Mkuu thanks kwanza kwa ilimu uliotoa.....pili kuna thread it was hot namshauri william asome kwanza.....William,
Nimesema soma hicho kitabu. Pia kuna kitabu kingine ameandika Godfrey Mwakikagile, "Nyerere and Africa: End of an Era". Kuna hoja za kujadilia humo kuhusu vita ya Nigeria. Huwezi kufikia hitimisho kwamba sera zetu wakati wa Mwalimu zilikuwa wrong bila kuwa na full knowledge of what you are talking about. That is what makes us great thinkers here. And yet still, hapa hapa JF kwenye archives zake kuna mjadala mrefu kuhusu vita vya Nigeria na kwa nini Tanzania iliunga mkono Biafra. Sasa unaanzisha thread ambayo umeshafikia hitimisho kwamba Tanzania tulifanya makosa kuiunga mkono Biafra bila kuwa na data sahihi na relevant. No research no speak.
- Kila ninapoangalia tulikotokea hili Taifa, ninapatwa wasi wasi sana kwamba hatukufika hapa tulipo kwa makosa, tumefanya makosa mengi sana nyuma in terms of policies mpaka leo hii kurekebisha inakuwa ni almost impossible, ingawa watawala wa sasa wanajitahidi sana.
- Eti ni kwa nini Tanzania tuliunga mkono Waasi wa Nigeria waliokuwa wanaongozwa na General Ojukwu, kwenye kiu yao ya kujitenga na Nigeria Federation? Ninakumbuka tukiwa wadogo Shuleni, tulivyokuwa tunaimbishwa nyimbo za kumsifu Ojukwu, why? I mean ni policies ngapi huko nyuma we were wrong maana inaonekana ni nyingi sana that ni vigumu sana sasa kurekebisha njia!
- JE have we ever apologize to the Nigerians kwa makosa yetu ya kuuunga mkono uasi wa Ojukwu, dhidi ya serikali halali ya nchi hiyo?
- MUNGU AIBARIKI TANZANIA!
William J. Malecela.
Tanzania ilivotuma jeshi kwenda kuikomboa Seychelles, na mpaka Seychelles iko jinsi ilivyo kwa sababu yale mapinduzi yalizimwa na jeshi letu, pia ni wrong policy?
Hapa ndio CCM wanapopotezana na wananchi. Wanatafuta point kwa lolote baya linalotokea sasa hivi kuwa ni kosa la history, kama vile sasa hivi nchi inatawaliwa na watoto. Huyo Mwalimu unayetaka kumlaumu kwa kila kitu, majority ya wananchi wa kawaida hawatakuelewa, hata wale waliozaliwa baada ya yeye kutoka madarakani. Hio inaleta picha kwa wananchi kuwa hata solutions za matatizo yanatokea sasa hivi hamna, mwenye nazo hizo solutions ni Mwalimu, ambaye hayupo tena.
Nenda leo Zanzibar kawaambie kuwa haya matatizo ya Uamsho yanatokana na Tanzania kui support Biafra 1967! Wrong policies hata kama zilikuwepo, ndio zinatakiwa kui shape nchi na kuwa na mwelekeo mzuri kwa kurekebishwa na watawala wanaofuata, sio kukaa na kusema kila saa tuna matatizo sasa hivi kwa sababu ya zamani. Mfufueni basi Mwalimu aje kuwarekebishia, then mumwache apumzke kwa amani.
Only in Tanzania.
W.J.Malecela pole kwa weledi duni kiasi cha kushusha mapigo ya moyo wangu.Katika thread zako ikiwemo hii yafuatayo nina baini kama hivi.Elimu yako hasa ya sera na uchambuzi ni ndogo sana,Mambo mengine ni muhimu kupata feedback kwa mzee cygwesima na kupata conclusion na kama unataka support toka kwenye jopo la great thinkers unakuja na mtazamo dhahiri badala ya kuyumba yumba.Pia ni kwamba pengine ili jina la Malecela unalitumia vibaya pengine ni mtoto wa shamba boy kiasi kwamba una direct contact za kuongea na kupata ufafanuzi kwa mzee huyo ambaye alibobea katika tasnia ya international relation wakati wa mwalimu.Na pia nashangaa kuabudu utawala wa sasa kwamba unafanya vizuri kuliko enzi ya mwalimu kwa lipi ?au umetumwa na mzee cygwesima kumchokonoa mwalimu kwa sababu hajawahi kujadiliwa kama presidintial candidate baada ya mwalimu ampige ban?.Na mwalimu wakati wa uhai wake alieleza wazi kuwa wakati wa uongozi wake kulikuwa na matatizo mengi na sehemu nyingine walifanya vizuri na pengine walifanya vibaya,Tatizo la uongozi wa sasa ambao Wiliam anapigaya debe wanachukua mabaya wanaacha mazuri.
Ningetaka kusikia toka kwa William ni kwa vipi policies za huko nyuma zinatutesa sasa, na ugumu wa kuzibadilisha unakuwa wapi?
Nasikitika sana pale ambapo JF inageuzwa kuwa kijiwe cha ubishi usio na tija.Tena hasa pale premium member anapokuwa ndiye sababu ya tabia hii.JF hasa jukwaa la siasa ni mahali pa hoja na kuelimishana yale tusiyoyajua kuhusu nchi yetu.Mtu unaweka mjadala mpana kama huu huku ukiwa reluctant kupokea lolote na kubishia kila kitu bila kujustify kwa hoja,unashangaza.Umeulizwa swali,umejibiwa.Umepewa mpaka vitabu usome, hutaki kwa hoja dhaifu kwamba haviko objective!Umeletewa government statement concerning the same issu unaigore na kuendeleza porojo zilezile za "tumefanya madudu mengi ndiyo maana tupo hapa tulipo".Inawezekana yapo madudu mengine lakini at least hili unaelimishwa hapa kuwa halikuwa dudu,si ukubali kuelimika kaka.Ukubali kuwa kuna vitu vinahitaji thorough research kabla ya kutaka kuvicriticize.Kama unapewa hoja with supporting documents na unazipinga basi tupe za kwako.Kama unapewa majina ya vitabu vya kusoma na unasema havipo objective(kabla hata hujavisoma)basi tupe vitabu ambavyo vipo objective na vinavyosapoti hoja yako(ambayo mpaka sasa haijulikani).Kinyume na hapo utakuwa ni ubishi usio na mwisho na JF itageuzwa kuwa kilinge cha ubishi.
- Kila ninapoangalia tulikotokea hili Taifa, ninapatwa wasi wasi sana kwamba hatukufika hapa tulipo kwa makosa, tumefanya makosa mengi sana nyuma in terms of policies mpaka leo hii kurekebisha inakuwa ni almost impossible, ingawa watawala wa sasa wanajitahidi sana.
- Eti ni kwa nini Tanzania tuliunga mkono Waasi wa Nigeria waliokuwa wanaongozwa na General Ojukwu, kwenye kiu yao ya kujitenga na Nigeria Federation? Ninakumbuka tukiwa wadogo Shuleni, tulivyokuwa tunaimbishwa nyimbo za kumsifu Ojukwu, why? I mean ni policies ngapi huko nyuma we were wrong maana inaonekana ni nyingi sana that ni vigumu sana sasa kurekebisha njia!
- JE have we ever apologize to the Nigerians kwa makosa yetu ya kuuunga mkono uasi wa Ojukwu, dhidi ya serikali halali ya nchi hiyo?
- MUNGU AIBARIKI TANZANIA!
William J. Malecela.
- Wewe ni msomi, so unapaswa kuelewa effect za binadam waliozoea kuishi kwenye failed policies, akiondoak kiongozi wa zile poilicies itawachua muda mrefu sana kuanza kujiamini, maana tatizo kubwa la kuzoea kuishi kwenye failed policies ni unapoteza kujiamini!
William.
Kama watu wanafuatilia vizuri mambo, CCM wamemgeuza Mwl Nyerere kuwa kinga. Kwa mfano CCM wakiambiwa hawana tena uwezo kuongoza nchi wanatakiwa waondoke wao wanajibu - Mwl Nyerere alisema bila CCM imara nchi itayumba. Lakini ukiwauliza kwa nini hii nchi inayumba wanasema Mwl alikuwa na sera mbovu sana!
Ndio maana nasuburi kwa hamu kubwa maelezo toka kwa William kwa nini policies za miaka ya 1960s zinatutesa sasa 2012? Na kwa nini CCM hawajaziondoa hizo policies wanazoona ni tatizo? Kama waliweza kufuta Azimio la Arusha (tena Mwl akiwa bado hai) wanashindwa nini kufuta hizo policies zingine wanazosema ni kero?
Huna haja ya kutuuliza sisi hebu sogea hatua chache tu mwuulize John Malecela kwani yeye wakati huo alikuwa mmojawapo wa Viongozi wa TZ