Hadithi: Kizuizi

Hadithi: Kizuizi

ila mizambwa kwanini usilete hata episod mbilimbili.
 
Last edited by a moderator:
Mmmh eti eeh? Lakini mbona hawa waliuawa mwanza na huyu alikuwa anawatafuta darisalama?

Mie nadhani ndo hao na yeye kaenda dar kumtafuta kindo ndo anajiuliza keto na mwenzie waliuawa kabla ya ndoa
 
Ya kweli hayo Landala?

kweli kabisa,kwa mfano hapa jf imeishia sehemu ya 19 wewe nenda google andika "kizuizi 20" itakuletea sehemu ya 20 na ukimaliza kuisoma andika sehemu inayofuata zote utaletewa.
 
Last edited by a moderator:
kweli kabisa,kwa mfano hapa jf imeishia sehemu ya 19 wewe nenda google andika "kizuizi 20" itakuletea sehemu ya 20 na ukimaliza kuisoma andika sehemu inayofuata zote utaletewa.

Mbona nimejaribu imegoma?
 
Kizuizi -20

“Atanitambua mimi ni nani, na pia atajulikana nani mjanja kati ya mjeruhi na mjeruhiwa.” Aliapa mwanamke huyu ambaye alikuwa na majeraha kadhaa mwilini mwake.Usiku wa siku hiyo akiwa na vijana wake kadhaa ambao alisafii nao kutoka mbali aliingia katika kupigania ukweli uliofichika.Siku kadhaa za kuwa katika jiji la Dar es salaam tayari alikuwa amepeleleza mambo kadhaa na alikuwa amepafahamu nyumbani kwa Kindo na mengine mawili matatu.Usiku wa siku hiyo hakufanya makosa.Akaivamia nyumba ya Kindo ambaye anajiita James.Akamteka Grace.Sasa amezua kizungumkuti, Emmy anahisi ni Lameck amemteka Grace.James bado hajawa na uhakika ni nani amemteka Grace na hataki kuamini kabisa kama Mariam anaweza kufanya hivyo.

Upelelezi haukuwa na lolote jipya. Mkono wa dola ulitapatapa huku na huku bila mafanikio. Bado Grace hakupatikana.James akajiona kuwa yeye ni ----- mkubwa. Anamuhisi mtu fulani kuwa yawezekana anaweza kuwa anahusika na utekeji huu lakini anapuuzia na kukaa kimya akiwangoja polisi wasioisha kusema neno lao la siku zote ‘upelelezi unaendelea.’James akatamani kumshirikisha Emmy juu ya hisia zake. Lakini akahofia maswali kadhaa kutoka kwa Emmy juu ya huyo Mariam.Akiniuliza tulikuwa na mahusiano gani na kwanini aandike kuwa ‘tutaona nani mjanja’ nitajibu nini? Maswali haya ambayo majibu yake ni magumu sana yakazua kizuizi kwa James kuthubutu kufanya jambo lile.Emmy naye alikuwa na tatizo kama la James. Alijua kitu lakini alihofia maswali kutoka kwa mumewe ambaye alimuamini kwa asilimia mia kuwa alikuwa yu mtakatifu pasi na hatia.Wote wakawa wanawaziana mazuri lakini wakikumbwa na kizingiti cha kuuachia ukweli huru.Sintofahamu ikawazunguka.Emmy akiwa katika kuwaza juu ya Grace, mara akamkumbuka Lameck na kauli yake kuwa ile mimba ilikuwa halali yake.Tumbo likaanza kutetemeka, akaanza kuhisi huenda kuna ukweli fulani katika maneno ya Lameck. Emmy akamfikiria Lameck kuwa si mtoto mdogo azalishe ghafla tu mada ile bila kuwa na hisia fulani.Mahesabu ya mimba yake kuingia yakamvuruga kabisa.Akafumba macho yake kabla ya kukatishwa na hodi getini, alipofungua macho yake akakutana na yule mwanaume aliyekuwa anamuwaza kichwani.Lameck!!Tumbo la kuhara likamkamata, akanyanyuka na kutimua mbio kuelekea ndani chumbani, safari ikaishia chooni.Hakuna kilichotoka. Ilikuwa hofu tu.Huko maliwatoni, Emmy akawaza kuwa hatimaye Lameck ameamua kumkomesha kwa namna nyingine.Pigo la mwisho lenye hatari kupita yote.Lameck ameamua kumshirikisha James siri nzito.“Emmy.....” James aliita.Emmy akauchuna kana kwamba hasikii lolote.Bado alikuwa maliwatoni bila lolote la kufanya.Nguo zake zilikuwa nusu zimevulika na nusu bado zikiutawala mwili wake. Alikuwa anajiuliza aitike ama aendelee kuuchuna.“Shem....” sauti ya Gloria ikaita kutokea mlangoni.Emmy akazidi kuchanganyikiwa.Emmy akapandisha nguo zake na kutoka nje.-“Kuna nini?” akauliza.“Simu yako ilikuwa inaita....naona imekatika....hii inaita tena...” Gloria kwa nidhamu akamkabidhi Emmy simu.Mlango ukafungwa akaitazama namba inayompigia.Mshtuko. Alikuwa ni Jose B waukweli ama Sam wapili.Simu ilikuwa imepigwa mara tatu bila kupokelewa.Jose matamaa . akaingiwa na tamaa na wivu kutokana na simu yake kuacha kupokelewa. Akatuma ujumbe.“Nakuja nyumbani kwako.” Ujumbe huu Emmy aliusoma baada ya kuwa amekata simu badala ya kupokea.Emmy akajikuta anapiga yowe, yowe ambalo halikusikiwa nje ya chumba hicho.Akapagawa na ujumbe ule. Mume wake alikuwa nyumbani na baba yake mdogo pia alikuwa nyumbani.Aibu ya karne!!Emmy akaingia maliwatoni akajisafisha uso wake kwa maji na sabuni.Mara akanogewa akaamua kuoga kabisa. Akajifungia maliwatoni.Hakuweza kuisikia simu ilivyoendelea kuita.Alitumia dakika kumi na tano bafuni.Aliporejea akakutana na simu saba zisizojibiwa.Akatamani kumtumia Jose B ujumbe lakini akajikuta akisahau na kuendelea kuvaa upesi upesi.Kosa kubwa!!Wakati akihangaika, Jose Matamaa alikuwa ametaharuki katika teksi aliyokodi imfikishe nyumbani kwa Emmy, Jose kijana mdogo kabisa asiyejua uchungu anaoupata mwanaume akiibiwa mke wake ama kijana mwingine yeyote anayempenda na kumthamini mpenzi wake anapogundua kuwa anasalitiwa. Alikuwa anafurahia kummiliki Emmy. Ilifikia wakati akawa anatamani kuwa mume wa Emmy ambaye ni mke wa mtu tayari.Kwa jinsi ambavyo Emmy alijirahisisha kuuachia mwili wake ndivyo Jose alivyopata nafasi ya kumtawala zaidi.Sasa bila kujali ni kwa kiasi gani anahatarisha ndoa ya Emmy alikuwa anaelekea nyumbani kwake.Emmy alitoka nje upesi akamuaga James kuwa anaonana na mtu kwa dakika kadhaa nje. Usoni alikuwa ametaharuki, James naye hakuwa na amani moyoni kwani ile hali ya kuona simu ya Emmy ikionyesha jina la Sam wapili. Akamkumbuka Jose B na jina hili lilikuwa na namba ya simu ya Jose.Alitamani kutoka pamoja na Emmy lakini ile tabia yake ya kutopenda kuwadharau ndugu wa mwanamke ikamtafuna akamheshimu Lameck na kuendelea kubaki akimsikiliza huku Emmy akitokomea nje ya geti upesi.Jose B hakuwa na utani hata kidogo. Hata yeye hakujielewa ni nini anafanya. Hakujisikia kumuogopa James, alifanya kile ambacho moyo wake ulimtuma kufanya. Sasa alikuwa jirani kabisa na nyumba ya Emmy. Penzi alilopewa na Emmy likamvuruga akili yake na kuwa kama mwendawazimu.Umri wake wa miaka ishirini na ushee uliruhusu kabisa kuwa katika hali hii. Hali ya kuwa mtumwa katika jambo jipya katika maisha.Emmy alikuwa wa kwanza kumuona Jose B akiwa amejiweka mbali kidogo na geti akiwa ameuegemea mti mkubwa wa mwembe usiokuwa na matunda.Emmy akatembea kwa mwendo kasi, akawa anatembea nusu na nusu anakimbia akiwa amelikamata gauni lake vyema.“Sam......nini hiki unanitaka...eeh”Jose B akageuka, alikuwa amenuna. Akamtazama Emmy kwa jicho kali.“Unataka kunifanya mtoto mdogo sivyo?” akahoji kwa jeuri.Emmy akashusha pumzi zake.“Sikia Sam...nakuomba tusizungumze kwa sasa kesho nakuja nyumbani kwako tutakaa muda mrefu tu....niamini tafadhali, James yupo hapo na bamdogo, wanatoka sasa hivi Sam, nitaelewekaje mie pliiz nakuomba Sam nakuomba sana.” Sauti yenye kitetemeshi cha hofu ilimkumba Emmy wakati anasihi. Hofu ilikuwa imetawala.Jose B akakumbwa na sintofahamu baada ya sauti ile kupenya katika masikio yake, akajikuta akitabasamu.Jose B alipenda sana kunyenyekewa.Akamkubalia Emmy. Wakaachana bila kuagana.James hakuwa anaelewa lolote lililosemwa na Lameck juu ya kupotea kwa watoto, alikuwa anawaza juu ya Jose B ambaye ana wasiwasi ndiye Sam wa ukweli.Ana hila gani na mkewe wa ndoa tena ambaye ana mimba tayari? Alijiuliza.Hakupata majibu.Akajisikia mchomo wa wivu ukimuandama, akaanza kupata suluba ya aina yake, akafumba macho na kumuona ----- mmoja waliyekutana jijini Mwanza, akamuuzia Kizuzizi kwa shilingi milioni sita, akapewa utangulizi wa shilingi milioni mbili akatoweka. Leo hii anaigusa ndoa yake.James akahisi kuwa Emmy anaweza kuwa ana mahusiano ya siri na Jose B ambaye kwa sasa anajiita Sam.Kwa hiyo huyu ----- amefikia hatua anamfuata mke wangu hapa hapa nyumbani kwangu? Haiwezekani hata kidogo wanichezee shere hawa. Hivi wananijua vizuri kweli?James alihamaki.Lameck aliigundua hali ya utulivu jinsi ilivyopotea katika uso wa James. Akaona asiendelee kuongea sana akamtazama na kumsikitikia kwa mengi.Likiwemo la kulea mimba ambayo si yake na sasa ana wasiwasi na mkewe baada ya kupigiwa simu kisha akatoka nje.Lameck akaamua kuaga na kuondoka zake.Kitendo cha Lameck kuaga kikampa James nafasi ya kipekee kujaribu kuuliza juu ya mtu aliyekuja nyumbani na kisha Emmy kutoka nje.James aliingia chumbani na kumkuta mkewe akiwa amejilaza kitandani, hakuwa na furaha hata kidogo, na kitendo cha mtu kuingia pale chumbani kikampagawisha.Akataharuki waziwazi.“Emmy...ni nani alikuja pale nje ukamkimbilia mbiombio.”“Nani? Mimi?” aliuliza swali la kipumbavu Emmy kwa hofu.“Kwani humu ndani tupo wangapi?” James alijaribu kuzuia jazba yake.“Hapana ni rafiki yangu...nani huyu mzoa taka alikuwa anadai.....naniii” Emmy alitia huruma, hakuwa na cha kujibu mbele ya mumewe.-James akakunja ngumi yake imara ili aweze kuikabili hasira yake. Akafanikiwa kwa kiasi kidogo.“Mlipeana namba lini na huyu mtupa uchafu?” James kwa sauti ya chini aliuliza, bado alikuwa amesimama na Emmy alikuwa ameketi.“Hajanipigia simu wala.”“Kwa hiyo alikuita kupitia dirisha la chumbani sivyo?” mwanaume akazidi kukoroma. Sasa alikuwa anatetemeka midomo.Haikuwahi kutokea hata siku moja katgika kipindi cha mahusiano yao.Emmy akakosa cha kujibu.James akaitwaa simu ya Emmy pasipo binti huyu kutarajia. Akapekuapekua sehemu ya namba zilizoingia, akakutana na majina kadhaa ya kike. Hapakuwa na jina la Sam wa pili.Akajaribu kulitafuta jina lile. Hakuna kitu.Kijasho chembamba kikamtoka.Akataka kuliendea kabati ili arejee na ile namba ya Jose B aiingize katika simu ya Emmy akahofia kuzua utata baadaye, alimjuaje Sam wa pili.Kama Emmy na Sam wana mahusiano lazima atamshirikisha na hapa ndipo mkanda utakapoharibika.“na uhakika hujapigiwa simu na mwanaume wakati nipo na baba yako?”“Haki ya Mungu tena mume wangu.” Akaapa.James akashikwa na hasira kali akakumbuka kuwa wanawake ni sumu kali, sumu isiyostahili kuguswa hovyo. Hasira zikampanda, ameua kwa ajili yake na sasa hana imani kwa ajili yake.Mkono ukawa mwepesi ukalishambulia shavu la Emmy.Kipigo kitakatgifu cha kwanza katika ndoa kikafuata.James akamwadhibu Emmy kwa kujaribu kumficha.Ugomvi wa kwanza ukazua kipigo.Emmy alidhani anapigwa kwa sababu za wivu pekee hakujua kama kuna lolote ambalo James anamuwazia kuwa huenda analifahamu.Wakati anapokea kipigo alijisifu kimya kimya kwa machale yaliyomcheza kwa kuifutilia mbali namba ya Sam wa pili, na pia meseji zake zote, hajui ni mizimu gani ilimtuma lakini alijikuta tu akitekeleza hisia.Emmy alijisifu kwa kuamini kuwa laiti kama James angeipata namba ya Sam angeweza kumpigia na mwisho wa siku angeujua ukweli juu ya mahusiano yake ya kimapenzi na baba mdogo. Jambo ambalo lingepelekea siri tatanishi ya mimba aliyonayo kuchukua nafasi ya kuwa wazi.Ilikuwa bora kupigwa kuliko siri hiyo kuvuja.Emmy hakujua kama mumewe naye kuna siri zake ametunziwa na Sam wa pili ambaye ni Jose B waukweli.Laiti angejua.......***EMMY anaitetea siri yake isifichuke kwa gharama yoyote......***JAMES anahisi Jose B anatembea na mkewe..hajui wameambiana nini.......***LAMECK naye kimya kimya anapigania damu anayoamini ni yak wake...**MWANAMKE aliyemteka Grace naye..........ITAENDELEA
 
hahahahah takrima at work

na wewe pia Analyse

umetuharibia uondo na copy paste yako ya maneno awili kwa line. muwe mnaheshimu thread za watu as zinaleta utamu na sie kusubiria usidhani ni misifa huku unandandia, anzisha yako as hatukukuomba uingilie humu. unajionyesha tabia ya kudandia ndio zako na hauna subira hata kuwa mke/mume utakuwa majanga tu ya kiaina yako.
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA ISHIRINI
“Atanitambua mimi ni nani, na
pia atajulikana nani mjanja kati
ya mjeruhi na mjeruhiwa.” Aliapa
mwanamke huyu ambaye alikuwa
na majeraha kadhaa mwilini
mwake.
Usiku wa siku hiyo akiwa na
vijana wake kadhaa ambao alisafii
nao kutoka mbali aliingia katika
kupigania ukweli uliofichika.
Siku kadhaa za kuwa katika jiji la
Dar es salaam tayari alikuwa
amepeleleza mambo kadhaa na
alikuwa amepafahamu nyumbani
kwa Kindo na mengine mawili
matatu.
Usiku wa siku hiyo hakufanya
makosa.
Akaivamia nyumba ya Kindo
ambaye anajiita James
.
Akamteka Grace.
Sasa amezua kizungumkuti,
Emmy anahisi ni Lameck
amemteka Grace.
James bado hajawa na uhakika ni
nani amemteka Grace na hataki
kuamini kabisa kama Mariam
anaweza kufanya hivyo.
Upelelezi haukuwa na lolote jipya.
Mkono wa dola ulitapatapa huku
na huku bila mafanikio. Bado
Grace hakupatikana.
James akajiona kuwa yeye ni
----- mkubwa. Anamuhisi mtu
fulani kuwa yawezekana anaweza
kuwa anahusika na utekeji huu
lakini anapuuzia na kukaa kimya
akiwangoja polisi wasioisha
kusema neno lao la siku zote
‘upelelezi unaendelea.’
James akatamani kumshirikisha
Emmy juu ya hisia zake. Lakini
akahofia maswali kadhaa kutoka
kwa Emmy juu ya huyo Mariam.
Akiniuliza tulikuwa na mahusiano
gani na kwanini aandike kuwa
‘tutaona nani mjanja’ nitajibu
nini? Maswali haya ambayo
majibu yake ni magumu sana
yakazua kizuizi kwa James
kuthubutu kufanya jambo lile.
Emmy naye alikuwa na tatizo
kama la James. Alijua kitu lakini
alihofia maswali kutoka kwa
mumewe ambaye alimuamini kwa
asilimia mia kuwa alikuwa yu
mtakatifu pasi na hatia.
Wote wakawa wanawaziana
mazuri lakini wakikumbwa na
kizingiti cha kuuachia ukweli
huru.
Sintofahamu ikawazunguka.
Emmy akiwa katika kuwaza juu
ya Grace, mara akamkumbuka
Lameck na kauli yake kuwa ile
mimba ilikuwa halali yake.
Tumbo likaanza kutetemeka,
akaanza kuhisi huenda kuna
ukweli fulani katika maneno ya
Lameck. Emmy akamfikiria
Lameck kuwa si mtoto mdogo
azalishe ghafla tu mada ile bila
kuwa na hisia fulani.
Mahesabu ya mimba yake kuingia
yakamvuruga kabisa.
Akafumba macho yake kabla ya
kukatishwa na hodi getini,
alipofungua macho yake
akakutana na yule mwanaume
aliyekuwa anamuwaza kichwani.
Lameck!!
Tumbo la kuhara likamkamata,
akanyanyuka na kutimua mbio
kuelekea ndani chumbani, safari
ikaishia chooni.
Hakuna kilichotoka. Ilikuwa hofu
tu.
Huko maliwatoni, Emmy akawaza
kuwa hatimaye Lameck ameamua
kumkomesha kwa namna
nyingine.
Pigo la mwisho lenye hatari kupita
yote.
Lameck ameamua kumshirikisha
James siri nzito.
“Emmy.....” James aliita.
Emmy akauchuna kana kwamba
hasikii lolote.
Bado alikuwa maliwatoni bila
lolote la kufanya.
Nguo zake zilikuwa nusu
zimevulika na nusu bado
zikiutawala mwili wake. Alikuwa
anajiuliza aitike ama aendelee
kuuchuna.
“Shem....” sauti ya Gloria ikaita
kutokea mlangoni.
Emmy akazidi kuchanganyikiwa.
Emmy akapandisha nguo zake na
kutoka nje.
“Kuna nini?” akauliza.
“Simu yako ilikuwa inaita....naona
imekatika....hii inaita tena...”
Gloria kwa nidhamu akamkabidhi
Emmy simu.
Mlango ukafungwa akaitazama
namba inayompigia.
Mshtuko. Alikuwa ni Jose B
waukweli ama Sam wapili.
Simu ilikuwa imepigwa mara tatu
bila kupokelewa.
Jose matamaa . akaingiwa na
tamaa na wivu kutokana na simu
yake kuacha kupokelewa.
Akatuma ujumbe.
“Nakuja nyumbani kwako.”
Ujumbe huu Emmy aliusoma
baada ya kuwa amekata simu
badala ya kupokea.
Emmy akajikuta anapiga yowe,
yowe ambalo halikusikiwa nje ya
chumba hicho.
Akapagawa na ujumbe ule. Mume
wake alikuwa nyumbani na baba
yake mdogo pia alikuwa
nyumbani.
Aibu ya karne!!
Emmy akaingia maliwatoni
akajisafisha uso wake kwa maji
na sabuni.
Mara akanogewa akaamua kuoga
kabisa. Akajifungia maliwatoni.
Hakuweza kuisikia simu
ilivyoendelea kuita.
Alitumia dakika kumi na tano
bafuni.
Aliporejea akakutana na simu
saba zisizojibiwa.
Akatamani kumtumia Jose B
ujumbe lakini akajikuta akisahau
na kuendelea kuvaa upesi upesi.
Kosa kubwa!!
Wakati akihangaika, Jose Matamaa
alikuwa ametaharuki katika teksi
aliyokodi imfikishe nyumbani kwa
Emmy, Jose kijana mdogo kabisa
asiyejua uchungu anaoupata
mwanaume akiibiwa mke wake
ama kijana mwingine yeyote
anayempenda na kumthamini
mpenzi wake anapogundua kuwa
anasalitiwa. Alikuwa anafurahia
kummiliki Emmy. Ilifikia wakati
akawa anatamani kuwa mume wa
Emmy ambaye ni mke wa mtu
tayari.
Kwa jinsi ambavyo Emmy
alijirahisisha kuuachia mwili wake
ndivyo Jose alivyopata nafasi ya
kumtawala zaidi.
Sasa bila kujali ni kwa kiasi gani
anahatarisha ndoa ya Emmy
alikuwa anaelekea nyumbani
kwake.
Emmy alitoka nje upesi akamuaga
James kuwa anaonana na mtu
kwa dakika kadhaa nje. Usoni
alikuwa ametaharuki, James naye
hakuwa na amani moyoni kwani
ile hali ya kuona simu ya Emmy
ikionyesha jina la Sam wapili.
Akamkumbuka Jose B na jina hili
lilikuwa na namba ya simu ya
Jose.
Alitamani kutoka pamoja na
Emmy lakini ile tabia yake ya
kutopenda kuwadharau ndugu wa
mwanamke ikamtafuna
akamheshimu Lameck na
kuendelea kubaki akimsikiliza
huku Emmy akitokomea nje ya
geti upesi.
Jose B hakuwa na utani hata
kidogo. Hata yeye hakujielewa ni
nini anafanya. Hakujisikia
kumuogopa James, alifanya kile
ambacho moyo wake ulimtuma
kufanya. Sasa alikuwa jirani
kabisa na nyumba ya Emmy.
Penzi alilopewa na Emmy
likamvuruga akili yake na kuwa
kama mwendawazimu.
Umri wake wa miaka ishirini na
ushee uliruhusu kabisa kuwa
katika hali hii. Hali ya kuwa
mtumwa katika jambo jipya
katika maisha.
Emmy alikuwa wa kwanza
kumuona Jose B akiwa amejiweka
mbali kidogo na geti akiwa
ameuegemea mti mkubwa wa
mwembe usiokuwa na matunda.
Emmy akatembea kwa mwendo
kasi, akawa anatembea nusu na
nusu anakimbia akiwa
amelikamata gauni lake vyema.
“Sam......nini hiki
unanitaka...eeh”
Jose B akageuka, alikuwa
amenuna. Akamtazama Emmy
kwa jicho kali.
“Unataka kunifanya mtoto mdogo
sivyo?” akahoji kwa jeuri.
Emmy akashusha pumzi zake.
“Sikia Sam...nakuomba
tusizungumze kwa sasa kesho
nakuja nyumbani kwako tutakaa
muda mrefu tu....niamini
tafadhali, James yupo hapo na
bamdogo, wanatoka sasa hivi Sam,
nitaelewekaje mie pliiz nakuomba
Sam nakuomba sana.” Sauti yenye
kitetemeshi cha hofu ilimkumba
Emmy wakati anasihi. Hofu
ilikuwa imetawala.
Jose B akakumbwa na
sintofahamu baada ya sauti ile
kupenya katika masikio yake,
akajikuta akitabasamu.
Jose B alipenda sana
kunyenyekewa.
Akamkubalia Emmy. Wakaachana
bila kuagana.
James hakuwa anaelewa lolote
lililosemwa na Lameck juu ya
kupotea kwa watoto, alikuwa
anawaza juu ya Jose B ambaye
ana wasiwasi ndiye Sam wa
ukweli.
Ana hila gani na mkewe wa ndoa
tena ambaye ana mimba tayari?
Alijiuliza.
Hakupata majibu.
Akajisikia mchomo wa wivu
ukimuandama, akaanza kupata
suluba ya aina yake, akafumba
macho na kumuona ----- mmoja
waliyekutana jijini Mwanza,
akamuuzia Kizuzizi kwa shilingi
milioni sita, akapewa utangulizi
wa shilingi milioni mbili
akatoweka. Leo hii anaigusa ndoa
yake.
James akahisi kuwa Emmy
anaweza kuwa ana mahusiano ya
siri na Jose B ambaye kwa sasa
anajiita Sam.
Kwa hiyo huyu ----- amefikia
hatua anamfuata mke wangu hapa
hapa nyumbani kwangu?
Haiwezekani hata kidogo
wanichezee shere hawa. Hivi
wananijua vizuri kweli?
James alihamaki.
Lameck aliigundua hali ya utulivu
jinsi ilivyopotea katika uso wa
James. Akaona asiendelee
kuongea sana akamtazama na
kumsikitikia kwa mengi.
Likiwemo la kulea mimba ambayo
si yake na sasa ana wasiwasi na
mkewe baada ya kupigiwa simu
kisha akatoka nje.
Lameck akaamua kuaga na
kuondoka zake.
Kitendo cha Lameck kuaga
kikampa James nafasi ya kipekee
kujaribu kuuliza juu ya mtu
aliyekuja nyumbani na kisha
Emmy kutoka nje.
James aliingia chumbani na
kumkuta mkewe akiwa amejilaza
kitandani, hakuwa na furaha hata
kidogo, na kitendo cha mtu
kuingia pale chumbani
kikampagawisha.
Akataharuki waziwazi.
“Emmy...ni nani alikuja pale nje
ukamkimbilia mbiombio.”
“Nani? Mimi?” aliuliza swali la
kipumbavu Emmy kwa hofu.
“Kwani humu ndani tupo
wangapi?” James alijaribu kuzuia
jazba yake.
“Hapana ni rafiki yangu...nani
huyu mzoa taka alikuwa
anadai.....naniii” Emmy alitia
huruma, hakuwa na cha kujibu
mbele ya mumewe.
James akakunja ngumi yake imara
ili aweze kuikabili hasira yake.
Akafanikiwa kwa kiasi kidogo.
“Mlipeana namba lini na huyu
mtupa uchafu?” James kwa sauti
ya chini aliuliza, bado alikuwa
amesimama na Emmy alikuwa
ameketi.
“Hajanipigia simu wala.”
“Kwa hiyo alikuita kupitia dirisha
la chumbani sivyo?” mwanaume
akazidi kukoroma. Sasa alikuwa
anatetemeka midomo.
Haikuwahi kutokea hata siku
moja katgika kipindi cha
mahusiano yao.
Emmy akakosa cha kujibu.
James akaitwaa simu ya Emmy
pasipo binti huyu kutarajia.
Akapekuapekua sehemu ya namba
zilizoingia, akakutana na majina
kadhaa ya kike. Hapakuwa na jina
la Sam wa pili.
Akajaribu kulitafuta jina lile.
Hakuna kitu.
Kijasho chembamba kikamtoka.
Akataka kuliendea kabati ili
arejee na ile namba ya Jose B
aiingize katika simu ya Emmy
akahofia kuzua utata baadaye,
alimjuaje Sam wa pili.
Kama Emmy na Sam wana
mahusiano lazima atamshirikisha
na hapa ndipo mkanda
utakapoharibika.
“na uhakika hujapigiwa simu na
mwanaume wakati nipo na baba
yako?”
“Haki ya Mungu tena mume
wangu.” Akaapa.
James akashikwa na hasira kali
akakumbuka kuwa wanawake ni
sumu kali, sumu isiyostahili
kuguswa hovyo. Hasira
zikampanda, ameua kwa ajili yake
na sasa hana imani kwa ajili yake.
Mkono ukawa mwepesi
ukalishambulia shavu la Emmy.
Kipigo kitakatgifu cha kwanza
katika ndoa kikafuata.
James akamwadhibu Emmy kwa
kujaribu kumficha.
Ugomvi wa kwanza ukazua kipigo.
Emmy alidhani anapigwa kwa
sababu za wivu pekee hakujua
kama kuna lolote ambalo James
anamuwazia kuwa huenda
analifahamu.
Wakati anapokea kipigo alijisifu
kimya kimya kwa machale
yaliyomcheza kwa kuifutilia mbali
namba ya Sam wa pili, na pia
meseji zake zote, hajui ni mizimu
gani ilimtuma lakini alijikuta tu
akitekeleza hisia.
Emmy alijisifu kwa kuamini kuwa
laiti kama James angeipata namba
ya Sam angeweza kumpigia na
mwisho wa siku angeujua ukweli
juu ya mahusiano yake ya
kimapenzi na baba mdogo. Jambo
ambalo lingepelekea siri tatanishi
ya mimba aliyonayo kuchukua
nafasi ya kuwa wazi.
Ilikuwa bora kupigwa kuliko siri
hiyo kuvuja.
Emmy hakujua kama mumewe
naye kuna siri zake ametunziwa
na Sam wa pili ambaye ni Jose B
waukweli.
Laiti angejua.......
***EMMY anaitetea siri yake
isifichuke kwa gharama
yoyote......
***JAMES anahisi Jose B
anatembea na mkewe..hajui
wameambiana nini.......
***LAMECK naye kimya kimya
anapigania damu anayoamini ni
yak wake...
**MWANAMKE aliyemteka Grace
naye..........
ITAENDELEA
 
na wewe pia Analyse

umetuharibia uondo na copy paste yako ya maneno awili kwa line. muwe mnaheshimu thread za watu as zinaleta utamu na sie kusubiria usidhani ni misifa huku unandandia, anzisha yako as hatukukuomba uingilie humu. unajionyesha tabia ya kudandia ndio zako na hauna subira hata kuwa mke/mume utakuwa majanga tu ya kiaina yako.

Umetumia maneno makali sana hapo mwishoni,ila yote kwa yote samahan kwa kukuboa.
 
Last edited by a moderator:
Wapendwa;

Endeleeni. Stimu imeshapotea.
 
  • Thanks
Reactions: ram
Back
Top Bottom