Government Ban Job Recruitment Agencies!

Government Ban Job Recruitment Agencies!

Huh? Wewe si kuna wakati ulinipa link ya mtu anayedai anaujua mshahara wa rais? Au nimesahau?

Eti The Boss, kwani mshahara wa rais si unajulikana?


inatakiwa ijulikane sababu inapitishwa na Bunge

lakini through media huwa tunasikia sikia mshahara wa Rais ukitajwa
mfano mwaka 1960 mshahara wa rais ulikuwa sh 5000
mwka 1992 ulikuwa 27,000..
 
Binafsi nimeguswa na tamko la serikali kupitia Wizara ya Kazi na Ajira ya kusitisha utaratibu wa udalali wa kukodisha wafanyakazi katika makampuni unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira nchini.

Nimewahi kuajiriwa katika system za hivyo na ni shahidi ni kiasi gani zinavyowasababishia wafanyakazi kero, hasa inapokuja swala la Kujiendeleza kimasomo na likizo. Pia imekuwa chanzo cha unyonyaji wa jasho la wafnyakazi kwani ili alipwe lazima hela yake ipitea kwa Kampuni iliyompatia kazi na hivyo anagawana nayo, mgawo ambao mara nyingi unampunja mfanyakazi huyo. Hii ni tabia common katika makampuni ya ulinzi kama KK Security na Venture Risk Management.

Naamini kama hili litatekelezwa lisaidia kuboresha maisha ya wengi na kwa niaba ya wote napongeza hatua hiyo.
Elly B sijaelewa tangazo hili vizuri. Mfano kampuni ya audit firm ikiombwa kupeleka staff wake kufanya kazi kwa mteja say "three months" hii itahitaji kibali cha commissioner? au nikiwakubalia wahitimu wasio na ujuzi kufanya kazi kwangu kwa kujitolea wakati wanatafuta kazi hii nayo itahitaji kibali? Kwa kiasi fulani Waziri amekurupuka kuna makampuni ambayo hayawezi kuajiri watu wa sekta zote mfano migodini ..canteen, dispensary, blusting, na ulinzi lazima wafuate mfumo huu wa kuajiri kampuni itoe wafanyakazi
 
Last edited by a moderator:
I have reason to believe that Robert Half being the leader that it has been for over half a century now, is operating far and beyond the "barely legal" standards used by the mushrooming mom and pops shops.

Kuna mama mmoja nusura apewe onyo na HR in one of these big global banks on Wall St, kisa aliwauliza consultants aliowaajiri yeye mwenyewe kwamba agencies zao zinawalipa kiasi gani.Turns out kumbe makubaliano kati ya HR ya bank na agency pamoja na makubaliano kati ya agency na consultants yalikuwa na confidentiality clause iliyokataza hawa consultants kujadili hili swali.

Marekani state laws pia zina complicate mambo, kwa hiyo mambo ya Gotham na kwa Atliens yanaweza kuwa si sawa.

Kwa Marekani hata minimum wages za states zinatofautiana, kuna states kama Alabama na Tennessee ambazo hata hazina state minimum wage. Kuna states zingine zenye minimum wage tofauti na minimum wage ya federal.

Zipo states zenye minimum wage iliyo chini na minimum wage ya federal na zipo ambazo minimum wage zake ni zaidi ya minimum wage ya federal.

Jamaa wana misheria mingi mpaka wao wenyewe hujichanganya.
 
inatakiwa ijulikane sababu inapitishwa na Bunge

lakini through media huwa tunasikia sikia mshahara wa Rais ukitajwa
mfano mwaka 1960 mshahara wa rais ulikuwa sh 5000
mwka 1992 ulikuwa 27,000..

Wewe ushawahi kusikia redioni mshahara wa rais ukitajwa? Kama ushawahi, ulisikia mshahara wa rais yupi?
 
Hawa jamaa wamenitesa sana...Mpaka nikatoswa na Demu wangu Halima,mana najulikana nafanya kazi,napata mshahara lkn hata demu wangu akija gheto hakuti mabadiliko,Room iko vilevile,tena chumba kimoja kapeti ya plastic...hakuna friji ya soda wala maji...nikinunua soda naweka kwa Mangi dukani ili zipate ubaridi,hii ilimuudhi sana Halima my sweet heart
Kamshahara hakatoshi hata kumtoa out...akija nikitoa nauli tu baasi ujue bajeti nzima inayumba.Kweli Erolink mmenitesa sana...nikaonekana ni mwanaume nisiye na mipango,sina malengo wala ujuzi wa kutumia kipato changu,Halima akanikimbia akijua mi si husband material,Asante Mama Gaudensia Mugosi Kabaka ni siku nyingi nilifunga na kuomba hawa Erolink wapate mkono wa sheria.
Nilijituma hadi overtime ili nimkumbuke Mama kule kijijini kwa vitenge na batiki,lkn hata hivyo vijihela vya overtime hivi ”vibepari“ uchwara vya Erolink vilinidhurumu...sikuwa na jinsi zaidi ya kupata hela ya kula na nauli ”from hand to mouth“,mshahara wangu haukuwahi kukutana,nakajiuliza au mimi sina nidhamu ya pesa??...Erolink umenitesa sana,ukanikimbizia Halima wangu,ukanikosanisha na masela kijiweni waliojua nawabania hela za stamp kutuma application kisa mie nina kazi kumbe laa..
Mpaka kesho mafao yangu ya NSSF sijawahi kuyapata sbb hawakuwa wanapeleka,baadae nikagundua kampuni iliyoniajili ilikuwa inanilipa laki nane na sitini,lkn ”wajanja“ Erolink walikuwa wananipa laki mbili na tisini.
Japo nilijinyofoa kwa kuchelewa lkn walininyonya sana na kusababisha kumpoteza Halima wangu,ufanyakazi wangu haukuwa na manufaa...kwangu hata May Mosi haikuwa na umuhimu...
Walinifanya nijikite katika ujasiliamali kuliko kiajiliwa...Nitakukumbuka Halima,kwenye simu yangu nimekusave ”Halima-Erolink“

Pole sana mkuu natumai hata bibie Halima anakusoma sasa.
 
Kosa kubwa hawa recruiting agencies walilofanya ni kufanya kazi ya kuajiri na kumlipa mfanyakazi mshahara badala ya ku'link mfanyakazi na prospect employer na kupata commision through doing that.

On the tax evasion i hope they will be charged in the court of law kwasababu this is a criminal act.

I suggest pia hao wafanyakazi ambao wamekuwa wakinyonywa waende mahakamani ku'demand compensations za mishahara yao na mafao yao waliyokuwa wakipunjwa.

I believe there must be a legal way round confidentiality clause as an excuse.

Tuwape hawa wafanyakazi whistleblower status mahakamani kwasababu wana'expose kitu ambacho ni harmful kwa uchumi wa nchi.
 
I am afraid that this is not solution to the problem and is not the end of your disappointment
Kaka better to try than not......
I personally strong support mama Gaudensia Kabaka...The Minister of labour,youth and employment
 
Sidhani kama njia muafaka ilikuwa ni kuzipiga marufuku hizo recruitment agencies, bali kuhakikisha kuwa zina-operate kwa mujibu wa sheria au taratibu zilizowekwa.

Ilichotakiwa kufanya serikali ni kulinda maslahi yake pamoja na haki za wale wanaojiriwa na kufanya kazi kupitia recruitment agencies.

Kama recruitment agencies haitafuata sheria au taratibu zilizowekwa, then kuwe na enforcement actions, following by huge fines. Lazima watatii tuu.

Lazima kuwe na restrictions and responsibilities on recruitment agencies na biashara zao, but siyo kuzipiga marufuku. Funga zile ambazo zimekataa kufuata sheria na taratibu tuu.

Kama hii habari ni kweli na imeripotiwa bila kupindishwa, then this is the worst decision for the government. Pia ni ushahidi kuwa serikali inashindwa ku-regulate the emerging businesses across the country.

Siamini kama recruitment agencies is a bad business for the country kiasi cha kuzipiga marufuku. What is bad is the failure of the government to regulate these agencies.

I think kilichopigwa marufuku siyo recruitment agencies bali ni recruitment process outsourcing. Kwa hiyo, agencies kama Radar Recruitment hawadhuriki na huu uamumzi.

Lakini kuna baadhi ya makampuni yanafanya both as recruitment agencies as well as recruitment process outsourcing. Kwa maana hiyo itabidi hizo kampuni ziachane na recruitment process outsourcing na kubakia kama recruitment agencies. Mfano: Erolink | Developing today's managers into tomorrow's leaders.

ila pia nilichonukuu kwa waziri wakati akiongea na clouds kwenye kipindi cha jahazi, amezipa muda kubadili mfumo wao wa kazi kwa kuhakikisha mfanyakazi yeyote anayepitia kwao anaajiriwa rasmi na kampuni husika kwa kupewa mkataba halali wa ajira wenye mafao ya uzazi, bima ya afya, kulipa kodi, mifuko ya jamii na mambo yote yanayohusika na kazi na wao kutohusika tena na mfanyakazi huyo mara baada ya kupewa mkataba rasmi wa ajira na wao watanufaika kwa commission watakazokuwa wanapewa na makampuni ya kazi.......................wamepewa muda wa siku 30 kukamilisha usajili rasmi wa makampuni yao...na kukabidhi wafanyakazi wote walio chini yao kwa makampuni husika..
 
ila pia nilichonukuu kwa waziri wakati akiongea na clouds kwenye kipindi cha jahazi, amezipa muda kubadili mfumo wao wa kazi kwa kuhakikisha mfanyakazi yeyote anayepitia kwao anaajiriwa rasmi na kampuni husika kwa kupewa mkataba halali wa ajira wenye mafao ya uzazi, bima ya afya, kulipa kodi, mifuko ya jamii na mambo yote yanayohusika na kazi na wao kutohusika tena na mfanyakazi huyo mara baada ya kupewa mkataba rasmi wa ajira na wao watanufaika kwa commission watakazokuwa wanapewa na makampuni ya kazi.......................wamepewa muda wa siku 30 kukamilisha usajili rasmi wa makampuni yao...na kukabidhi wafanyakazi wote walio chini yao kwa makampuni husika..

Hapa naona a clash of civilizations.

Wakati dunia iliyopita ilikuwa na msisitizo zaidi kwa hayo yaliyotajwa, dunia ijayo haina msisitizo huo.

Moja ya sababu hizi staffing agencies zimeshamiri sana, hasa Marekani, ni kwa sababu waajiri hawataki ku deal na headaches za mafao, insurance, severance pay, social security payments etc. Wao wanataka wapewe figure tu ya kuilipa agency, halafu agency inachukua mzigo wa ku deal na hayo yote, mfanyakazi anakuwa anafanya kazi kwa muajiri x lakini kaajiriwa na agency Y. Muajiri X anakuwa ni client wa agency Y. Mfanyakazi akipata matatizo anahitaji health insurance, muajiri X hahusiki, kwani mfanyakazi huyu si mfanyakazi wake, ni wa agency Y. Mfanyakazi anataka 401 k iwe matched (kama makato ya NSSF/ PPF) muajiri x hahusiki, hii ni kazi ya agency Y. Vivyo hivyo mfanyakazi akifariki, muajiri x hahusiki kwenye ma life insurance huko. Mfanyakazi akivunjika mguu kazini, muajiri x hahusiki, ni kazi ya agency Y.

Hii ndiyo sababu ya kuwa na agencies sehemu kama Marekani. It is simply an exercise in cost reduction in a system that looks at labor as a commodity.

Hii ndiyo sababu nzima ya kufanya agencies hizi zishamiri, hasa Marekani.

Marekani ni nchi inayothamini soko huria, mwenye nguvu mpishe, matajiri wanaamua sheria zinakuwaje. Kwa hiyo ukitaka kugusa hii habari na kuisema vibaya, watakuambia unaingilia soko huria, waache watu wafanye biashara huru. Wafanyakazi wana uhuru wa kudai malipo wanayoyaona yanawafaa (ingawa ukosekanaji wa kazi na kufifia kwa vyama vya wafanyakazi kunawafanya wafanyakazi wasiwe na sauti).

Sasa sie Tanzania tumeiga kwa mkumbo, tunapelekwa ki Marekani Marekani katika nchi ambayo imepiga vita ukupe kwa miaka mingi, mara tu tunastuka kwamba huu mfumo hautufai.

Hatujui kama bado ni wajamaa tukatae ukupe, au ni mabepari tukubali uchumi uendeshwe na soko huria.

Na hata kuchanganya viwili hivi tupate a viable mixed economy ni tabu!
 
Izi agency zinatunyonyaaaa saaana.kuna mshikaj wangu yupo tigo customer service anapata lak 5.kutoka campum moja ipo mikochen Nft.wakat mwajir analipa milion na kitu.yaana anagawana pasu kwa pasu.maternity mtu akienda halipwi.likizo shidaaa.health insuaranca mtu mmoja tu.imagn kama una mtoto.nimefurahishwa saaana na waziri.NFT mtaaibika sasa
 
  • 28 January 2014


TAMKO LA SERIKALI KUHUSU KUSITISHA UTARATIBU WA KUKODISHA WAFANYAKAZI UNAOFANYWA NA BAADHI YA WAKALA BINAFSI WA HUDUMA ZA AJIRA

1. Wizara ya Kazi na Ajira imekua ikipokea malalamiko toka kwa wadau mbalimbali kuhusu utaratibu wa udalali wa kukodisha wafanyakazi katika makampuni unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira nchini.


2. Wizara imefanya uchunguzi wa kina kuhusu suala hili na kubaini kuwa utaratibu wa kukodisha wafanyakazi unaofanywa na baadhi ya Wakala Binafsi wa Huduma za Ajira ni kinyume cha Sheria ya Huduma za Ajira Na. 9 ya Mwaka 1999 [Sura 243 kama ilivyorejewa Mwaka 2002]. Kwa mujibu wa Kifungu 4 cha Sheria hii, majukumu ya msingi ya Wakala wa Huduma za Ajira ni kuwaandaa na kuwaunganisha Watafuta Kazi na Waajiri kwa kutoa mafunzo na ushauri elekezi kwa watafuta kazi, kutafuta fursa za ajira na kutoa taarifa za soko la ajira. Hivyo, Mawakala hawapaswi kuwa waajiri wa wafanyakazi waliowatafutia kazi kwa niaba ya Waajiri wengine.


3. Aidha, uchunguzi umebaini kwamba utaratibu huu ni ujanja unaotumiwa na baadhi ya Waajiri na Mawakala kwa lengo la kukwepa kodi na kujipatia faida kwa kukwepa kutoa haki za msingi za wafanyakazi kwa mujibu wa Sheria za Kazi. Baadhi ya makampuni yanayokodisha wafanyakazi yamefanyiwa uhakiki na TRA na kubainika kukwepa kodi ya mapato ya ajira (PAYE) na na kodi ya mapato ya kampuni kinyume na Kifungu cha 7 cha Sheria ya Kodi ya Mapato ya Mwaka 2004 [Sura 332 kama ilivyorejewa Mwaka 2008].


4.Uchunguzi huu umebaini athari mbalimbali kwa wafanyakazi wanaoajiriwa kwa utaratibu huu. Athari hizo ni pamoja na:


-Wafanyakazi kukosa haki ya hifadhi ya jamii kama vile likizo ya uzazi na matibabu kinyume na Sheria mbalimbali za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii;


-Uwepo wa ubaguzi katika malipo ya mishahara kwa kazi ya aina moja kinyume na kifungu cha 7(10) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini Na.6 ya mwaka 2004 ambacho kinamtaka mwajiri kuchukua hatua stahiki kwa kuhakikisha kuwa wafanyakazi bila kujali jinsia zao wanalipwa mishahara linganifu na ya haki kwa kazi yenye uzito na thamani sawa;


-Kukosa fursa za kujiendeleza kielimu na mafunzo;


-Kukosekana kwa usalama na uhakika wa ajira ;


-Wafanyakazi kulipwa mishahara ya kima cha chini kinyume na sekta wanayofanyia kazi.


5. Kwa taarifa hii, Wizara ya Kazi na Ajira imeamua kusitisha mara moja utaratibu wa Mawakala kuwaajiri wafanyakazi wanaowatafutia kazi. Aidha, Mawakala na Kampuni husika waliopo katika utaratibu huu kwa sasa wanapaswa kuwahamisha wafanyakazi waliokodishwa kutoka kwa Wakala kwenda kwa Kampuni husika. Waajiri na Wakala wanatakiwa kukamilisha zoezi hili ndani ya kipindi cha mwezi mmoja na kuwasilisha taarifa za utekelezaji kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Kazi na Ajira kabla au ifikapo tarehe 28/02/2014.


6. Uchunguzi zaidi unaendelea kubaini kama kuna wafanyakazi wa Kigeni wanaohusishwa katika utaratibu wa kukodishwa ili hatua zinazotahili ziweze kuchukuliwa ikiwa ni pamoja na kuwataka waombe vibali vya ajira kwa mujibu wa Sheria ya Uhamiaji Na.7 ya mwaka 1995 na Sheria ya Huduma za Ajira Na.9 ya mwaka 1999. Wageni watakao kidhi vigezo wataajiriwa na kampuni walipokodishwa; ambazo kwa wakati huo zitakua ndiyo mwajiri wao.


7. Wizara ya Kazi na Ajira inawaelekeza Wakala wa Huduma za Ajira nchini kwamba, kwa utaratibu wa sasa watapaswa kuwasilisha barua za maombi ya usajili wa Uwakala kwa KAMISHNA WA KAZI kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Ajira Na. 9 ya mwaka 1999 [Sura 243 kama ilivyorejewa Mwaka 2002] ili waweze kufanya shughuli za Uwakala wa Huduma za Ajira kisheria. Maombi haya yawasilishwe ndani ya kipindi cha mwezi mmoja tangu kutolewa kwa tangazo hili. Baada ya muda huo Wakala asiye na kibali cha Kamishna wa Kazi hatoruhusiwa kuendesha shuguli za huduma za ajira nchini. Aidha, Mawakala watakaopata leseni ya Kamishna wa Kazi yatakua yakitangazwa ili yatambuliwe na Umma.


8. Nasisitiza, maelekezo haya yatatolewa kwa Makampuni na Wakala waliohusishwa katika uchunguzi kwa ajili ya utekelezaji.


IMETOLEWA NA

GAUDENTIA MUGOSI KABAKA (MB)
WAZIRI WA KAZI NA AJIRA
27/01/2014


 
Nampongeza waziri na serikali kwa kuliona suala hili kama kero ktk jamii,ni hivi karibuni nilimsikia kiongozi mmoja kutoka chama shindani wakiichukua hii hoja kama hoja ktk kampeni zao za uchaguzi.
Naomba nimpe angalizo Mhe.waziri,ameingia ktk vita na mafisadi walioshamiri ktk taifa letu,najua wataleta vitisho na mizengwe lakini tunakuhakikishia Mhe. waziri tupo pamoja na wewe ktk kutenda haki.
Na mwisho natoa ushauri,hawa waajiri waliokiuka utaratibu wa ajira kulingana na sheria wawalipe haki stahili waajiriwa waliowadhulumu stahiki zao,kumbukumbu zote zipo kinachotakiwa wawalipe haki zao zote za nyuma tangu walipowajiri ikiwemo michango yako ya mifuko ya jamii !
Hongera waziri.
 
well noted mkuu EMT

Sidhani kama njia muafaka ilikuwa ni kuzipiga marufuku hizo recruitment agencies, bali kuhakikisha kuwa zina-operate kwa mujibu wa sheria au taratibu zilizowekwa.

Ilichotakiwa kufanya serikali ni kulinda maslahi yake pamoja na haki za wale wanaojiriwa na kufanya kazi kupitia recruitment agencies.

Kama recruitment agencies haitafuata sheria au taratibu zilizowekwa, then kuwe na enforcement actions, following by huge fines. Lazima watatii tuu.

Lazima kuwe na restrictions and responsibilities on recruitment agencies na biashara zao, but siyo kuzipiga marufuku. Funga zile ambazo zimekataa kufuata sheria na taratibu tuu.

Kama hii habari ni kweli na imeripotiwa bila kupindishwa, then this is the worst decision for the government. Pia ni ushahidi kuwa serikali inashindwa ku-regulate the emerging businesses across the country.

Siamini kama recruitment agencies is a bad business for the country kiasi cha kuzipiga marufuku. What is bad is the failure of the government to regulate these agencies.

I think kilichopigwa marufuku siyo recruitment agencies bali ni recruitment process outsourcing. Kwa hiyo, agencies kama Radar Recruitment hawadhuriki na huu uamumzi.

Lakini kuna baadhi ya makampuni yanafanya both as recruitment agencies as well as recruitment process outsourcing. Kwa maana hiyo itabidi hizo kampuni ziachane na recruitment process outsourcing na kubakia kama recruitment agencies. Mfano: Erolink | Developing today's managers into tomorrow's leaders.
 
kaka hv umesoma vizuri hiyo report.. acha kukurupuka tu.. isome vizuri... nyie ndiyo mna mislead raia.
 
Katika mambo machache niliyokubaliana na Papa mwenzangu Benedict XVI mojawapo lilikuwa hili la kupinga ajira zisizo za kudumu.

Watu wanashindwa kufanya mambo ya kudumu kwa sababu ajira zao zinaelea elea hewani.

Halafu, hii nchi inabidi tuelezane ukweli kwamba ujamaa ushazikwa.

I can almost hear mchonga on his Mbeya May day speech lamenting about the perils of the commoditization of labor.

We ni Papa wa wasio amini Mungu yupo?
 
Wanajamvi hivi majuzi Waziri wa kazi na ajira alitangaza kufungia mawakala wa ajira hapa nchini. Swali langu kwa waziri husika je hizi ni siasa kwa sababu uchaguzi unakaribia au ni juhudi za kuwasaidia vijana wanaonyanyaswa na hawa makabaila na wanyonyaji wa vijana wetu.

Kwa bahati nzuri baadhi yetu ni wahanga. Waziri, kama kweli hizi sio siasa futa kabisa haya makampuni maana yanaunyanyasaji na unyonyaji wa hali ya juu.

Kwanza wafanyakazi walioko huko hawana security. Wapo baadhi yao mpaka wanasema eti "We hire and fire". Waweza fukuzwa kazi hata na team leader. Ngono kwa ajili ya kupewa nafasi ni mambo ya kawaida. Namshauri waziri afuatilie hasa kampuni kama Erolink na wafanyakazi wao pale call centre vodacom. Wafanyakazi hapa tunanyanyaswa sana na hatuna hata pakusemea. Tulijaribu kutaka kuanzisha chama cha wafanyakazi lakini Erolink wamejitahidi kuzuia kwa nguvu zote. Hila wanayotumia ni kukupangia ratiba ngumu mfano, kuna wafanyakazi wa TPHD wanaingia saa 2asb hadi 12 jioni kisha baada ya hapo eti ndo watoke mlimani city kwenda Masaki kuonana na viongozi wa chama cha wafanyakazi.

Swali la pili kwa waziri,kama haya makampuni hayalipi kodi serikalini yanawezaje kumjali mfanyakazi wa kawaida?

Mheshimiwa waziri njoo vodacom mlimani city uongee na wafanyakazi wa Erolink call centre ndio utajua nini tunachokisema. Baadhi yetu tunafanyishwa kazi masaa 10 bila overtime.Hatupewi muda wa kupumzika(kazi siku 6 bila off). Nssf zetu hazipelekwi kwa wakati na mikataba mibovu. Tuna mifano ya wenzetu waliolazimika kutoa rushwa ya ngono ili wasipokee simu wapelekwe idara nyingine.

Mheshimiwa waziri. Erolink ni mfano
mmoja tu wa kinachoendelea kwa haya makampuni. Kama kweli umedhamiria kutusaidia sisi vijana na sio siasa tunasubiri kuona wataalam wako wa wizara wakichukua hatua stahiki. Huu udalali wa ajira ufike kikomo.
 
Waache siasa hawa mawakala wafungiwe mara moja wananyonya watu badala ya watu kufaidika
 
Back
Top Bottom