Gundu la kinyesi

Gundu la kinyesi

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,170
Reaction score
829,115
Gundu ni kiambishi cha kuelezea mambo kwenda mrama mambo kuharibika, mambo kutanzika! Hali ya kuchukiwa na hata kutengwa.
Kinyesi pamoja na kwamba ni samadi nzuri kikishaoza na uvundo kwisha lakini. ! ni makapi ya chochote ulichokula, yani mwili umeshachukua vyote vya maana kwahiyo hicho kilichobaki ni uchafu

Kinyesi ni kitu kingine kabisa licha ya uvundo wake lakini ukikikanyaga lazima uchechemee kama mtu aliyechomwa na mwiba..yani unapata hisia fulani mbaya kabisa akilini ukiwa umekikanyaga....na ndio maana hakuna nyumba inayokamilika bila kuwa na choo ya kuhifadhia hiyo kitu
Ukisikia mtu ana kimavi, muonee huruma maana ni mwendo wa mikosi mwanzo mwisho

Sasa hebu pata picha hii
Unaamka asubuhi na kukuta barazani kwako au getini kuna bonge la kimba! Unajiuliza na kutafakari mengi lakini unapuuzia na kufanya maarifa ya kusafirisha

Hii inaweza kutokea hata zaidi ya mara tatu na kudhani ni watu wakorofi au pengine wavuta bhangi....pole sana ni heri wawe ni hao kuliko kama ni mambo ya kishirikina..kwakuwa baada ya hapo kila kitu kitaanza kuyumba, vile watu wanavyokiogopa kinyesi na kujitenga nacho ndio hivyo hivyo nawe utakuwa
Ni mambo mabaya ya kishetani huja na madawa na manuizi ya uharibifu mbaya...na akimaliza huseta ukuta kwa makalio yake

Naamini wengi walishakutana na jambo kama hili kwa namna moja au nyingine na baada ya hapo ukaanza kukutana na milima na mabonde, hutakiwi kutafuta waganga wa kienyeji. ....kwa imani yako fanya utaratibu wa ibada ya kutakasa makazi. ..hiyo ndio dawa pekee ya kuweza kukuokoa na hili janga

NB: ushauri wa bure
Kama wewe si mpenzi wa hizi mada nakushauri upite kimya
 
Habari bila picha ni sawa na mboga bila viungo vyote lakini mmh kwa habari hii picha zake zinaweza kuchafua hali ya hewa basi walau ngoja niweke hii
1466648117533.jpg
 
Asante kwa taarifa, kuna wapumbavu walitupaga kinyesi ktk NYUMBA isiyoisha tukajua hii ni mkosi tukakemea,sasa hivi NYUMBA Ina mpangaji,jina LA bwana libarikiwe

Ni kweli watu wanatumia sana kimba kuroga nyumba zinazojengwa
Ndio maana ile sehemu ya kutolea kinyesi ni kharamu kubwa kuitumia kama sehemu ya starehe za kingon...ile dhambi ile husimamisha jua na hata shetani akiona hicho kitendo hutimua mbio
Ni kuku pekee ambaye ameruhusiwa kutumia sehemu hiyo kwa mambo yote
Haja kubwa
Haja ndogo
Mapenzi
Uzazi
 
Naomba nifafanue kidogo hapa kuhusu huo ushirikina
1.kinyesi kinachopakazwa kwenye kuta lengo lake ni kuitia nyumba gundu ujenzi usiendelee
2. Kile cha Kuwekwa getini au mlangoni aidha kinamlenga atakayeanza kutoka au mlengwa aliyetajwa kwa jina kwenye huo ushirikina
Kumbuka mada ya malango na ile ya nafsi katika utambulisho
 
Back
Top Bottom