Cherenganya
JF-Expert Member
- Jan 21, 2018
- 2,309
- 1,775
Wananzengo habari zenu.
Takribani saa 24 zilizopita nimekuwa nikijaribu kusoma na kutafakuri kwa kina yaliyotokana na mambo mawili, kwanza CHADEMA kushiriki katika sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru la kwanza na lapili hotuba ambayo Mh. Mbowe aliyoiunda na kuhakikisha arafa yake inapatikana katika dakika tatu tu! (Sina hakika kama protokali ndizo zilimtaka afanye hivyo au Ni utashi wake)
Zitto kasema, kaponda, kalaumu kakosoa na kaonyesha ni namna gani moyo wake umesambaratika. Maria Sarungi kachana kanung'unika, kaonyesha ni namna gani wanasiasa hawana muamana. Shangazi Fatma kashindwa kuwa muwazi kajikuta anasema tu I WAS WRONG japo Nina mashaka kama anajua kweli kwamba SHE WAS WRONG.
Hayo Ni ya kwao nami ninayo yangu. Ila kabla ya yangu ni pende kusema kwamba Mh. Mbowe ni aina ya watu wanaojua kurisk na ni aina ya kiongozi ambaye hudumbukiza mkono kwenye shimo lenye kiza na asijue ataambulia nini.
Mh. Mbowe kwanini Sasa Kama ambavyo kichwa cha habari hii kinavyouliza, kwa takribani miaka mitatu na ushee CHADEMA wamekua wakisusia kabisa shughuli zote za serikali kitaifa, na lililonistua zaidi yapata miezi 2 iliyopita aliita waandishi wa vyombo vya habari na kutangaza kujitoa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa sababu wagombea wake hawakutendewa haki. Ghafla msimamo ule umeyeyuka na Sasa kilio katika MARIDHIANO, unataka kuridhia nini? Je Ni uhalali wa Rais Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania, au kuridhia yeye kuendelea kuchepusha baadhi ya Sheria ili kuleta maendeleo ya haraka nchini?.
Je, Maridhiano haya ni yapi ya kuomba Uhuru wa kufanya mikutano ya siasa ya nje na ndani pahala popote na wakati wowote? Au Ni Maridhiano ya kumkosoa na yeye kuwachekea?, Unahitaji kuridhia nini naye kwakua CCM na yeye mwenyewe wanayatenda haya kimkakati kwakua muda wa miaka mitano ni mdogo na mambo wanayotaka kufanya ni mengi.
Katika ridhaa mwenye mamlaka ni mtoa ridhaa na sio mpewa ridhaa, Kwanini Magufuli aridhie maoni yako ili hali yakwakwe bado hajaridhika nayo.
TUAMBIE MH. MBOWE KWANINI SASA?
Wamesimama nawe, wamehuzunika nawe wamepambana nawe, umeamua kuachana nao? Au unamkimbiza mwizi kimya kimya?
Mh. Mbowe, mimi naamini ninyi wanasiasa mna dini yenu, mnaye Mungu wa kwenu, na mnayo maisha yasiyoamiliana na yakwetu.
Ulichokitenda kwa walio na hasira watakiita usaliti (bahati zuri unahistoria pana kwenye hili) Ila kwa wenye busara watakuuliza kwanini Sasa? hudhani kwamba maridhiano, wakati umeshindwa vita ni woga? Wataenda mbali zaidi na kuhoji Mh. Mbona inaonekana kama ZILONGWA MBALI NA ZITENDWA MBALI.
Kesho ukituambia tuandamane tunaweza kuthubutu kunjanyua tendegu zetu na kuzipeleka barabarani? Ili baada ya kuvunjwa miguu na mikono ukae uombe kuridhiana?
KAMA NI KWELI NINACHOWAZA NDICHO
1. Umeamua ku-feki kunyoosha mikono ili maumivu yapungue uweze kujipanga kwa ajili ya nafasi za Udiwani, Ubunge na Urais kwa mwaka 2020. Kimsingi mbinu hizi husaidia kwa mtu aliyekua akilifanya Jambo hilo kukukomoa lakini si kwa mtu aliyekua au anayeyafanya kwa ajili ya kutimiza mambo yake, atakukanyaga tu utapo thubutu kusimaa kwenye nyia yake hatokua na msalie Mtume.
2. Umeamua kuziaminisha jumuia za kimataifa kwamba CHADEMA wanayo nia ya kuendesha siasa za kistaarabu, ukapewa jukwaa ukaandika speech fupi iliyolenga kusudio lako, sawa na Safi ambacho hujatizama kwa undani ni kwamba Mh. Magufuli hazihofii hizo jumuia na wala hatokosa usingizi, Ipo mifano inayodhihirisha kwamba hilo halimuumizi kichwa.
3. Kama lengo Ni kuomba huruma japo mwakani chama kipate WABUNGE ili kiendelee kuishi kwa ruzuku, utakua umejitekenya na kujikuta unacheka mwenyewe.
Mlituaminisha kwamba ananunua wapinzani. Iwapo waliweza kuingia mfukoni kuwanunua wapinzania leo mnajitongozesha wenyewe kweli hata hela ya sabuni kuwapa baada ya tendo si itakua ni hiari yake?
NAWASHAURI NINI
Nimegundua kwamba dunia inakawaida ya kuheshimu watu walio katika makundi haya matatu
1. Msimamo juu ya kile unachokiamini, MARTIN LUTHER KING JR, MALCOM X (Malick al Shabaaz), ERNEATO CHE, FIDEL CASTO na wengine wengi.
2. Wasema kweli hata kama unawadhalilisha, heshima aliyoipata BILL CLINTON ALIPOKUBALI KUCHEPUKA MAMA AKATOKA HADHARANI AKAMTEYEA AKAUAMBIA UMMA YEYE NDIYE MWENYE MAKOSA, Mzee Nelson Mandela alipoutangazia UMMA kwamba mwanae kafa kwa UKIMWI, na mengine mengi.
3. Kukubali kushindwa, Ni dhahiri, nafsi haitajisikia vizuri lakini jamii iliyokuzunguka inaridhika kwamba tumejaribu na tumeshindwa na sasa tujopange upya au tuendelee na mambo mengine.
Wasalaam.
Takribani saa 24 zilizopita nimekuwa nikijaribu kusoma na kutafakuri kwa kina yaliyotokana na mambo mawili, kwanza CHADEMA kushiriki katika sherehe za maadhimisho ya miaka 58 ya Uhuru la kwanza na lapili hotuba ambayo Mh. Mbowe aliyoiunda na kuhakikisha arafa yake inapatikana katika dakika tatu tu! (Sina hakika kama protokali ndizo zilimtaka afanye hivyo au Ni utashi wake)
Zitto kasema, kaponda, kalaumu kakosoa na kaonyesha ni namna gani moyo wake umesambaratika. Maria Sarungi kachana kanung'unika, kaonyesha ni namna gani wanasiasa hawana muamana. Shangazi Fatma kashindwa kuwa muwazi kajikuta anasema tu I WAS WRONG japo Nina mashaka kama anajua kweli kwamba SHE WAS WRONG.
Hayo Ni ya kwao nami ninayo yangu. Ila kabla ya yangu ni pende kusema kwamba Mh. Mbowe ni aina ya watu wanaojua kurisk na ni aina ya kiongozi ambaye hudumbukiza mkono kwenye shimo lenye kiza na asijue ataambulia nini.
Mh. Mbowe kwanini Sasa Kama ambavyo kichwa cha habari hii kinavyouliza, kwa takribani miaka mitatu na ushee CHADEMA wamekua wakisusia kabisa shughuli zote za serikali kitaifa, na lililonistua zaidi yapata miezi 2 iliyopita aliita waandishi wa vyombo vya habari na kutangaza kujitoa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa sababu wagombea wake hawakutendewa haki. Ghafla msimamo ule umeyeyuka na Sasa kilio katika MARIDHIANO, unataka kuridhia nini? Je Ni uhalali wa Rais Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania, au kuridhia yeye kuendelea kuchepusha baadhi ya Sheria ili kuleta maendeleo ya haraka nchini?.
Je, Maridhiano haya ni yapi ya kuomba Uhuru wa kufanya mikutano ya siasa ya nje na ndani pahala popote na wakati wowote? Au Ni Maridhiano ya kumkosoa na yeye kuwachekea?, Unahitaji kuridhia nini naye kwakua CCM na yeye mwenyewe wanayatenda haya kimkakati kwakua muda wa miaka mitano ni mdogo na mambo wanayotaka kufanya ni mengi.
Katika ridhaa mwenye mamlaka ni mtoa ridhaa na sio mpewa ridhaa, Kwanini Magufuli aridhie maoni yako ili hali yakwakwe bado hajaridhika nayo.
TUAMBIE MH. MBOWE KWANINI SASA?
Wamesimama nawe, wamehuzunika nawe wamepambana nawe, umeamua kuachana nao? Au unamkimbiza mwizi kimya kimya?
Mh. Mbowe, mimi naamini ninyi wanasiasa mna dini yenu, mnaye Mungu wa kwenu, na mnayo maisha yasiyoamiliana na yakwetu.
Ulichokitenda kwa walio na hasira watakiita usaliti (bahati zuri unahistoria pana kwenye hili) Ila kwa wenye busara watakuuliza kwanini Sasa? hudhani kwamba maridhiano, wakati umeshindwa vita ni woga? Wataenda mbali zaidi na kuhoji Mh. Mbona inaonekana kama ZILONGWA MBALI NA ZITENDWA MBALI.
Kesho ukituambia tuandamane tunaweza kuthubutu kunjanyua tendegu zetu na kuzipeleka barabarani? Ili baada ya kuvunjwa miguu na mikono ukae uombe kuridhiana?
KAMA NI KWELI NINACHOWAZA NDICHO
1. Umeamua ku-feki kunyoosha mikono ili maumivu yapungue uweze kujipanga kwa ajili ya nafasi za Udiwani, Ubunge na Urais kwa mwaka 2020. Kimsingi mbinu hizi husaidia kwa mtu aliyekua akilifanya Jambo hilo kukukomoa lakini si kwa mtu aliyekua au anayeyafanya kwa ajili ya kutimiza mambo yake, atakukanyaga tu utapo thubutu kusimaa kwenye nyia yake hatokua na msalie Mtume.
2. Umeamua kuziaminisha jumuia za kimataifa kwamba CHADEMA wanayo nia ya kuendesha siasa za kistaarabu, ukapewa jukwaa ukaandika speech fupi iliyolenga kusudio lako, sawa na Safi ambacho hujatizama kwa undani ni kwamba Mh. Magufuli hazihofii hizo jumuia na wala hatokosa usingizi, Ipo mifano inayodhihirisha kwamba hilo halimuumizi kichwa.
3. Kama lengo Ni kuomba huruma japo mwakani chama kipate WABUNGE ili kiendelee kuishi kwa ruzuku, utakua umejitekenya na kujikuta unacheka mwenyewe.
Mlituaminisha kwamba ananunua wapinzani. Iwapo waliweza kuingia mfukoni kuwanunua wapinzania leo mnajitongozesha wenyewe kweli hata hela ya sabuni kuwapa baada ya tendo si itakua ni hiari yake?
NAWASHAURI NINI
Nimegundua kwamba dunia inakawaida ya kuheshimu watu walio katika makundi haya matatu
1. Msimamo juu ya kile unachokiamini, MARTIN LUTHER KING JR, MALCOM X (Malick al Shabaaz), ERNEATO CHE, FIDEL CASTO na wengine wengi.
2. Wasema kweli hata kama unawadhalilisha, heshima aliyoipata BILL CLINTON ALIPOKUBALI KUCHEPUKA MAMA AKATOKA HADHARANI AKAMTEYEA AKAUAMBIA UMMA YEYE NDIYE MWENYE MAKOSA, Mzee Nelson Mandela alipoutangazia UMMA kwamba mwanae kafa kwa UKIMWI, na mengine mengi.
3. Kukubali kushindwa, Ni dhahiri, nafsi haitajisikia vizuri lakini jamii iliyokuzunguka inaridhika kwamba tumejaribu na tumeshindwa na sasa tujopange upya au tuendelee na mambo mengine.
Wasalaam.