Form 4 na wengine, angalieni hapa!

Asante mkuu
 
Asante mkuu, hakika nimepata kitu kutoka kwako
 
Mpeleke NIT akasomee udereva... Dereva mzuri wa dala dala kwa siku anaondoka na sh elfu thelasini hadi hamsini.... Pesa ambayo hata mwalimu anaisikia kwenye bomba. Achana na vitabu vya mzungu hivi havina future kiviiile. Wasomi kibao wamepiga buku lakini wana miaka wanazunguka na vibahasha hata hela ya kununua boxer hawana! Too sad...
 

Mpe muda wa kutulia na kukubali matokeo hayo; muwezeshe akatembelee ndugu na jamaa kubadilisha mazingira; 2-4 weeks; akirudi mzungumzie future yake na anachotaka kufanya then try to manage the transition; amejikwaa; atanyanyuka na kusonga mbele kwa uhakika zaidi. Best wishes!
 
Akubali yaliyotokea, aanze upya ila kwa kufanya kitu tofauti... tusilazimishe watu waende darasani maana si kila mtu anauwezo huo
 
Hapo hakuna kumsikiliza kama.alikuwa anategemea kufaulu basibarudie mitihani ndio solution basi
 
duh hii ni kiboko!
 
Kama alisomea dar hiyo secondary mpeleke ufundi mikoa mingine sometimes mazingira nayo yanachangia
 
Wewe ulikuwa unafuatilia maendeleo yake shuleni kwa ukaribu?
Angalia usije ukawa unatupa pesa yako mkuu. Nakushauri km hukuwa nae karibu jaribu kudurusu taarifa zake za maendeleo ya shule. Hapo utapata mwanga wapi aelekee. Vinginevyo najua dini yako inaruhusu kufuga na kula nguruwe, kama ndivyo basi mtengenezee mabanda ya kutosha na umnunulie piglets haraka sana aanze ufugaji. Utakuwa umemkomboa sana kuliko kupoteza muda wa miaka3 ya kusoma akikomaa na huu mradi hakika utamtamani na hatakusahau maishani.
 
Nitafanya hivyo mkuu, ningoje atulie kwanza
hapo hamna namna arudie tu mtihani ili apate cheti cha form 4 ambacho kitamsaidia kuendelea mbele. Kama kwenda ufundi kama wengi wanavyoshauri ni baada ya kurudia na kupata cheti otherwise atakuwa sawa na mtu aliyemaliza darasa la saba hivyo muda wote wa miaka minne itakuwa amepoteza bure.

Mtafutie kituo na walimu sahiihi akijutia kosa ataongeza juhudi na kufaulu na pia mumpe sapoti sana haswa ya kisaikolojia
 

Very strange. Eti halutegemea wala kijana hakutegemea. Hii ni sawa na kijana kutosoma ili baadaye aje aombewe afaulu!

Mzazi/mlezi asiyejua nini cha kutegemea kwa kijana wake ni dhahiri alikuwa hafuatilii maendeleo yake. Sijui jipu la mzazi wa namna hiyo atatumbua nani.
 
Usijidanganye mrudisha shule ataja juta bure ati
 
Mi niko tayari kuozeshwa
 
Kama bado ana nia ya kusoma na wewe unauwezo wa kumsomesha mtafutie shule aanze form two.
Nasema hivi kwani hii situation ilinitokea na mimi. Nina mjomba angu nae alipata div 0 ila nikamtafutia shule akarudia form two na amefanya mtihani last year jana matokeo yametoka amepata division two ya points 19.
Kwahiyo msikilize yeye kama anataka shule bado do like that ila usimlazimishe.
Atleast kwa sasa hivi mtoto ukitaka aende vzr apate angalau first degree maisha ni magumu sana kitaa bila hata kadegree kimoja.
 
.....ANGELIKUWA KATIKA MFUMO ULE WA AWALI WA GPA HIYO ZERO ALIYOPATA INGEKUWA NI UFAULU TENA WA HALI YA JUU KABISA.Div 1++>>
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…