Kwetu uchagani miaka ya nyuma sana kabla ya wamisionari kuingia na kutangaza dini na kuileta biblia, wale wazee wa kichaga walikuwa wanaamini kuna nguvu iko mahali anaitwa Ruwa.
Walikuwa wanaamini Hii nguvu ukiiomba chochote inakupa kama kunyesha nchi mvua, kuepusha magonjwa na balaa.
Na wachaga kipindi hicho walikuwa na utaratibu wa kukutana chini ya mti mkubwa kuchinja mbuzi na kumwaga pombe ya mbege na kumuomba Ruwa awasaidie katika mambo mbalimbali
Wamisionari walivyokuja wakatangaza na kushawishi huyo Ruwa mnayemuomba ni Mungu, wakafundishwa neno la Mungu na maandiko ya biblia.
Mpaka sasa hivi Mungu anaitwa Ruwa lakini Ruwa original alikuwa Mungu wa wachaga nguvu isiyoonekana inayotenda makuu.