Kwanza sitaki kuamini kuwa Mbowe alishiriki katika lile tukio hivi hivi tu bali kushawishiwa na watu wa sytem na wasaidi wengine wa Bwana mkubwa na pia sitaki kuamini kuwa alikwenda kushirikia bila kushirikisha viongozi wenzake ndani ya chama hivyo kuna uwekano mkubwa Mbowe alitoa kauli ile akijua kinachoendelea ingawa pia inawezekana kaingia katika mtego kwa faida ya Bwana yule asietaka kuonekana kuwa anaweza kushindwa katika misimamo yake(nitaeleza huko mbele).
Kosa alilolifanya Mbowe na chama chake kwa ujumla, ni kushiriki tukio lile bila kushauriana na viongozi wengine wa upinzani ambao naamini wangeshirikishwa,basi aliyoyasema Zitto yasingetokea hata kama wasingefikia muafaka wa pamoja kuwa Mbowe ashiriki.
Nikirudi kwenye mada,nitakuwa wa mwisho kuamini kuwa Bwana yule alikuwa hajui Mbowe ataongea alichoongea bali alitaka Mbowe ndio aonekana mtafuta suluhu kwanini yeye siku zote hataki kuonekane ameshindwa(hataki kupangiwa).
Na ndio maana baada tu ya Mbowe kuongea,vijana wa Lumumba wakaanza propaganda za kusema Mbowe kaomba suluhu na maneno mengine mengi ili mwisho wa siku wapinzani ndio waonekane wameshindwa katika mapambano ya kudai haki na sasa wanategemea huruma ya Bwana yule kumbe Bwana yule nae anabanwa na pressure ya ndani na nje ya nchi kutokana na aina ya uongozi wake hasa uminyaji wa demokrasia na unyanyasaji kwa wapinzani.
Naamini katika kujisafisha na ili asiendelee kuvurugana na Bwana wakubwa wa hii dunia,Bwana yule ameona kuna umuhimu wa kujirudi japo kidogo, hivyo anaweza kuja kufanyia kazi wazo la Mbowe ingawa anaweza kufanya hivyo kwa kuwazuga tu mabeberu hivyo wawe makini nae.
Ni imani yangu pia, Mbowe kwa upande wake, aliamua kujishusha ili atumie fursa iliojitokeza(akijua kinachoendelea) hivyo akaongea alichoongea ikiwa ni utekelezaji wa kinachoendelea chini ya kapaeti.
Inawezekana kabisa watu wa system hawakumshirikisha Zitto na chama chake hasa kutokana na Zitto kwa sasa kuonekana ni mtu anaemkosoa na kumpinga vibaya sana Bwana yule na pia wakiamini chama cha Zitto hakina wafuasi wengi kama CHADEMA hivyo impact yake haitokuwa kubwa ingawa kwa hili wanaweza kuwa hawakuwaza sawaswa.
Huu ni mtazamo wangu ila muda ndio msema kweli.