Habari ya ITV usiku huu kuhusu uchangiaji wa Figo haipo sahihi, itaogopesha wachangiaji

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Upandikizaji wa figo (renal transplant) sasa hivi unafanyika hapa hapa nchini kwetu. Na tuko mbioni pia kuanza upandikizaji wa maini (liver transplant). Huko nyuma tulilazimika kuwapeleka wagonjwa wanaohitaji huduma hii nje ya nchi, hasa India kwa gharama kubwa ya fedha za nje za USA dollars. Wagonjwa wengi walikosa huduma hii kutokana na gharama hiyo kuwa kubwa.

Upandikizaji huu huhitaji ndugu wa karibu wa mgonjwa kumchangia figo moja mgonjwa. Hakuna madhara yo yote ya kiafya yanayotokana na kuchangia figo kama ilivyo kwenye kuchangia damu.

Jamii inatakiwa ielimishwe hivyo. Kwamba hakuna madhara ye yote ya kiafya yanayotokana na uchangiaji figo. Cha muhimu ni kuwa anayechangia awe ni ndugu wa karibu wa mgonjwa yaani watoto wake, au kaka au dada wa mgonjwa tu. Hawa ndiyo wenye uwezekano mkubwa wa tissue za miili yao ikiwemo hiyo ya figo kuwa compatible kwani wana share vinasaba (DNA) vingi kwenye tissue zao. Mtu baki tu ambaye siye ndugu wa damu hawezi kuwa compatible ku donate figo kwani mwili wa mgonjwa utaikataa ( reject) hiyo figo kwa vyo vyote vile.

Sasa taarifa ya leo ya habari ya ITV imepotosha kuhusu uchangiaji huu wa figo. Imetoa taswira kuwa vijana wanaochangia figo hupata madhara makubwa ya kiafya. Imeogopesha vijana kuchangia figo. Hii itafanya huduma hii ya upandikizaji wa figo kukwama kwa kukosa donors.

Ila kwa upotoshaji huu, wa kulaumu siyo ITV au vyombo vingine vya habari bali ni wizara ya afya imeshindwa kufanya uhamasishaji sahihi kwa umma kuhusiana na huduma hii ya renal transplant. Uuzaji au ununuzi wa figo ni kosa la jinai kisheria duniani kote. Hili vijana wanatakiwa kulijua, kwanza ni kinyume na sheria na pili kisayansi mchangiaji ni lazima awe ndugu wa karibu kinasaba ili upandikizaji huo kuwa na mafanikio. Hata mke au mume hawezi kumchangia figo mke au mume wake kwani vinasaba vyao ni tofauti kwani hawana undugu wo wote wa damu.

Ni vyema sasa wizara ya afya ikatoa ufafanuzi sahihi kwa vyombo vyote vya habari na sehemu mbali mbali kuhusu huu uchangiaji figo ili kuondoa hii taharuki inayoendelea kwa sasa ya utoaji figo na uuzaji figo hasa kwa vijana ambao ndiyo wachangiaji wakubwa.
 
Ugonjwa wa figo,kwasasa ni tatizo kubwa sana,elimu izidi kutolewa namna ya kujiepusha na visababishi vya ugonjwa huu.

Ni ugonjwa ghali sana kuuhudumia,nikimaanisha kufanya dialysis,na hata kumpata mtu wa kumtolea mgonjwa,bado ni changamoto,wengi ni waoga wa kutoa figo,kumsaidia mgonjwa.

Wizara ya afya iangalie namna bora ya kuhamasisha uchangiaji figo.
 
Niliona pia siku ya figo duniani kwamba unapopewa hiyo figo bado unatakiwa kuendelea kutumia dawa zinazozuia kinga za mwili kuishambulia hii figo kwa sababu zinafanya hivo naturally kuulinda mwili dhidi ya kitu kipya mwilini.

Gharama ya hizi dawa ni milioni 6. Nikasema dah sasa mbona kama kwa masikini unaweza kufa tena pamoja na kupata donor! Milion 6 usawa huu sio mchezo. Ila pia we hapa kama unasema kuchangia figo ni sawa na kuchangia damu mbona unasema lazima itoke kwa ndugu wa damu, kwani na damu inahitajika itoke kwa ndugu?
 
Niliona pia siku ya figo duniani kwamba unapopewa hiyo figo bado unatakiwa kuendelea kutumia dawa zinazozuia kinga za mwili kuishambulia hii figo kwa sababu zinafanya hivo naturally kuulinda mwili dhidi ya kitu kipya mwilini.

Gharama ya hizi dawa ni milioni 6. Nikasema dah sasa mbona kama kwa masikini unaweza kufa tena pamoja na kupata donor! Milion 6 usawa huu sio mchezo. Ila pia we hapa kama unasema kuchangia figo ni sawa na kuchangia damu mbona unasema lazima itoke kwa ndugu wa damu, kwani na damu inahitajika itoke kwa ndugu?
Ugonjwa wa figo,kwasasa ni tatizo kubwa sana,elimu izidi kutolewa namna ya kujiepusha na visababishi vya ugonjwa huu.

Ni ugonjwa ghali sana kuuhudumia,nikimaanisha kufanya dialysis,na hata kumpata mtu wa kumtolea mgonjwa,bado ni changamoto,wengi ni waoga wa kutoa figo,kumsaidia mgonjwa.

Wizara ya afya iangalie namna bora ya kuhamasisha uchangiaji figo.
Sababu kubwa zinazoharibu figo aka ugonjwa wa figo aka Chronic Kidney Disease aka CKD - end stage ni ugonjwa wa kisukari (Diabetes mellitus) na shinikizo la damu (Hypertension). Haya magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu kusema kweli hakuna njia ya kuyakwepa na kiini chake kiko kwenye kinasaba (genetical). Yameenea dunia nzima na huku kwetu jinsi tunavyoendelea kuyatokomeza yale magonjwa ya kuambukizana ndivyo haya magonjwa yasiyokuwa ya kuambukizana yanavyozidi kuonekana kwa wingi na kuongoza.

Ni kweli gharama ya kutibu ugonjwa kama CKD end stage ni kubwa sana: kuanzia haemodialysis, renal transplant hadi life long immunosuppressive drugs. Ndiyo sababu kuu ya kuwa na bima ya afya kwa wote. Bima hii haitakiwi kuwa kwa ajili ya magonjwa madogo madogo kama malaria, uti, typhoid na vidonda vya tumbo. Mtu anakata bima kwa mambo makubwa kama haya ya figo na siyo kwa mambo hayo madogo madogo ya uti na kisonono ambayo gharama zake ana uwezo wa kuzilipia kwa cashe hata kama ni kwa kuuza kajogoo kake kamoja tu. Wizara ya afya needs to be serious kuwezesha bima ya afya ya gharama ambayo kila mtanzania ataweza ku afford ya shillingi isiyozidi TSh 30,000 kwa mwaka kwa kila kaya.
 
unasema kuchangia figo ni sawa na kuchangia damu mbona unasema lazima itoke kwa ndugu wa damu, kwani na damu inahitajika itoke kwa ndugu?
Figo ni organ yenye tissues nyingi za aina mbali mbali na vinasaba vya aina nyingi tofauti na damu. Damu wanasayansi wengine wanaichukulia kama nayo ni tissue na wengine wanaihesabu siyo tissue. Kuna aina tatu tu za damu ya binadamu kinasaba ambazo ni A, B na O. Tissues za figo na organs zingine zina maelfu ya HLA (Human Leukocyte Antigens) alleles. Samahahi Basata haina translation ya kiswahili ya maneno haya ya kiganga. HLA ni genetic make up ya mtu ambayo hurithiwa kutoka kwa wazazi wake. It is more complex than the blood group compatibility.
 
Upandikizaji wa figo (renal transplant) sasa hivi unafanyika hapa hapa nchini kwetu. Na tuko mbioni pia kuanza upandikizaji wa maini (liver transplant). Huko nyuma tulilazimika kuwapeleka wagonjwa wanaohitaji huduma hii nje ya nchi, hasa India kwa gharama kubwa ya fedha za nje za USA dollars. Wagonjwa wengi walikosa huduma hii kutokana na gharama hiyo kuwa kubwa.

Upandikizaji huu huhitaji ndugu wa karibu wa mgonjwa kumchangia figo moja mgonjwa. Hakuna madhara yo yote ya kiafya yanayotokana na kuchangia figo kama ilivyo kwenye kuchangia damu.

Jamii inatakiwa ielimishwe hivyo. Kwamba hakuna madhara ye yote ya kiafya yanayotokana na uchangiaji figo. Cha muhimu ni kuwa anayechangia awe ni ndugu wa karibu wa mgonjwa yaani watoto wake, au kaka au dada wa mgonjwa tu. Hawa ndiyo wenye uwezekano mkubwa wa tissue za miili yao ikiwemo hiyo ya figo kuwa compatible kwani wana share vinasaba (DNA) vingi kwenye tissue zao. Mtu baki tu ambaye siye ndugu wa damu hawezi kuwa compatible ku donate figo kwani mwili wa mgonjwa utaikataa ( reject) hiyo figo kwa vyo vyote vile.

Sasa taarifa ya leo ya habari ya ITV imepotosha kuhusu uchangiaji huu wa figo. Imetoa taswira kuwa vijana wanaochangia figo hupata madhara makubwa ya kiafya. Imeogopesha vijana kuchangia figo. Hii itafanya huduma hii ya upandikizaji wa figo kukwama kwa kukosa donors.

Ila kwa upotoshaji huu, wa kulaumu siyo ITV au vyombo vingine vya habari bali ni wizara ya afya imeshindwa kufanya uhamasishaji sahihi kwa umma kuhusiana na huduma hii ya renal transplant. Uuzaji au ununuzi wa figo ni kosa la jinai kisheria duniani kote. Hili vijana wanatakiwa kulijua, kwanza ni kinyume na sheria na pili kisayansi mchangiaji ni lazima awe ndugu wa karibu kinasaba ili upandikizaji huo kuwa na mafanikio. Hata mke au mume hawezi kumchangia figo mke au mume wake kwani vinasaba vyao ni tofauti kwaniF hawana undugu wo wote wa damu.

Ni vyema sasa wizara ya afya ikatoa ufafanuzi sahihi kwa vyombo vyote vya habari na sehemu mbali mbali kuhusu huu uchangiaji figo ili kuondoa hii taharuki inayoendelea kwa sasa ya utoaji figo na uuzaji figo hasa kwa vijana ambao ndiyo wachangiaji wakubwa.
Figo ya nguruwe vipi??
 
Back
Top Bottom