Mundungus Fletcher
JF-Expert Member
- Jun 7, 2009
- 327
- 79
Hili jambo linahitaji umakini sana. Kwanza, ni lazima kufafanua vizuri walengwa hasa ni kina nani. Nimeona hata ofisi nyingi tu za serikali au mashirika ya umma kwa sasa wana outsource baadhi ya kazi (mf: usafi, ulinzi, huduma za ndani, catering, madereva, etc). Sasa kama hoja ni kuwa kwa ku outsource huduma hizo wanaoajiriwa "wanapunjwa", then hata serikali na mashirika ya umma pia yatakumbwa na katazo hili?
Waziri anagusia pia mishahara, lakini anasahau kuwa kama ni kupunja serikali ndiyo inayoongoza - rejea malalamiko ya walimu, madakatari etc. Kwa hiyo pamoja na kuyabana makampuni ya kibinafsi, na serikali pia iangalie waajiriwa wake.
Jingine ni impacts za katazo hilo - kuna watu watapoteza ajira, kuna makampuni sasa itabidi "yafe" maana hayana biashara tena, baadhi ya kazi zinaweza kuwa exported kwenye nchi ambazo zina sharia nafuu (eg. makampuni ya simu yanaweza kuhamishia call centre zake Kenya, India etc), gharama za huduma/bidhaa zinaweza pia kupanda - mishahara na marupurupu mengine ni gharama ambazo mwisho wa siku zinakuwa factored in kwenye bei ya huduma/bidhaa husika. Au mishahara ya wafanyakazi waliopo inaweza kushuka ili kuongeza mishahara ya hao wengine ambao watatoka huko walipokuwa outsource na kuajiriwa moja kwa moja na kampuni husika.
Je makampuni ambayo yalikuwa yanafanya huduma hiyo yatakubaliana kirahisi na katazo hili. Kama ilikuwa biashara halali miaka mitano iliyopita, iweje leo inakuwa haramu (bila hata mabadiliko yoyote ya sheria)?
well said.
ndio hzo sheria zinazo lalamikiwa waziri akiamka anatoa maamuzi ambayo implications zake zinaathiri taifa