Habari hii haijanifurahisha kabisa

Habari hii haijanifurahisha kabisa

Sisi tuanaangalia D mbili basi ndio utaalam ulipoishia
 
Wewe ni mtu mweusi halisi,watu weupe wanayajua hayo yote uliyobwabwaja na bado wakaja kuangalia ubunifu yet hawakuridhika na kuishia kuangalia ,wakampa na mwaliko kabisa ,
Swali rahisi :- Kati yako wewe na hawa wazungu waliokufundisha hicho ulichokariri ,nani mwenye akili ...!!???
Hii ni roho mbaya,mijitu kama nyinyi ndio mliojaa huko TCCA,elimu ya kuungaunga,umeiba nafasi za watu lakini hata hiyo 1+1=2 uliojifunza bado huwezi kuitumia maana ungelijua usingelifikia hatua hii.
Kwani nani dunia ya leo anatengeneza ndege mpya kwa maana ya jet system zaidi ya kufanyia marekebisho kile walichobuni. WRIGHT BROTHERS ,
Utakufa kwa roho mbaya,mnfyuuuuuuuuuu....!!!!
Tena ukifa,ukafie mbali usije kuwapa watu shida ya kufukia mzoga wako.
Umemjibu vizuri, inasikitisha sana kuona watu wana mawazo mgando na roho mbaya kiasi hiki, kwa namna hii tutasubiri sana.
 
Tupende kusoma kwanza, elimu ndio utatufikisha mbali... bila shule ubunifu na uvumbuz wetu utakuwa huu wa kuunga unga vipisi vya skrepa na nondo
Ntajie Hao wenye elimu wana nini cha ziada?hata kuunda gari toy hawawezi.....hii ndiyo shida ya wasomi kusoma kwa kukariri....
Mtu akionekana Ana uwezo lazima itafutwe njia
Ya kumuendelezea....
Maana tz hatujambo kwa kuuwa vipaji
 
Tupende kusoma kwanza, elimu ndio utatufikisha mbali... bila shule ubunifu na uvumbuz wetu utakuwa huu wa kuunga unga vipisi vya skrepa na nondo
Eti vipisi vya skrepa,acha dharau dogo
 
Mtoa mada huna taarifa sahihi,jamaa hajakatazwa kuendeleza ubunifu wake,ila mamlaka husika imesema mtu anapaswa kuomba kibali ili aendelee na project,na huyo mtu wa helikopta alishaomba na kukubaliwa,sasa we unakuja hapa na kutokwa mapovu bila taarifa sahihi,kila kitu kinahitaji regulation, vinginevyo haina maana kuwepo kwa hizo taasisi husika,hebu jifikirie ikitokea ile helikopta imefabikiwa kuruka alafu ikawaangukia watu,unafikiri wa kulaumiwa atakuwa nani!?
 
Kama mtanzania anatengeneza helicopter inaruka na kutua safely halafu anapigwa marufuku na idara ya serikali yaani serikali kuendelea na innovation yake halafu wazungu wanamtembelea, na kumwalika kwenye kiwanda chao.

Waziri mwenye dhamana na science na technolojia yuko wapi? Anawaza GPA na Division tu? Waziri wa viwanda yupo wapi? Hivi haelewi kuwa huu ndio mwanzo wa kuwa na viwanda vya helikopta nchini?

Kama wangelijua kuwa hizo helikopta nchini zingetatua matatizo makubwa ya wananchi wasingekubali huyu jamaa akutane na hawa wazungu, mfano, air lifting za wagonjwa vijijini, uokoaji, ulinzi, na kwenye vita.

Sasa kama jamaa atawaambia utaalamu wake na jinsi alivyotengeneza hio kitu basi Tanzania hii kuendelea ni kazi sana. Kwanza alitakiwa kuelimishwa kuwa utaalamu huo alionao ni 'classified' sio wa kumwambia mtu na serikali ingesaidia kuifadhi hazina hiyo. Sasa helikopta ya jamaa itanunuliwa na Tanzania kwa mikopo ya kuongeza umasikini.

Waliopewa dhamana hii sijiui wako wapi in terms of their minds.

Great nations zinatokana na great people ambao ni wachache sana na ni bidhaa hadimu mno!

Source: Wazungu wamtembelea mtengenezaji helikopta Tunduma


Iliwahi kuruka? Ujinga huu..
 
Ile Chopa haikuwahi kuruka hata cku moja! jamaa alitengeneza sanamu la helicopter na c helicopter inayoweza kupaa..

Serikali imefanya la maana sana kumpiga marufuku, maana anaonekana ni mgonjwa wa akili mwenye kuleta mzaha na taaluma za watu.
 
Ile Chopa haikuwahi kuruka hata cku moja! jamaa alitengeneza sanamu la helicopter na c helicopter inayoweza kupaa..

Serikali imefanya la maana sana kumpiga marufuku, maana anaonekana ni mgonjwa wa akili mwenye kuleta mzaha na taaluma za wat
u.
Hivi ni kitu gani ushawahi kubuni?Nyie ndiyo mliyojaa na roho za korosho...tu
Wenzenu wana nini Vitu alafu mijitu Kama Nyie kutwa mnafikiria style za kuwat.....m madem zenu tu
 
Tatizo Watanzania hatuamini kwamba MTU anaweza kuwa mwenye ujuzi unaofaa ni mpaka ajue kuongea kiingereza na akiwa na degree hapo tunanyoosha mikoni lkn ukitafakari sana utangundua utambuzi wa ujuzi kwa njia ya vyeti pasi na kuwa na njia mbadala za kuwatambua watu wenye ujuzi ni tatizo kubwa pia tunashindwa kuelewa tofauti iliyopo baina ya ujuzi na elimu hivi ni vitu viwili tofauti na utambuzi wake ulipaswa kufanyika tofauti lkn kwanza ili uitwe kwenye usaili kwanza uwe na cheti, this is a problem. Ukienda kwenye makampuni yanayotambua hii kitu ninayoandaka hapa utakutana na watu wameajiriwa kwenye kampuni wanalipwa mishahara mikubwa kuliko elimu uliyonayo ukigundua utakuta unajisemea yaani Mimi ninadegree lkn wananilipa kidogo kuliko Fulani mwenye diploma lkn hujiulizi thamani yake kwenye kampuni ambayo wewe pamoja na kadegree kako huwezi kufikia tunahitaji kubadili mifumo ya utambuzi wa ujuzi pasi na kutumia vyeti kama kweli tunataka kwenda kwenye uchumi wa viwanda maana uchumi wa viwanda ambao watanzania hawatashiriki hautakiwa na faida ya moja kwa moja kwa Watanzania Tutafakari
 
Tatizo Watanzania hatuamini kwamba MTU anaweza kuwa mwenye ujuzi unaofaa ni mpaka ajue kuongea kiingereza na akiwa na degree hapo tunanyoosha mikoni lkn ukitafakari sana utangundua utambuzi wa ujuzi kwa njia ya vyeti pasi na kuwa na njia mbadala za kuwatambua watu wenye ujuzi ni tatizo kubwa pia tunashindwa kuelewa tofauti iliyopo baina ya ujuzi na elimu hivi ni vitu viwili tofauti na utambuzi wake ulipaswa kufanyika tofauti lkn kwanza ili uitwe kwenye usaili kwanza uwe na cheti, this is a problem. Ukienda kwenye makampuni yanayotambua hii kitu ninayoandaka hapa utakutana na watu wameajiriwa kwenye kampuni wanalipwa mishahara mikubwa kuliko elimu uliyonayo ukigundua utakuta unajisemea yaani Mimi ninadegree lkn wananilipa kidogo kuliko Fulani mwenye diploma lkn hujiulizi thamani yake kwenye kampuni ambayo wewe pamoja na kadegree kako huwezi kufikia tunahitaji kubadili mifumo ya utambuzi wa ujuzi pasi na kutumia vyeti kama kweli tunataka kwenda kwenye uchumi wa viwanda maana uchumi wa viwanda ambao watanzania hawatashiriki hautakiwa na faida ya moja kwa moja kwa Watanzania Tutafakari
 
Inawezekana chopper haikuwahi kuruka wala haikuwahi kusogea hata nchi moja, lakini kama nia na malengo ya mtengenezaji wa ule muundo wa chopper ilikuwa ni kutengeneza chopper basi kungekuwa na haja ya kumpatia wataalamu zaidi na kumpeleka sehemu ili ajifunze zaidi.
Kunaweza kukaja watu wakasema hiyo bajeti ya hiyo ziara na mafunzo itatoka wapi? Lakini kumbuka hakuna kizuri bila jasho, ni uthubutu mzuri wa mbunifu kujaribu kutengeneza brand ya chopper kutoka nchini.
Unaweza jiuliza yale magari ya nyumbu kwanini hayapewi nafasi yaweze kutumika nchini ili tuache kuingiza magari toka nje?? Kwanini tusiwatumie vijana watengeneza vipuri ili kuomba leseni ya kutengeneza vipuri vya aina mbalimbali za magari yanayotoka nje??
Kuna tatizo sehemu, kuna tatizo katika utendaji wetu, kuna tatizo katika ufikiri wetu na nafikiri kuna tatizo zaidi katika uzalendo wetu, hatupendani na hatutamani kuona mwenzetu akitoboa hili ni zaidi ya tatizo kwakweli.
Mfano mdogo tu, huyo mmoja akifanikiwa ina maana watanzania wengi watakuwa wamefanikiwa, tutakuwa tumepunguza kwa kiasi tatizo la ajira. Nafikiri ni wakati wa kujitathimini kuhusu upendo na uzalendo wetu baina yetu na kwa ajili ya nchi yetu.
 
Sisi tumelaaniwa

Hatuna utamaduni wa kujali na kuthamini vyetu, chukua mfano mdogo tu leo hii vijana wetu wanauza imported apples toka South Africa wakati tuna ardhi tele kule Lushoto, Makete na Njombe inayoweza kustawisha matunda hayo kwa wingi kabisa, tumeshindwa kuwajengea uwezo vijana hao wakajiajiri kwa kuwa na mashamba yao hapahapa nchini, mfano mwingine ni kuagiza vijiti vya kuchokonolea meno kutika China wakati mianzi imejaa karibu kila mkoa hapa nchini na tungeweza kuingiza kwenye stadi za kazi watoto wetu wakajifunza kutengeneza vijiti hivyo (elimu ya kujitegemea - enzi zetu)

Tunatumia nguvu nyingi kuabudu na kuthamini imports badala ya kutumia nguvu hizo kusaidia wabunifu wa ndani, nashangaa viongozi wetu huko ulaya na kwingineko huwa wanaenda kujifunza au kushangaa!
 
Hata kama helikopta inaweza kuruka(ninayo shaka na hili) huu si ubunifu bali kukopi. Ubunifu ni pale kitu kilichobuniwa ni aina pekee, kipya hakijawai kuwepo.
 
Katika mambo yanatoka kufuata utarati u ni aviation.Huwezi jitengenezea midude na kuirusha angani.ndo maana irkut mc21 mpaka leo haijaruka sababu ya utaratibu
 
Kama Nchi mpaka leo tuna uhaba wa madawati,vyumba vya madarasa, unafikiri nani atauthamini mchango wa huyu dogo,hawaoni kama hii ni fursa ,wao fursa ni kuwa na bomba la mafuta kupita kule Tanga.
 
Huyo kijana kibinafsi kashafanikiwa lakini kama nchi inabidi ilifuatilie iliswala kwakaribu sana
 
Umesema kweli mkuu
Jana kupitia TBC nilimuona jamaa Kaunda injini ya pikipiki
Kiukweli aliongea mambo mengi na mazuri.

Tanzania tuna vijana wazuri
Zaidi ya wale wanaotumika kupewa Viroba na kuropoka hovyo mitandaoni.

Serikali iwa angalie watu wenye ubunifu wao

Tanzania ina vijana wenye akili sio kama vilazaa wa lumumba wanaotegemea buku 7 na kugombea uongozi wa kuteuliwa.
 
Back
Top Bottom