Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Imenishitua sana lakini ndiyo matumizi ya pesa wacha turudi tena ulingoni
 
Yani ni mambo ya ajabu sana hv wanadhani wanaweza kulichukua tena hilo jimbo, mbn mfano hai ni arumeru, mbaya zaidi lema anaweza tena kugombea, mh ccm wataadhiriki sana. hawawezi hata kufikiria, inaonekana wameishiwa mawazo sasa, maybe nao wamechanganyikiwa ndo mana wanajifanyia mambo hovyo2
 
Nchi hii kwa rushwa mbona imeota mizizi,wewe unashangaa nini au hujawahi kwenda mahakamani? Basi utakua mgeni na mambo haya.
 

Heshima kwako Mkuu Makene.

We hope Arusha ni ngome ya CDM no matter what lakini lazima tukio hili la kuvuliwa ubunge kwa Lema tulipe uzito stahiki. Kuna vita iko mbele ya kurejesha jimbo hili, tusiipuuze kama tulivyojipanga na kushinda Arumeru lazima tuweke juhudi zaidi kushinda Arusha Mjini.

Katika hili lazima ieleweke kwamba, CCM wamekuwa kwa muda wote wakilitamani jimbo la Arusha mjini na kutawala halmashauri hiyo ndiyo maana walikuwa radhi kupindisha sheria ili meya wao ashinde na walitumia kila aina ya umafia imekuwa.

Haitashangaza kama watafanya umafia na ujambazi dhidi ya Demokrasia kulichukua jimbo hili. We really need to be serious na kuweka mkakati wa makusudi dhidi ya mbinu chafu za CCM. Wako tayari kufanya lolote kupata wanachokihitaji. Mfano; ni tukio la kuwakatakata mapanga wabunge wa CDM kule Mwanza.
 
wasipokaa sawa, Libya nyingine itaanzia Arusha. Kama makamba kampigia mtu asubuhi kumtaka ajiandae kwa kura za maoni, basi ni dhahiri kwamba CCM wanalitaka lile jimbo. Tofauti na ilivyokuwa Arumeru CCM watapeleka nguvu kubwa sana kutafuta ushindi kutoka Arusha mjini, na yumkini watalazimisha ushindi. Hili litapelekea mapinduzi ya serikali nchini. Mimi siyo Shehe Yahya, lakini nawaambieni maamuzi haya ndiyo yatakayofanya mageuzi makubwa ya kisiasa hapa Tanzania. Kama hamuamini ninyi subirini, mtakuja itafuta hii post.
 
Naona umechukuwa mikoba ya Sheikh Yahya...
 
This is ridiculous judgement baada ya ile ya case ya Mtikila 2,
mahakama imejiingiza kwenye siasa.
Sasa tunapiga kura za hasira njema.

Uzuri ni kwamba wananchi tumejua nini chakufanya!!
Haitasumbua CCM kuigaragaza kwa mara nyingine!
 
Saafi sana. IMEKULA KWA MAGWANDA.

Kama imekula kwa Magwanda,tutajua siku ya kura.Yetu macho.Hata CCM wawahamishie viongozi wote wa serikali hapa A town, pamoja na wastaafu wote wa Chama na serikali! CCM hawana chao Arusha, watupishe na Arusha yetu.Sasa kura walizopata CHADEMA 2010, safari hii itakuwa mara mbili.Nashangaa CCM wameshaanza kujigamba kuapa eti watashinda Arusha mjini!!! Hapa sio Igunga bwana.Hapa sio pa kudanganya watu na unga, wala pesa bwana. Hapa ni Arusha kwa wajanja.CCM wakatafute tena yatima wa Kigogo wamwombee kura hapa.CCM,CCM,CCM nawaambia tena hamna chenu Arusha,hili jimbo tunaomba mlisahau kabisa,wala msijisumbue.
 

Hakuna ngoma droo kwa sababu jimbo liko wazi.
Kwa taarifa za jikoni ni kwamba CDM haikati rufaa na Lema anasimama upya tunamtia aibu shetani.
Wao wana pesa, sisi tuna Mungu.
 
Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema kupitia CHADEMA, amepoteza kiti hicho kwa kuenguliwa na Mahakama katika kesi iliyokuwa inamkabili ya kupinga ubunge wake.Kesi hiyo iliyofunguliwa na makada watatu wa CCM, Mussa Mkanga (55), Happy Kivuyo (49) na Agnes Mollel (44) ambao walikuwa wanamtuhumu Mbunge huyo kwa kutoa kauli za udhalilishaji, matusi na kashifa kwa aliyekuwa mgombea wa Ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Dkt. Batilda Buriani.

Hukumu hiyo iliyosomwa na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila.

Katika hukumu hiyo, Lema hakuondolewa haki ya kugombea ubunge huo kwa kuwa kosa lililomtia hatiani ni matumizi mabaya ya lugha tofauti na ilivyodhaniwa kuwa ni vitendo vya rushwa. Uamuzi wa kugombea ama kutokugombea kiti hicho tena utatokana na maamuzi yake mwenyewe na ridhaa ya chama chake ikiwa kitamteua na kumpitisha kugombea.

Taarifa za watu wa karibu zinasema kuwa Lema hatakata rufaa mahakamani juu ya hukumu ya kesi hiyo, bali atakata rufaa kupitia kura ya wananchi wa Arusha Mjini wakati wa kugombea kiti hicho.

Hivyo tutarajie uchaguzi mpya ndani ya siku 90. Tanzania, nchi ya uchaguzi kila uchao...!
 

Wala siyo DROOOO! Nassari alipata hukumu ya wananchi, na Lema alipata hukumu ya vyombo vya serikali ya CCM. Upande upi unatoa haki zaidi.
 
Nipo hapa viwanja vya mahakama kuu kanda ya Arusha, Kilaza LEMA kapigwa chini. Semeni sasa nyie magwanda. Chezea CCM nyie!!!!! Niliwaambia jana mkaleta mboyoyo zenu
We kunguni hapa ukatambike CCM Arusha haishindi ng'o!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…