Ni andiko gani katika Biblia linalomzuia Gwajima kumkemea Bashite kama muovu? Biblia imejaa makemeo. Isome vizuri. Kuna watu waliambiwa wazi wazi kuwa ni wachawi, sembuse Gwajima kumsema Bashite kuwa ni zero brain na hiyo zero brain ndio inamfanya awe mhalifu na asiyefaa kupewa nafasi aliyopewa. Ukizama kiroho utabaini kuwa Gwajima anaisaidia nchi na anamsaidia mkuu wa nchi. Anachokifanya kinapunguza kasi ya vitendo vya kihalifu vinayofadhiliwa na Bashite, lakini ukimtazama katika jicho la kutopenda kumgusa Bashite kwa sababu zozote zile za kimwili, utamwona Gwajima kama anahangaika tu na hamhubiri Mungu. Kumbe ni Mungu yupi anaruhusu udanganyifu na hila?Gwajima anahangaika bure tu na mambo yasiyomuhusu. Anamuhubiri Makonda badala ya Mungu, alafu na waumini wake wanaitikia ameeee...eennn!! Ajabu sana