Freeman Mbowe amefanya jambo zuri sana na la kupigiwa mfano. Ila mimi kama shabiki wa cdm sifurahishwi sana na hali hii ya kutoa mambo ya maendeleo haswa mwaka wa uchaguzi. Kwa kiasi kikubwa hali hii tunaipigia kelele huko ccm kwani ikifika wakati wa uchaguzi ndio unawaona viongozi wao wakianza kurekebisha miundo mbinu kama ya maji, barabara, umeme nk. Lakini wakishapata kura huwaoni tena jimboni. Kama amewahi kutoa misaada mingine yenye tija katika jimbo lake kabla ya mwaka huu ni sawa lakini kama ni sasa naona tunaanza kutumia mbinu zilezile za kiccm.
Kwa mtu anayeangalia ukweli hapa anaweza kupata shida na dhamira ya mtoaji. Ni kweli kwamba ni muwajibikaji ama ndi walewale wanaotumia uelewa finyu wa wananchi kuwapiga bao? Nasema hivo huku nikizingatia wajibu mkubwa sana wa mbunge ni kuisimamia na kuiwajibisha serekali na wala sio mfadhili, lakini hazuiwi kutoa msaada kutoka kwenye mfuko wake au kuhamisisha watu waliokaribu naye kusaidia kutatua kero zilizo jimboni mwake na taifa kwa ujumla. Ila hali hii isisubiri tu mwaka wa kampeni maana kuna uwezekano wa kuwa ni walewale. Watanzania tuwe makini ili tusirudie kosa.