasa.

Emmy kimya.

Akampapasa tena bado Emmy alikuwa kimya.

Kigiza kikawalaghai wawili hawa kikazitwaa aibu zao na kusafiri nazo mbali.
Mama mjamzito hatakiwi kuvaa nguo ngumu wala zile zinazombana. Emmy naye akiwa na kitumbo kidogo alifuata masharti haya na alikuwa amevaa dela la kitambaa chepesi.

Joto likapenya na kumpasha Jose B katika namna ya kushangaza.

Akasahau mahesabu yote aliyopanga kumpigia Emmy. Shetani akabisha hodi, akapokelewa kama mfalme mwenye kuheshimiwa.

Akawaomba wawili hawa akae kati yao, wakakubali kwa roho safi.
Shetani akawaomba awafundishe kitu. Wakakubali. Shetani akachukua chaki akaanza kuwafundisha. Wawili hawa walikuwa werevu sana hawakusumbua katika kuuliza maswali ya itakuwaje baada ya hapa.
Wakatenda walilofundishwa.

Baada ya saa zima shetani alikuwa amewakimbia akawaacha wakijitambua.
Aibu tupu. Wawili hawa walikuwa wamezini.
Hakuna aliyeanza kumsemesha mwenzake.


***
Emmy alirejea nyumbani majira ya saa mbili usiku, hakumkuta James. Na aliambiwa kuwa James hakuwa amerejea. Hali hii ilikuwa tofauti sana, James kuchelewa kurudi nyumbani bila kutoa taarifa yoyote.
Emmy hakutaka kuhoji zaidi, akaingia chumbani kwake huku akijutia kitendo chake cha kuzini na Jose B, aliamini kuwa amejiongezea kizuizi kingine katika maisha yake.

Alinyanyua simu yake na kumpigia Jose B.

Simu ikachelewa kupokelewa lakini hatimaye ilipokelewa, kwa sauti tulivu ya Jose B.
"Sam...." aliita Emmy, Jose B akaitika.

Wakati Emmy anataka kuanza kuzungumza, mara mlango uligongwa, akaingia James akiwa katika taharuki fulani. Emmy akaligundua hilo.

Akamkaribisha na kisha kumuuliza huku akikumbwa na hatia juu ya kitendo alichotoka kufanya na Jose B.

"Una nini husband."

"Nimepata safari ya ghafla natakiwa kuondoka kuelekea Mwanza kuna tatizo la kifamilia." Alijibu kwa ufupi.

Kisha akajieleza kwa urefu, akaeleweka.
Akamkabidhi Emmy majukumu kadhaa aliyoyaacha ya kiofisi. Emmy akayapokea.

Asubuhi ya siku iliyofuata James akaondoka.

Haikuwa safari ya kwenda Mwanza, alikuwa anaelekea machale yake yalipomtuma.
James hakuamini hata kidogo juu ya misiba mitatu iliyotokea. Baba kuchomwa visu, mdogo wake kunyongwa
na mama mkwe kuuwawa kwa sumu kali.

James alirejesha akili yake miaka kadhaa, kisha akazikumbuka siri kadhaa alizokuwa anazihifadhi katika moyo wake. Akakumbuka kuwa si katika moyo wake tu bali pia katika moyo wa marehemu baba yake.

Akapanga majina kadhaa ambayo aliamini kuwa yanaweza kuwa yanahusika katika mauaji haya.
James aliamua kuchukua maamuzi upesi baada ya kuhisi kuwa hataweza kuishi tena ulimwenguni iwapo atapata taarifa ya kuuwawa kwa Emmy na mwanaye aliye katika tumbo lake.

Kamwe asingeweza kumshirikisha juu ya siri hizo kwani huo ungekuwa mwanzo wa kuvuruga penzi lao na yeye kujiweka katika hatihati ya usalama wake hasahasa katika vyombo vya dola.

James anaamua kuondoka kimyakimya huku akidanganya kuwa anaenda Mwanza kutatua matatizo ya kifamilia.
James alikiri kimya kimya kuwa upendo wake kwa Emmy ulikuwa unakua kwa kasi kadri mimba inavyozidi kukomaa.

Subira ya mtoto ilimfanya James awe mtumwa wa mapenzi. Alimfanyia Emmy kila kitu alichokuwa nahitaji. Hata pesa ambazo zilitumika kumpangishia Jose B nyumba zilikuwa za James.
James alikuwa radhi kufanya lolote kwa ajili ya Emmy. Sasa aliamua kuwasaka wabaya wake kwa manufaa ya penzi na mtoto mtarajiwa.

Katika orodha ndefu iliyopita katika kichwa cha James ilihitimishwa kwa jina ambalo halikuwa na uzito sana.
Mamu. Hili lilikuwa jina la mwisho kabisa ambalo halikumtetemesha James, na aliamini kuwa huenda halipo tena katika ulimwengu huu.

James akalikimbia jiji, safari ya kwenda kuwasaka anaohisi wanamuharibia mipango yake.
Usiku wa manane James alikumbuka kitu, akakurupuka kutoka usingizini. Akaliendea kabati, akatoka na kibegi kidogo, kile alichokiwaza akakikuta. Kilikuwa kijitabu kidogo.

Akakutana na namba ya simu. Akafanya mfanyo wa tabasamu, akaitwaa simu yake akajaribu kuipiga ile namba, badala ya kuita akapokea taarifa ya kuwa hana salio la kutosha katika simu yake. Alitamani kununua salio kutoka katika akaunti yake ya benki lakini akahisi ni kupoteza muda.

Akaiona simu ya mkewe ambaye alikuwa anakoroma.

Akatazama salio lilikuwepo la kutosha.

Akaingiza zile namba katika simu ya mkewe kwa matarajio kwamba baadaye ataifuta ile namba na mkewe hatajua aliwasiliana na nani.

Akaenda jikoni aweze kumsikia Jose B.

Alipoanza kupiga mara likatokea jina. Jina katika simu ya mkewe.
SAM WA PILI.......

James akataharuki, akakata ile simu mara moja.
Wasiwasi ukatanda, Sam wa Pili ndiye Jose B waukweli. Maajabu.
Na ameanza lini kuwasiliana na mkewe, na alimjuaje? Ina maana mkewe anajua juu ya KIZUIZI ambacho kiliondoka na roho za Bibiana na Deo.

James akahisi kijasho chembamba kikipenya katika uti wa mgongo wake.
Kisha akagundua kuwa alikuwa anatetemeka.
Hofu. Hofu kubwa ikatanda.

KIZUNGUMKUTI........

***JOSE B ameonja tunda asilotaraji...EMMY anajutia.....
***LAMECK asiyekuwa na uwezo wa kuzalisha anaamini mimba ya EMMY ni halali yake.....ANATAKA DAMU YAKE.....
***JAMES...akiwa anajiandaa kuipigania ndoa yake na uhai wa Emmy na mtoto...ghafla anakutana na jambo la ajabu..namba za Jose B....jina linalotokea ni SAM WA PILI....mauzauza...
***MAMU hatiliwi mashaka na James.....je ni nani anayetuhumiwa???

Ni KIZUIZI kinachotafuna kila muhusika........kukikimbia kizuizi aidha uuache ukweli huru ama uuache ulimwengu ukimbilie kaburini....

ITAENDELEA.......
 
Back
Top Bottom