FT: Simba SC 7-0 Horoya AC | CAF Champions League | Benjamin Mkapa | 18.03.2023

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Jan 1, 2017
20,722
45,128
Mnyama Mkubwa Mwituni asiyefugika, Simba Sports Club anashuka dimbani leo kuikabili Horoya AC katika mchezo muhimu wa kundi C.

Simba itaingia uwanjani ikiwa na alama 6 huku Horoya wakiwa na alama 4. Ushindi wa aina yoyote utawafanya Simba wafuzu robo fainali.

Leo ni ama afe kipa au afe beki, ushindi ni lazima kwa Mnyama, na kwa uzoefu wangu, mechi za namna hii Simba akiwa kwa Lupaso huwa tunashinda goli zisizopungua 3.

Shime wana Simba tujitokeze kwa wingi hapo Lupaso ili tukahanikize ushindi wetu mapema, najua friends of Horoya watakuwepo ila hawatosumbua.

Mchezo utakuwa mubashara saa 1:00 usiku na kama kawaida, ZBC 2 ya AzamTv na Variety 4 ya DStv watakuwa live.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Simba Sports Club. 🦁🦁🦁

====
Kikosi cha Simba SC

E3FDBBBD-DCBC-4591-B267-E99F10158211.jpeg
Timu zinaingia uwanjani
Mchezo unaanza
2' Timu zinasomana mchezo
5' Simba wanaongeza kasi ya mashambulizi
10' Goooooooooo
Chama anafunga goli kwa faulo ya moja kwa moja
15' Simba wanakosa nafasi ya wazi baada ya Kibu Denis kuteleza
20' Horoya wanaonesha kujibu mashambulizi
27' Kidogo kasi ya mchezo imepungua lakini timu zote zinatengeneza mashambulizi
29' Kadi ya njano kwa Kibu Denis
31' Gooooooooo
Baleke anafunga goli la pili
35' Penatiiii kwa Simba baada ya mlinzi wa Horoya kuunawa mpira
Gooooooo
Chama anaipatia Simba goli la tatu kwa penati
45' Zinaongezwa dakika 2

MAPUMZIKO: Simba wanaongeza kwa Magoli 3-0

Kipindi cha pili kinaanza
Horoya wanafanya mabadiliko ya kipa

55' Goooooooo
Kanoute anafunga kwa shuti akimalizia pasi ya Chama
57' Anatoka Kibu Denis anaingia Sakho
60' Horoya wanaamka na kufanya mashambulizi
65' GOOOOOOOOOOOOOOOOOOO
Chama anafunga goli la 6 kwa Simba na la 3 kwake katika mchezo huu akimalizia pasi ya Sakho
87' Kanoute anafunga goli la pili kwake na la saba kwa Simba
90' FULL TIME

Saba.JPG
 
Back
Top Bottom