Government Ban Job Recruitment Agencies!

Government Ban Job Recruitment Agencies!

Umeshaambiwa Erolink wanadaiwa back taxes na serikali takriban 3 billion TZS

serikali muda wote ilikuwepo wapi mpk tax inafika hela yote hiyo??hapo wamefanya uzembe,anyway kwa hiyo sasa watu itabidi wapambane wenyewe kutafuta kazi wasitumie thirrd party
 
wezi tu hao,kama EROLINK ndo ipigwe life bana hadi ofice zao zipigwe kiberiti.

wahindi wanyonyaji sana wale,wamerajirikia mishahara yetu pale voda na tigo.

Good move Kabaka!
 
Kuna watu wanalala nje (walinzi) wanaambulia laki 2 wakati huo huo hayo ma agency wana take more than that yani likiwezekana hili mama hautasahaulika kwenye kizazi hiki
 
Sijui hata kama umejua nilichoandika. Unasoma juu juu tuu. Completely lack of attention to details.

Katafute kwanza maana na tofauti kati ya "recruitment agency" na "recruitment process outsourcing."

Nakusoma vyema sana mkuu... Ila nadhani wewe ndio hujamuelewa vizuri Waziri wa Kazi na Ajira.

An employment agency is an organization which matches employers to employees. In all developed countries there is a publicly funded employment agency and multiple private businesses which also act as employment agencies.

Recruitment Process Outsourcing is a form of business process outsourcing (BPO) where an employer outsources or transfers all or part of its recruitment activities to an external service provider.
The Recruitment Process Outsourcing Association defines RPO as follows: "when a provider acts as a company's internal recruitment function for a portion or all of its jobs. RPO providers manage the entire recruiting/hiring process from job profiling through the onboarding of the new hire, including staff, technology, method and reporting. A properly managed RPO will improve a company's time to hire, increase the quality of the candidate pool, provide verifiable metrics, reduce cost and improve governmental compliance."
 
Hili halitatekelezwa kwa sababu makampuni haya ni ya watu wazito kama vile lowassa, rostam, msekwa, etc
 
yan recruitment agencies ziwepo lakini I think ts better wanapo watafutia ajira watu wakate percentage yao then wawahandle employee kwa employer,they job must be to link and not otherwise
 
kama customer care wa kampuni flani ya simu eti walishushiwa mshahara badala ya kupandishiwa matokeo yake wafanyakazi kibao wakaacha kazi na waliobaki ni majanga ukipiga simu wanakujibu wezerewezere mradi mradi yaaani ni full magumashi
 
kama customer care wa kampuni flani ya simu eti walishushiwa mshahara badala ya kupandishiwa matokeo yake wafanyakazi kibao wakaacha kazi na waliobaki ni majanga ukipiga simu wanakujibu wezerewezere mradi mradi yaaani ni full magumashi
Hahaa voda nini?
 
Naunga mkono uamuzi wa serikali. Ni kwamba kampuni au shirika linapochukua mfanyakaxi kupitia outsourcing company inakwepa liability. Inahamisha liability kwa kikampuni kidogo kisichoogopa kuharibu jina lake hata ikikiuka haki za msingi za mfanyakazi. Pili ni kwamba mshahara halali wa mfanyakazi anagawiwa huyo muonevu ili aonee wafanyakazi kwa niaba ya shirika linalohitaji wafanyakazi.
Tatu shirika mama linakwepa kulipa mishahara mikubwa hivyo inajishikiza nyuma ya kampuni ndogo ili ikwepe gharama halisi za mfanyakazi.

Aisee nimependa ulichoandika.
 
Sidhani kama njia muafaka ilikuwa ni kuzipiga marufuku hizo recruitment agencies, bali kuhakikisha kuwa zina-operate kwa mujibu wa sheria au taratibu zilizowekwa.

Ilichotakiwa kufanya serikali ni kulinda maslahi yake pamoja na haki za wale wanaojiriwa na kufanya kazi kupitia recruitment agencies.

Kama recruitment agencies haitafuata sheria au taratibu zilizowekwa, then kuwe na enforcement actions, following by huge fines. Lazima watatii tuu.

Lazima kuwe na restrictions and responsibilities on recruitment agencies na biashara zao, but siyo kuzipiga marufuku. Funga zile ambazo zimekataa kufuata sheria na taratibu tuu.

Kama hii habari ni kweli na imeripotiwa bila kupindishwa, then this is the worst decision for the government. Pia ni ushahidi kuwa serikali inashindwa ku-regulate the emerging businesses across the country.

Siamini kama recruitment agencies is a bad business for the country kiasi cha kuzipiga marufuku. What is bad is the failure of the government to regulate these agencies.

I think kilichopigwa marufuku siyo recruitment agencies bali ni recruitment process outsourcing. Kwa hiyo, agencies kama Radar Recruitment hawadhuriki na huu uamumzi.

Lakini kuna baadhi ya makampuni yanafanya both as recruitment agencies as well as recruitment process outsourcing. Kwa maana hiyo itabidi hizo kampuni ziachane na recruitment process outsourcing na kubakia kama recruitment agencies. Mfano: Erolink | Developing today's managers into tomorrow's leaders.

Hawa jamaa wamekuwa wanyonyaji kupita maelezo na kwa kiasi kikubwa kikwazo kwa baadhi ya watu kufanya kazi na kulipwa wanavyostahili. Kwenye oil and gas sasa hivi ni balaa.
 
SPANCO wanatakiwa wafukuzwe kabisa nchini ni wanyonyaji wakubwa.
 
[h=3][/h]





[h=3][/h]










[TABLE="class: yiv7300179507tr-caption-container, align: center"]


[TR]

[TD] [/TD]
[/TR]

[TR]

[TD="class: yiv7300179507tr-caption"]
Waziri wa Kazi na Ajira Bi.Gaudentia
Kabaka akitoa tamko la Serikali kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) juu
ya usitishwaji wa utaratibu
wa kukodisha wafanyakazi unaofanywa na baadhi ya mawakala binafsi wa huduma za
ajira wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa idara ya habari(MAELEZO)
leo Jijini Dar es Salaam.

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA



WIZARA YA KAZI NA AJIRA



[TABLE="align: left"]


[TR]

[TD="width: 272"][/TD]
[/TR]

[TR]

[TD][/TD]

[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]







TAMKO LA SERIKALI KUHUSU KUSITISHA UTARATIBU WA KUKODISHA WAFANYAKAZI
UNAOFANYWA NA BAADHI YA WAKALA BINAFSI WA HUDUMA ZA AJIRA



1. Wizara ya Kazi na Ajira imekua ikipokea malalamiko toka kwa wadau
mbalimbali kuhusu utaratibu wa udalali wa kukodisha wafanyakazi katika makampuni
unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira
nchini.





2. Wizara imefanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hili na kubaini kuwa
utaratibu wa kukodisha wafanyakazi unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa
Huduma za Ajira ni kinyume cha Sheria ya Huduma za Ajira Na. 9 ya
Mwaka 1999
[Sura 243 kama ilivyorejewa Mwaka 2002]. Kwa mujibu wa
Kifungu 4 cha Sheria hii, majukumu ya msingi ya Wakala wa Huduma za Ajira
ni kuwaandaa na kuwaunganisha Watafuta Kazi na Waajiri kwa kutoa mafunzo
na ushauri elekezi kwa watafuta kazi, kutafuta fursa za ajira na kutoa taarifa
za soko la ajira. Hivyo, Mawakala hawapaswi kuwa waajiri wa wafanyakazi
waliowatafutia kazi kwa niaba ya Waajiri wengine.





3. Aidha, uchunguzi umebaini kwamba utaratibu huu ni ujanja unaotumiwa
na baadhi ya Waajiri na Mawakala kwa lengo la kukwepa kodi na kujipatia faida
kwa kukwepa kutoa haki za msingi za wafanyakazi kwa mujibu wa Sheria za Kazi.
Baadhi ya makampuni yanayokodisha wafanyakazi yamefanyiwa uhakiki na TRA na
kubainika kukwepa kodi ya mapato ya ajira (PAYE) na na kodi ya mapato ya
kampuni kinyume na Kifungu cha 7 cha Sheria ya Kodi ya Mapato ya Mwaka
2004 [Sura 332 kama ilivyorejewa Mwaka 2008].






4.Uchunguzi huu umebaini athari mbalimbali kwa wafanyakazi
wanaoajiriwa kwa utaratibu huu. Athari hizo ni pamoja
na:


· Wafanyakazi kukosa haki ya hifadhi ya
jamii kama vile likizo ya uzazi na matibabu kinyume na Sheria mbalimbali za
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii;


· Uwepo wa ubaguzi katika malipo ya
mishahara kwa kazi ya aina moja kinyume na kifungu cha 7(10) cha Sheria ya
Ajira na Mahusiano Kazini Na.6 ya mwaka 2004 ambacho kinamtaka mwajiri kuchukua
hatua stahiki kwa kuhakikisha kuwa wafanyakazi bila kujali jinsia zao wanalipwa
mishahara linganifu na ya haki kwa kazi yenye uzito na thamani
sawa;


· Kukosa fursa za kujiendeleza kielimu na
mafunzo;


· Kukosekana kwa usalama na uhakika wa
ajira ;


· Wafanyakazi kulipwa mishahara ya kima
cha chini kinyume na sekta wanayofanyia kazi.





5. Kwa taarifa hii, Wizara ya Kazi na Ajira imeamua kusitisha mara moja
utaratibu wa Mawakala kuwaajiri wafanyakazi wanaowatafutia
kazi.Aidha,Mawakala na Kampuni husika waliopo katika utaratibu
huu kwa sasa wanapaswa kuwahamisha wafanyakazi waliokodishwa kutoka kwa Wakala
kwenda kwa Kampuni husika. Waajiri na Wakala wanatakiwa kukamilisha zoezi hili
ndani ya kipindi cha mwezi mmoja na kuwasilisha taarifa za utekelezaji kwa
Katibu Mkuu, Wizara ya Kazi na Ajira kabla au ifikapo
tarehe 28/02/2014.





6. Uchunguzi zaidi unaendelea kubaini kama kuna wafanyakazi wa Kigeni
wanaohusishwa katika utaratibu wa kukodishwa ili hatua zinazotahili ziweze
kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwataka waombe vibali vya ajira kwa mujibu
wa Sheria ya Uhamiaji Na.7 ya mwaka 1995 na Sheria ya Huduma za Ajira
Na.9 ya mwaka 1999.
Wageni watakao kidhi vigezo wataajiriwa na kampuni
walipokodishwa; ambazo kwa wakati huo zitakua ndiyo mwajiri
wao.





7. Wizara ya Kazi na Ajira inawaelekeza Wakala wa Huduma za Ajira nchini
kwamba, kwa utaratibu wa sasa watapaswa kuwasilisha barua za maombi ya usajili
wa Uwakala kwa KAMISHNA WA KAZI kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za
Ajira
Na. 9 ya mwaka 1999 [Sura 243 kama ilivyorejewa Mwaka 2002] ili
waweze kufanya shughuli za Uwakala wa Huduma za Ajira kisheria. Maombi haya
yawasilishwe ndani ya kipindi cha mwezi mmoja tangu kutolewa kwa tangazo hili.
Baada ya muda huo Wakala asiye na kibali cha Kamishna wa Kazi hatoruhusiwa
kuendesha shuguli za huduma za ajira nchini. Aidha, Mawakala watakaopata leseni
ya Kamishna wa Kaziyatakua yakitangazwa ili yatambuliwe na
Umma.





8. Nasisitiza, maelekezo haya yatatolewa kwa Makampuni na
Wakala waliohusishwa katika uchunguzi kwa ajili ya
utekelezaji.








IMETOLEWA
NA



GAUDENTIA MUGOSI KABAKA
(MB)


WAZIRI WA KAZI NA
AJIRA
27/01/2014
 
Yeye anasitisha ni ajira zipi anazotoa?

hao waliofutwa sio kwamba ndio wanaotoa ajira bali ni mawakala wa ajira, ni sawa na kuondoa madalali katika deal na kubakia muuzaji na mnunuzi kuna shida hapo, ila kwa upande mwingine walirahisisha utafutaji wa ajira kwa watu wasio aggressive na kuhodhi nafasi nyingi, ila tatizo kubwa lililoonekana na kutoa mishahara pungufu kwa mgongo wa uwakala jambo lililopunguza mantiki nzima ya huduma yenyewe, jambo la busara ingekua kuweka sheria ambayo ingewabana hawa mawakala kutojipatia faida kubwa kuliko wafanyakazi wenyewe. Kipindi hiki kingetumika kwa waziri na wadau kukutana na kujadili the best way on how to operate on a win win situation...
 
Sidhani kama njia muafaka ilikuwa ni kuzipiga marufuku hizo recruitment agencies, bali kuhakikisha kuwa zina-operate kwa mujibu wa sheria au taratibu zilizowekwa.

Ilichotakiwa kufanya serikali ni kulinda maslahi yake pamoja na haki za wale wanaojiriwa na kufanya kazi kupitia recruitment agencies.

Kama recruitment agencies haitafuata sheria au taratibu zilizowekwa, then kuwe na enforcement actions, following by huge fines. Lazima watatii tuu.

Lazima kuwe na restrictions and responsibilities on recruitment agencies na biashara zao, but siyo kuzipiga marufuku. Funga zile ambazo zimekataa kufuata sheria na taratibu tuu.

Kama hii habari ni kweli na imeripotiwa bila kupindishwa, then this is the worst decision for the government. Pia ni ushahidi kuwa serikali inashindwa ku-regulate the emerging businesses across the country.

Siamini kama recruitment agencies is a bad business for the country kiasi cha kuzipiga marufuku. What is bad is the failure of the government to regulate these agencies.

I think kilichopigwa marufuku siyo recruitment agencies bali ni recruitment process outsourcing. Kwa hiyo, agencies kama Radar Recruitment hawadhuriki na huu uamumzi.

Lakini kuna baadhi ya makampuni yanafanya both as recruitment agencies as well as recruitment process outsourcing. Kwa maana hiyo itabidi hizo kampuni ziachane na recruitment process outsourcing na kubakia kama recruitment agencies. Mfano: Erolink | Developing today's managers into tomorrow's leaders.

Mkuu naomba nikusahihishe... nielewavyo...kilishizuiwa sio recruitment process outsourcing BALI ni labour brokerage. kuna tofauti hapo.

labour broker ni yule ambae mimi kama kampuni namwambia nahitaji assistant accountants 5, na yeye anawaajiri na kuwaleta kwangu mimi principal. in turn mimi namlipa mshahara wao plus namchaji commission-about 20% of salary..
 
Sasa Waziri ba timu yake waiangalie na hii Tume ya Ajira (Public Service Recruitment Secretariat-PSRS) kwa jicho makini. Kama vipi ajira ziwe zinatolewa na wizara/office husika tu na usaili huko huko...
 
Sidhani kama njia muafaka ilikuwa ni kuzipiga marufuku hizo recruitment agencies, bali kuhakikisha kuwa zina-operate kwa mujibu wa sheria au taratibu zilizowekwa.

Ilichotakiwa kufanya serikali ni kulinda maslahi yake pamoja na haki za wale wanaojiriwa na kufanya kazi kupitia recruitment agencies.

Kama recruitment agencies haitafuata sheria au taratibu zilizowekwa, then kuwe na enforcement actions, following by huge fines. Lazima watatii tuu.

Lazima kuwe na restrictions and responsibilities on recruitment agencies na biashara zao, but siyo kuzipiga marufuku. Funga zile ambazo zimekataa kufuata sheria na taratibu tuu.

Kama hii habari ni kweli na imeripotiwa bila kupindishwa, then this is the worst decision for the government. Pia ni ushahidi kuwa serikali inashindwa ku-regulate the emerging businesses across the country.

Siamini kama recruitment agencies is a bad business for the country kiasi cha kuzipiga marufuku. What is bad is the failure of the government to regulate these agencies.

I think kilichopigwa marufuku siyo recruitment agencies bali ni recruitment process outsourcing. Kwa hiyo, agencies kama Radar Recruitment hawadhuriki na huu uamumzi.

Lakini kuna baadhi ya makampuni yanafanya both as recruitment agencies as well as recruitment process outsourcing. Kwa maana hiyo itabidi hizo kampuni ziachane na recruitment process outsourcing na kubakia kama recruitment agencies. Mfano: Erolink | Developing today's managers into tomorrow's leaders.


Nafikiri uko sawa, wanachofanya sasa hivi ni kufungia wale wahuni na kuweka mikataba mizuri kwa masilahi ya walengwa.
 
Sasa Waziri ba timu yake waiangalie na hii Tume ya Ajira (Public Service Recruitment Secretariat-PSRS) kwa jicho makini. Kama vipi ajira ziwe zinatolewa na wizara/office husika tu na usaili huko huko...

Hawa nao wabaguzi sana
 
Binafsi nadhani hatua ambazo serikali imechukua katika suala hili ni sahihi kabisa. Hizi Recruitment Agencies (baadhi) zimekuwa zikiwanyonya sana wafanyakazi, unakuta mfanyakazi analipwa pesa kidogo sana (aliyeaijiriwa kwa kupitia agency) ukilinganisha na yule aliyeajiriwa na kampuni husika wakati wote wanafanya kazi ya aina moja.
 
Big result now imeleta heri kwa vijana wanonyonywa na makabaila wanaojiita Recruitment Agency.
Erolink, Spanco wanaongoza kwa huu mchezo mchafu. Ni kwanini Vodacom na Airtel wasishitakiwe na Serikali kwa kuelewa Fouls zinazochezwa na ma HR Directors na hizi Recruiting agencies wao wanaoingia mikataba ya kinyonyaji kunyonya waajiriwa wazawa tena Vijana. Kuna upotevu mkubwa wa Kodi, Department ya Fraud pale Voda ipo kuangalia na hizi deal za kinyonyaji au ipo kwa ajili ya neema ya kampuni tuu?

Connect dots ni kwa nini Waziri wa kazi atoe uamuzi huu kipindi hikikaribu na 2015, Au ndio mrejesho wa Nia ya Mh Mwigulu ya kushughulikia Tatizo la ajira duni( Indecent work for nationals)

Mh Waziri wa kazi Jaribu kuangalia upya Jobs occupied by Foreigners na Succession Plan Strategy ya kila Kampuni. Kuna wageni wengi wanaziba nafasi za wazawa hili nadhani liko ndani ya majukumu ya Serikali chini ya wizara ya Kazi. Kuna foreigners wengi wanaishi magodown mikocheni tuanonana nao usiku tuu kwenye ma bar. Bangladesh,India ,Chinese,Nepal etc.
 
Back
Top Bottom