Bongo bwana, sasa huyu mama katumia sheria gani kuzifungia??!! Hao jamaa kama wako makini wakienda mahakamani wanashinda.
Kama kuna kitu ambacho kimekuwa kikichefua moyo wangu, ni pamoja na hili la makampuni kuwaona wafanyakazi wao kama viraka tu! Nimekuwa nikijiuliza hawa recruters agences wanamilikije idadi kubwa ya wafanyakazi wakati ofisi zao zipo kwenye mikoba tu?! Na kwanini mfanyakazi wa kampuni unayofanyia kazi pindi upatwapo na tatizo, kampuni inakuambia kuwa wewe si mwajiriwa wetu bali wewe ni wa agent aliyekuleta! Hili lipo tanzania tu. Kwa tangazo hili la wafanyakazi kumilikiwa na kampuni wanazofanyia kazi ni la kupongezwa sana. Kama si matamshi ya kisiasa ngoja tusubiri matokeo ndani ya hizi cku 30.
Nakusoma vyema sana mkuu... Ila nadhani wewe ndio hujamuelewa vizuri Waziri wa Kazi na Ajira.
Naona dhana nzima ya staffing services bado haijazoeleka na kueleweka Tanzania, kulingana na malalamiko ya watu humu.
Kwa uzoefu wangu sijawahi kuona sehemu yoyote ile ambapo mtu anatafuta kazi kupitia staffing agency halafu agency isipate asilimia fulani ya malipo kutoka kwa waajiriwa wake.
Habari hii si Tanzania tu, Marekani hii issue imekuwa bonge la industry kwa wajanja wachache. Mtu analipwa dola 60 kwa saa sehemu anapofanya kazi, lakini kwa agency kaambiwa analipwa dola 50 kwa saa, kwa kila saa anayofanya kazi agency inachukua dola 10. Maana yake akifanya kazi wiki mbili masaa 40 agency inachukua dola 400, kwa mwezi inachukua dola 800, kwa mtu mmoja tu.
Agency ikiwa na vichwa 100 tu vya namna hii, you are talking about $80,000 kwa mwezi.
Kazi yao kufungua kiofisi tu na kukuunganishia, kitu ambacho hata www.monster.com inaweza kufanya.
Ni wizi mtupu.
Mkuu naomba nikusahihishe... nielewavyo...kilishizuiwa sio recruitment process outsourcing BALI ni labour brokerage. kuna tofauti hapo.
labour broker ni yule ambae mimi kama kampuni namwambia nahitaji assistant accountants 5, na yeye anawaajiri na kuwaleta kwangu mimi principal. in turn mimi namlipa mshahara wao plus namchaji commission-about 20% of salary..
Mimi sina tatizo na agencies kuchukua chao, mbona tushazoea hata madalali wa nyumba wanakuunganishia na kuchukua chao?
If this is a one time fee, sina tatizo, unawalipa gharama za uwakala wa kukuunganishia (ideally this should be done by the company you will work for).
Tatizo langu linakuja pale agency inapochukua sehemu ya hourly wages/ salary kama vile baada ya kukuunganisha wanafanya sehemu fulani ya kazi zako, wakati wamekaa tu wanakusanya chajuu. Fine, kama umeajiriwa na agency kuna habari za kodi zao na makato and all that, wanaweza kuwajibika kwa hayo, hususan kama umeandikishwa kama muajiriwa wao na sio wa unakofanya kazi (consultancy based assignments), lakini hata katika hayo, mfanyakazi awe na haki basi hata ya kuopata full disclosure.
Kinacholipwa na anapofanya kazi ni kipi,
agency yake inamkata vipi kwa ajili ya health insurance na mafao etc, na yeye anacholipwa ni kipi.
Sasa hivi unaona huyu Ng'wanakilala (is this Lulu?) kaulizwa kitu cha kwanza kusema ni ku cite confidentiality clauses.
I am all for the protection of a healthy business environment, I wrote a lenghty and balanced article at vijana.fm on the subject if I may say so myself,. But at some point workers fundamental rights must be protected.
I am all for the free market, but the free market without some obvious regulations is not good even for itself.
Lakini, hivi kuna mtu ambaye anapitia hizi staffing agencies halafu hajui kwamba kama wakikutafutia kazi, tuseme temp-to-hire, na wao wanakuwa wanapata cha kwao mpaka utapoajiriwa 'permanently' na huko walikokutafutia kazi?
I thought that was common knowledge but the specifics are the ones that were supposed to be confidential?
That's common knowledge.
What is not common knowledge is the percentage. Ukitaka kuulizia habari hizo tu unakuta kabla hata ya agency kuku interview ilikwisha kusainisha confidentiality clauses kwamba hutakiwi kujadili kule utakapofanya kazi watawalipa kiasi gani agency yako.
Watu wengi hufikiri kwamba tofauti ya wanacholipwa na agencies na agencies inacholipwa na kule wanakoishia kufanya kazi ni ndogo sana na inakuwa justified na gharama inazoingia agency (payroll, taxes, administration etc) lakini ukweli ni kwamba jamaa wanachukua hata zaidi ya 10 bucks an hour in some cases.
Katika mambo machache niliyokubaliana na Papa mwenzangu Benedict XVI mojawapo lilikuwa hili la kupinga ajira zisizo za kudumu.
Mazee, hiyo ya staffing agency kupata kiasilimia fulani kutoka kwenye wage mbona ni standard practice? Almost all of them do it.
Nimeshawahi kupokea temps kutoka Robert Half na mkataba wa makubaliano ya staffing uliweka bayana kwamba katika hourly wage ya temps wao watachukua kiasi fulani mpaka pale assignment itakapoisha au mpaka pale temps watakapoajiriwa. But in the meantime watakuwa ni waajiriwa wa Robert Half.
Sijui kwa Tanzania lakini kwa Marekani ukitaka kujua wao watu wa staffing agency wanachukua kiasi gani ni kiasi cha kuomba tu hizo taarifa na utapewa. Robert Half does that.
Maelezo kama ya health insurance na other benefits mara nyingi huwa yapo kwenye employee handbooks na mi nazijua baadhi ya hizo agencies ambazo hutoa hizo benefits.
Kwa Tanzania huenda kabisa hiyo industry haiko regulated vizuri.
Pope Emeritus Benedict or Pope Francis?
Sidhani kama alimaanisha recruitment companies. Ila nafikiri alimaanisha outsourci ng companies. Yaani kampuni moja onachukua tender ya kufanya kazi flani kwenye kampuni nyingine. ile inayotoa tender inamlipa outsouced company hela nyingi na ile outsourced company inawalipa wafanyakazi ujira kidogo ili ibaki na faida.
Recruitment agents ni tofauti maana wao wanalipwa one time payment na mteja wao. Mara zote haiathiri mshahara wa mwajiriwa kwa sababu hakuna monthly payment.
Outsourcing ni trend ya kibiashara ambayo haiwezi kuondoka kwa maneno ya waziri. inaelekea waziri hajui inachokiongea kwa kuwa sera ya serikali ni kuoutsource non core activities. Na kazi kama ulinzi na usafi kwenye taasisi almost zote za serikali zimekuwa outsourced. Je ataanza kuwaajiri wote hao. Ni trend ya dunia nzima.