Habari za afya ya Dr. Harrison Mwakyembe

Fungeni hii topic,muda tunaotumia hapa ni wa thamani sana,wakuu toeni
Ingependeza kutoa sababu za kufunga bandiko hili.. "kusema funga tu" haitoshi. Toa sababu a, b, c, n.k then wajumbe watajadili sababu zako na iwapo zitakuwa za msingi hapana shaka bandiko litafungwa..
 
Kuna mtu yoyote ambaye ana taarifa sahihi husiana na hali ya kiafya ya Mh. Mwakyembe maana mtaani kuna habari tata mno.

Naomba tushirikiane.
Imejulikana kuwa yu bhuheri wa afya!sasa kwa nini hii habari iendelee kujadiliwa?
 
Jina na huyo "mchawi" ni nani?

Ni Ujinga wa hali ya Juu viongozi wa nchi kuamini kuna uchawi wa kufanya kazi kipindi hiki 21st century. Si wangefanya huo uchawi utoe UMEME wa bure vijijini na majimboni na pia nyumba zijengeke na mabarabara

Tuache huu Ujinga uliokithiri kwenye mawazo ya Jamii zetu. Kuna mengi ya maana ya kufanya tena extremely challenging and rewarding too.
 
Waafrika ndivyo tulivyo, hata tukasome Havard sijui Oxford, hatubadiliki, ndivyo tulivyo.

Siku tunashuka Airport kurudi nyumbani tunakarudisha kale kaujinga ketu ambako kamelifanya bara letu liendelee kuwa maskini.

Nakubaliana na Nyani, sisi ndivyo tulivyo.

Ila kama mbunge wetu kaumwa kwasababu Chenge kanyunyizia dawa, hii ni kashfa kubwa sana kwa wana Kyela. Ina maana nguvu zetu ndogo sana na tumeshindwa kumlinda mheshimiwa wetu.

Iweje tuzidiwe na Wanyamwezi (Spika), Wahehe(Makinda), Wasukuma (Stela) na wengine? Iweje wao watoto wao washindwe kuathirika na hilo juju la msukuma Chenge?

Inabidi twende Malawi tukalitafuta lenye nguvu zaidi, next time mtatukoma! kwi kwi kwi!!!!!
 
Jina na huyo "mchawi" ni nani?

Ni Ujinga wa hali ya Juu viongozi wa nchi kuamini kuna uchawi wa kufanya kazi kipindi hiki 21st century. Si wangefanya huo uchawi utoe UMEME wa bure vijijini na majimboni na pia nyumba zijengeke na mabarabara

Tuache huu Ujinga uliokithiri kwenye mawazo ya Jamii zetu. Kuna mengi ya maana ya kufanya tena extremely challenging and rewarding too.

Chenge msomi wa Havard University.

Hana uchawi wowote, anatishia tu, waoga wakapata mshutuko, wanaojiamini hakuna kitu.
 
Naona msomi wa Harvad aliishiwa mbinu! Labda tumuulize Sumaye kama huwa pia wanafundishwa somo kama hilo! Kweli haya ni maajabu na kweli!!
 
Wote waliofanya haya ni wabunge wa CCM au sio? Najaribu kuunganisha na habari zilizozagaa wakati wa uchaguzi kuhusu misusuru ya wagombea wa CCM huko Bagamoyo.

Hayo ndiyo matokeo ya kujenga mfumo wa mediocre. Wana CCM hawaamini tena kama wanaweza kufanikiwa katika maisha kwa njia za kisayansi ikiwemo kufanya kazi kwa bidii. Wao ni ujanjaujanja, uchawi, etc. So long as wanaendelea kutawala habari ya maendeleo tusahau. Aibu!
 
Naona msomi wa Harvad aliishiwa mbinu! Labda tumuulize Sumaye kama huwa pia wanafundishwa somo kama hilo! Kweli haya ni maajabu na kweli!!

Kwani is it confirmed kuwa mlozi ni Chenge ndipo tudodose ikiwa Havard wanafundisha hilo somo??

On a serious note jamani..ushirikina hauna msomi wala nini..... hasa kwa wanasiasa wetu.... wanahofu na uchu wa madaraka kiasi kuwa wako radhi kutumia a cocktail of strategies to get into or cling to power....na hii inatiliwa nguvu na sie wananchi kushindwa kusema kwa nguvu..NO...YOU HAVE NO CAPACITY NOR MORAL LEGITIMACY TO REPRESENT US...katika ngazi yeyote ile...inachekesha kuona kuwa hata wanaowania vijitaji hata vya ulimbwende nao hukimbilia nguvu za giza!! Jamani WaTz we are doomed...
QUO VADIS???
 
Kwa habari hii inamaanisha kwamba ili mbunge aweze ku-persevere bungeni inampasa atembelee Bagamoyo kwanza.

Swali langu ni moja; Huyu mheshimiwa aliyemwaga mavituzz bungeni hakumwaga kwenye himaya ya Mwakyembe peke yake.. Alivimwaga na kwenye himaya za Spika, Naibu Spika na vilevile kwenye himaya za wengine "wateule". Je, hawa wengine ambao hawakupigwa "stroke" bungeni walikuwa na "kinga" za Bagamoyo?

Yaani nashindwa kupata picha mtu aliyewahi kupewa madaraka makubwa serikalini anaweza kufanya "ujinga" wa dizaini hizi. Kwahiyo huyu jamaa alikua anatumia "mazingaombwe" katika utendaji wake wa kazi nyeti alizopewa serikalini. Mtu za dizaini hizi zina-deserve kulala Keko maisha yao yote. @#$%&^58@#^ kabisa.
 
kuna mahali mkuu halisi ameonyesha wasiwasi wake wa hili jambo kuhusishwa zaidi na matumizi ya utaalamu wa kijadi (uchawi) n sio utaalamu wa kisasa
(sumu). mi naona ana hoja na tujaribu kuangalia pia kama huyo "mbunge" alikuwa anamwaga vitu vinavyohusiana na utaalamu wa kisasa zaidi.

aidha nilitumaini kwamba baada ya taarifa hizi hizi kupatikana ukumbi wa
bunge ungefungwa na wale jamaa wanaovaa nguo nyeupe zinazokinga mwili mzima au wanaofanana nao wangeingia kazini kabla ya kuruhusu ukumbi huo kutumika tena. lakini naona hata wahusika wa juu kabisa nao wamejikita
kwenye imani uwezekano wa matumizi ya utaalamu wa jadi.

naomba tu ifikapo karibu na 2010 tusianze kuona waheshimiwa wetu wakianguka moja baada ya mwengine na itakuwa tooo late. mola pishilia mbali hili balaa.
 
kafara said:
Aidha nilitumaini kwamba baada ya taarifa hizi hizi kupatikana ukumbi wa
bunge ungefungwa na wale jamaa wanaovaa nguo nyeupe zinazokinga mwili mzima au wanaofanana nao wangeingia kazini kabla ya kuruhusu ukumbi huo kutumika tena. lakini naona hata wahusika wa juu kabisa nao wamejikita
kwenye imani uwezekano wa matumizi ya utaalamu wa jadi.QUOTE]

Hao wanaoingia na hizo protective gears...wanafanya hivyo kwa kuwa wako scientific minded. Na kama kweli bunge zima lingekuwa haliamini uchawi katika hali ya kutia aibu na kujidhalilisha..lazima hao toxicologist/chemist etc..wangeshaitwa. Ofisi ya mkemea mkuu ingeshatinga hapo.

But the question is why not?

Kwa sababu mentality za tasisi yote ya bunge na washiriki wao..moja kwa moja imelenga kuwa tukio hilo is not scientific ni zimzinga wa vodoos!

Na hakuna shaka hao ndio viongozi wetu. Totaly primitive kama ..the oldest reptilia...on the deep ocean.

Hao ndio viongozi wetu..How dare.... wataweza kukemea ..mapigo yanayowapata Albino, wazee wenye macho mekundu, wachuna ngozi au wafanya biashara za vioungo vya watu?
 
Mungu atamlinda dhidi ya wale wote wenye nia mbaya juu yake, na huyu yampasa ajue kuwa watz twamwangalia anaweza kujikuta akiwa na wakati mgumu hata kupita in public places.
 
Data zinasema Dr. Mwakyembe alikuwa Muhimbili jana kwa masaa kama matano kwa uchunguzi zaidi. Aliambiwa alipata stroke ndogo.

Kwasasa yuko nyumbani kwake Dar akipumzika.

Mchapo: Nimewaambia kamati ya ufundi Kyela wote wafukuzwe kazi kwa kumpeleka mwanao Dodoma akiwa mtupu. Haiwezekani mbunge wao akadondoka kwa juju ya Chenge huku wengine wote hawajatetereka. Itabidi tuchague kamati nyingine kwi kwi kwi!!!!
 
mzee Dr. Ameenda Muhimbili leo asubuhi (jumamosi).. unajua hawa jamaa wanatufanya hata kuona unyasi tu sisi tunadhania Nyoka.. damn.. mafisadi!!
 
Kuna kiongozi mmoja mwandamizi aliwahi kuniambia, kuwa kuna baadhi yao wakati tayari kutmia njia yoyote ile kuhakikisha wanalinda maslahi yao, hata ikibidi "kuua". Hii ilikuwa mwaka jana.
"Desperate times, calls for desparate measures". Hapa kisomo huwekwa pembeni. Sishangai matendo ya Mzee vijisenti.
 
Hivi Dk nae kaanguka kama wakati ule alivyoanguka Mh. Sagaf????

Yaonyesha mafisadi walianzia zamani!!!!
 
Huyo Mbunge mbona hajaanikwa hapa na kama inzi wa walikuwepo waking'ong'a ,watuekee hiyo clip maana mambo ya siku hizi bila ya ushahidi inakuwa ni majungu yaliopikwa tu ,hapa kama hatajwi mtu basi huku ndiko kuchafuliana ,nashangaa magazeti hayakumtaja basi hata JF ,sijui kule KL ambako wana bango linalosema wao ndio wa mwanzo kuweka habari nyeti japo harufu au sifa za mhusika .
 
Back
Top Bottom