Freeman Mbowe, kwanini maridhiano sasa?

Freeman Mbowe, kwanini maridhiano sasa?

Masiya,
Mkuu umeongea vema.
Mbowe na wanao mpondea hili wazo lake la maridhiano nawafananisha Luther King Jr na Malcolm X.
Mbowe ni kama Luther King Jr na wakosoaji wake ni kundi la Malcolm X.

Wakati fulani lazima utumie njia za kidiplomasia zaidi kulingana na mazingira ya vita na aina ya adui wako na nyenzo zake.
Nasimama na Mbowe, maridhiano sio kushindwa vita.
 
Sukuwahi kufikiri kama mbowe ni mlaini kiasi hiki, kama alijiua mambo yamemkalia kibaya angeachia uenyekiti
Wewe na wenzako wote hamjui chochote kinachoendelea kwa sasa..kama hujui kitu kubakia kimya nayo ni busara.
 
Mnakumbuka mtifuano mkali uliotokea baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya kati ya muungano wa vyama vya upinzani, NASA, ambapo mgombea urais alikuwa Raila na mgombea mwenza alikuwa Msyoka?

Mtifuano huu ulimpa shuruba mateso na adha za kila namna mwanasheria Miguna Miguna mpaka akanyang'anywa uraia, akapakiwa kama ndizi toka uwanja wa ndege na kuondoshwa nchini.

Alinyanyasika mno Miguna Miguna kwasababu tu alisimama kidete kutetea maslahi na haki za NASA. Hakika alipata tabu sana Miguna Miguna. Lakini kumbe chini ya kapeti Raila akawa anayasaka maridhiano yaliyokuja kujulikana kama "Hand shaking" (HS).

Hii HS ilizua mgawanyiko ndani ya NASA na maneno makali, dhihaka na matusi dhidi ya Raila. Lakini Raila aliendelea kuwa hard headed na kukomaa na mpango wake wa HS.

Miguna Miguna akatelekezwa mpk leo hajulikani yuko wapi. Wala Raila hana time naye kabisa. Alitumika na akatupwa. Hali kama hii ya Miguna naiona ikimnyemelea Lissu. Lissu amepambana sana dhidi ya Chadema.

Pamoja na kushambuliwa mchana kweupe katika nyumba za serikali na serikali ikakaa kimya, ikamnyima matibabu, ikamnyang'anya ubunge, lakini bado hakukata tamaa, na wala hakuunga juhudi mkono.

Kumbe wakati madhila haya dhidi ya Lissu yakiendelea Mbowe chini ya kapeti anatafuta maridhiano. Watu wanapiga kelele na wataendelea kupiga kelele lakini Mbowe ataweka pamba masikioni.

Yakipatikana maridhiano haya Lissu atakuwa kama Miguna Miguna. Atatoswa na kuonekana hafai kwa kauli zake kali za ukosoaji dhidi ya serikali hii. Atatelekezwa kama Miguna Miguna.
 
Usipotoshe nia nzuri ya Mbowe

Maridhiano ndiyo njia pekee ya kistaarabu kufikia maelewano

Ngoja nikuulize swali dogo tu, hivi kina Mandela walifkia maridhiano Afrika Kusini, kuna mtu alilaumu uamuzi huo??

Hivi Uhuru Kenyatta wa Kenya kufanya maridhiano na Odinga, kuna watu wanalaumu??

Unapoweka nchi mbele zaidi ya ubinafsi, unaweza ukafikia maridhiano, lakini unaooweka ubinafsi mbele ni lazima hutapendekeza yafikiwe maridhiano

Kwa hiyo wapinzani wa nchi hii wanalazimika kumpongeza Mbowe, kwa kuamwambia Rais Magufuli kuwa wao upinzani wako tayari kwa maridhiano..........

Kwa hiyo kazi kwake yeye Rais Magufuli, kama ataweka mbele.maslahi ya Taifa, ataridhia ombi hilo la Mbowe na kama ataweka mbele maslahi binafsi yake yeye mwenyewe binafsi, atayakataa
 
Hichi kinachoitwa maridhiano na hawa jamaa sijui ni kitu gani a see..

Wao ndio waliotamka nchi haitawaliki..bado kuna Yule Msanii wa Maigizo na uchekeshaji Mr.Tundu kutwa kuzurura kuichafua nchi.

Waombe radhi kwanza
 
Kwanza unatakiwa ujijue kuwa huna upeo. Achana na tabia yako hii ya kujaza server na kuchosha watu humu.
 
Sexless,
Unajua kabla Miguna Miguna hajawa kambi ya Raila ule uchaguzi ambao Raila alikuwa anashiriki kama waziri mkuu mstaafu Miguna alikuwa anamchukilia vipi? Emb fuatilia kisha ujue tofauti zilizopo.."Come baby come..I have all things right here..." Unajua huo msemo ulitoka wapi? Uwe unafuatilia kwanza kabla ya kulipuka!
 
Kwanza unatakiwa ujijue kuwa huna upeo. Achana na tabia yako hii ya kujaza server na kuchosha watu humu.
Huyu jamaa hovyo sana. Hajui kuwa uchaguzi wa awamu ya kwanza ya Uhuru ndiyo Miguna alikuwa anaingia Kenya kutokea Canada uhamishoni akaingia Kenya kwa gear ya kumponda Raila aliyekuwa waziri mkuu ndani ya serikali ya Kibaki? Akapigwa tanganyika jeki akiwa Mombasa hadi sisi vijana tuliokuwa wadogo tukaona kipande cha soksi alichovaa ndani ya kiatu ( maana ilikuwa imechanika yote) baada ya kiatu kuvuka? Emb aende arudi upya tafadhali! Hajui ule msemo uliotawala Kenya uchaguzi wa awamu ya kwanza ya Uhuru wa " Come baby come" ulitoka wapi?
 
Hebu fanyeni hata tafiti kidogo ndipo mtagundua appearance ya KUB kwenye sherehe za uhuru ni maazimio yaliyopitishwa na kamati kuu ya Chadema na sio maamuzi binafsi ya Kamanda Mbowe na taarifa ya kamati kuu ipo ilisambazwa.
 
Bila maridhiano hakuna uchaguzi mkuu 2020; ccm itapita bila kupingwa. Nchi hii haijapata uhuru jana, hivyo kuna watu wanajua athari za hali hiyo. Baadhi ya watu hao ni wazee wa nchi hii ambao wengi wao wako ccm. Hakuna mzee hata mmoja aliyefurahisishwa na vituko vya chaguzi zetu ndogo tangu uchaguzi mkuu umalizike 2015. Turning point ni uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 uliothibitisha kuwa all is not well. Baada ya uchaguzi huo haiwezekani tena kakudanganya kwambà yuko salama.

Uchaguzi wa 2020 ukivurugwa nchi yetu inaweza kujikuta katika matatizo ya itatengwa na jumuia ya kimataifa na hata kuwekewa vikwazo vya kiuchumi. Watu wote makini hawaoni sababu yoyote ya kufika huko. Wapo pia wana-ccm wengi wasiopenda hata kupata ushindi bila kushindana; hiyo siyo demokrasia. Kwa sababu hii maridhiano yameanza kutafutwa. Wanaotafuta maridhiano siyo wapinzani bali ni watu wenye mapenzi mema wanaotaka kuinusuru nchi yetu. Wapinzani hawawezi kuanzisha mchakato wa maridhiano kwani wanachojua wao na kushuhudia ni kuwa dhamira ya dola ni kuwafuta na kwamba hawana sababu yoyote ya kuwafanya kuamini kuwa dhamira hiyo imebadilika na sasa dola inataka maridhiano. Badala yake, nadhani ni watu wenye mapenzi mema ndio wanajaribu kuwashawishi wapinzani kuamini kuwa maridhiano yanawezekana na kwambà nao wanayo nafasi ya kusaidia mchakato huo kwa vitendo na kauli.
 
Kwa Wasioelewa kilichotokea Kwa Miguna wataishia kukutukana lakini kweli utabaki kuwa ukweli hii movie haina tofauti kabsa na ya hapa kwetu
 
Kesha waacheni solemba nyinyi waramba miguu sasa yeye na upinzani ni 100%
Maridhiano yaje baada ya uchaguzi 2020. Tumeshagundua janja yenu mnajua mwaka kesho hampati hata mbunge mmoja. Rais Magufuli usikubali janja ya nyani...!!
 
Back
Top Bottom