Freeman Mbowe, kwanini maridhiano sasa?

Freeman Mbowe, kwanini maridhiano sasa?

Kwa hiyo chadema wamewahi ili wasijekosa fedha za uchaguzi kutoka serikarini au unamaanisha nni
 
Sasa unalaumu tu wakati hujui hayo maridhiano yatalenga wapi labda ndio mwanzo wa kupata tume huru na katiba mpya who knows.
Unatania wewe CCM watoe tume huru ya uchaguzi kwenye kisahani.?
 
Ni wakati muafaka kwa vyama vya Upinzani KUDAI Marekebisho ya Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi
 
Mkuu umeongea vema.
Mbowe na wanao mpondea hili wazo lake la maridhiano nawafananisha Luther King Jr na Malcolm X.
Mbowe ni kama Luther King Jr na wakosoaji wake ni kundi la Malcolm X.

Wakati fulani lazima utumie njia za kidiplomasia zaidi kulingana na mazingira ya vita na aina ya adui wako na nyenzo zake.
Nasimama na Mbowe, maridhiano sio kushindwa vita.
Kaka vita vimekwisha toka msituni tujenge nchi.
 
NewOrder,
SIASA NI JAMBO LINALOONGOZWA KWA NYAKATI? kwahiyo NYAKATI za Sasa Ni kuwasaliti uliovuja nao jasho na kutanguliza maslahi yako binafsi?

Inavyoonekana umesoma uzi Ila hujaelewa au umepita na kuchagua maeneo ambayo unaweza ukayajengea hoja japo hoja zenyewe imejikita katika fasihi badala ya mada.
 
Kuna watu hapa bongo ikisha kuwa ni swala la kupata pesa, wanakuaga "kama ni mbwai iwe mbwai". Watu wana waza ruzuku itapatikanaje baada ya mwakani full stop.
 
Kama Mh. Mbowe nafsi aimsuti kwa hili la kuomba poo, basi CHADEMA kuna ombwe kubwa la uongozi.
 
Maridhiano yaje baada ya uchaguzi 2020. Tumeshagundua janja yenu mnajua mwaka kesho hampati hata mbunge mmoja. Rais Magufuli usikubali janja ya nyani...!!
Kweli kabisa umenena Rais aendelee kuchapa kazi tu, eti maridhiano !
 
Niwe mkweli, sioni mwisho mzuri wa Mbowe na Lissu. Sidhani yupo aliyefikiri ipo siku Mbowe ataingia kwenye mgogoro na Dr Slaa lakini Mbowe hajali inapokuja jambo ambalo yeye anaona lina manufaa kwake.

Pona ya Lissu ni awe kama akina Lema na Boni lakini akitaka kutumia akili zake kisawasawa mtaona kitachotokea. Save this post ..
 
SIASA NI JAMBO LINALOONGOZWA KWA NYAKATI? kwahiyo NYAKATI za Sasa Ni kuwasaliti uliovuja nao jasho na kutanguliza maslahi yako binafsi?

Inavyoonekana umesoma uzi Ila hujaelewa au umepita na kuchagua maeneo ambayo unaweza ukayajengea hoja japo hoja zenyewe imejikita katika fasihi badala ya mada.

Kama hujui umuhimu wa nyakati katika siasa, huwezi kuwa na mamlaka ya kuzungumzia siasa. Kila siku tunasikia humu na sehemu nyingine watu "wakiunga mkono juhudi" - unadhani huo ni usaliti? Unadhani hayo ni maslahi yao binafsi?? Miaka ya Kikwete kulikuwa na mambo ya kisiasa ambayo leo hatuoni yakifanywa na Magufuli. Ni nani msaliti au anayeendeleza maslahi binafsi katika hao??

Nitarudia kukufundisha hili - siasa hufanywa kwa kuongozwa na mahitaji ya nyakati. Ikiwa unataka kuzungumzia usaliti au maslahi binafsi - sio point ya mada hii. Mada hii iliuliza kwanini Mbowe kamua kuomba maridhiano "sasa"?? Na kama hukumbuki kuona neno "sasa" na kuliona katika mtazamo wa muda au wakati - usirejee hapa kuzungumzia mada hii!!

Nilikushauri mwanzo kuwa uliza swali - usijikite kuweza allegations, assertions, opinions na viewpoints zako kama ndio mada - ukidhani kwa kufanya hivo unakuwa unaelezea mawazo au nia za Mbowe za kuomba maridhiano. Ungeweza tu kuwa na mada inayotoa shutuma kwa Mbowe badala ya kuuliza swali. Kabla hujatoa hoja, pima kama una hoja ya msingi!!
 
Hichi kinachoitwa maridhiano na hawa jamaa sijui ni kitu gani a see..

Wao ndio waliotamka nchi haitawaliki..bado kuna Yule Msanii wa Maigizo na uchekeshaji Mr.Tundu kutwa kuzurura kuichafua nchi.

Waombe radhi kwanza
Wakiomba watasamehewa hakuna shida wote ni wa TZ.
 
Usipotoshe nia nzuri ya Mbowe

Maridhiano ndiyo njia pekee ya kistaarabu kufikia maelewano

Ngoja nikuulize swali dogo tu, hivi kina Mandela walifkia maridhiano Afrika Kusini, kuna mtu alilaumu uamuzi huo??

Hivi Uhuru Kenyatta wa Kenya kufanya maridhiano na Odinga, kuna watu wanalaumu??

Unapoweka nchi mbele zaidi ya ubinafsi, unaweza ukafikia maridhiano, lakini unaooweka ubinafsi mbele ni lazima hutapendekeza yafikiwe maridhiano

Kwa hiyo wapinzani wa nchi hii wanalazimika kumpongeza Mbowe, kwa kuamwambia Rais Magufuli kuwa wao upinzani wako tayari kwa maridhiano..........

Kwa hiyo kazi kwake yeye Rais Magufuli, kama ataweka mbele.maslahi ya Taifa, ataridhia ombi hilo la Mbowe na kama ataweka mbele maslahi binafsi yake yeye mwenyewe binafsi, atayakataa
Maridhiano juu ya nini? Sema Chadema imenyoosha mikono. Imeushindwa muziki wa Jiwe sasa wanaomba poo kiaina, eti maridhiano. Na vijana wa Chadema mliojana humu mmeshupalia maridhiano, maridhiano! Yapi? Ninyi si mna msemo "mpaka kieleweke"? Vipi sasa kubembeleza maeidhiano!!!?
 
Huyo msaliti wa nchi anapashwa kutoswa kabisa akae huko huko!
Hii ndio falsafa ya wasio na hoja! Yaani mawazo yenu mgando hamtaki wenye akili kubwa kuyakandia! Kwa taarifa yako, huyo ndiye rais wako ajaye 2020! Lamba jivu upooze kiungulia!
 
Back
Top Bottom