Inaendelea...
"Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea. Lutu akawaambia, Sivyo, bwana wangu! Tazama, mtumwa wako ameona kibali machoni pako, nawe umezidisha rehema zako ulizonifanyia kwa kuponya nafsi yangu, nami siwezi kukimbilia mlimani nisipatwe na yale mabaya, nikafa. Basi mji huu u karibu, niukimbilie, nao ni mdogo, nijiponye sasa huko, sio mdogo huu? Na nafsi yangu itaishi. Akamwambia, Tazama, nimekukubali hata kwa neno hili, kwamba sitauangamiza mji huo uliounena. Hima, ujiponye huko, maana siwezi kufanya neno lo lote, hata uingiapo humo. Kwa hiyo jina la mji ule likaitwa Soari."
MWANZO. 19:17-22.
Tukiangalia mistari hiyo hapo juu Lutu bado anaendelea kufanya makosa, amepewa maagizo kwanza asitazame nyuma ili ajiponye nafsi yake,pili asisimame katika bonde hilo popote pale ajiponye nafsi yake aende milimani asije akapotea....ameshaambiwa wapi aende nini afanye lakini Lutu akakataa ushauri ule na kusema kwamba hataweza kukimbilia mlimani asipatwe na mabaya yale asije akafa,akachagua mji mdogo ulio jirani yake ambao ulikuwa kwenye plan ya kuangamizwa,akafanya makosa ya uchaguzi kama aliyofanya mwanzo lakini hapa anapata rehema anaambiwa amesikilizwa mji huo hautaangamizwa. Mungu wetu ni wa rehema huchukuliana nasi hata katika madhaifu tuliyonayo.
Mstari wa 23-26 tunaona Lutu akiwasiri Soari na ndipo miji ya sodoma na Gomora ilipoangamizwa,sijui Lutu alikuwa anasisitiza kiasi gani kwa familia yake walitii agizo hilo,sijui alikuwa akiwakumbusha familia yake namna gani yale waliyoambiwa kwamba Mungu anaenda kuangamiza miji ile?
Mstari wa 26 tunaona mkewe akigeuka nyuma na anageuka kuwa nguzo ya chumvi,nyuma tunaweza kutafsiri vyovyote vile tupendavyo au tunaonavyo na kama nilivyosema awali kila mtu anaweza kufunuliwa kama Bwana apendavyo na kwa ufahamu wake aweze kuelewa,kama ambavyo ilikuwa agizo kwa Adamu asile tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya(kumbuka kulikuwa na miti mingi pale ila katikati kulikuwa na mti wa uzima na mwingine wa ujuzi wa mema na mabaya,mti huu kila mtu anatafsiri vile apendavyo,na ndiyo hapo shetani alipomuweza mwanamke) "Agizo ni moja tu usigeuke nyuma ujiponye nafsi yako,Usile tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya maana utakapokula Hakika utakufa".....Je ni kwa namna gani tunatii maagizo ya Mungu anayotuagiza ni hilo tu ndo Mungu anataka,anasema utii ni bora kuliko sadaka( 1Samweli 15:22)...undani wa kile kitu wakati mwingine hauhitajiki kuujua mambo yote utayajua baada ta kutii,ndo hapa ambapo palimfurahisha Mungu hata kumuita Ibrahimu ni rafiki yake,kwanza alimtii kuondoka katika jamaa yake kwenda kusikojulikana,alitii kumtoa Isaka Sadaka hata hakutaka kujua maisha yangekuwaje bila ya Isaka,vipi ahadi za Mungu zingetimia baada ya Isaka kutolewa sadaka je ungekuwa mwisho wa uzao wake? ALITII TU KAMA BWANA ALIVYOMUAGIZA.
Tuendelee kujifunza kwa Lutu katika Mwanzo hiyo 19.....
Mstari wa 29 unatuthibitishia moja kwa moja Lutu na nyumba yake aliokolewa kwa neema tu ni kwasababu ya Ibrahim,agano la Ibrahimu na Mungu lilipiga kelele na ikawa neema hata kwa ndugu yake,kumbe sisi tukisimama imara tukatembea vizuri na Mungu tunakuwa sababu ya wengine kuponywa kupitia sisi.
Lutu anaendelea kufanya makosa tu, Mstari wa 30 anatoka Soari akakaa katika pango yeye na binti zake,tukumbuke katika mstari wa 20 yeye mwenyewe ndo aliomba akae katika mji huo na akapata kibali cha Mungu,halafu yeye mwenyewe tena anaogopa kukaa hapo anaenda tena mahali ambapo hapakuwa na kibali cha Mungu,hivi alitegemea angekuwa na mwisho mzuri? Mungu amemrehemu amemleta tena kwenye kusudi akakataa option ya Mungu kwenda mlimani ikawa siyo tatizo kwa Mungu,akajichagulia alipopataka akapewa baraka zote bado tena anapakimbia!!,naamini Lutu angeendelea kukaa Soari wokovu wa Bwana ungemtokea huko maana mahali pale palikuwa na kibali tayari cha Mungu.
Anakimbilia pangoni yeye na wanawe tu,hivi tujiulize tu kwa akili zetu ndogo nini kingeendelea tena pale? Kama si Lutu kuwabaka wanae basi ndo kama hivyo wanae wakambaka baba yao,tunajifunza kwamba mazingira nayo yanachangia sana haijalishi ni nini wala nini miili yetu ni dhaifu,tunashinda ni kwa neema ya Bwana,usiintatein(chochea) mazingira ya kutenda dhambi,usijitengenezeee nafasi ya kutenda dhambi,mara nyingi tunamsingizia shetani eti alinipitia,kweli umepita anga zake utegemee utoke salama kweli??? Tuache visingizio visivyo na maana!!!
Lutu hakuwa na mwisho mzuri yeye na uzao wake,uzao wake ukaja kuwa adui wakubwa wa Israel(Waamoni na Wamoabi)dhambi ya uzinzi na usaliti wa sheria za Mungu hakuwaacha,Katika yote haya yamemfikisha Lutu hapo alipokuwa ni sababu ya kutotembea katika kusudi lake,hata alipoletwa kwenye kusudi lake bado akashindwa,Inaumiza sana kupoteza mke uliyempenda,inaumiza sana kulala na watoto wako wa kuwazaa,inaumiza sana kuwa na kizazi chenye maovu. Inaumiza sana kuishi maisha ya kutanga tanga.
Mungu tusaidie tusahihishe makosa yetu,Mungu tusaidie tukuelewe pale unaposema nasi,Mungu tusaidie tulielewe kusudi la kuumbwa kwetu hapa duniani.Sisi peke yetu hatuwezi ila tunayaweza mambo yote katika wewe ututiaye nguvu,Katika Jina la Yesu tunarudi kwenye kusudi letu,Amina.
mshana jr asante sana kutumiwa na Mungu kuleta mada hii nimejifunza mengi,Umenifanya nami nijitafakari kwa upya safari yangu,Mungu amesema nasi sisi sote,ubarikiwe sana na Bwana azidi kukutumia na akufunulie siri nyingine nyingi ambazo macho hayakupata kuona,wala sikio halikupata kusikia wala hayakuwepo katika moyo wa mwanadamu yoyote yule.