mv mapinduzi
New Member
- Apr 19, 2013
- 3
- 0
Bora vilio vya wanyonge vina sikika sasa
Elly B sijaelewa tangazo hili vizuri. Mfano kampuni ya audit firm ikiombwa kupeleka staff wake kufanya kazi kwa mteja say "three months" hii itahitaji kibali cha commissioner? au nikiwakubalia wahitimu wasio na ujuzi kufanya kazi kwangu kwa kujitolea wakati wanatafuta kazi hii nayo itahitaji kibali? Kwa kiasi fulani Waziri amekurupuka kuna makampuni ambayo hayawezi kuajiri watu wa sekta zote mfano migodini ..canteen, dispensary, blusting, na ulinzi lazima wafuate mfumo huu wa kuajiri kampuni itoe wafanyakazi
Mkuu Nyani Ngabu,Kwa kweli huduma zao ni nzuri maana huwa zinawaunganisha watu na sehemu za ajira. Sasa kwa Tanzania karibu kila kitu ni balaa. Hakuna nafuu popote pale.
Kwani hao jamaa wa bongo wao wanatoa huduma gani sasa hivi? Wana temp-to-hire services? Hicho unachopendekeza wewe si kizuri kwa mtazamo wangu kwa sababu kitaibania sana hiyo sekta na itayanyima makampuni fursa ya kumtathmini mtu kwenye utendaji wake wa kazi.
Kwa sababu kuna makampuni mengine huwa yanatumia hao mawakala katika kutafuta prospective employees. Mtu anaajiriwa kwanza na wakala (na mshahara anakuwa analipwa na wakala) halafu wakala kulingana na sifa za mtu ndo anatoa assignment kwamba fulani atapangiwa sehemu fulani na kadhalika.
Huko unakoenda kufanya kazi waweza kukuta baada ya kipindi fulani (tuseme miezi miwili au mitatu) kulingana na utendaji wako wa kazi unaweza kuajiriwa na hivyo kuwa mwajiriwa wa kampuni ambayo ulipelekwa kufanya assignment na hiyo temp agency.
Kwa hiyo ni kama namna fulani ya kuchuja waajiriwa watarajiwa kuliko kuajiri tu mtu moja kwa moja bila kujua hata utendaji wake wa kazi kiuhalisia ukoje.
Mkuu umemuelewa Waziri kwa 100%, huo ndio msingi wa usitishaji huu! Kampuni nyingi za uwakala zinakiuka hicho kipengele; to mention few ni pamoja na Erolink, Infinity Communication, Spanco, NFT Consultant...hawa wote, unaingia nao wao mkataba na kugeuka kuwa waajiri badala ya recruitment agency huku wakipanga benefit ipi na ipi wampe mwajiriwa na ipi wasimpe!
kama nilivyo ainisha kwa alama nyekundu hapo juu, Recruitment agency nyingi zinakiuka utaratibu huu na kufanya wao kuwa waajiri wakati kisheria wao na waunganishi kati ya mwajiri na watafuta kazi.
Mfano ni: Baadhi ya Bank teller wa National Bank of Commerce(NBC) na Vodacom Customer Care ambao wapo chini ya ERONLINK wao si waajiriwa wa NBC wala Vodacom, bali wao wameajiriwa na Eronlink. Hii ndio kitu waziri wa kazi anataka iachwe mara moja na kuifungia kabisa isifanyike tena.
Wafanya kazi waliopo katika mfumo huu wananyimwa haki zao za msingi na kufanya utaratibu huu kuwa ni mbaya na nikinyume na sheria ya Huduma za Ajira.
www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa...pi-utekelezaji-wa-agizo-lenu.html#post9716644
Nmeamua kukumbushia hii!!