Habari hii haijanifurahisha kabisa

Habari hii haijanifurahisha kabisa

Mwanamayu

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2010
Posts
11,701
Reaction score
6,936
Kama mtanzania anatengeneza helicopter inaruka na kutua safely halafu anapigwa marufuku na idara ya serikali yaani serikali kuendelea na innovation yake halafu wazungu wanamtembelea, na kumwalika kwenye kiwanda chao.

Waziri mwenye dhamana na science na technolojia yuko wapi? Anawaza GPA na Division tu? Waziri wa viwanda yupo wapi? Hivi haelewi kuwa huu ndio mwanzo wa kuwa na viwanda vya helikopta nchini?

Kama wangelijua kuwa hizo helikopta nchini zingetatua matatizo makubwa ya wananchi wasingekubali huyu jamaa akutane na hawa wazungu, mfano, air lifting za wagonjwa vijijini, uokoaji, ulinzi, na kwenye vita.

Sasa kama jamaa atawaambia utaalamu wake na jinsi alivyotengeneza hio kitu basi Tanzania hii kuendelea ni kazi sana. Kwanza alitakiwa kuelimishwa kuwa utaalamu huo alionao ni 'classified' sio wa kumwambia mtu na serikali ingesaidia kuifadhi hazina hiyo. Sasa helikopta ya jamaa itanunuliwa na Tanzania kwa mikopo ya kuongeza umasikini.

Waliopewa dhamana hii sijiui wako wapi in terms of their minds.

Great nations zinatokana na great people ambao ni wachache sana na ni bidhaa hadimu mno!

Source: Wazungu wamtembelea mtengenezaji helikopta Tunduma
 
Umesema kweli mkuu
Jana kupitia TBC nilimuona jamaa Kaunda injini ya pikipiki
Kiukweli aliongea mambo mengi na mazuri.

Tanzania tuna vijana wazuri
Zaidi ya wale wanaotumika kupewa Viroba na kuropoka hovyo mitandaoni.

Serikali iwa angalie watu wenye ubunifu wao
 
Umesema kweli mkuu
Jana kupitia TBC nilimuona jamaa Kaunda injini ya pikipiki
Kiukweli aliongea mambo mengi na mazuri.

Tanzania tuna vijana wazuri
Zaidi ya wale wanaotumika kupewa Viroba na kuropoka hovyo mitandaoni.

Serikali iwa angalie watu wenye ubunifu wao
Kama wewe ulivyo. Umejisema mkuu
 
Kwan hiyo helicopter ilifanikiwa kurushwa angani??? Au ndo ile ilirushwa kwa photoshop??
Ni kipaji kizuri na angefika mbali iwapo angesimamiwa vizur
 
Sijajua kipengele gani kinazuia ubunifu ndani ya nchi, nimejiuliza sana hivi angekuwa ni mtoto wa muheshimiwa yeyote wangempiga marufuku?
 
Elimu haijapewa umuhimu unaostahili katika nchi yetu, huyo ilitakiwa hao wanaomzuia wamtafutie fursa zaidi afikie lengo na kutukomboa hapa tulipo
 
Hizo ni roho za huu mmea
1469996947495.jpg
 
Japo wanasema magenius wapo India kwa wingi lkn si haba hata Tz tukawanao wachache. Ila leo ukajitambua wewe ni shidaa kama huyu jamaa,,,, utaambiwa peleka shida zako kulee! Ila nitafurahi kusikia jamaa anapata shavu la kuhamia bondeni ndo hapo utasikia vigisu vya serikali..... ''Mchawi wako ni yule wanyumbani mwako''
 
Nani kakwambia inaruka na kutua safely, wewe usipoteze muda wako kufagilia ujinga
 
Umesema kweli mkuu
Jana kupitia TBC nilimuona jamaa Kaunda injini ya pikipiki
Kiukweli aliongea mambo mengi na mazuri.

Tanzania tuna vijana wazuri
Zaidi ya wale wanaotumika kupewa Viroba na kuropoka hovyo mitandaoni.

Serikali iwa angalie watu wenye ubunifu wao
Teh teh umeona usipoponda kidogo ufipa hutosikia raha? Hata pia wale ma IT badala ya kudeal nataaluma zao wameingiwa na tamaa ya 7000 wanazotamanishwa nazo na chama cha kijani. Taaluma yao umeushia kinunulika kwa 7000.
 
Back
Top Bottom