Tanzania kati ya mataifa 10 yenye madeni makubwa Afrika

Tanzania kati ya mataifa 10 yenye madeni makubwa Afrika

Elias Msuya

Platinum Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
217
Reaction score
860


Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi 10 zenye madeni makubwa katika Bara la Afrika ikishika nafasi ya nane kwa kuwa na deni kubwa la nje, huku nchi ya Misri ikiongoza kwa kuwa na deni la zaidi ya dola bilioni 7.2 (Sh 18.76 trilioni).

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Utangazaji la Uingereza BBC imezitaja nchi nyingine kuwa pamoja na Côte d'Ivoire inayoshika nafasi ya pili kwa zaidi ya dola bilioni 3.6 (Sh9.40 trilioni), ya tatu ni Kenya ikiwa na deni la zaidi ya dola bilioni 2.87 (Sh7.48 trillion), Ghana ikiwa na deni la zaidi ya dola bilioni 2.72 (S 7.09 (trilioni) na Angola yenye dei la zaidi ya dola bilioni 2.43 (Sh6.33 trilioni).

Nyingine ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ikiwa na deni la zaidi ya dola bilioni 2.19 (Sh5.71 trilioni), Ethiopia yenye deni la zaidi ya dola bilioni 1.76 (Sh4.58 trilioni) na Tanzania yenye deni la dola bilioni 1.33 (Sh3.46 trilioni) ikifuatiwa na Zambia yenye zaidi ya dola bilioni 1.27 (Sh3.31 trilioni) na Cameroon ikishika nafasi ya 10 kwa deni la dola bilioni 1.15 (Tsh3 trilioni).
 
Siku hizi waziri kombo anawakaribisha maraisi na watu wengine kwa ndege ya abiria ya wananchi
Screenshot_20260609-082331.png
 
Zifuatazo ni nchi za Afrika zenye madeni makubwa zaidi ya IMF mwaka huu .
1.Misri 7,245,182,524
2.Cote D'Ivoire. 3, 603,438 ,776
3.Kenya. 2, 873,418, 234
4.Ghana 2,728,468,500
5.Angola 2,437,716,676
6.DRC 2,196,550,004
7.Ethiopia 1,764,502,000
8.Tanzania. 1,335,730,000
9.Zambia 1,271,660,000
10.Cameroon. 1,152,990,000
FB_IMG_1782998256911.jpg
 
Kobaz mmoja yupo juu lkn kiuhalisia deni lake linaendana na maendeleo yake

Hawa makafiri wengne ndo sijui hela wanapelekaga wapi

Exclusion ya Tanzania naipa kipaumbele hii case sensitive maana 😁😁
 
Kobaz mmoja yupo juu lkn kiuhalisia deni lake linaendana na maendeleo yake

Hawa makafiri wengne ndo sijui hela wanapelekaga wapi

Exclusion ya Tanzania naipa kipaumbele hii case sensitive maana 😁😁
Tufanye tuwafikie misri pengine tukaona maendeleo
 
Back
Top Bottom