MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Alikuwepo jamaa mmoja kijijini aliyekuwa mwema na kupendwa na watu wote. Aliwajuwa watu wote. Alimsaidia kila mtu kwa uwezo wake. Watu wote walimjuwa. Alikijijuwa kijiji chote, kila kipembe, kila mtaa, kila barabara, kila uchochoro.
Baada ya muda Mungu alimjaalia upofu, akawa haoni kabisaa. Lakini upofu haukua tatizo kwake kwani alikijua kijiji chote, hivyo aliweza kuenda huku na kule bila ya msaada hata wa bakora.
Siku moja, usiku wa giza totoro, hakuna mbalamwezi, alitoka akiwa amechukua kandili na kuanza kutembea mitaani. Mtu mmoja aliona mwanga, akatoka nje na kumfata. Alipogundua kuwa ni yule kipofu kwanza alicheka, kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwaaa!
Mimi nilidhani ni mtu amepotea au amepotelewa, kumbe wewe! Unatembeaje na kandili huku ukijuwa kuwa huoni?, aliuliza yule mtu.
Kwa nini bwana kipofu alitembea na kandili usiku wa giza ilhali yeye haoni?
Kama utapata jawabu alilojibu yule bwana kipofu, utakuwa umeelewa fundisho la hadithi hii. :confused2:
Baada ya muda Mungu alimjaalia upofu, akawa haoni kabisaa. Lakini upofu haukua tatizo kwake kwani alikijua kijiji chote, hivyo aliweza kuenda huku na kule bila ya msaada hata wa bakora.
Siku moja, usiku wa giza totoro, hakuna mbalamwezi, alitoka akiwa amechukua kandili na kuanza kutembea mitaani. Mtu mmoja aliona mwanga, akatoka nje na kumfata. Alipogundua kuwa ni yule kipofu kwanza alicheka, kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwaaa!
Mimi nilidhani ni mtu amepotea au amepotelewa, kumbe wewe! Unatembeaje na kandili huku ukijuwa kuwa huoni?, aliuliza yule mtu.
Kwa nini bwana kipofu alitembea na kandili usiku wa giza ilhali yeye haoni?
Kama utapata jawabu alilojibu yule bwana kipofu, utakuwa umeelewa fundisho la hadithi hii. :confused2: