mojoki
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 1,314
- 290
KIONGOZI wa Libya aliyeuawa juzi na wapiganaji wa Serikali ya Mpito (NTC), anadaiwa kuacha utajiri wa Sh 139 trioni kiasi ambacho ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka 12.
Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa fedha hizo ni zile zinazofahamika, alizoweka kwenye benki za nchi kadhaa duniani, huenda alikuwa na hazina zaidi mbali na hiyo. Kwa mujibu wa habari hizo, Gaddafi alikuwa anamiliki Pauni 29 bilioni nchini Uingereza (Sh78 trilioni), Dola 32 bilioni nchini Marekani (Sh54 trilioni), Dola 2.4 bilioni nchini Canada( Sh4 trilioni) na Dola 1.7 bilioni nchini Australia (Sh3 trilioni). Kwa fedha ya Tanzania.
Pauni moja ya Uingereza ni sawa na Sh 2,720, Dola moja ya Marekani Sh 1,704, Dola moja ya Canada, Sh 1,692 na Dola ya Australia ni Sh 1,769. Fedha hiyo kwa ujumla wake ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka 12.
Juni mwaka huu, Bunge lilipitisha jumla ya Sh11 trilioni kwa matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012 .Kiasi hicho kikizidishwa mara miaka 12 zitakuwa Sh132 trilioni, hivyo ukichukulia kiwango hicho, inamaana kuwa fedha za Gaddafi zinatosha kuendesha Tanzania kwa miaka 12 na bado zitabaki Sh trilioni saba.
Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa fedha hizo ni zile zinazofahamika, alizoweka kwenye benki za nchi kadhaa duniani, huenda alikuwa na hazina zaidi mbali na hiyo. Kwa mujibu wa habari hizo, Gaddafi alikuwa anamiliki Pauni 29 bilioni nchini Uingereza (Sh78 trilioni), Dola 32 bilioni nchini Marekani (Sh54 trilioni), Dola 2.4 bilioni nchini Canada( Sh4 trilioni) na Dola 1.7 bilioni nchini Australia (Sh3 trilioni). Kwa fedha ya Tanzania.
Pauni moja ya Uingereza ni sawa na Sh 2,720, Dola moja ya Marekani Sh 1,704, Dola moja ya Canada, Sh 1,692 na Dola ya Australia ni Sh 1,769. Fedha hiyo kwa ujumla wake ni sawa na bajeti ya Tanzania kwa miaka 12.
Juni mwaka huu, Bunge lilipitisha jumla ya Sh11 trilioni kwa matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2011/2012 .Kiasi hicho kikizidishwa mara miaka 12 zitakuwa Sh132 trilioni, hivyo ukichukulia kiwango hicho, inamaana kuwa fedha za Gaddafi zinatosha kuendesha Tanzania kwa miaka 12 na bado zitabaki Sh trilioni saba.