mama D
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 19,760
- 35,205
Nilikua napitia report ya afya nimesikitika kuona 34% ya vifo nchini hutokana magonjwa yasiyoambukiza na ugonjwa wa moyo ukiongoza. Magonjwa mengine sukari na cancer ambayo tunayaona yanavyozidi kutuvamia kwa kasi. Kwa tafakari ndogo maisha tunayoishi yamechangia hili kwa kiasi kikubwa.... Ifike mahali sisi wenyewe tusimame na kukataa maisha yanayotupelekea kwenye haya magonjwa hatarishi.
Turudi na kuangalia kile tunachokula na kunywa, na tuangalie shughuli zetu za kila siku kama vina mchango wowote kwenye kuimaraisha au kubomoa afya zetu.
Na katika maisha yale yanayotufurahisha basi yatupatie motisha wa kuendelea kuyafanya katika ubora zaidi na yale yanayotuumiza yatufundishe kwamba tunaweza kujibidisha sana lakini bado tukashindwa kuwa kila kitu tunachotaka au na hiyo isitunyime furaha
Kwa wale waamini wa uwepo wa Mungu basi tujifunze kumtanguliza kwa kila jambo; na tujifunze kumshukuru yeye kwa kila jambo... liwe lile tulilotaka au liwe kinyume chake tumshukuru kwani yeye anatuwazia mema kuliko tunayoyajua sisi.
Hata upate mafanikio unayoyaona kuwa madogo kiasi gani kumbuka zawadi uhai uliyopewa bure... Kumbuka uhai ulio nao ni nafasi nyingine kubwa aliyokupa Mungu ili kuweza kutimiza kile ulichomuomba na alichokutuma kufanya katika dunia hii
Kwa wale waumini wa Mungu na hata wale tusiokua waumini wa Mungu tufanye kazi kwa bidii na maarifa, tujifunze kuyaangalia maisha yetu kama zawadi kwa dunia hii, tujipende na kuwapenda wenzetu.
Tufurahie mafanikio yetu; na Tujifunze kukubali ukweli pale mambo yanavyoenda tusivyotaka sisi, hii itatusaidia sana kufanya maamuzi sahihi na kuendelea kuyafurahia maisha yetu hapa duniani
Cc Extrovert Wangari Maathai Rebeca 83 Saint Anne mrangi
Turudi na kuangalia kile tunachokula na kunywa, na tuangalie shughuli zetu za kila siku kama vina mchango wowote kwenye kuimaraisha au kubomoa afya zetu.
Na katika maisha yale yanayotufurahisha basi yatupatie motisha wa kuendelea kuyafanya katika ubora zaidi na yale yanayotuumiza yatufundishe kwamba tunaweza kujibidisha sana lakini bado tukashindwa kuwa kila kitu tunachotaka au na hiyo isitunyime furaha
Kwa wale waamini wa uwepo wa Mungu basi tujifunze kumtanguliza kwa kila jambo; na tujifunze kumshukuru yeye kwa kila jambo... liwe lile tulilotaka au liwe kinyume chake tumshukuru kwani yeye anatuwazia mema kuliko tunayoyajua sisi.
Hata upate mafanikio unayoyaona kuwa madogo kiasi gani kumbuka zawadi uhai uliyopewa bure... Kumbuka uhai ulio nao ni nafasi nyingine kubwa aliyokupa Mungu ili kuweza kutimiza kile ulichomuomba na alichokutuma kufanya katika dunia hii
Kwa wale waumini wa Mungu na hata wale tusiokua waumini wa Mungu tufanye kazi kwa bidii na maarifa, tujifunze kuyaangalia maisha yetu kama zawadi kwa dunia hii, tujipende na kuwapenda wenzetu.
Tufurahie mafanikio yetu; na Tujifunze kukubali ukweli pale mambo yanavyoenda tusivyotaka sisi, hii itatusaidia sana kufanya maamuzi sahihi na kuendelea kuyafurahia maisha yetu hapa duniani
Cc Extrovert Wangari Maathai Rebeca 83 Saint Anne mrangi