Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Mimi sipati hofu na ukumu iliyotolewa kwani tendo hili litasaidia CHADEMA kuimarika zaidi sio Arusha tu bali kwa Tanzania nzima, kwani wakati wa kampeni za Uchaguzi ulioisha Arumeru umetufungua akili wengi na kujua mengi ambayo hata sikio halikutegemea kuyasikia. Uchaguzi wa Arusha utakuwa na umuhimu wa pekee hasa kwasababu ya umaarufu wa Lema.

Nchi nzima na hata nchi za nje zitafuatilia kwa karibu sana uchaguzi huu, na huko ndio kuimarika na kufahamika zaidi kwa CHADEMA. Najua na ninaamini CHADEMA itashinda, kwani jinsi tulivyoweza kulinda kura zetu Arumeru, tutashinda kihalali kabisa. Mungu ibarika Tanzania Mungu ibariki CHADEMA.
 
Natafakari juu ya mstakabali wa tanzania juu ya watanzania walio maskini unanipa tabu kupata jawabu!ivi kama lema alishinda na akaapishwa leo anakuwa si mbunge tena kwa maamuzi ya mtu au kikundi cha watu kwa maslahi yao!

Hebu tafakari uchaguzi unarudiwa tena kwa gharama kubwa, upotevu wa mda kwa viongozi na watendaji wa serikali ambao hakika unarudisha maendeleo nyuma hauwezi fidiwa wala ghala kurudishwa, hii ni shahiri dhahiri wana ccm wamekata tamaa ya kurudi tena madarakani hivyo wanataka serikali ijayo ianze upya!

Kinacho niuma mm ni gharama kubwa za uchaguzi ambazo ni kodi za walalahoi!mahospitalini dawa hakuna,watumishi wengi waidai serikali,mishahara kidogo ukilinganisha na ghalama za maisha.inakera sana.
 
Ni kweli wanaweza wasiapeal wasubiri kuingia kwenye uchaguzi lakini inadepend na hukumu maana kuna kulipwa fidia kubwa kwa walalamikaji mfano yawezaamriwa alipe milioni mia nane na hivyo ikawa ngumu sana kulipa hiyo fidia, na hivyo kama atasimamisha Lema wanaweza weka Pingamizi na Magamba wakapita bila kupingwa, magamba wana hila nyingi sana, ila nguvu ya umma ni sauti ya Mungu. Kama kuna mwenye nakala ya hukumu iwekeni jamvini!
 
Ninashangaa sana kuna watu walikua wameshakata roho baada ya matokeo ya uchaguzi kule Arumeru Mashariki kina Rejao na wenzake leo wamefufuka halafu eti wanachekelea, chakushangaza wanachekelea nini na wakati jimbo liko wazi na uchaguzi unarudiwa na mgombea aliyevuliwa Ubunge anaruhusiwa kugombea?? Jipe moyo Rejao na wenzako bado namsubiri FaizaFox nahisi naye atafufuka muda si mrefu.
 
Hakuna jipya, yaliyotokea yaliyashasemwa kuanzia jana, yalitarajiwa na sasa yamekuwa. Mafisadi at work!!!!

Tiba
 
This is very positive.
Hakuna haja ya kutafuta mchawi.
hakuna haja ya maandamano.
hakuna haja ya kufanya fujo.
Kama wana Arusha walimachagua Lema kwa ridhaa yao, basi wana nafasi ya kufanya hivyo tena, na kuonyesha kwamba hawakufanya makosa.
 
Chadema msijazane ujinga bana ,bwana Lema ameona asikate rufaaa kwasababu anauhakika ashapoteza hivyo na kweli alifanya upuuzi kutoa lugha chafu, ,mbunge gani anafujo namna hiyo na kuutukana mkono uliomlisha toka akiwa mdogo, sasa kakua anajikuta na yeye anamabavu ya kuleta fujo na matusi sasa imemcost...

matusi gani tena.
Ni makubwa kushinda yale ya kubwa jinga mwenzio Lusinde?
 
Jamani mmeshaambiwa kamanda anaruhusiwa kugombea tena. Magamba watapata shida.
 


Hapo ndipo ushangae zaidi anaruhusiwa kugombea sasa walikuwa wanataka nini kumdhibiti kwa style gani kumbu CHADEMA tunaweza mweka mgombea mwingine ambaye akawa ndio fundisho kubwa zaidi kwa CCM twamweka Dr. Slaaaa tune je watafurukuta tena au? Maaana hukumu hivyo tayari ilisha ona mbali sana na ndiko huko wanataka na mawazo yao wanataka CDM imweketena kwenye ubunge ili wamwondoe mapema ila janja yao twisha ijua kabisa

kesi ambayo kidogo ina mvuto ni ile kesi ya Ukonga ya Mahanga maana hata mashahidi wanasema ukweli kuliko kesi ya Lema na Tundu Lisu.

Twataka kujua Jaji alitoa hukumu kwa vigezo vipi?? Isije ikawa kuwa Sheria zetu za nchi bado ziki mlinda zaidi Mwanamke kuliko mwanaume!!!!


Lema atagombea tena na Atashinda kwa kishindo....
Ametangaza Nasari Mbunge
 
Aiceee hii page inakwenda balaa!, dha!

Hii serikali imelaniwa kabisa, hiyo grarama ya kurudia uchaguzi tutapoteza shs ngapi??? aaaarrrrrrrrrrrr
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom