Wanabodi
Kwa mnaotaka kuifahamu Freemasons, angalia Clouds TV now, Mkuu wa Freemasons Kanda ya Afrika Mashariki na Kati, Sir Andy Chande anaweka kila kitu wazi!.
Kipindi kimekwisha!.
My Take!.
Andy Chande ame mention about Freemasons lakini hakusema lolote kuhusu freemasons!.
Mtangazaji Gerald Hando, very unfortunately didn't do his homework well!.
1. Alipoambiwa ili mtu kuwa freemasons lazima ufanyiwe "initiation" alipaswa kuuliza inafanikaje na inafanyika ili iweje?.
2. Alipoelezwa huwa wanafanya "ceremonies" hakukuliza ni sherehe za nini na zinafanyikaje?.
3. Alipoelezwa Freemasons sio dini, ila ili kuwa member lazima kwanza uwe na dini, kwa nini wasio na dini hawaruhusiwi?.
4. Ameeleza hawana siri zozote ila tuu ya jinsi ya kujuana, alipaswa aseme kama sio secret society hizo siri ni za nini?.
5. Alipoelezwa kuwa hicho ni chama cha kutoa misaada alipaswa aulize misaada gani wametoa au wameshasaidia nini?.
6. Alipoambiwa kuwa MV Bukoba ilipozama, freemasons wa Uingereza walitoa Pauni 10,000, alipaswa kuuliza why only that wajati taifa limepata majanga kibao?.
7. Alipoambiwa freemasons wala level fulani fulani na grand lodge za kila level, kama hujafikia level fulani huwezi kuingia lodge fulani, alipaswa aulize hizo levels ni za nini?, kuna vigezo gani kufikia level fulani? na kwa nini watu wa level fulani hawaruhusiwi kuingia lodge za level fulani?, nini kinafichwa humo?.
8. Alipaswa kuuliza what time of a day do they meet and why?. Hukutana usiku wa manane?.
9. Angeuliza kwenye hizo karamu zao za usiku wa manane, wanakula vyakula gani na wanakunywa vinywaji gani?.
10. Alipaswa kumuuliza kwa nini wanawake hawaruhusiwi? na zaidi ya yeye, ma freemasons wengine prominent Tanzania ni akina nani?.
Kusema ukweli, Andy Chande has taken Gerald Hando with a ride kwa leading questions za maswali mboga mboga ili kuipromote freemasons, nimejikumbuka enzi zangu nilipokuwa nikifanya interview programs, ilikuwa ni grilling time and leave no stone unturned!.
All and all tuishukuru Clouds FM, something is better than nothing!.
Thanks
Pasco.